Yeremia 50 – NEN & OL

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 50:1-46

Ujumbe Kuhusu Babeli

150:1 Isa 13:1; Za 137:8; Mwa 10:10Hili ndilo neno alilosema Bwana kupitia nabii Yeremia kuhusu Babeli na nchi ya Wakaldayo:

250:2 Kum 30:4; Yer 4:16; 51:31, 47; Isa 21:9; Za 20:5; Isa 13:2; Yer 46:6; Law 26:30“Tangazeni na mhubiri katikati ya mataifa,

twekeni bendera na mkahubiri;

msiache kitu chochote, bali semeni,

‘Babeli utatekwa;

Beli ataaibishwa,

Merodaki atajazwa na hofu kuu.

Sanamu zake zitaaibishwa

na vinyago vyake vitajazwa hofu kuu.’

350:3 Isa 14:22-23; Yer 9:11; Sef 1:3; Isa 13:17; 41:25; Yer 25:26Taifa kutoka kaskazini litamshambulia,

na kuifanya nchi yake ukiwa.

Hakuna hata mmoja atakayeishi ndani yake,

watu na wanyama wataikimbia.

450:4 Eze 37:22; Ezr 3:12; Yer 31:9; Isa 9:13; Hos 3:5; Yer 3:18“Katika siku hizo, wakati huo,”

asema Bwana,

“watu wa Israeli pamoja na watu wa Yuda

wataenda wakilia ili kumtafuta Bwana Mungu wao.

550:5 1Sam 29:1; Yer 33:7; Kum 29:14; Ebr 8:6-10; Isa 11:16; Yer 31:21; 32:40Wataiuliza njia iendayo Sayuni

na kuelekeza nyuso zao huko.

Watakuja na kuambatana na Bwana

katika agano la milele

ambalo halitasahaulika.

650:6 Isa 53:6; Mt 10:6; Yer 3:6; Eze 34:6; Za 119:176; Mt 9:36; Yer 10:21; Za 95:10“Watu wangu wamekuwa kondoo waliopotea;

wachungaji wao wamewapotosha

na kuwasababisha kuzurura

juu ya milima.

Walitangatanga juu ya mlima na kilima,

na kusahau mahali pao wenyewe pa kupumzikia.

750:7 Yer 2:3; 14:8; Za 22:4; Yer 5:17; 10:25; Eze 35:12Yeyote aliyewakuta aliwala;

adui zao walisema, ‘Sisi hatuna hatia,

kwa kuwa wao walitenda dhambi dhidi ya Bwana, malisho yao halisi,

Bwana, aliye tumaini la baba zao.’

850:8 Isa 48:20; Ufu 18:4; Yer 51:6“Kimbieni kutoka Babeli;

ondokeni katika nchi ya Wakaldayo

tena kuweni kama mbuzi wale waongozao kundi.

950:9 Isa 13:17; Yer 25:14; Isa 41:25; Yer 25:26Kwa maana nitaamsha na kuleta dhidi ya Babeli

muungano wa mataifa makubwa kutoka nchi ya kaskazini.

Watashika nafasi zao dhidi yake,

naye kutokea kaskazini atatekwa.

Mishale yao itakuwa kama mishale ya mashujaa walio hodari,

ambao hawawezi kurudi mikono mitupu.

10Kwa hiyo Ukaldayo utatekwa nyara;

wote wamtekao nyara watapata za kutosha,”

asema Bwana.

1150:11 Isa 47:6; Yer 31:18“Kwa sababu hushangilia na kufurahi,

wewe utekaye urithi wangu,

kwa sababu unachezacheza kama mtamba anayepura nafaka,

na kulia kama farasi dume,

1250:12 Yer 51:47; 25:12; 51:26mama yako ataaibika mno,

yeye aliyekuzaa atatahayari.

Atakuwa mdogo kuliko mataifa mengine yote,

atakuwa nyika, nchi kame na jangwa.

1350:13 Eze 27:36; Hab 2:6; Kum 29:22; Yer 49:17; 9:11; 48:9; 51:62; 18:16Kwa sababu ya hasira ya Bwana hatakaliwa na mtu,

lakini ataachwa ukiwa kabisa.

Wote watakaopita Babeli watatiwa hofu na kudhihaki

kwa sababu ya majeraha yake yote.

14“Shikeni nafasi zenu kuzunguka Babeli,

enyi nyote mvutao upinde.

Mpigeni! Msibakize mshale wowote,

kwa kuwa ametenda dhambi dhidi ya Bwana.

1550:15 Yer 51:14; 2Nya 30:8; Yer 51:44-58; 2Fal 25:4; Yer 51:6; Ufu 18:6; Isa 10:3; Hab 2:7-8Piga kelele dhidi yake kila upande!

Anajisalimisha, minara yake inaanguka,

kuta zake zimebomoka.

Kwa kuwa hiki ni kisasi cha Bwana,

mlipizeni kisasi;

mtendeeni kama alivyowatendea wengine.

1650:16 Yer 25:38; Isa 13:14; Yer 51:9Katilieni mbali mpanzi kutoka Babeli,

pamoja na mvunaji na mundu wake akivuna.

Kwa sababu ya upanga wa mdhalimu

kila mmoja na arejee kwa watu wake mwenyewe,

kila mmoja na akimbilie

kwenye nchi yake mwenyewe.

1750:17 2Fal 24:1; Yer 2:15; Kum 4:27; 2Fal 17:6; 24:10-17; 1Pet 2:25; Yer 2:15; Hes 24:8“Israeli ni kundi lililotawanyika

ambalo simba wamelifukuzia mbali.

Wa kwanza kumla alikuwa mfalme wa Ashuru,

wa mwisho kuponda mifupa yake

alikuwa Nebukadneza mfalme wa Babeli.”

1850:18 Isa 10:12; Eze 31:3; Sef 2:13Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo:

“Nitamwadhibu mfalme wa Babeli na nchi yake

kama nilivyomwadhibu mfalme wa Ashuru.

1950:19 Yer 31:10; Eze 34:13; Yer 33:12; Isa 65:10; Mik 7:14; Zek 10:10Lakini nitamrudisha Israeli katika malisho yake mwenyewe

naye atalisha huko Karmeli na Bashani;

njaa yake itashibishwa

juu ya vilima vya Efraimu na Gileadi.

2050:20 Za 103:12; Zek 3:4-9; Isa 33:24; Yer 31:34; Rum 9:27; Isa 10:20-22; Eze 36:16Katika siku hizo, wakati huo,”

asema Bwana,

“uchunguzi utafanyika kwa ajili ya kosa la Israeli,

lakini halitakuwepo,

kwa ajili ya dhambi za Yuda,

lakini haitapatikana hata moja,

kwa kuwa nitawasamehe

mabaki nitakaowaacha.

2150:21 Eze 23:23; Isa 10:6“Shambulieni nchi ya Merathaimu

na wale waishio huko Pekodi.

Wafuatieni, waueni

na kuwaangamiza kabisa,”

asema Bwana.

“Fanyeni kila kitu nilichowaamuru.

2250:22 Yer 4:19-21; 51:54Kelele ya vita iko ndani ya nchi,

kelele ya maangamizi makuu!

2350:23 Isa 14:16; Yer 51:20; Isa 10:5Tazama jinsi nyundo ya dunia yote

ilivyovunjika na kuharibika!

Tazama jinsi Babeli ilivyokuwa ukiwa

miongoni mwa mataifa!

2450:24 Yer 51:12; Dan 5:30-31; Yer 51:31; Ay 9:4Nimetega mtego kwa ajili yako, ee Babeli,

nawe ukakamatwa kabla haujafahamu;

ulipatikana na ukakamatwa

kwa sababu ulimpinga Bwana.

2550:25 Isa 13:5Bwana amefungua ghala lake la silaha

na kuzitoa silaha za ghadhabu yake,

kwa kuwa Bwana Mwenyezi Mwenye Nguvu Zote

anayo kazi ya kufanya

katika nchi ya Wakaldayo.

2650:26 Isa 14:22-23; Yer 51:11; Rut 3:7Njooni dhidi yake kutoka mbali.

Zifungueni ghala zake za nafaka;

mlundikeni kama lundo la nafaka.

Mwangamizeni kabisa

na msimwachie mabaki yoyote.

2750:27 Za 68:30; Yer 48:15; Ay 18:20; Yer 25:34Waueni mafahali wake wachanga wote;

waacheni washuke machinjoni!

Ole wao! Kwa kuwa siku yao imewadia,

wakati wao wa kuadhibiwa.

2850:28 Isa 48:20; Yer 51:10; 2Fal 24:13; Yer 52:13Wasikilizeni watoro na wakimbizi kutoka Babeli

wakitangaza katika Sayuni

jinsi Bwana, Mungu wetu alivyolipiza kisasi,

kisasi kwa ajili ya Hekalu lake.

2950:29 Ay 21:19; Ufu 18:6; Oba 1:15; Dan 5:23; Isa 14:13-14; Mao 3:24; Isa 13:18; Kum 32:41“Waiteni wapiga mishale dhidi ya Babeli,

wote wale wavutao upinde.

Pigeni kambi kumzunguka kabisa,

asitoroke mtu yeyote.

Mlipizeni kwa matendo yake;

mtendeeni kama alivyotenda.

Kwa kuwa alimdharau Bwana,

yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

3050:30 Isa 13:18; Yer 49:26; 51:4Kwa hiyo, vijana wake wanaume wataanguka barabarani;

askari wake wote watanyamazishwa siku ile,”

asema Bwana.

3150:31 Yer 21:13; Ufu 18:7-8“Tazama, niko kinyume nawe, ewe mwenye majivuno,”

asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote,

“kwa kuwa siku yako imewadia,

yaani, wakati wako wa kuadhibiwa.

3250:32 Yer 21:14; 49:27; Amo 5:2; Za 20:8; 119:21Mwenye majivuno atajikwaa na kuanguka,

wala hakuna yeyote atakayemuinua;

nitawasha moto katika miji yake,

utakaowateketeza wote wanaomzunguka.”

3350:33 Isa 58:6; 14:17Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote:

“Watu wa Israeli wameonewa,

nao watu wa Yuda pia.

Wote waliowateka wamewashikilia sana,

wanakataa kuwaachia waende.

3450:34 Yer 31:35; 51:19; Za 119:154; Mao 3:58; Kut 6:6; Ay 19:25; Isa 49:25Lakini Mkombozi wao ana nguvu;

Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake.

Atatetea kwa nguvu shauri lao

ili alete raha katika nchi yao,

lakini ataleta msukosuko

kwa wale waishio Babeli.

3550:35 Yer 47:6; Dan 5:7; Isa 37:13; 45:1“Upanga dhidi ya Wakaldayo!”

asema Bwana,

“dhidi ya wale waishio Babeli

na dhidi ya maafisa wake na watu wenye busara!

36Upanga dhidi ya manabii wake wa uongo!

Watakuwa wapumbavu.

Upanga dhidi ya mashujaa wake!

Watajazwa na hofu kuu

3750:37 Yer 25:20; 2Fal 19:23; Isa 19:16; Yer 51:21; Nah 3:13; Isa 45:3Upanga dhidi ya farasi na magari yake ya vita

pamoja na askari wake wote wa kigeni katika safu zake!

Wao watakuwa kama wanawake.

Upanga dhidi ya hazina zake!

Hizo zitatekwa nyara.

3850:38 Isa 11:15; Yer 51:36; Ufu 16:12Ukame juu ya maji yake!

Nayo yatakauka.

Kwa kuwa ni nchi ya sanamu,

wao wanaenda wazimu kwa ajili ya sanamu.

3950:39 Isa 34:13-15; Ufu 18:2; Isa 13:19-22; Za 74:14; Yer 51:37“Kwa hiyo, viumbe vya jangwani na fisi wataishi humo,

nao bundi watakaa humo.

Kamwe haitakaliwa tena

wala watu hawataishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.

4050:40 Mwa 19:24; Mt 10:15; 2Pet 2:6; Yer 51:62Kama vile Mungu alivyoangamiza Sodoma na Gomora

pamoja na miji iliyokuwa jirani nayo,”

asema Bwana,

“vivyo hivyo hakuna mtu yeyote

atakayeishi humo.

Naam, hakuna mtu yeyote

atakayekaa humo.

4150:41 Isa 41:25; Yer 6:22; Isa 13:14; Yer 51:22-28; Ufu 17:16; Isa 23:17“Tazama! Jeshi linakuja kutoka kaskazini;

taifa kubwa na wafalme wengi

wanaamshwa kutoka miisho ya dunia.

4250:42 Isa 13:18; 5:30; 47:1; Yer 6:23; Ay 30:21Wamejifunga pinde na mikuki;

ni wakatili na wasio na huruma.

Wanatoa sauti kama bahari inayonguruma

wanapoendesha farasi zao;

wanakuja kama watu waliojipanga tayari kwa vita

ili kukushambulia, ee Binti Babeli.

4350:43 Yer 47:3; 6:22-24Mfalme wa Babeli amesikia habari kuwahusu,

nayo mikono yake imelegea.

Uchungu umemshika,

maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.

4450:44 Hes 16:5; Ay 41:10; Isa 46:9; Yer 12:5; 49:19Kama simba anayepanda kutoka vichaka vya Yordani

kuja kwenye nchi ya malisho mengi,

ndivyo nitamfukuza Babeli kutoka nchi yake ghafula.

Ni nani aliye mteule,

nitakayemweka kwa ajili ya jambo hili?

Ni nani aliye kama mimi,

na ni nani awezaye kunipinga?

Tena ni mchungaji yupi

awezaye kusimama kinyume nami?”

4550:45 Isa 24:14; Mdo 4:28; Isa 48:14; Yer 51:11Kwa hiyo, sikia kile Bwana alichokipanga dhidi ya Babeli,

kile alichokusudia dhidi ya nchi ya Wakaldayo:

Aliye mchanga katika kundi ataburutwa mbali.

Yeye ataharibu kabisa malisho yao kwa sababu yao.

4650:46 Ay 24:12; Ufu 18:9-10; Amu 5:4; Yer 49:21Kwa sauti ya kutekwa kwa Babeli, dunia itatetemeka;

kilio chake kitasikika pote miongoni mwa mataifa.

O Livro

Jeremias 50:1-46

Uma mensagem sobre a Babilónia

1Esta é a mensagem do Senhor contra a Babilónia e contra os caldeus, proferida por Jeremias, o profeta. 2“Diz a todo o mundo que a Babilónia será destruída; não façam segredo disso. O seu ídolo Bel foi humilhado, o seu deus Merodaque caiu totalmente em desgraça! 3Porque uma outra nação virá sobre ela do norte e com tal destruição que ninguém poderá continuar a viver ali; toda a gente partirá, homens e animais, todos fugirão.

4Então os povos de Israel e de Judá se juntarão e chorarão, buscando o Senhor, seu Deus. 5Perguntarão pelo caminho para Sião e começarão a regressar. ‘Vamos!’, dirão eles. ‘Unamo-nos ao Senhor, por meio duma aliança eterna que nunca mais será quebrado!’

6O meu povo é como uma ovelha perdida. Os seus pastores fizeram-no errar no caminho, desviando-os para os montes. Perdeu-se e não sabe voltar atrás. 7Todos os que o encontram devoram-no e dizem: ‘Podemos atacá-lo à vontade, visto que pecou contra o Senhor, o Deus da justiça, a esperança dos seus antepassados.’

8Mas agora, fujam da Babilónia, a terra dos caldeus! Que o meu povo volte para casa, como os bodes, sempre à frente do rebanho! 9Pois estou a levantar um exército de grandes nações do norte e vou trazê-lo contra a Babilónia, a qual será atacada e destruída. As setas deles, dos inimigos, não falharão o alvo, terão pontaria certeira! 10A Caldeia será saqueada até que cada combatente esteja saciado com o despojo que obteve, diz o Senhor.

11Ainda que tenham ficado bem contentes, ó caldeus, saqueadores do meu povo, e tenham engordado como bezerras pastando em verdes pradarias, e relinchando como cavalos vigorosos e fartos, 12mesmo assim a vossa mãe morrerá de vergonha, porque se tornarão na última das nações, num deserto, numa terra seca e abandonada. 13Por causa da cólera do Senhor, a Babilónia tornar-se-á num descampado estéril e todos os que por ali passarem ficarão atónitos e até se hão de rir das pragas que lhe sobrevieram.

14Sim, preparem-se para combater a Babilónia, ó nações suas vizinhas! Que os atiradores façam pontaria sobre ela, porque pecou contra o Senhor! 15Vejam! Ela já se rendeu! As suas muralhas cederam e estão a cair. O Senhor está-se a vingar. Façam-lhe como ela fez aos outros! 16Que os fazendeiros se vão todos embora! Que fujam rapidamente para os seus locais de origem, antes que o inimigo os apanhe!

17Os israelitas foram como cordeiros perseguidos por leões. Primeiro, foi o rei da Assíria a comê-los; depois foi Nabucodonozor, o rei da Babilónia, que se lançou sobre os seus ossos.”

18Por isso, o Senhor dos exércitos, o Deus de Israel, diz assim: “Agora chegou a altura de castigar o rei da Babilónia e a sua terra, da mesma forma que puni o rei da Assíria. 19E trarei Israel de novo para a sua terra natal, para se fartar com a abundância do Carmelo e de Basã, e para ser feliz, uma vez mais, nas colinas de Efraim e Gileade. 20Naqueles dias, diz o Senhor, não se encontrará pecado nem em Israel nem em Judá, porque perdoarei tudo ao restante povo que eu proteger.

21Subam, ó meus valentes guerreiros, contra a terra de Merataim e o povo de Pecode! Sim, avancem contra ela, terra de rebeldes, terra que eu hei de julgar! Aniquilem-na tal como vos mandei! 22Que se ouçam os brados de guerra nessa terra, gritos de grande destruição! 23A Babilónia, que foi um poderoso martelo sobre toda a Terra, jaz ela própria esmigalhada e feita em bocadinhos. A Babilónia está arruinada no meio de todas as outras nações. 24Ó Babilónia, armei-te um laço e foste apanhada, visto que lutaste contra o Senhor.”

25O Senhor abriu o seu arsenal e trouxe para fora as munições, para fazer explodir a sua ira sobre os inimigos. O terror que se há de abater sobre a Babilónia é obra de Deus, o Senhor dos exércitos. 26Sim, venham contra ela de terras distantes! Abram os seus celeiros e derrubem as suas muralhas e os seus edifícios, fazendo deles montões de ruínas, numa destruição absoluta! Que nada seja poupado! 27Nem sequer o gado! Matem tudo o que vive! Veio realmente o tempo em que a Babilónia terá de ser devastada. 28Mas o meu povo escapará; correrá para o seu próprio país, para contar como o Senhor, seu Deus, desencadeou a sua cólera sobre aqueles que antes tinham destruído o seu templo.

29“Convoquem todos os atiradores para que venham à Babilónia. Cerquem a cidade para que ninguém fuja. Façam com ela como ela fez com os outros, pois desafiou arrogantemente o Senhor, o Santo de Israel. 30Os seus jovens cairão no meio das ruas e morrerão; todos os seus guerreiros serão mortos, diz o Senhor. 31Compreendam, ó povo altivo, que estou contra vocês e que agora chegou a vossa vez de prestar contas. 32Terra orgulhosa, tropeçarás e cairás, sem que ninguém se incomode a procurar levantar-te. Deus, o Senhor dos exércitos, ele mesmo acenderá o lume de enormes incêndios nas cidades do reino da Babilónia, os quais chegarão a queimar tudo o que há em volta.”

33Diz o Senhor dos exércitos: “O povo de Israel e Judá foi injuriado. Os seus captores retiveram-nos; não os deixaram ir. 34Mas o seu Redentor é forte. O seu nome é Senhor dos exércitos. Intervirá a favor deles e tomará as medidas necessárias para que sejam soltos e possam ir viver de novo para o sossego do seu país.Quanto ao povo da Babilónia não haverá descanso para ele!

35A espada da destruição ferirá os caldeus, diz o Senhor; ferirá o povo da Babilónia, tanto os seus nobres como os sábios. 36Todos os sábios conselheiros se tornarão como loucos! Os valentes militares serão acometidos de pânico! 37A guerra devorará os cavalos e os carros de combate; os seus aliados de outras terras tornar-se-ão tão fracos como mulheres; os seus tesouros serão pilhados. 38Até as fontes de águas secarão. Tudo isso porquê? Porque toda a terra está cheia de imagens de ídolos e o povo está como que apaixonado por eles.

39Por isso, esta grande cidade da Babilónia há de ser habitada somente por corujas do deserto e por chacais; será o abrigo de todos os animais selvagens do deserto. Nunca mais tornará a ser habitada por seres humanos; ficará assim desolada para sempre. 40A Babilónia será destruída tal como foi Sodoma e Gomorra e as localidades vizinhas. Ninguém mais ali viveu, a partir de então, tal como nunca ninguém mais viverá na Babilónia. Assim diz o Senhor.

41Vejam-no aproximar-se! Esse grande exército que vem do norte! Vêm nele integrados muitos reis que Deus mandou vir de muitas terras. 42Estão armados e preparados para a matança; são cruéis e não se deve esperar deles uma centelha sequer de misericórdia; os seus gritos guerreiros rugem como o barulho das vagas rebentando contra a costa. Ó Babilónia, eles cavalgam contra ti, prestes a travar batalha!

43Quando o rei da Babilónia recebeu esta notícia, deixou cair os braços, desfalecido; a angústia apoderou-se dele como de uma mulher em trabalho de parto.

44Enviarei contra eles um invasor que os assolará repentinamente, como um leão que surge dos matagais do Jordão e que salta repentinamente sobre os cordeiros a pastar. Porei os seus defensores a fugir dali e nomearei outros, da minha escolha, do meu agrado. Porque quem é semelhante a mim? Qual é o governante que se poderia opor aos meus mandamentos? Quem ousaria pedir-me contas?”

45Deem atenção aos planos do Senhor contra a Babilónia, a terra dos caldeus, pois até as criancinhas serão arrastadas e levadas como escravos. 46Oh! Terror! Terror! Toda a Terra tremerá aquando da queda da Babilónia e o seu grito de desespero ouvir-se-á em todo o mundo.