Yeremia 48 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 48:1-47

Ujumbe Kuhusu Moabu

148:1 Hes 32:37; Yos 13:19; Mwa 19:37; Kum 23:6Kuhusu Moabu:

Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo:

“Ole wake Nebo, kwa maana utaharibiwa.

Kiriathaimu utaaibishwa na kutekwa;

Misgabu itaaibishwa na kuvunjavunjwa.

248:2 Hes 21:25; Isa 16:14; Yos 23:16Moabu haitasifiwa tena;

huko Heshboni watu watafanya shauri baya la anguko lake:

‘Njooni na tuangamize taifa lile.’

Wewe nawe, ee Madmena, utanyamazishwa;

upanga utakufuatia.

3Sikiliza kilio kutoka Horonaimu,

kilio cha maangamizi makuu na uharibifu.

4Moabu utavunjwa,

wadogo wake watapiga kelele.

548:5 Isa 15:5Wanapanda kwenda njia ya kuelekea Luhithi,

wakilia kwa uchungu wanapotembea,

kwenye njia inayoshuka kwenda Horonaimu,

kilio cha uchungu kwa ajili ya uharibifu kinasikika.

648:6 Yer 17:6; Mwa 19:17Kimbieni! Okoeni maisha yenu,

kuweni kama kichaka jangwani.

748:7 Hes 21:29; Isa 46:1-2; Yer 49:3; 9:23; Za 49:6; Mk 11:28; Amo 2:3Kwa kuwa mmetumainia matendo yenu na mali zenu,

ninyi pia mtachukuliwa mateka,

naye Kemoshi48:7 Kemoshi alikuwa mungu wa Wamoabu. atakwenda uhamishoni,

pamoja na makuhani wake na maafisa wake.

848:8 Kut 12:23; Yer 4:7; Yos 13:9Mharabu atakuja dhidi ya kila mji,

wala hakuna mji utakaookoka.

Bonde litaangamizwa na uwanda utaharibiwa,

kwa sababu Bwana amesema.

948:9 Amu 9:45; Yer 51:29Wekeni chumvi kwa ajili ya Moabu,

kwa kuwa ataangamizwa;

miji yake itakuwa ukiwa,

pasipo kuwa na mtu atakayeishi ndani yake.

1048:10 Yer 47:6; 1Fal 20:42; 1Sam 15:3, 11; 2Fal 13:15-19“Alaaniwe yeye afanyaye kazi ya Bwana kwa hila!

Alaaniwe yeye auzuiaye upanga wake usimwage damu!

1148:11 Zek 1:15; Sef 1:12“Moabu amestarehe tangu ujana wake,

kama divai iliyoachwa kwenye machujo yake,

haikumiminwa kutoka chombo kimoja hadi kingine,

hajaenda uhamishoni.

Kwa hiyo ana ladha ile ile kama aliyokuwa nayo,

nayo harufu yake haijabadilika.

12Lakini siku zinakuja,”

asema Bwana,

“nitakapotuma watu wamiminao kutoka kwenye magudulia,

nao watamimina;

wataacha magudulia yake yakiwa matupu

na kuvunja mitungi yake.

1348:13 Hos 10:6; Amu 11:24; Yos 7:2Kisha Moabu atamwonea aibu mungu wao Kemoshi,

kama vile nyumba ya Israeli walivyoona aibu

walipotegemea mungu wa Betheli.48:13 Betheli ina maana ya Nyumba ya Mungu; lakini pia ni mahali ambapo Mfalme Yeroboamu alisimamisha moja ya sanamu za ndama ili kuabudiwa; nyingine aliiweka huko Dani (1Fal 12:29-33).

1448:14 Mhu 9:11; Za 33:16“Mwawezaje kusema, ‘Sisi ni mashujaa,

watu jasiri katika vita’?

1548:15 Yer 50:27; 51:40, 57; 46:18; Isa 9:17Moabu ataangamizwa na miji yake itavamiwa,

vijana wake waume walio bora sana watachinjwa,”

asema Mfalme, ambaye jina lake

ni Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote.

16“Kuanguka kwa Moabu kumekaribia,

janga kubwa litamjia kwa haraka.

1748:17 Za 110:2; 2Fal 3:4-5Ombolezeni kwa ajili yake, ninyi nyote mnaomzunguka,

ninyi nyote mnaojua sifa zake,

semeni, ‘Tazama jinsi ilivyovunjika fimbo ya kifalme yenye nguvu,

tazama jinsi ilivyovunjika fimbo iliyotukuka!’

1848:18 Isa 47:1; Hes 21:30; Yos 13:9“Shuka kutoka fahari yako

na uketi katika ardhi iliyokauka,

enyi wenyeji wa Binti wa Diboni,

kwa maana yeye aangamizaye Moabu atakuja dhidi yako,

na kuangamiza miji yako iliyozungushiwa maboma.

1948:19 Hes 32:34; Kum 2:36Simama kando ya barabara na utazame,

wewe unayeishi Aroeri.

Muulize mwanaume anayekimbia

na mwanamke anayetoroka,

waulize, ‘Kumetokea nini?’

2048:20 Isa 16:7; Hes 21:13Moabu amefedheheshwa, kwa kuwa amevunjavunjwa.

Lieni kwa huzuni na kupiga kelele!

Tangazeni kando ya Arnoni

kwamba Moabu ameangamizwa.

2148:21 Hes 21:23; Isa 15:4; Yos 13:18; 15:51; 13:9, 21Hukumu imefika kwenye uwanda wa juu:

katika Holoni, Yahasa na Mefaathi,

2248:22 Hes 21:30; Yos 13:9, 17; Hes 32:38katika Diboni, Nebo

na Beth-Diblathaimu,

2348:23 Hes 32:38; Yos 13:17-19katika Kiriathaimu, Beth-Gamuli

na Beth-Meoni,

2448:24 Amo 2:2; Yer 49:13; Isa 15:1katika Keriothi na Bosra;

kwa miji yote ya Moabu,

iliyoko mbali na karibu.

2548:25 Za 75:10; Eze 30:21; Za 37:17Pembe48:25 Pembe hapa ni ishara ya nguvu. ya Moabu imekatwa,

mkono wake umevunjwa,”

asema Bwana.

2648:26 Yer 25:16, 27; 51:39; Isa 28:8; 1Sam 17:26“Mlevye,

kwa kuwa amemdharau Bwana.

Moabu na agaegae katika matapishi yake,

yeye na awe kitu cha dhihaka.

2748:27 Mit 24:17; Yer 2:26; Ay 16:4; Za 44:14; Mik 7:8-10; Kum 7:8-10; Sef 2:8Je, Israeli hakuwa kitu chako cha kudhihakiwa?

Je, alikamatwa miongoni mwa wezi,

kiasi cha kutikisa kichwa chako kwa dharau

kila mara unapozungumza juu yake?

2848:28 Za 55:6-7; Wim 1:15; Amu 6:2; Wim 2:14; Mwa 8; 8Ondokeni kwenye miji yenu, mkaishi katikati ya miamba,

enyi mnaoishi Moabu.

Kuweni kama huwa ambaye hutengeneza kiota chake

kwenye mdomo wa pango.

2948:29 Law 26:19; Isa 16:6; Ay 40:12; Mit 10:5; 16:18“Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu:

kutakabari kwake kwa kiburi na majivuno,

kiburi chake na ufidhuli wake,

na kujivuna kwa moyo wake.

30Ninaujua ujeuri wake, lakini ni bure,”

asema Bwana,

“nako kujisifu kwake hakumsaidii chochote.

3148:31 Isa 15:5-6; 2Fal 3:25Kwa hiyo namlilia Moabu,

kwa ajili ya Moabu yote ninalia,

ninaomboleza kwa ajili

ya watu wa Kir-Haresethi.

3248:32 Hes 32:3; 21:13; Isa 16:8-9; Yos 13:25Ninalia machozi kwa ajili yenu, kama Yazeri aliavyo,

enyi mizabibu ya Sibma.

Matawi yako yameenea hadi baharini;

yamefika hadi bahari ya Yazeri.

Mharabu ameyaangukia matunda yako yaliyoiva

na mizabibu yako iliyoiva.

3348:33 Isa 16:10; 24:7; Amo 5:17; Yoe 1:12Shangwe na furaha vimetoweka

kutoka bustani na mashamba ya Moabu.

Nimekomesha kutiririka kwa divai kutoka mashinikizo;

hakuna hata mmoja ayakanyagaye kwa kelele za shangwe.

Ingawa kuna kelele,

sio kelele za shangwe.

3448:34 Isa 15:4-6; Hes 32:3; 21:23; Mwa 13:10; Yos 13:26; Hes 21:25“Sauti ya kilio chao inapanda

kutoka Heshboni hadi Eleale na Yahazi,

kutoka Soari hadi Horonaimu na Eglath-Shelishiya,

kwa kuwa hata maji ya Nimrimu yamekauka.

3548:35 Isa 15:2; 16:12; Yer 11:13Nitakomesha wale wote katika Moabu

watoao sadaka mahali pa juu,

na kufukiza uvumba kwa miungu yao,”

asema Bwana.

3648:36 Isa 16:11; 15:7; Mit 11:4; 2Fal 3:25“Kwa hiyo moyo wangu unaomboleza kwa ajili ya Moabu kama filimbi;

unaomboleza kama filimbi kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi.

Utajiri waliojipatia umetoweka.

3748:37 Isa 15:2; Eze 29:18; Isa 3:24; Amo 8:10; Eze 27:31; 2Sam 10:4Kila kichwa kimenyolewa

na kila mwenye ndevu zimekatwa;

kila mkono umekatwa

na kila kiuno kimefunikwa kwa nguo ya gunia.

3848:38 Yer 22:28; Isa 15:3Juu ya mapaa yote katika Moabu

na katika viwanja

hakuna kitu chochote isipokuwa maombolezo,

kwa kuwa nimemvunja Moabu

kama gudulia ambalo hakuna mtu yeyote anayelitaka,”

asema Bwana.

39“Tazama jinsi alivyovunjikavunjika!

Jinsi wanavyolia kwa huzuni!

Tazama jinsi Moabu anavyogeuka kwa aibu!

Moabu amekuwa kitu cha kudhihakiwa,

kitu cha kutisha kwa wale wote

wanaomzunguka.”

4048:40 Kum 28:29; Hab 1:8; Isa 8:8; Yer 49:22Hili ndilo asemalo Bwana:

“Tazama! Tai anashuka chini,

akitanda mabawa yake juu ya Moabu.

4148:41 Isa 21:3; Mik 4:9; Amo 2:16; Isa 15:1Miji itatekwa na ngome zake

zitatwaliwa.

Katika siku hiyo, mioyo ya mashujaa wa Moabu

itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wa kuzaa.

4248:42 Za 83:4; Isa 16:14; Mit 16:18Moabu ataangamizwa kama taifa

kwa sababu amemdharau Bwana.

4348:43 Isa 24:17, 18; Yer 49:5Hofu kuu, shimo na mtego vinawangojea,

enyi watu wa Moabu,”

asema Bwana.

4448:44 1Fal 19:17; Ay 20:24; Yer 11:23; 23:12; Isa 24:18“Yeyote atakayeikimbia hiyo hofu kuu

ataanguka ndani ya shimo,

yeyote atakayepanda kutoka shimoni,

atanaswa katika mtego,

kwa sababu nitaletea Moabu

mwaka wa adhabu yake,”

asema Bwana.

4548:45 Hes 21:21, 26-28; Yos 12:2; Hes 24:17“Katika kivuli cha Heshboni,

wakimbizi wamesimama pasipo msaada,

kwa kuwa moto umezimika huko Heshboni,

mwali wa moto kutoka katikati ya Sihoni;

unaunguza vipaji vya nyuso za Moabu,

mafuvu yao wenye kujivuna kwa kelele.

4648:46 Hes 21:29; Amu 11:24Ole wako, ee Moabu!

Watu wa Kemoshi wameangamizwa;

wana wako wamepelekwa uhamishoni

na binti zako wamechukuliwa mateka.

4748:47 Za 14:7; Dan 11:41; Yer 49:6; Isa 11:1; Yer 12:15; Eze 16:53“Lakini nitarudisha mateka wa Moabu,

katika siku zijazo,”

asema Bwana.

Huu ndio mwisho wa hukumu juu ya Moabu.

King James Version

Jeremiah 48:1-47

1Against Moab thus saith the LORD of hosts, the God of Israel; Woe unto Nebo! for it is spoiled: Kiriathaim is confounded and taken: Misgab is confounded and dismayed.48.1 Misgab: or, the high place 2There shall be no more praise of Moab: in Heshbon they have devised evil against it; come, and let us cut it off from being a nation. Also thou shalt be cut down, O Madmen; the sword shall pursue thee.48.2 be cut…: or, be brought to silence48.2 pursue…: Heb. go after thee 3A voice of crying shall be from Horonaim, spoiling and great destruction. 4Moab is destroyed; her little ones have caused a cry to be heard. 5For in the going up of Luhith continual weeping shall go up; for in the going down of Horonaim the enemies have heard a cry of destruction.48.5 continual…: Heb. weeping with weeping 6Flee, save your lives, and be like the heath in the wilderness.48.6 the heath: or, a naked tree

7¶ For because thou hast trusted in thy works and in thy treasures, thou shalt also be taken: and Chemosh shall go forth into captivity with his priests and his princes together. 8And the spoiler shall come upon every city, and no city shall escape: the valley also shall perish, and the plain shall be destroyed, as the LORD hath spoken. 9Give wings unto Moab, that it may flee and get away: for the cities thereof shall be desolate, without any to dwell therein. 10Cursed be he that doeth the work of the LORD deceitfully, and cursed be he that keepeth back his sword from blood.48.10 deceitfully: or, negligently

11¶ Moab hath been at ease from his youth, and he hath settled on his lees, and hath not been emptied from vessel to vessel, neither hath he gone into captivity: therefore his taste remained in him, and his scent is not changed.48.11 remained: Heb. stood 12Therefore, behold, the days come, saith the LORD, that I will send unto him wanderers, that shall cause him to wander, and shall empty his vessels, and break their bottles. 13And Moab shall be ashamed of Chemosh, as the house of Israel was ashamed of Beth-el their confidence.

14¶ How say ye, We are mighty and strong men for the war? 15Moab is spoiled, and gone up out of her cities, and his chosen young men are gone down to the slaughter, saith the King, whose name is the LORD of hosts.48.15 his…: Heb. the choice of 16The calamity of Moab is near to come, and his affliction hasteth fast. 17All ye that are about him, bemoan him; and all ye that know his name, say, How is the strong staff broken, and the beautiful rod! 18Thou daughter that dost inhabit Dibon, come down from thy glory, and sit in thirst; for the spoiler of Moab shall come upon thee, and he shall destroy thy strong holds. 19O inhabitant of Aroer, stand by the way, and espy; ask him that fleeth, and her that escapeth, and say, What is done?48.19 inhabitant: Heb. inhabitress 20Moab is confounded; for it is broken down: howl and cry; tell ye it in Arnon, that Moab is spoiled, 21And judgment is come upon the plain country; upon Holon, and upon Jahazah, and upon Mephaath, 22And upon Dibon, and upon Nebo, and upon Beth-diblathaim, 23And upon Kiriathaim, and upon Beth-gamul, and upon Beth-meon, 24And upon Kerioth, and upon Bozrah, and upon all the cities of the land of Moab, far or near. 25The horn of Moab is cut off, and his arm is broken, saith the LORD.

26¶ Make ye him drunken: for he magnified himself against the LORD: Moab also shall wallow in his vomit, and he also shall be in derision. 27For was not Israel a derision unto thee? was he found among thieves? for since thou spakest of him, thou skippedst for joy.48.27 skippedst…: or, movedst thyself 28O ye that dwell in Moab, leave the cities, and dwell in the rock, and be like the dove that maketh her nest in the sides of the hole’s mouth. 29We have heard the pride of Moab, (he is exceeding proud) his loftiness, and his arrogancy, and his pride, and the haughtiness of his heart. 30I know his wrath, saith the LORD; but it shall not be so; his lies shall not so effect it.48.30 his lies…: or, those on whom he stayeth (Heb. his bars) do not right 31Therefore will I howl for Moab, and I will cry out for all Moab; mine heart shall mourn for the men of Kir-heres. 32O vine of Sibmah, I will weep for thee with the weeping of Jazer: thy plants are gone over the sea, they reach even to the sea of Jazer: the spoiler is fallen upon thy summer fruits and upon thy vintage. 33And joy and gladness is taken from the plentiful field, and from the land of Moab; and I have caused wine to fail from the winepresses: none shall tread with shouting; their shouting shall be no shouting. 34From the cry of Heshbon even unto Elealeh, and even unto Jahaz, have they uttered their voice, from Zoar even unto Horonaim, as an heifer of three years old: for the waters also of Nimrim shall be desolate.48.34 desolate: Heb. desolations 35Moreover I will cause to cease in Moab, saith the LORD, him that offereth in the high places, and him that burneth incense to his gods. 36Therefore mine heart shall sound for Moab like pipes, and mine heart shall sound like pipes for the men of Kir-heres: because the riches that he hath gotten are perished. 37For every head shall be bald, and every beard clipped: upon all the hands shall be cuttings, and upon the loins sackcloth.48.37 clipped: Heb. diminished 38There shall be lamentation generally upon all the housetops of Moab, and in the streets thereof: for I have broken Moab like a vessel wherein is no pleasure, saith the LORD. 39They shall howl, saying, How is it broken down! how hath Moab turned the back with shame! so shall Moab be a derision and a dismaying to all them about him.48.39 back: Heb. neck 40For thus saith the LORD; Behold, he shall fly as an eagle, and shall spread his wings over Moab. 41Kerioth is taken, and the strong holds are surprised, and the mighty men’s hearts in Moab at that day shall be as the heart of a woman in her pangs.48.41 Kerioth: or, The cities 42And Moab shall be destroyed from being a people, because he hath magnified himself against the LORD. 43Fear, and the pit, and the snare, shall be upon thee, O inhabitant of Moab, saith the LORD. 44He that fleeth from the fear shall fall into the pit; and he that getteth up out of the pit shall be taken in the snare: for I will bring upon it, even upon Moab, the year of their visitation, saith the LORD. 45They that fled stood under the shadow of Heshbon because of the force: but a fire shall come forth out of Heshbon, and a flame from the midst of Sihon, and shall devour the corner of Moab, and the crown of the head of the tumultuous ones.48.45 tumultuous…: Heb. children of noise 46Woe be unto thee, O Moab! the people of Chemosh perisheth: for thy sons are taken captives, and thy daughters captives.48.46 captives, and: Heb. in captivity, etc

47¶ Yet will I bring again the captivity of Moab in the latter days, saith the LORD. Thus far is the judgment of Moab.