Yeremia 52 – NEN & BPH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 52:1-34

Anguko La Yerusalemu

(2 Wafalme 24:18–25:30)

152:1 2Fal 24:17-18; Yos 10:29; Hes 33:20; 2Fal 8:22Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia, kutoka Libna. 252:2 Yer 36:30Alifanya maovu machoni pa Bwana, kama alivyofanya Yehoyakimu. 352:3 Eze 17:12-16; Kut 33:15; Mwa 4:14Ilikuwa ni kwa sababu ya hasira ya Bwana haya yote yalitokea Yerusalemu na Yuda, naye mwishoni akawaondoa mbele zake.

Basi, Sedekia akaasi dhidi ya mfalme wa Babeli.

452:4 Zek 8:19; 2Fal 25:1-7; Yer 34:1; Eze 24:1-2; Kum 28:52-57Hivyo katika mwaka wa tisa wa utawala wa Sedekia, katika siku ya kumi ya mwezi wa kumi, Nebukadneza mfalme wa Babeli akiwa na jeshi lake lote alifanya vita dhidi ya Yerusalemu. Wakapiga kambi nje ya mji na kuuzunguka mji pande zote. 5Mji ulizungukwa na jeshi mpaka mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Mfalme Sedekia.

652:6 Law 26:26; Mao 1:11; Eze 4:16Ilipowadia siku ya tisa ya mwezi wa nne, njaa ikazidi kuwa kali sana ndani ya mji, hadi hapakuwa na chakula kwa ajili ya watu. 752:7 Mao 4:19Kisha ukuta wa mji ukavunjwa na jeshi lote likakimbia. Wakaondoka mjini usiku kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili karibu na bustani ya mfalme, ingawa Wakaldayo walikuwa wameuzunguka mji. Wakakimbia kuelekea Araba. 8Lakini jeshi la Wakaldayo likamfuatia Mfalme Sedekia na kumpata katika sehemu tambarare za Yeriko. Askari wake wote wakatengwa naye na kutawanyika, 952:9 Yer 21:7; 32:4; Hes 34:11; 13:21naye akakamatwa.

Akapelekwa kwa mfalme wa Babeli huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mahali ambapo alimtangazia hukumu. 1052:10 Yer 22:30; 39:6-7Huko Ribla mfalme wa Babeli aliwachinja wana wa Sedekia mbele ya macho yake. Pia akawaua maafisa wote wa Yuda. 1152:11 Eze 12:13; 17:16; Yer 34:4Kisha akayangʼoa macho ya Sedekia, akamfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli, alipomweka gerezani mpaka siku ya kifo chake.

1252:12 Zek 8:19; Yer 39:9; Zek 7:5Mnamo siku ya kumi ya mwezi wa tano, katika mwaka wa kumi na tisa wa utawala wa Nebukadneza mfalme wa Babeli, Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme, aliyemtumikia mfalme wa Babeli, alikuja Yerusalemu. 1352:13 2Nya 36:19; Kum 29:24; Mik 3:12; Za 74:8; Yer 19:13; Kum 13:16; Mao 2:6Alichoma moto Hekalu la Bwana, jumba la kifalme, na nyumba zote za Yerusalemu. Aliteketeza kila jengo muhimu. 14Jeshi lote la Wakaldayo chini ya jemadari wa askari walinzi wa mfalme walivunja kuta zote zilizoizunguka Yerusalemu. 1552:15 2Fal 24:1; Yer 38:19; 1:3Nebuzaradani, jemadari wa askari walinzi, akawapeleka uhamishoni baadhi ya watu maskini sana na wale waliobaki katika mji, pamoja na mabaki ya watu wa kawaida, na wale waliojisalimisha kwa mfalme wa Babeli. 16Lakini Nebuzaradani akawaacha mabaki ya wale watu maskini kabisa ili watunze mashamba ya mizabibu na mashamba mengine.

1752:17 1Fal 7:15, 27-37; Yer 27:19-22Wakaldayo walivunja vipande zile nguzo za shaba, vile vishikilio vya shaba vilivyohamishika, na ile Bahari ya shaba, ambavyo vyote vilikuwa katika Hekalu la Bwana. Hivyo wakaichukua hiyo shaba yote na kuipeleka Babeli. 1852:18 Kut 27:3; 1Fal 7:45; Hes 4:14Wakachukua pia vyungu, masepetu, mikasi ya kusawazishia tambi, mabakuli ya kunyunyizia, sahani na vyombo vyote vya shaba vilivyotumika katika huduma ya Hekalu. 1952:19 Law 10:1; 1Fal 7:50; Hes 3:31; Kut 25:29; Hes 4:7; Dan 5:2; Ezr 1:7Jemadari wa askari walinzi wa mfalme akachukua yale masinia, vile vyetezo, yale mabakuli ya kunyunyizia, zile sufuria, vile vinara vya taa, zile sahani na yale mabakuli yaliyotumika kwa sadaka za vinywaji, vitu vyote vile vilivyokuwa vimetengenezwa kwa dhahabu safi au fedha.

2052:20 1Fal 7:25, 47Shaba iliyotokana na zile nguzo mbili, ile Bahari na wale mafahali kumi na mawili wa shaba waliokuwa chini yake, pamoja na vile vishikilio vilivyohamishika, ambavyo Mfalme Solomoni alikuwa ametengeneza kwa ajili ya Hekalu la Bwana, ilikuwa na uzito usioweza kupimika. 21Kila nguzo ilikuwa na urefu wa dhiraa kumi na nane, kimo chake na mzunguko dhiraa kumi na mbili, na unene wa nyanda nne, na zote zilikuwa wazi ndani. 2252:22 1Fal 7:15-16, 20, 47; Kut 28:33Sehemu ya shaba juu ya ile nguzo moja ilikuwa na urefu wa dhiraa tano, na ilikuwa imepambwa kwa wavu na makomamanga ya shaba kuizunguka kote. Ile nguzo nyingine pamoja na makomamanga yake ilifanana na hiyo ya kwanza. 23Kulikuwa na makomamanga tisini na sita pembeni; jumla ya makomamanga juu ya wavu uliokuwa umezunguka yalikuwa mia moja.

2452:24 2Fal 25:18; Yer 37:3; 21:1; 2Fal 12:9Yule jemadari wa askari walinzi akawachukua kama wafungwa Seraya kuhani mkuu, kuhani Sefania aliyefuata kwa cheo, na mabawabu watatu. 2552:25 Yer 36:10Miongoni mwa wale watu waliokuwa wamesalia katika mji, alimchukua afisa kiongozi wa wapiganaji, na washauri saba wa mfalme. Akamchukua pia mwandishi aliyesimamia uandikishaji wa watu wa nchi, pamoja na watu wake sitini waliopatikana ndani ya mji. 26Nebuzaradani jemadari akawachukua hao wote na kuwapeleka kwa mfalme wa Babeli huko Ribla. 2752:27 Yer 20:4; Law 26:33; Hes 34:11Huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mfalme wa Babeli akaamuru wanyongwe.

Hivyo Yuda wakaenda utumwani, mbali na nchi yao. 2852:28 2Fal 24:14-16; Neh 1:2; 2Nya 36:20; Kum 28:36Hii ndiyo hesabu ya watu ambao Nebukadneza aliwachukua kwenda uhamishoni:

katika mwaka wa saba,

Wayahudi 3,023;

29katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Nebukadneza,

watu 832 kutoka Yerusalemu;

3052:30 Yer 43:3; 13:19katika mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wake,

Wayahudi 745 walichukuliwa kwenda uhamishoni na Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme.

Jumla ya watu wote walikuwa 4,600.

Yehoyakini Anaachiwa Huru

3152:31 2Fal 25:27-30; Mwa 40:13-20Katika mwaka wa thelathini na saba tangu Yehoyakini mfalme wa Yuda apelekwe uhamishoni, katika mwaka ule ambao Evil-Merodaki52:31 Pia aliitwa Ameli-Mariduki. alifanyika mfalme wa Babeli, alimwacha huru Yehoyakini mfalme wa Yuda, na kumfungua kutoka gerezani siku ya ishirini na tano ya mwezi wa kumi na mbili. 32Alizungumza naye kwa upole na kumpa kiti cha heshima zaidi kuliko wale wafalme wengine aliokuwa nao huko Babeli. 3352:33 2Sam 9:7, 13Hivyo Yehoyakini akayavua mavazi yake ya mfungwa, na siku zote za maisha yake zilizobaki alikula mezani mwa mfalme. 3452:34 2Sam 9:10Siku kwa siku mfalme wa Babeli alimpa Yehoyakini posho siku zote za maisha yake, hadi siku ya kifo chake.

Bibelen på hverdagsdansk

Jeremiasʼ Bog 52:1-34

Historisk oversigt over Jerusalems fald

1Zidkija var 21 år gammel, da han blev konge, og han regerede i Jerusalem i 11 år. Hans mor hed Hamutal og var datter af Jirmeja fra byen Libna. 2Han gjorde, hvad der var ondt i Herrens øjne, ligesom Jojakim havde gjort. 3Til sidst var Jerusalems og Judas oprør og ugudelighed blevet så voldsom, at Herren var nødt til at straffe dem og sende dem i eksil. Det varede ikke længe, før Zidkija gjorde oprør imod den babyloniske konge.

4Derfor mobiliserede kong Nebukadnezar igen sin hær og drog mod Jerusalem. I kong Zidkijas niende regeringsår, på den tiende dag i den tiende måned, begyndte den babyloniske hær en svær belejring af byen. De byggede angrebsramper op imod bymuren. 5Belejringen varede til kong Zidkijas 11. regeringsår. 6På den niende dag i den fjerde måned af det år var alt spiseligt sluppet op og befolkningen totalt udsultet. 7På det tidspunkt brød fjenden hul gennem bymuren og den judæiske hær prøvede at flygte. Nogle forlod byen om natten gennem paladsets have, igennem en korridor mellem to mure, ud af en port i bymuren og videre i retning af Jordandalen. Men de babyloniske tropper holdt vagt rundt omkring byen, 8og de satte efter kong Zidkija og indhentede ham på sletten ved Jeriko. Hans soldater flygtede i alle retninger, 9men han selv blev fanget og ført til den babyloniske konge i byen Ribla i Hamat-området, hvor han blev anklaget og dømt. 10Han blev tvunget til at overvære sine sønners og nærmeste embedsmænds henrettelse, 11hvorefter hans øjne blev stukket ud. Så blev han lagt i lænker og ført til Babylon, hvor han blev holdt fængslet til sin død.

12På den tiende dag i den femte måned i kong Nebukadnezars 19. regeringsår kom Nebuzaradan til Jerusalem fra Babylon. Nebuzaradan var chef for den babyloniske konges livvagt. 13Han nedbrændte Herrens tempel, kongens palads og alle byens mest betydningsfulde bygninger, 14hvorefter han beordrede sine tropper til at rive Jerusalems bymur ned. 15Så samlede han resten af byens indbyggere, håndværkerne og de, der havde overgivet sig, for at føre dem til Babylon i eksil. 16Kun de fattigste lod Nebuzaradan blive tilbage, så der var nogen til at dyrke jorden og passe vingårdene.

17Babylonierne slog templets bronzesøjler, bronzehavet og alle rullebordene i stykker og tog alt metallet med sig hjem til Babylon. 18De tog alt, hvad der var lavet af bronze: askebakkerne, skovlene, vægesaksene, fadene, skålene og de bronzeredskaber der blev brugt ved ofringerne i templet. 19Nebuzaradan tog selv, hvad der var af guld og sølvting: skålene, bakkerne til gløder, stænkeskålene, fadene, lysestagerne og de forskellige drikofferskåle. 20Det hele blev vejet, undtagen de to søjler, bronzehavet, de 12 bronzetyre og rullebordene, som kong Salomon i sin tid havde ladet fremstille til Herrens tempel. De var for store til at blive vejet. 21Søjlerne var 8,1 m høje og 5,4 m i omkreds. De var hule med en tykkelse på fire fingre. 22Foroven havde de et søjlehoved på 2,25 m med en dekoration af fletværk og granatæbler i bronze. 23På siderne var der 96 granatæbler og øverst på søjlehovedet yderligere 100 granatæbler hele vejen rundt.

24Af tempelpersonalet tog Nebuzaradan følgende krigsfanger: Ypperstepræsten Seraja, andenpræsten Zefanja og de tre dørvogtere. 25Fra byen tog han den øverstkommanderende officer, en rekrutteringsofficer, syv af kongens tidligere rådgivere og 60 andre betydningsfulde mænd, som var gået under jorden. 26Han førte disse mænd til den babyloniske konge i Ribla i Hamat-området, 27hvor de alle blev henrettet. Judas folk var nu ført bort fra deres land og måtte leve i eksil.

28I Nebukadnezars syvende regeringsår blev i alt 3023 judæere ført i eksil, 29i hans 18. regeringsår yderligere 832 fanger fra Jerusalem, 30og i hans 23. regeringsår bortførte Nebuzaradan 745 fanger fra Juda, alt i alt 4600 fanger.

Jojakin får bedre forhold under sit fangenskab

31Mange år senere kom der en ny konge på tronen i Babylon, som hed Evil-Merodak. Han besluttede at benåde Jojakin og løslade ham fra fængslet. Det skete den 27. dag i den 12. måned i Jojakins 37. år i fangenskab. 32Den nye konge behandlede Jojakin venligt, bedre end de andre konger, som også var i fangenskab. 33Jojakin fik nyt tøj i stedet for fangedragten, og han spiste i kongens palads indtil sin dødsdag. 34Så længe han levede, gav kongen ham fra dag til dag, hvad han havde brug for.