Yeremia 52 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 52:1-34

Anguko La Yerusalemu

(2 Wafalme 24:18–25:30)

152:1 2Fal 24:17-18; Yos 10:29; Hes 33:20; 2Fal 8:22Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia, kutoka Libna. 252:2 Yer 36:30Alifanya maovu machoni pa Bwana, kama alivyofanya Yehoyakimu. 352:3 Eze 17:12-16; Kut 33:15; Mwa 4:14Ilikuwa ni kwa sababu ya hasira ya Bwana haya yote yalitokea Yerusalemu na Yuda, naye mwishoni akawaondoa mbele zake.

Basi, Sedekia akaasi dhidi ya mfalme wa Babeli.

452:4 Zek 8:19; 2Fal 25:1-7; Yer 34:1; Eze 24:1-2; Kum 28:52-57Hivyo katika mwaka wa tisa wa utawala wa Sedekia, katika siku ya kumi ya mwezi wa kumi, Nebukadneza mfalme wa Babeli akiwa na jeshi lake lote alifanya vita dhidi ya Yerusalemu. Wakapiga kambi nje ya mji na kuuzunguka mji pande zote. 5Mji ulizungukwa na jeshi mpaka mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Mfalme Sedekia.

652:6 Law 26:26; Mao 1:11; Eze 4:16Ilipowadia siku ya tisa ya mwezi wa nne, njaa ikazidi kuwa kali sana ndani ya mji, hadi hapakuwa na chakula kwa ajili ya watu. 752:7 Mao 4:19Kisha ukuta wa mji ukavunjwa na jeshi lote likakimbia. Wakaondoka mjini usiku kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili karibu na bustani ya mfalme, ingawa Wakaldayo walikuwa wameuzunguka mji. Wakakimbia kuelekea Araba. 8Lakini jeshi la Wakaldayo likamfuatia Mfalme Sedekia na kumpata katika sehemu tambarare za Yeriko. Askari wake wote wakatengwa naye na kutawanyika, 952:9 Yer 21:7; 32:4; Hes 34:11; 13:21naye akakamatwa.

Akapelekwa kwa mfalme wa Babeli huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mahali ambapo alimtangazia hukumu. 1052:10 Yer 22:30; 39:6-7Huko Ribla mfalme wa Babeli aliwachinja wana wa Sedekia mbele ya macho yake. Pia akawaua maafisa wote wa Yuda. 1152:11 Eze 12:13; 17:16; Yer 34:4Kisha akayangʼoa macho ya Sedekia, akamfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli, alipomweka gerezani mpaka siku ya kifo chake.

1252:12 Zek 8:19; Yer 39:9; Zek 7:5Mnamo siku ya kumi ya mwezi wa tano, katika mwaka wa kumi na tisa wa utawala wa Nebukadneza mfalme wa Babeli, Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme, aliyemtumikia mfalme wa Babeli, alikuja Yerusalemu. 1352:13 2Nya 36:19; Kum 29:24; Mik 3:12; Za 74:8; Yer 19:13; Kum 13:16; Mao 2:6Alichoma moto Hekalu la Bwana, jumba la kifalme, na nyumba zote za Yerusalemu. Aliteketeza kila jengo muhimu. 14Jeshi lote la Wakaldayo chini ya jemadari wa askari walinzi wa mfalme walivunja kuta zote zilizoizunguka Yerusalemu. 1552:15 2Fal 24:1; Yer 38:19; 1:3Nebuzaradani, jemadari wa askari walinzi, akawapeleka uhamishoni baadhi ya watu maskini sana na wale waliobaki katika mji, pamoja na mabaki ya watu wa kawaida, na wale waliojisalimisha kwa mfalme wa Babeli. 16Lakini Nebuzaradani akawaacha mabaki ya wale watu maskini kabisa ili watunze mashamba ya mizabibu na mashamba mengine.

1752:17 1Fal 7:15, 27-37; Yer 27:19-22Wakaldayo walivunja vipande zile nguzo za shaba, vile vishikilio vya shaba vilivyohamishika, na ile Bahari ya shaba, ambavyo vyote vilikuwa katika Hekalu la Bwana. Hivyo wakaichukua hiyo shaba yote na kuipeleka Babeli. 1852:18 Kut 27:3; 1Fal 7:45; Hes 4:14Wakachukua pia vyungu, masepetu, mikasi ya kusawazishia tambi, mabakuli ya kunyunyizia, sahani na vyombo vyote vya shaba vilivyotumika katika huduma ya Hekalu. 1952:19 Law 10:1; 1Fal 7:50; Hes 3:31; Kut 25:29; Hes 4:7; Dan 5:2; Ezr 1:7Jemadari wa askari walinzi wa mfalme akachukua yale masinia, vile vyetezo, yale mabakuli ya kunyunyizia, zile sufuria, vile vinara vya taa, zile sahani na yale mabakuli yaliyotumika kwa sadaka za vinywaji, vitu vyote vile vilivyokuwa vimetengenezwa kwa dhahabu safi au fedha.

2052:20 1Fal 7:25, 47Shaba iliyotokana na zile nguzo mbili, ile Bahari na wale mafahali kumi na mawili wa shaba waliokuwa chini yake, pamoja na vile vishikilio vilivyohamishika, ambavyo Mfalme Solomoni alikuwa ametengeneza kwa ajili ya Hekalu la Bwana, ilikuwa na uzito usioweza kupimika. 21Kila nguzo ilikuwa na urefu wa dhiraa kumi na nane, kimo chake na mzunguko dhiraa kumi na mbili, na unene wa nyanda nne, na zote zilikuwa wazi ndani. 2252:22 1Fal 7:15-16, 20, 47; Kut 28:33Sehemu ya shaba juu ya ile nguzo moja ilikuwa na urefu wa dhiraa tano, na ilikuwa imepambwa kwa wavu na makomamanga ya shaba kuizunguka kote. Ile nguzo nyingine pamoja na makomamanga yake ilifanana na hiyo ya kwanza. 23Kulikuwa na makomamanga tisini na sita pembeni; jumla ya makomamanga juu ya wavu uliokuwa umezunguka yalikuwa mia moja.

2452:24 2Fal 25:18; Yer 37:3; 21:1; 2Fal 12:9Yule jemadari wa askari walinzi akawachukua kama wafungwa Seraya kuhani mkuu, kuhani Sefania aliyefuata kwa cheo, na mabawabu watatu. 2552:25 Yer 36:10Miongoni mwa wale watu waliokuwa wamesalia katika mji, alimchukua afisa kiongozi wa wapiganaji, na washauri saba wa mfalme. Akamchukua pia mwandishi aliyesimamia uandikishaji wa watu wa nchi, pamoja na watu wake sitini waliopatikana ndani ya mji. 26Nebuzaradani jemadari akawachukua hao wote na kuwapeleka kwa mfalme wa Babeli huko Ribla. 2752:27 Yer 20:4; Law 26:33; Hes 34:11Huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mfalme wa Babeli akaamuru wanyongwe.

Hivyo Yuda wakaenda utumwani, mbali na nchi yao. 2852:28 2Fal 24:14-16; Neh 1:2; 2Nya 36:20; Kum 28:36Hii ndiyo hesabu ya watu ambao Nebukadneza aliwachukua kwenda uhamishoni:

katika mwaka wa saba,

Wayahudi 3,023;

29katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Nebukadneza,

watu 832 kutoka Yerusalemu;

3052:30 Yer 43:3; 13:19katika mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wake,

Wayahudi 745 walichukuliwa kwenda uhamishoni na Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme.

Jumla ya watu wote walikuwa 4,600.

Yehoyakini Anaachiwa Huru

3152:31 2Fal 25:27-30; Mwa 40:13-20Katika mwaka wa thelathini na saba tangu Yehoyakini mfalme wa Yuda apelekwe uhamishoni, katika mwaka ule ambao Evil-Merodaki52:31 Pia aliitwa Ameli-Mariduki. alifanyika mfalme wa Babeli, alimwacha huru Yehoyakini mfalme wa Yuda, na kumfungua kutoka gerezani siku ya ishirini na tano ya mwezi wa kumi na mbili. 32Alizungumza naye kwa upole na kumpa kiti cha heshima zaidi kuliko wale wafalme wengine aliokuwa nao huko Babeli. 3352:33 2Sam 9:7, 13Hivyo Yehoyakini akayavua mavazi yake ya mfungwa, na siku zote za maisha yake zilizobaki alikula mezani mwa mfalme. 3452:34 2Sam 9:10Siku kwa siku mfalme wa Babeli alimpa Yehoyakini posho siku zote za maisha yake, hadi siku ya kifo chake.

Swedish Contemporary Bible

Jeremia 52:1-34

Sidkia regerar i Jerusalem

(2 Kung 24:18-20; 2 Krön 36:11-14)

1Sidkia var tjugoett år gammal när han blev kung, och han regerade i elva år i Jerusalem. Hans mor hette Hamutal och var dotter till Jeremia från Livna. 2Han gjorde det som var ont i Herrens ögon, precis som Jojakim hade gjort. 3Herren förkastade till sist i sin vrede både Jerusalem och Juda.

Jerusalems fall, förstörelse och folkets bortförande

(2 Kung 24:20—25:21; 2 Krön 36:15-20; Jer 39:1-10)

Men Sidkia gjorde uppror mot kungen i Babylonien. 4I Sidkias nionde regeringsår, på den tionde dagen i tionde månaden, kom Nebukadnessar, kungen av Babylonien, tågande med hela sin armé mot Jerusalem och belägrade det. De byggde en belägringsvall omkring staden. 5Belägringen varade ända till kung Sidkias elfte regeringsår. 6På nionde dagen i fjärde månaden var hungersnöden i staden så svår att folket inte längre hade någon mat i landet. 7Då stormades staden, och alla trupper flydde på natten genom en port som fanns mellan de båda murarna i närheten av den kungliga trädgården, medan de kaldeiska trupperna omringade staden. De flydde mot Jordandalen.

8Men den kaldeiska armén förföljde kungen och tog honom till fånga på Jerikoslätten. Alla hans män lämnade honom och skingrades. 9Kaldéerna grep honom och förde honom till den babyloniske kungen i Rivla i Hamat, där denne dömde honom. 10Den babyloniske kungen lät avrätta Sidkias söner inför hans ögon, och likaså lät han i Rivla avrätta alla de förnämsta männen i Juda. 11Sedan lät han sticka ut ögonen på Sidkia. Den babyloniske kungen band honom med kopparkedjor och förde honom till Babylon och satte honom i fängelse, och där fick han sitta ända tills han dog.

12På tionde dagen i femte månaden av den babyloniske kungen Nebukadnessars nittonde regeringsår kom Nebusaradan, befälhavaren för livgardet och en av den babyloniske kungens närmaste män, till Jerusalem. 13Han brände ner Herrens hus, kungapalatset, och även alla andra byggnader av värde i Jerusalem. 14De kaldeiska trupperna som han var befälhavare för rev ner alla Jerusalems murar. 15Nebusaradan, befälhavaren för livgardet, förde bort till exilen några av de fattigaste som var kvar i staden, tillsammans med de desertörer som hade gått över till den babyloniske kungen och de hantverkare som var kvar, 16men några av de fattigaste i landet lämnade befälhavaren Nebusaradan kvar för att sköta om vingårdar och åkrar.

17Kaldéerna högg ner kopparpelarna i Herrens hus, ställningen och kopparhavet som fanns där och tog med sig all koppar till Babylonien. 18De tog också kärlen, skovlarna, knivarna, skålarna, fyrfaten och alla kopparföremål som användes i gudstjänsten. 19Befälhavaren för livgardet tog också faten, fyrfaten, offerskålarna, grytorna, lampställen, skålarna och bägarna, allt som var av rent guld och rent silver.

20Pelarna, kopparhavet, de tolv koppartjurarna under det och ställningarna, som Salomo låtit göra till Herrens hus, bestod sammantaget av så mycket koppar att det inte gick att väga. 21Pelarna var 9 meter höga, 6 meter i omkrets och ihåliga med väggar tjocka som fyra fingrars bredd.52:21 Uppgifterna om pelarna, liksom en del andra detaljer i templet, varierar något, jfr 1 Kung 7 och 2 Krön 3-5 (spec. 3:15). Tjockleken på pelarna/pelarväggarna kan tolkas olika, men det troligaste är att pelarväggarna (även om ordet inte finns i grundtexten här) var fyra fingerbredder, dvs. ca 10 cm. 22På var och en av dem fanns ett pelarhuvud av koppar, som var 2,5 meter högt och hade ornament i form av granatäpplen som dekoration runt pelarhuvudet. Allt var gjort av koppar. 23Det fanns nittiosex granatäpplen på utsidan och sammanlagt etthundra granatäpplen i ett flätverk runtom.

24Befälhavaren för livgardet tog till fånga översteprästen Seraja och prästen närmast honom, Sefanja, samt tre av dörrvakterna. 25Från staden tog han en hovman som var befälhavare i armén, sju av kungens närmaste män i staden, och sekreteraren åt den överbefälhavare som skrev ut folket till krigstjänst, samt ytterligare sextio män i staden. 26Nebusaradan, befälhavaren för livgardet, tog dem och förde dem till den babyloniske kungen i Rivla. 27Den babyloniske kungen lät avrätta dem i Rivla i Hamat. Så fördes Juda bort från sitt land.

28Detta är de som Nebukadnessar förde bort:

under det sjunde året 3 023 judar,

29under Nebukadnessars artonde regeringsår 832 personer från Jerusalem,

30och under Nebukadnessars tjugotredje regeringsår 745 personer,

som Nebusaradan, befälhavaren för livgardet, förde bort,

sammanlagt 4 600 personer.

Jojakins benådning

(2 Kung 25:27-30)

31Under det trettiosjunde året som Judas kung Jojakin var i fångenskap, den tjugofemte dagen i tolfte månaden, samma år som Evil Merodak blev kung i Babylonien, benådade denne Jojakin, Juda kung, och släppte ut honom ur fängelset. 32Han talade vänligt till honom och gav honom den främsta platsen bland de kungar som var hos honom i Babylon. 33Jojakin fick lägga av sig fångdräkten och alltid äta vid kungens bord under resten av sitt liv. 34Så länge han levde gav den babyloniske kungen honom också ett dagligt underhåll.