Yeremia 49 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 49:1-39

Ujumbe Kuhusu Amoni

149:1 Amo 1:13; Mwa 19:38; 1Sam 11:1-11; 2Sam 10:1-9; Law 18:21; Mwa 30:11Kuhusu Waamoni:

Hili ndilo asemalo Bwana:

“Je, Israeli hana wana?

Je, hana warithi?

Kwa nini basi Moleki amechukua milki ya Gadi?

Kwa nini watu wake wanaishi katika miji yake?

249:2 Yer 4:19; Kum 3:11; Isa 1:2; Eze 25:2-11; Kum 13:16; Yer 30:16; Eze 21:28-32Lakini siku zinakuja,”

asema Bwana,

“nitakapopiga kelele ya vita

dhidi ya Raba mji wa Waamoni;

utakuwa kilima cha magofu,

navyo vijiji vinavyouzunguka

vitateketezwa kwa moto.

Kisha Israeli atawafukuza

wale waliomfukuza,”

asema Bwana.

349:3 Mwa 12:8; Yos 8:28; 13:26; Mwa 37:34“Lia kwa huzuni, ee Heshboni, kwa kuwa Ai umeangamizwa!

Pigeni kelele, enyi wakazi wa Raba!

Vaeni nguo za gunia na kuomboleza,

kimbieni hapa na pale ndani ya kuta,

kwa kuwa Moleki atakwenda uhamishoni,

yeye pamoja na makuhani na maafisa wake.

449:4 Yer 21:13; 9:23; 1Tim 6:17; Yer 3:6Kwa nini unajivunia mabonde yako,

kujivunia mabonde yako yaliyozaa sana?

Ee binti usiye mwaminifu, unayeutumainia utajiri wako na kusema,

‘Ni nani atakayenishambulia?’

549:5 Yer 44:14Nitaleta hofu kuu juu yako

kutoka kwa wale wote wanaokuzunguka,”

asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote.

“Kila mmoja wenu ataondolewa,

wala hakuna hata mmoja atakayekusanya wakimbizi.

649:6 Yer 12:14-17; 48:47“Lakini hatimaye,

nitarudisha mateka wa Waamoni,”

asema Bwana.

Ujumbe Kuhusu Edomu

749:7 Ay 5:12-14; Za 83:6; Eze 25:12; Mwa 36:11-15, 34; 25:30Kuhusu Edomu:

Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote:

“Je, hakuna tena hekima katika Temani?

Je, shauri limewapotea wenye busara?

Je, hekima yao imechakaa?

849:8 Mwa 10:7; Yer 25:23; Isa 2:19; Amu 6:2; Mwa 25:3Geuka na ukimbie, jifiche katika mapango marefu kabisa,

wewe uishiye Dedani,

kwa kuwa nitaleta maafa juu ya Esau

wakati nitakapomwadhibu.

9Je, kama wachuma zabibu wangekuja kwako,

wasingebakiza zabibu chache?

Kama wezi wangekujia usiku,

je, si wangeiba tu kiasi ambacho wangehitaji?

1049:10 Eze 35:4; Isa 17:14; Mao 1:18; Mwa 3:8; Isa 34:10-12; Yer 11:23Lakini nitamvua Esau nguo abaki uchi,

nitayafunua maficho yake,

ili asiweze kujificha.

Watoto wake, jamaa na majirani wataangamia,

naye hatakuwepo tena.

1149:11 Hos 14:3; Mit 23:10-11; Kum 10:18; Yak 1:27Waache yatima wako; nitayalinda maisha yao.

Wajane wako pia

wanaweza kunitumaini mimi.”

1249:12 Isa 51:23; Mt 20:22; Mit 11:31; Yer 25:28-29; 25:15Hili ndilo asemalo Bwana: “Kama wale wasiostahili kukinywea kikombe ni lazima wakinywe, kwa nini wewe usiadhibiwe? Hutakwepa kuadhibiwa, ni lazima ukinywe. 1349:13 Mwa 22:16; 36:33; Isa 34:6; Yer 42:18; Eze 35:9; Yer 42:18Ninaapa kwa nafsi yangu,” asema Bwana, “kwamba Bosra utakuwa magofu na kitu cha kutisha, cha aibu na cha kulaania; miji yake yote itakuwa magofu milele.”

14Nimesikia ujumbe kutoka kwa Bwana:

Mjumbe alitumwa kwa mataifa kusema,

“Jikusanyeni ili kuushambulia!

Inukeni kwa ajili ya vita!”

15“Sasa nitakufanya uwe mdogo miongoni mwa mataifa,

aliyedharauliwa miongoni mwa watu.

1649:16 Ay 39:27-28; Amo 9:2; Eze 35:13; Oba 1:12Vitisho vyako na kiburi cha moyo wako

vimekudanganya,

wewe unayeishi katika majabali ya miamba,

wewe unayedumu katika miinuko ya kilima.

Ujapojenga kiota chako juu sana kama cha tai,

nitakushusha chini kutoka huko,”

asema Bwana.

1749:17 Kum 29:22; Yer 50:13; Eze 35:7“Edomu atakuwa kitu cha kuogofya;

wote wapitao karibu

watashangaa na kuzomea

kwa sababu ya majeraha yake yote.

1849:18 Mwa 19:24; Kum 29:23; Amo 4:11; Isa 34:10; Yer 23:14Kama vile Sodoma na Gomora zilivyoangamizwa,

pamoja na miji iliyokuwa jirani nayo,”

asema Bwana,

“vivyo hivyo hakuna mtu yeyote atakayeishi humo.

Naam, hakuna mtu yeyote atakayekaa humo.

1949:19 Yer 12:5; Ay 9:19; Yer 50:44; Za 89:6-8; 1Sam 17:34; Kut 8:10; 2Nya 20:6“Kama simba anayepanda kutoka vichaka vya Yordani

kuja kwenye nchi ya malisho mengi,

ndivyo nitamfukuza Edomu kutoka nchi yake ghafula.

Ni nani aliye mteule nitakayemweka kwa ajili ya jambo hili?

Ni nani aliye kama mimi,

na ni nani awezaye kunipinga?

Tena ni mchungaji yupi awezaye

kusimama kinyume nami?”

2049:20 Isa 14:27; Yer 50:45; Mao 1:10; Mal 1:3-4; Isa 34:5; Mwa 36:11Kwa hiyo, sikia kile Bwana alichokipanga dhidi ya Edomu,

kile alichokusudia dhidi ya wale waishio Temani:

Aliye mchanga katika kundi ataburutwa mbali;

yeye ataharibu kabisa malisho yao kwa sababu yao.

2149:21 Za 114:7; Eze 31:16; Yer 51:29; Eze 26:18; Yer 50:46; Eze 26:15; 27:28Kwa sauti ya anguko lao, dunia itatetemeka.

Kilio chao kitasikika hadi Bahari ya Shamu.49:21 Kwa Kiebrania ni Bahari ya Mafunjo.

2249:22 Kum 28:49; Hab 1:8; Isa 13:8; Yer 48:40-41; 4:13; Hos 8:1; Nah 3:13; Mwa 36:33Tazama! Tai atapaa juu angani na kuruka chini kwa ghafula,

akitandaza mabawa yake juu ya Bosra.

Katika siku hiyo, mioyo ya mashujaa wa Edomu

itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wa kuzaa.

Ujumbe Kuhusu Dameski

2349:23 2Fal 14:28; Mdo 9:2; 1Fal 8:65; Eze 47:16; 2Fal 18:34; Mwa 49:4; Isa 57:20Kuhusu Dameski:

“Hamathi na Arpadi imetahayarika,

kwa kuwa wamesikia habari mbaya.

Wamevunjika moyo na wametaabika

kama bahari iliyochafuka.

2449:24 Yer 13:21Dameski amedhoofika,

amegeuka na kukimbia,

hofu ya ghafula imemkamata sana;

amepatwa na uchungu na maumivu,

maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.

25Kwa nini mji ambao unajulikana haujaachwa,

mji ambao ninaupenda?

2649:26 Isa 17:12-14; Yer 50:30; Isa 9:17; 13:18Hakika, vijana wake wanaume wataanguka barabarani;

askari wake wote watanyamazishwa siku hiyo,”

asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.

2749:27 Eze 39:6; Amo 1:4; 1Fal 15:18; Yer 21:14; 43:12; Eze 39:6; Mwa 14:15“Nitatia moto kuta za Dameski;

utaangamiza ngome za Ben-Hadadi.”

Ujumbe Kuhusu Kedari Na Hazori

2849:28 Mwa 25:13; Amu 6:3; Isa 21:13; Yer 10:22; Yos 11:1Kuhusu Kedari na falme za Hazori, ambazo Nebukadneza mfalme wa Babeli alizishambulia:

Hili ndilo asemalo Bwana:

“Inuka, ushambulie Kedari

na kuwaangamiza watu wa mashariki.

2949:29 Yer 6:25; 46:5; Za 120:5Hema zao na makundi yao ya kondoo yatachukuliwa;

vibanda vyao vitatwaliwa

pamoja na mali zao zote na ngamia zao.

Watu watawapigia kelele,

‘Hofu kuu iko kila upande!’

3049:30 Amu 6:2; Yos 11:1; Yer 10:22“Kimbieni haraka!

Kaeni kwenye mapango marefu sana, ninyi mkaao Hazori,”

asema Bwana.

“Nebukadneza, mfalme wa Babeli amepanga shauri baya dhidi yenu;

amebuni hila dhidi yenu.

3149:31 Eze 38:11; Hes 23:9; Mik 7:14“Inuka na ulishambulie taifa lililo starehe,

linaloishi kwa kujiamini,”

asema Bwana,

“taifa lisilo na malango wala makomeo;

watu wake huishi peke yao.

3249:32 Yer 9:26; 25:22; Amu 6:5; Yer 13:24Ngamia wao watakuwa nyara,

nayo makundi yao makubwa ya ngʼombe yatatekwa.

Wale walio maeneo ya mbali

nitawatawanya pande zote,

nami nitaleta maafa juu yao

kutoka kila upande,”

asema Bwana.

3349:33 Yer 10:22; 48:9; Isa 13:22; Hos 11:1“Hazori itakuwa makao ya mbweha,

mahali pa ukiwa milele.

Hakuna yeyote atakayeishi humo;

hakuna mtu atakayekaa ndani yake.”

Ujumbe Kuhusu Elamu

3449:34 Mwa 10:22; 2Fal 24:18Hili ndilo neno la Bwana lililomjia nabii Yeremia kuhusu Elamu, mapema katika utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda:

3549:35 Za 37:15; Ezr 4:9; Dan 8:2; Isa 22:6Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo:

“Tazama, nitavunja upinde wa Elamu,

ulio tegemeo la nguvu zao.

3649:36 Dan 11:4Nitaleta pepo nne dhidi ya Elamu

toka pande nne za mbingu,

nitawatawanya katika hizo pande nne,

wala hapatakuwa na taifa

ambalo watu wa Elamu waliofukuzwa

hawatakwenda.

3749:37 Yer 44:2; 30:24; 9:16; Eze 32:24Nitamfadhaisha Elamu mbele ya adui zao,

mbele yao wale wanaotafuta uhai wao;

nitaleta maafa juu yao,

naam, hasira yangu kali,”

asema Bwana.

“Nitawafuatia kwa upanga

mpaka nitakapowamaliza.

38Nitaweka kiti changu cha enzi huko Elamu

na kumwangamiza mfalme wake na maafisa wake,”

asema Bwana.

3949:39 Yer 48:47“Lakini nitarudisha mateka wa Elamu

katika siku zijazo,”

asema Bwana.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

耶利米书 49:1-39

审判亚扪的预言

1论到亚扪人,耶和华说:

“难道以色列没有子孙,

没有继承人吗?

为什么祭拜米勒公的人占据了迦得,住在城邑中?”

2耶和华说:

“看啊,时候将到,

我要使亚扪人的拉巴城外响起战争的呐喊。

拉巴必沦为废墟,

它周围的乡村都要被焚烧,

以色列人必收复失地。

这是耶和华说的。

3希实本啊,哀哭吧!

因为城毁灭了。

拉巴的居民啊,痛哭吧!

披上麻衣悲伤地在城墙内跑来跑去吧!

因为米勒公及其祭司和官长都要被掳走。

4背叛的人民啊,

你们为肥沃的山谷而感到自豪吗?

你们依仗财富以为无人敢来侵犯。”

5上帝——万军之耶和华说:

“看啊,我要使你们四面受敌,

惊恐万状,四散奔逃,

溃不成军。

6然而,日后我要使被掳的亚扪人重建家园。

这是耶和华说的。”

审判以东的预言

7论到以东,万军之耶和华说:

提幔再没有智者了吗?

谋士已无计可施了吗?

他们都失去智慧了吗?

8底但的居民啊,

你们要转身逃命,

藏在深洞里,

因为我必降灾祸惩罚以东

9人们来以东摘葡萄,不会摘尽;

盗贼夜间来偷东西,不会偷光。

10但我要夺走以东人所有的一切,

我要使他们无处藏身。

他们及其孩子、弟兄和邻居必一同灭亡。

11撇下你们的孤儿吧!

我必使他们存活;

你们的寡妇也可以倚靠我。”

12耶和华说:“看啊,那些本不该喝这杯愤怒的人尚且要喝,更何况你们呢?你们必难逃惩罚,你们一定要喝这杯愤怒。 13因为我已凭自己起誓,波斯拉必沦为废墟,令人惊惧,被人嘲笑和咒诅。它周围的村镇要永远荒凉。这是耶和华说的。”

14我从耶和华那里听到消息,

有位使者被派去联合列国来攻打以东

15耶和华说:

以东啊,我要使你在列国中成为被藐视的弱国。

16你这栖身在石缝间、盘踞在高山上的民族啊,

你令人惊惧、心高气傲,

其实只是自欺。

尽管你像老鹰在高处搭窝,

我也必把你拉下来。

这是耶和华说的。

17以东的下场将很可怕,它的满目疮痍令路人惊惧、嗤笑。 18那里要像所多玛蛾摩拉及其周围的村镇一样被毁灭,荒无人烟。这是耶和华说的。 19看啊,我必在瞬间把以东人赶离家园,如约旦河边丛林中跳出的狮子赶散草场的羊群。我要派我拣选的人统治这地方。谁能与我相比?谁能与我较量?哪位首领能抵挡我?” 20因此,你们要听听耶和华攻击以东的策略,听听祂攻击提幔居民的计划。他们的孩子要被拖走,他们的家园要被毁灭。 21以东倾覆的声音震动大地,哭喊声直传到海。 22看啊,敌人必像展翅飞来的鹰一样攻击波斯拉。到那日,以东的勇士必像临盆的妇女一样胆战心惊。

审判大马士革的预言

23论到大马士革,耶和华说:

哈马亚珥拔惊恐不安,

因为他们听见了坏消息。

他们心惊胆战,像大海一样无法平静。

24大马士革丧失勇气,转身逃命。

她像分娩的妇人一样惊恐不安,

充满痛苦和忧愁。

25我所喜悦的名城为何还没有被撇弃?

26城中的青年将倒毙街头,

那时所有的战士都要灭亡。

这是万军之耶和华说的。

27我要焚烧大马士革的城墙和便·哈达的宫殿。”

审判基达和夏琐的预言

28论到被巴比伦尼布甲尼撒打败的基达夏琐的各城邦,耶和华说:

迦勒底人啊,去攻打基达

消灭那些东方人吧!

29你们要抢走他们的帐篷、

幔子、器皿、羊群和骆驼。

他们必听见呼喊声,

‘真恐怖!四面都是敌人。’

30夏琐的居民啊,快逃命吧!

逃得远远的藏起来,

因为巴比伦尼布甲尼撒已计划攻击你们,

准备消灭你们。

这是耶和华说的。

31迦勒底人啊,

上去攻打那安逸无忧、无门无闩、独居一方的国家吧!

这是耶和华说的。

32他们的骆驼必被掳去,

大群的牲畜必成为战利品。

我要把剃去鬓发的人驱散到四方,

使灾祸从四面八方临到他们。

这是耶和华说的。

33夏琐要永远荒凉,

杳无人迹,

成为豺狼出没的地方。”

审判以拦的预言

34犹大西底迦执政初期,耶和华告诉了耶利米先知有关以拦的事。 35万军之耶和华说:“看啊,我要摧毁以拦的弓箭手——他们的精锐之师。 36我要使敌人从四面八方如风而来,把以拦人驱散到四方,使他们流落到列国。 37我要让仇敌击溃他们,我要发烈怒降祸给他们,用刀剑追杀他们,直到彻底消灭他们。这是耶和华说的。 38我要在以拦设立我的宝座,消灭那里的君王和官长。这是耶和华说的。 39但将来有一天,我要使被掳的以拦人重建家园。这是耶和华说的。”