Yeremia 48 – NEN & CARSA

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 48:1-47

Ujumbe Kuhusu Moabu

148:1 Hes 32:37; Yos 13:19; Mwa 19:37; Kum 23:6Kuhusu Moabu:

Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo:

“Ole wake Nebo, kwa maana utaharibiwa.

Kiriathaimu utaaibishwa na kutekwa;

Misgabu itaaibishwa na kuvunjavunjwa.

248:2 Hes 21:25; Isa 16:14; Yos 23:16Moabu haitasifiwa tena;

huko Heshboni watu watafanya shauri baya la anguko lake:

‘Njooni na tuangamize taifa lile.’

Wewe nawe, ee Madmena, utanyamazishwa;

upanga utakufuatia.

3Sikiliza kilio kutoka Horonaimu,

kilio cha maangamizi makuu na uharibifu.

4Moabu utavunjwa,

wadogo wake watapiga kelele.

548:5 Isa 15:5Wanapanda kwenda njia ya kuelekea Luhithi,

wakilia kwa uchungu wanapotembea,

kwenye njia inayoshuka kwenda Horonaimu,

kilio cha uchungu kwa ajili ya uharibifu kinasikika.

648:6 Yer 17:6; Mwa 19:17Kimbieni! Okoeni maisha yenu,

kuweni kama kichaka jangwani.

748:7 Hes 21:29; Isa 46:1-2; Yer 49:3; 9:23; Za 49:6; Mk 11:28; Amo 2:3Kwa kuwa mmetumainia matendo yenu na mali zenu,

ninyi pia mtachukuliwa mateka,

naye Kemoshi48:7 Kemoshi alikuwa mungu wa Wamoabu. atakwenda uhamishoni,

pamoja na makuhani wake na maafisa wake.

848:8 Kut 12:23; Yer 4:7; Yos 13:9Mharabu atakuja dhidi ya kila mji,

wala hakuna mji utakaookoka.

Bonde litaangamizwa na uwanda utaharibiwa,

kwa sababu Bwana amesema.

948:9 Amu 9:45; Yer 51:29Wekeni chumvi kwa ajili ya Moabu,

kwa kuwa ataangamizwa;

miji yake itakuwa ukiwa,

pasipo kuwa na mtu atakayeishi ndani yake.

1048:10 Yer 47:6; 1Fal 20:42; 1Sam 15:3, 11; 2Fal 13:15-19“Alaaniwe yeye afanyaye kazi ya Bwana kwa hila!

Alaaniwe yeye auzuiaye upanga wake usimwage damu!

1148:11 Zek 1:15; Sef 1:12“Moabu amestarehe tangu ujana wake,

kama divai iliyoachwa kwenye machujo yake,

haikumiminwa kutoka chombo kimoja hadi kingine,

hajaenda uhamishoni.

Kwa hiyo ana ladha ile ile kama aliyokuwa nayo,

nayo harufu yake haijabadilika.

12Lakini siku zinakuja,”

asema Bwana,

“nitakapotuma watu wamiminao kutoka kwenye magudulia,

nao watamimina;

wataacha magudulia yake yakiwa matupu

na kuvunja mitungi yake.

1348:13 Hos 10:6; Amu 11:24; Yos 7:2Kisha Moabu atamwonea aibu mungu wao Kemoshi,

kama vile nyumba ya Israeli walivyoona aibu

walipotegemea mungu wa Betheli.48:13 Betheli ina maana ya Nyumba ya Mungu; lakini pia ni mahali ambapo Mfalme Yeroboamu alisimamisha moja ya sanamu za ndama ili kuabudiwa; nyingine aliiweka huko Dani (1Fal 12:29-33).

1448:14 Mhu 9:11; Za 33:16“Mwawezaje kusema, ‘Sisi ni mashujaa,

watu jasiri katika vita’?

1548:15 Yer 50:27; 51:40, 57; 46:18; Isa 9:17Moabu ataangamizwa na miji yake itavamiwa,

vijana wake waume walio bora sana watachinjwa,”

asema Mfalme, ambaye jina lake

ni Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote.

16“Kuanguka kwa Moabu kumekaribia,

janga kubwa litamjia kwa haraka.

1748:17 Za 110:2; 2Fal 3:4-5Ombolezeni kwa ajili yake, ninyi nyote mnaomzunguka,

ninyi nyote mnaojua sifa zake,

semeni, ‘Tazama jinsi ilivyovunjika fimbo ya kifalme yenye nguvu,

tazama jinsi ilivyovunjika fimbo iliyotukuka!’

1848:18 Isa 47:1; Hes 21:30; Yos 13:9“Shuka kutoka fahari yako

na uketi katika ardhi iliyokauka,

enyi wenyeji wa Binti wa Diboni,

kwa maana yeye aangamizaye Moabu atakuja dhidi yako,

na kuangamiza miji yako iliyozungushiwa maboma.

1948:19 Hes 32:34; Kum 2:36Simama kando ya barabara na utazame,

wewe unayeishi Aroeri.

Muulize mwanaume anayekimbia

na mwanamke anayetoroka,

waulize, ‘Kumetokea nini?’

2048:20 Isa 16:7; Hes 21:13Moabu amefedheheshwa, kwa kuwa amevunjavunjwa.

Lieni kwa huzuni na kupiga kelele!

Tangazeni kando ya Arnoni

kwamba Moabu ameangamizwa.

2148:21 Hes 21:23; Isa 15:4; Yos 13:18; 15:51; 13:9, 21Hukumu imefika kwenye uwanda wa juu:

katika Holoni, Yahasa na Mefaathi,

2248:22 Hes 21:30; Yos 13:9, 17; Hes 32:38katika Diboni, Nebo

na Beth-Diblathaimu,

2348:23 Hes 32:38; Yos 13:17-19katika Kiriathaimu, Beth-Gamuli

na Beth-Meoni,

2448:24 Amo 2:2; Yer 49:13; Isa 15:1katika Keriothi na Bosra;

kwa miji yote ya Moabu,

iliyoko mbali na karibu.

2548:25 Za 75:10; Eze 30:21; Za 37:17Pembe48:25 Pembe hapa ni ishara ya nguvu. ya Moabu imekatwa,

mkono wake umevunjwa,”

asema Bwana.

2648:26 Yer 25:16, 27; 51:39; Isa 28:8; 1Sam 17:26“Mlevye,

kwa kuwa amemdharau Bwana.

Moabu na agaegae katika matapishi yake,

yeye na awe kitu cha dhihaka.

2748:27 Mit 24:17; Yer 2:26; Ay 16:4; Za 44:14; Mik 7:8-10; Kum 7:8-10; Sef 2:8Je, Israeli hakuwa kitu chako cha kudhihakiwa?

Je, alikamatwa miongoni mwa wezi,

kiasi cha kutikisa kichwa chako kwa dharau

kila mara unapozungumza juu yake?

2848:28 Za 55:6-7; Wim 1:15; Amu 6:2; Wim 2:14; Mwa 8; 8Ondokeni kwenye miji yenu, mkaishi katikati ya miamba,

enyi mnaoishi Moabu.

Kuweni kama huwa ambaye hutengeneza kiota chake

kwenye mdomo wa pango.

2948:29 Law 26:19; Isa 16:6; Ay 40:12; Mit 10:5; 16:18“Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu:

kutakabari kwake kwa kiburi na majivuno,

kiburi chake na ufidhuli wake,

na kujivuna kwa moyo wake.

30Ninaujua ujeuri wake, lakini ni bure,”

asema Bwana,

“nako kujisifu kwake hakumsaidii chochote.

3148:31 Isa 15:5-6; 2Fal 3:25Kwa hiyo namlilia Moabu,

kwa ajili ya Moabu yote ninalia,

ninaomboleza kwa ajili

ya watu wa Kir-Haresethi.

3248:32 Hes 32:3; 21:13; Isa 16:8-9; Yos 13:25Ninalia machozi kwa ajili yenu, kama Yazeri aliavyo,

enyi mizabibu ya Sibma.

Matawi yako yameenea hadi baharini;

yamefika hadi bahari ya Yazeri.

Mharabu ameyaangukia matunda yako yaliyoiva

na mizabibu yako iliyoiva.

3348:33 Isa 16:10; 24:7; Amo 5:17; Yoe 1:12Shangwe na furaha vimetoweka

kutoka bustani na mashamba ya Moabu.

Nimekomesha kutiririka kwa divai kutoka mashinikizo;

hakuna hata mmoja ayakanyagaye kwa kelele za shangwe.

Ingawa kuna kelele,

sio kelele za shangwe.

3448:34 Isa 15:4-6; Hes 32:3; 21:23; Mwa 13:10; Yos 13:26; Hes 21:25“Sauti ya kilio chao inapanda

kutoka Heshboni hadi Eleale na Yahazi,

kutoka Soari hadi Horonaimu na Eglath-Shelishiya,

kwa kuwa hata maji ya Nimrimu yamekauka.

3548:35 Isa 15:2; 16:12; Yer 11:13Nitakomesha wale wote katika Moabu

watoao sadaka mahali pa juu,

na kufukiza uvumba kwa miungu yao,”

asema Bwana.

3648:36 Isa 16:11; 15:7; Mit 11:4; 2Fal 3:25“Kwa hiyo moyo wangu unaomboleza kwa ajili ya Moabu kama filimbi;

unaomboleza kama filimbi kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi.

Utajiri waliojipatia umetoweka.

3748:37 Isa 15:2; Eze 29:18; Isa 3:24; Amo 8:10; Eze 27:31; 2Sam 10:4Kila kichwa kimenyolewa

na kila mwenye ndevu zimekatwa;

kila mkono umekatwa

na kila kiuno kimefunikwa kwa nguo ya gunia.

3848:38 Yer 22:28; Isa 15:3Juu ya mapaa yote katika Moabu

na katika viwanja

hakuna kitu chochote isipokuwa maombolezo,

kwa kuwa nimemvunja Moabu

kama gudulia ambalo hakuna mtu yeyote anayelitaka,”

asema Bwana.

39“Tazama jinsi alivyovunjikavunjika!

Jinsi wanavyolia kwa huzuni!

Tazama jinsi Moabu anavyogeuka kwa aibu!

Moabu amekuwa kitu cha kudhihakiwa,

kitu cha kutisha kwa wale wote

wanaomzunguka.”

4048:40 Kum 28:29; Hab 1:8; Isa 8:8; Yer 49:22Hili ndilo asemalo Bwana:

“Tazama! Tai anashuka chini,

akitanda mabawa yake juu ya Moabu.

4148:41 Isa 21:3; Mik 4:9; Amo 2:16; Isa 15:1Miji itatekwa na ngome zake

zitatwaliwa.

Katika siku hiyo, mioyo ya mashujaa wa Moabu

itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wa kuzaa.

4248:42 Za 83:4; Isa 16:14; Mit 16:18Moabu ataangamizwa kama taifa

kwa sababu amemdharau Bwana.

4348:43 Isa 24:17, 18; Yer 49:5Hofu kuu, shimo na mtego vinawangojea,

enyi watu wa Moabu,”

asema Bwana.

4448:44 1Fal 19:17; Ay 20:24; Yer 11:23; 23:12; Isa 24:18“Yeyote atakayeikimbia hiyo hofu kuu

ataanguka ndani ya shimo,

yeyote atakayepanda kutoka shimoni,

atanaswa katika mtego,

kwa sababu nitaletea Moabu

mwaka wa adhabu yake,”

asema Bwana.

4548:45 Hes 21:21, 26-28; Yos 12:2; Hes 24:17“Katika kivuli cha Heshboni,

wakimbizi wamesimama pasipo msaada,

kwa kuwa moto umezimika huko Heshboni,

mwali wa moto kutoka katikati ya Sihoni;

unaunguza vipaji vya nyuso za Moabu,

mafuvu yao wenye kujivuna kwa kelele.

4648:46 Hes 21:29; Amu 11:24Ole wako, ee Moabu!

Watu wa Kemoshi wameangamizwa;

wana wako wamepelekwa uhamishoni

na binti zako wamechukuliwa mateka.

4748:47 Za 14:7; Dan 11:41; Yer 49:6; Isa 11:1; Yer 12:15; Eze 16:53“Lakini nitarudisha mateka wa Moabu,

katika siku zijazo,”

asema Bwana.

Huu ndio mwisho wa hukumu juu ya Moabu.

Священное Писание (Восточный перевод), версия с «Аллахом»

Иеремия 48:1-47

Пророчество о Моаве

1О Моаве.

Так говорит Вечный, Повелитель Сил, Бог Исраила:

– Горе Нево – он будет опустошён!

Кириатаим будет опозорен и захвачен;

крепость48:1 Или: «Мизгав». будет опозорена и разрушена.

2Минует слава Моава;

в Хешбоне замышляют против него зло:

«Идём, покончим с этим народом».

И ты, Мадмен, замолкнешь48:2 На языке оригинала наблюдаются игры слов: название Хешбон и глагол «замышлять» (хашав); название Мадмен и глагол «замолкнуть» (дамам).;

меч будет преследовать тебя.

3Слышны крики из Хоронаима,

крики великого опустошения и разрушения.

4Погибнет Моав,

заплачут его малые дети.

5Поднимаются жители на Лухит

и на ходу горько плачут;

на дороге, ведущей в Хоронаим,

слышен скорбный плач о разорении.

6Бегите! Спасайте свои жизни!

Будьте как одинокий можжевельник в пустыне.

7За то, что вы надеялись на свои дела и богатства,

вас тоже захватят.

В плен отправится Хемош48:7 Хемош – божество из пантеона моавитян, в жертвы которому приносились люди.

со своими священнослужителями и вождями.

8Губитель придёт в каждый город –

ни один город не спасётся.

Долина погибнет,

равнина придёт в запустение,

как и сказал Вечный.

9Дайте Моаву крылья,

чтобы он мог улететь48:9 Или: «Посыпьте Моав солью, чтобы он был опустошён»..

Его города опустеют,

останутся без горожан.

10Проклят тот, кто небрежен, исполняя дело Вечного!

Проклят тот, кто удерживает меч от кровопролития!

11Моав от юности пребывал в покое,

и в плен его не уводили.

Он – как вино над осадком,

которое не переливали из сосуда в сосуд,

так что вкус у него, как и прежде,

и запах не изменился48:11 Ср. Соф. 1:12 со сноской..

12Но наступают дни, –

возвещает Вечный, –

когда Я пошлю к нему виноделов,

чтобы перелить его,

опустошить его сосуды

и разбить его кувшины вдребезги.

13Моав тогда постыдится Хемоша,

как Исраил постыдился Вефиля,

своей надежды48:13 Исраильский царь Иеровоам I приказал отлить двух золотых тельцов и одного из них поставил в Вефиле. Он возвёл поклонение тельцам в ранг национальной религии (см. 3 Цар. 12:25-33)..

14Как же вы можете говорить: «Мы храбрецы,

мы отважные в битве воины»?

15Моав будет разрушен, его города будут взяты;

его лучшие юноши пойдут на бойню, –

говорит Царь, Чьё имя Вечный, Повелитель Сил. –

16Падение Моава близко;

день его бедствия спешит.

17Плачьте о нём, все его соседи,

все, кто знал его славу,

говорите: «Как сломан могучий скипетр,

как сломан жезл прославленный!»

18Сойдите с почётного места

и сядьте на иссохшую землю,

жители Дивона,

потому что губитель Моава

двинется на вас

и разрушит ваши укреплённые города.

19Встаньте у дороги и смотрите,

живущие в Ароере.

Расспрашивайте беженца и уцелевшую,

спрашивайте: «Что случилось?»

20Моав обесславлен, ведь он сломлен;

рыдайте и плачьте!

Расскажите вдоль побережий Арнона,

что разрушен Моав.

21Суд пришёл на города в плоскогорье:

на Холон, Иахац и Мефаат,

22на Дивон, Нево и Бет-Дивлатаим,

23на Кириатаим, Бет-Гамул и Бет-Меон,

24на Кериот и Боцру,

на все дальние и ближние города Моава.

25Рог Моава отрублен,

и его рука48:25 Рог и рука были символами могущества, власти и силы. сломана, –

возвещает Вечный. –

26Напоите его допьяна,

потому что он возносился перед Вечным.

Пусть он вываляется в своей блевотине,

пусть он станет посмешищем.

27Разве не посмешищем был у тебя Исраил?

Разве пойман он был с ворами,

что ты презрительно качал головой

каждый раз, когда говорил о нём?

28Оставьте города и селитесь в скалах,

жители Моава.

Будьте как голуби, что гнездятся

на краях расщелин.

29– Слышали мы о гордости Моава,

о его чрезмерной гордости и тщеславии,

о его гордости и надменности,

о его заносчивом сердце.

30– Знаю Я его наглость, –

возвещает Вечный, –

но пуста его похвальба,

и дела его ничего не стоят.

31Поэтому плачу Я о Моаве,

рыдаю обо всём Моаве,

скорблю о жителях Кир-Харесета.

32О виноградники Сивмы,

Я плачу о вас, как я плакал о городе Иазере.

Ваши лозы тянулись к Мёртвому морю,

достигали Иазера48:32 Букв.: «достигали моря Иазер»..

Разрушитель набросился на летние плоды,

на спелый виноград.

33Веселье и радость ушли

с плодородной земли Моава.

Иссякло вино в давильнях;

никто не топчет в них виноград с радостным криком.

Хотя и стоит крик,

но не радостный он.

34От Хешбона до Элеале раздаются рыдания;

крики слышны до самого Иахаца,

от Цоара до Хоронаима и Эглат-Шлешии,

ведь даже воды реки Нимрим пересохнут.

35Я истреблю в Моаве тех,

кто приносит жертвы в капищах на возвышенностях

и возжигает благовония своим богам, –

возвещает Вечный. –

36Поэтому моё сердце плачет о Моаве, как свирель,

плачет, как свирель, о жителях Кир-Харесета.

Богатство, которое они скопили, погибло.

37В знак скорби все головы острижены,

все бороды сбриты;

на всех руках порезы,

и одеты они в рубище.

38На всех крышах Моава

и на площадях все рыдают,

потому что Я разбил Моав,

как сосуд, который никому не нужен, –

возвещает Вечный. –

39Как он раскололся! Как они рыдают!

Как позорно Моав показал спину!

Моав стал посмешищем

и ужасом для всех соседей.

40Так говорит Вечный:

– Орёл налетит на свою добычу,

простирая свои крылья над Моавом.

41Кериот будет взят48:41 Или: «Города будут взяты».,

крепости будут захвачены.

В тот день сердца воинов Моава

затрепещут, словно сердце роженицы.

42Не будет больше такого народа, как Моав,

потому что он возносился перед Вечным.

43Ужас, яма и западня ждут тебя,

народ Моава, –

возвещает Вечный. –

44Всякий, кто побежит от ужаса,

упадёт в яму;

всякий, выбравшийся из ямы,

угодит в западню.

Я нашлю эти беды на Моав

в год его наказания, –

возвещает Вечный. –

45В тени Хешбона

замерли изнурённые беженцы:

полыхает огонь из Хешбона,

пышет пламя из дома Сигонова,

обжигает лоб Моаву,

темя народу мятежному.

46Горе тебе, Моав!

Погиб народ Хемоша48:46 Хемош – божество из пантеона моавитян, в жертвы которому приносились люди.;

твои сыновья взяты в плен,

твои дочери – в неволе48:45-46 См. Чис. 21:28-29; Втор. 2:26-30..

47Но в будущем Я верну Моаву благополучие, –

возвещает Вечный.

Здесь кончается приговор Моаву.