Yeremia 48 – NEN & TCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 48:1-47

Ujumbe Kuhusu Moabu

148:1 Hes 32:37; Yos 13:19; Mwa 19:37; Kum 23:6Kuhusu Moabu:

Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo:

“Ole wake Nebo, kwa maana utaharibiwa.

Kiriathaimu utaaibishwa na kutekwa;

Misgabu itaaibishwa na kuvunjavunjwa.

248:2 Hes 21:25; Isa 16:14; Yos 23:16Moabu haitasifiwa tena;

huko Heshboni watu watafanya shauri baya la anguko lake:

‘Njooni na tuangamize taifa lile.’

Wewe nawe, ee Madmena, utanyamazishwa;

upanga utakufuatia.

3Sikiliza kilio kutoka Horonaimu,

kilio cha maangamizi makuu na uharibifu.

4Moabu utavunjwa,

wadogo wake watapiga kelele.

548:5 Isa 15:5Wanapanda kwenda njia ya kuelekea Luhithi,

wakilia kwa uchungu wanapotembea,

kwenye njia inayoshuka kwenda Horonaimu,

kilio cha uchungu kwa ajili ya uharibifu kinasikika.

648:6 Yer 17:6; Mwa 19:17Kimbieni! Okoeni maisha yenu,

kuweni kama kichaka jangwani.

748:7 Hes 21:29; Isa 46:1-2; Yer 49:3; 9:23; Za 49:6; Mk 11:28; Amo 2:3Kwa kuwa mmetumainia matendo yenu na mali zenu,

ninyi pia mtachukuliwa mateka,

naye Kemoshi48:7 Kemoshi alikuwa mungu wa Wamoabu. atakwenda uhamishoni,

pamoja na makuhani wake na maafisa wake.

848:8 Kut 12:23; Yer 4:7; Yos 13:9Mharabu atakuja dhidi ya kila mji,

wala hakuna mji utakaookoka.

Bonde litaangamizwa na uwanda utaharibiwa,

kwa sababu Bwana amesema.

948:9 Amu 9:45; Yer 51:29Wekeni chumvi kwa ajili ya Moabu,

kwa kuwa ataangamizwa;

miji yake itakuwa ukiwa,

pasipo kuwa na mtu atakayeishi ndani yake.

1048:10 Yer 47:6; 1Fal 20:42; 1Sam 15:3, 11; 2Fal 13:15-19“Alaaniwe yeye afanyaye kazi ya Bwana kwa hila!

Alaaniwe yeye auzuiaye upanga wake usimwage damu!

1148:11 Zek 1:15; Sef 1:12“Moabu amestarehe tangu ujana wake,

kama divai iliyoachwa kwenye machujo yake,

haikumiminwa kutoka chombo kimoja hadi kingine,

hajaenda uhamishoni.

Kwa hiyo ana ladha ile ile kama aliyokuwa nayo,

nayo harufu yake haijabadilika.

12Lakini siku zinakuja,”

asema Bwana,

“nitakapotuma watu wamiminao kutoka kwenye magudulia,

nao watamimina;

wataacha magudulia yake yakiwa matupu

na kuvunja mitungi yake.

1348:13 Hos 10:6; Amu 11:24; Yos 7:2Kisha Moabu atamwonea aibu mungu wao Kemoshi,

kama vile nyumba ya Israeli walivyoona aibu

walipotegemea mungu wa Betheli.48:13 Betheli ina maana ya Nyumba ya Mungu; lakini pia ni mahali ambapo Mfalme Yeroboamu alisimamisha moja ya sanamu za ndama ili kuabudiwa; nyingine aliiweka huko Dani (1Fal 12:29-33).

1448:14 Mhu 9:11; Za 33:16“Mwawezaje kusema, ‘Sisi ni mashujaa,

watu jasiri katika vita’?

1548:15 Yer 50:27; 51:40, 57; 46:18; Isa 9:17Moabu ataangamizwa na miji yake itavamiwa,

vijana wake waume walio bora sana watachinjwa,”

asema Mfalme, ambaye jina lake

ni Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote.

16“Kuanguka kwa Moabu kumekaribia,

janga kubwa litamjia kwa haraka.

1748:17 Za 110:2; 2Fal 3:4-5Ombolezeni kwa ajili yake, ninyi nyote mnaomzunguka,

ninyi nyote mnaojua sifa zake,

semeni, ‘Tazama jinsi ilivyovunjika fimbo ya kifalme yenye nguvu,

tazama jinsi ilivyovunjika fimbo iliyotukuka!’

1848:18 Isa 47:1; Hes 21:30; Yos 13:9“Shuka kutoka fahari yako

na uketi katika ardhi iliyokauka,

enyi wenyeji wa Binti wa Diboni,

kwa maana yeye aangamizaye Moabu atakuja dhidi yako,

na kuangamiza miji yako iliyozungushiwa maboma.

1948:19 Hes 32:34; Kum 2:36Simama kando ya barabara na utazame,

wewe unayeishi Aroeri.

Muulize mwanaume anayekimbia

na mwanamke anayetoroka,

waulize, ‘Kumetokea nini?’

2048:20 Isa 16:7; Hes 21:13Moabu amefedheheshwa, kwa kuwa amevunjavunjwa.

Lieni kwa huzuni na kupiga kelele!

Tangazeni kando ya Arnoni

kwamba Moabu ameangamizwa.

2148:21 Hes 21:23; Isa 15:4; Yos 13:18; 15:51; 13:9, 21Hukumu imefika kwenye uwanda wa juu:

katika Holoni, Yahasa na Mefaathi,

2248:22 Hes 21:30; Yos 13:9, 17; Hes 32:38katika Diboni, Nebo

na Beth-Diblathaimu,

2348:23 Hes 32:38; Yos 13:17-19katika Kiriathaimu, Beth-Gamuli

na Beth-Meoni,

2448:24 Amo 2:2; Yer 49:13; Isa 15:1katika Keriothi na Bosra;

kwa miji yote ya Moabu,

iliyoko mbali na karibu.

2548:25 Za 75:10; Eze 30:21; Za 37:17Pembe48:25 Pembe hapa ni ishara ya nguvu. ya Moabu imekatwa,

mkono wake umevunjwa,”

asema Bwana.

2648:26 Yer 25:16, 27; 51:39; Isa 28:8; 1Sam 17:26“Mlevye,

kwa kuwa amemdharau Bwana.

Moabu na agaegae katika matapishi yake,

yeye na awe kitu cha dhihaka.

2748:27 Mit 24:17; Yer 2:26; Ay 16:4; Za 44:14; Mik 7:8-10; Kum 7:8-10; Sef 2:8Je, Israeli hakuwa kitu chako cha kudhihakiwa?

Je, alikamatwa miongoni mwa wezi,

kiasi cha kutikisa kichwa chako kwa dharau

kila mara unapozungumza juu yake?

2848:28 Za 55:6-7; Wim 1:15; Amu 6:2; Wim 2:14; Mwa 8; 8Ondokeni kwenye miji yenu, mkaishi katikati ya miamba,

enyi mnaoishi Moabu.

Kuweni kama huwa ambaye hutengeneza kiota chake

kwenye mdomo wa pango.

2948:29 Law 26:19; Isa 16:6; Ay 40:12; Mit 10:5; 16:18“Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu:

kutakabari kwake kwa kiburi na majivuno,

kiburi chake na ufidhuli wake,

na kujivuna kwa moyo wake.

30Ninaujua ujeuri wake, lakini ni bure,”

asema Bwana,

“nako kujisifu kwake hakumsaidii chochote.

3148:31 Isa 15:5-6; 2Fal 3:25Kwa hiyo namlilia Moabu,

kwa ajili ya Moabu yote ninalia,

ninaomboleza kwa ajili

ya watu wa Kir-Haresethi.

3248:32 Hes 32:3; 21:13; Isa 16:8-9; Yos 13:25Ninalia machozi kwa ajili yenu, kama Yazeri aliavyo,

enyi mizabibu ya Sibma.

Matawi yako yameenea hadi baharini;

yamefika hadi bahari ya Yazeri.

Mharabu ameyaangukia matunda yako yaliyoiva

na mizabibu yako iliyoiva.

3348:33 Isa 16:10; 24:7; Amo 5:17; Yoe 1:12Shangwe na furaha vimetoweka

kutoka bustani na mashamba ya Moabu.

Nimekomesha kutiririka kwa divai kutoka mashinikizo;

hakuna hata mmoja ayakanyagaye kwa kelele za shangwe.

Ingawa kuna kelele,

sio kelele za shangwe.

3448:34 Isa 15:4-6; Hes 32:3; 21:23; Mwa 13:10; Yos 13:26; Hes 21:25“Sauti ya kilio chao inapanda

kutoka Heshboni hadi Eleale na Yahazi,

kutoka Soari hadi Horonaimu na Eglath-Shelishiya,

kwa kuwa hata maji ya Nimrimu yamekauka.

3548:35 Isa 15:2; 16:12; Yer 11:13Nitakomesha wale wote katika Moabu

watoao sadaka mahali pa juu,

na kufukiza uvumba kwa miungu yao,”

asema Bwana.

3648:36 Isa 16:11; 15:7; Mit 11:4; 2Fal 3:25“Kwa hiyo moyo wangu unaomboleza kwa ajili ya Moabu kama filimbi;

unaomboleza kama filimbi kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi.

Utajiri waliojipatia umetoweka.

3748:37 Isa 15:2; Eze 29:18; Isa 3:24; Amo 8:10; Eze 27:31; 2Sam 10:4Kila kichwa kimenyolewa

na kila mwenye ndevu zimekatwa;

kila mkono umekatwa

na kila kiuno kimefunikwa kwa nguo ya gunia.

3848:38 Yer 22:28; Isa 15:3Juu ya mapaa yote katika Moabu

na katika viwanja

hakuna kitu chochote isipokuwa maombolezo,

kwa kuwa nimemvunja Moabu

kama gudulia ambalo hakuna mtu yeyote anayelitaka,”

asema Bwana.

39“Tazama jinsi alivyovunjikavunjika!

Jinsi wanavyolia kwa huzuni!

Tazama jinsi Moabu anavyogeuka kwa aibu!

Moabu amekuwa kitu cha kudhihakiwa,

kitu cha kutisha kwa wale wote

wanaomzunguka.”

4048:40 Kum 28:29; Hab 1:8; Isa 8:8; Yer 49:22Hili ndilo asemalo Bwana:

“Tazama! Tai anashuka chini,

akitanda mabawa yake juu ya Moabu.

4148:41 Isa 21:3; Mik 4:9; Amo 2:16; Isa 15:1Miji itatekwa na ngome zake

zitatwaliwa.

Katika siku hiyo, mioyo ya mashujaa wa Moabu

itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wa kuzaa.

4248:42 Za 83:4; Isa 16:14; Mit 16:18Moabu ataangamizwa kama taifa

kwa sababu amemdharau Bwana.

4348:43 Isa 24:17, 18; Yer 49:5Hofu kuu, shimo na mtego vinawangojea,

enyi watu wa Moabu,”

asema Bwana.

4448:44 1Fal 19:17; Ay 20:24; Yer 11:23; 23:12; Isa 24:18“Yeyote atakayeikimbia hiyo hofu kuu

ataanguka ndani ya shimo,

yeyote atakayepanda kutoka shimoni,

atanaswa katika mtego,

kwa sababu nitaletea Moabu

mwaka wa adhabu yake,”

asema Bwana.

4548:45 Hes 21:21, 26-28; Yos 12:2; Hes 24:17“Katika kivuli cha Heshboni,

wakimbizi wamesimama pasipo msaada,

kwa kuwa moto umezimika huko Heshboni,

mwali wa moto kutoka katikati ya Sihoni;

unaunguza vipaji vya nyuso za Moabu,

mafuvu yao wenye kujivuna kwa kelele.

4648:46 Hes 21:29; Amu 11:24Ole wako, ee Moabu!

Watu wa Kemoshi wameangamizwa;

wana wako wamepelekwa uhamishoni

na binti zako wamechukuliwa mateka.

4748:47 Za 14:7; Dan 11:41; Yer 49:6; Isa 11:1; Yer 12:15; Eze 16:53“Lakini nitarudisha mateka wa Moabu,

katika siku zijazo,”

asema Bwana.

Huu ndio mwisho wa hukumu juu ya Moabu.

Tagalog Contemporary Bible

Jeremias 48:1-47

Ang Mensahe tungkol sa Moab

1Ito ang sinabi ng Panginoong Makapangyarihan, ang Dios ng Israel, tungkol sa Moab:

“Nakakaawa ang Nebo dahil wawasakin ito. Mapapahiya at bibihagin ang Kiriataim at matitibag ang mga muog nito. 2Hindi na papupurihan ang Moab; ang mga kaaway sa Heshbon ay nagbabalak na wasakin ang Moab. At ikaw naman Madmen ay sasalakayin ng mga kaaway at magiging mapanglaw. 3Pakinggan nʼyo ang sigawan sa Horonaim, dahil sa matinding digmaan at kapahamakan. 4Mawawasak ang Moab at mag-iiyakan ang mga bata. 5Ang mga mamamayan ng Moab ay mag-iiyakan nang malakas habang paakyat sila sa Luhit at pababa sa Honoraim. Mag-iiyakan sila dahil sa kapahamakan.

6“Iligtas ninyo ang inyong sarili! Tumakas kayo papuntang ilang. 7Mga taga-Moab, nagtitiwala kayo sa kakayahan at kayamanan ninyo kaya bibihagin kayo pati ang dios-diosan ninyong si Kemosh at ang mga pari at mga pinuno nito.

8“Darating ang manlilipol sa bawat bayan at walang bayan na makakaligtas. Mawawasak ang mga bayan sa lambak at talampas. Mangyayari ito dahil sinabi mismo ng Panginoon. 9May pakpak sana ang Moab para makalipad siya papalayo,48:9 May pakpak … papalayo: o, Lagyan ng asin ang Moab para wala nang tumubong halaman dito. dahil wala nang kabuluhan ang mga bayan nito at wala nang maninirahan dito. 10Sumpain ang taong pabaya sa paggawa ng gawain ng Panginoon laban sa Moab. Sumpain ang taong hindi papatay sa mga taga-Moab. 11Tahimik ang pamumuhay ng Moab mula pa noon. Hindi pa ito nakaranas ng pagkabihag. Parang alak ito na hindi nagagalaw o naisasalin man sa isang sisidlan. Kaya ang lasa at amoy nitoʼy hindi nagbabago.

12“Pero darating ang araw na isusugo ko ang mga kaaway para ibuhos ang Moab mula sa kanyang lalagyan at pagkatapos ay babasagin ang lalagyan nito. 13At ikakahiya ng mga taga-Moab ang dios-diosan nilang si Kemosh, gaya ng nangyari sa Betel nang ikahiya ng mga Israelita ang dios-diosan nila. 14Ipinagmamalaki ng mga taga-Moab na matatapang ang sundalo nila sa pakikipaglaban. 15Pero mawawasak ang Moab at ang mga bayan nito. Papatayin ang kanilang matatapang na kabataan. Ako, ang Panginoon na Haring Makapangyarihan, ang nagsasabi nito.

16“Malapit na ang kapahamakan ng Moab. 17Umiyak kayo, kayong lahat na kakampi ng Moab!48:17 kakampi ng Moab: o, nakatira sa paligid ng Moab. Sabihin nʼyo, ‘Wala na ang Moab! Nabali na ang tungkod niya, ang tungkod na sagisag ng kapangyarihan at katanyagan niya.’

18“Kayong mga taga-Dibon, magpakumbaba kayo at maupo sa lupa dahil ang nagwasak sa Moab ay sasalakay din sa inyo at gigibain ang mga lungsod nʼyo na napapalibutan ng mga pader. 19Kayong mga nasa Aroer, tumayo kayo sa tabi ng daan at magbantay. Magtanong kayo sa mga nakatakas kung ano ang nangyari. 20Sasagot sila, ‘Nawasak at napahiya ang Moab. Humiyaw kayo at umiyak. Isigaw nʼyo sa Arnon na nawasak ang Moab.’

21“Parurusahan din ang mga bayan sa talampas: ang Holon, Jaza, Mefaat, 22Dibon, Nebo, Bet Diblataim, 23Kiriataim, Bet Gamul, Bet Meon, 24Keriot at Bozra. Darating na ang parusa sa lahat ng bayan ng Moab, sa malayo at malapit. 25Wala nang kapangyarihan ang Moab at mahina na ito ngayon. Ako, ang Panginoon, ang nagsasabi nito.

26“Lasingin nʼyo ang Moab dahil naghimagsik siya sa akin. Gugulong siya sa sariling suka at magiging katawa-tawa. 27Kayong mga taga-Moab, hindi baʼt kinutya ninyo ang Israel? Bakit, nahuli ba siyang nagnakaw? Bakit iiling-iling pa kayo sa pagkutya nʼyo sa kanya? 28Umalis na kayo sa bayan nʼyo at tumira sa mababatong lugar, na parang mga kalapating nagpupugad sa mga bitak ng matatarik at mababatong lugar. 29Napakayabang ninyo. Narinig ko kung gaano kayo kayabang at kapalalo. 30Ako, ang Panginoon, nalalaman ko kung gaano kayo kayabang, pero iyan ay walang kabuluhan. 31Kaya iiyak ako para sa mga taga-Moab at mga taga-Kir Hareset.48:31 Kir Hareset: o, Kir Heres. 32Iiyak din ako para sa mga taga-Sibna ng higit kaysa sa pag-iyak ko sa mga taga-Jazer. Sibma, para kang halamang ubas na ang mga sanga ay umabot sa kabila ng Dagat na Patay hanggang sa Jazer. Pero ngayon, inubos ng mga maninira ang bunga mo. 33Wala nang maririnig na kasayahan at katuwaan sa mga bukid at mga ubasan sa lupain ng Moab. Hindi na umaagos ang katas ng ubas sa mga pisaan. Wala ng mga pumipisa ng ubas na sumisigaw sa tuwa. May mga sumisigaw nga, pero hindi na sigaw ng tuwa. 34Ang iyakan ng mga taga-Heshbon ay naririnig hanggang sa Eleale at Jahaz. Ang iyakan ng mga taga-Zoar ay naririnig hanggang sa Horonaim at sa Eglat Shelishiya. Sapagkat kahit ang batis ng Nimrim ay tuyo na. 35Patitigilin ko sa Moab ang mga naghahandog sa mga sambahan sa matataas na lugar48:35 sambahan sa matataas na lugar: Tingnan sa Talaan ng mga Salita sa likod. at nagsusunog ng insenso sa mga dios-diosan nila. Ako, ang Panginoon, ang nagsasabi nito.

36“Kaya umiiyak ang aking puso para sa Moab at sa mga taga-Kir Hareset, gaya ng malungkot na tugtog ng plauta sa patay. Wala na ang mga kayamanang nakamit nila. 37Ang bawat isaʼy nagpahayag ng kalungkutan nila sa pamamagitan ng pagpapakalbo, pag-aahit, pagsugat sa mga kamay nila at pagsusuot ng damit na pangluksa. 38Nag-iiyakan ang mga tao sa mga bahay nila at sa mga plasa, dahil winasak ko ang Moab na parang banga na binasag at wala nang pumapansin. 39Gayon na lamang ang pagkawasak ng Moab! Pakinggan nʼyo ang iyakan ng mga mamamayan. Nakakahiya ang Moab. Kinukutya at kinamumuhian ito ng mga bansa sa palibot nito.”

40Sinabi pa ng Panginoon, “Tingnan nʼyo! Ang kaaway ng Moab ay parang agila na lumilipad para dagitin ito. 41Sasakupin ang mga lungsod48:41 mga lungsod: o, Keriot. at ang mga kampo ng Moab. Sa mga araw na iyon, matatakot ang mga sundalo ng Moab katulad ng isang babaeng malapit nang manganak. 42Mawawasak ang Moab dahil sa paghihimagsik niya sa Panginoon. 43Ang sasapitin ng mga taga-Moab ay takot, hukay at bitag.

44“Ang sinumang tatakas dahil sa takot ay mahuhulog sa hukay. At ang sinumang makakaligtas sa hukay ay mahuhuli sa bitag, dahil talagang parurusahan ko ang Moab sa takdang panahon. Ako, ang Panginoon, ang nagsasabi nito. 45Ang mga kawawang nakatakas ay nais magtago sa Heshbon. Pero ang Heshbon na pinagharian ni Haring Sihon ay nagliliyab sa apoy at nilamon pati ang mga kabundukan na pinagtataguan ng mga taga-Moab na ang gusto ay digmaan. 46Hala! Tapos na kayo, kayong mga taga-Moab! Kayong mga sumasamba sa dios-diosang si Kemosh ay bibihagin ang inyong mga anak. 47Pero darating ang araw na ibabalik ko ang mabuting kalagayan ng Moab. Ako, ang Panginoon, ang nagsasabi nito.” Ito ang mensahe tungkol sa Moab.