Yeremia 40 – NEN & NRT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 40:1-16

Yeremia Aachiwa Huru

140:1 Yer 39:14; Mt 2:18; Yos 18:25; Nah 3:10; 1Sam 8:4Neno likamjia Yeremia kutoka kwa Bwana baada ya Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme kumfungua huko Rama. Alikuwa amemkuta Yeremia akiwa amefungwa kwa minyororo miongoni mwa mateka wote kutoka Yerusalemu na Yuda waliokuwa wakipelekwa uhamishoni Babeli. 240:2 Yos 23:15; Yer 50:7; Mao 2:17; Rum 13:4; Isa 10:22; 2Nya 34:24; Za 18:18; Gal 6:7-8Kiongozi wa walinzi alipomwona Yeremia, akamwambia, “Bwana Mungu wako aliamuru maafa haya kwa mahali hapa. 340:3 Mit 13:21; Yak 1:15; Law 26:33; Mdo 7:39; Rum 6:23; Kum 29:24-28; Dan 9:14; Rum 2:5-9Sasa Bwana ameyaleta haya, amefanya sawasawa na vile alivyosema angefanya. Yote haya yametokea kwa sababu ninyi mlifanya dhambi dhidi ya Bwana na hamkumtii. 440:4 Mwa 13:9; Yer 39:11-12; Mwa 20:15; Za 105:18-20; Yer 37:14; Mao 3:7Lakini leo ninakufungua minyororo iliyo kwenye viwiko vya mikono yako. Twende pamoja mpaka Babeli ikiwa unataka, nami nitakutunza. Lakini kama hutaki, basi usije. Tazama, nchi yote iko mbele yako, nenda kokote unakotaka.” 540:5 2Fal 25:22; Yer 39:14; Yos 15:18; Mit 15:16; 2Fal 22:12-14; Neh 5:14; Zek 1:12Lakini kabla Yeremia hajageuka kuondoka, Nebuzaradani akaongeza kusema, “Rudi kwa Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani, ambaye mfalme wa Babeli amemchagua awe juu ya miji ya Yuda, ukaishi naye miongoni mwa watu, au uende popote panapokupendeza.”

Kisha huyo kiongozi akampa posho yake na zawadi, akamwacha aende zake. 640:6 Amu 20:1; 1Sam 7:5-17Kwa hiyo Yeremia akaenda kwa Gedalia mwana wa Ahikamu huko Mispa, na kuishi naye miongoni mwa watu walioachwa katika nchi.

Gedalia Auawa

(2 Wafalme 25:22-26)

740:7 Yer 39:10; Mdo 24:17; Mwa 41:41; Neh 5:14; Yak 2:5; 2Fal 24:14Maafisa wote wa jeshi na watu wao waliokuwa bado wapo kwenye eneo la wazi waliposikia kwamba mfalme wa Babeli amemteua Gedalia mwana wa Ahikamu kuwa mtawala wa nchi, na amemweka kuwa kiongozi wa wanaume, wanawake na watoto waliokuwa maskini zaidi katika nchi ambao hawakuchukuliwa kwenda uhamishoni Babeli, 840:8 Yer 41:1-2; 2Sam 23:28; Kum 3:14wakamjia Gedalia huko Mispa. Hawa walikuwa Ishmaeli mwana wa Nethania, Yohanani na Yonathani wana wa Karea, Seraya mwana wa Tanhumethi, wana wa Efai Mnetofathi, na Yezania mwana wa Mmaaka, pamoja na watu wao. 940:9 Yer 5:19; Efe 6:5-8; Yer 38:20; Rum 13:1-2; Eze 23:23Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani akaapa ili kuwatia moyo wao na watu wao. Akasema: “Msiogope kuwatumikia Wakaldayo. Kaeni katika nchi na kumtumikia mfalme wa Babeli, na itakuwa vyema kwenu. 1040:10 Kum 1:39; 16:13; Mwa 27:28; Kut 7:19; 23:16; 2Kor 4:7Mimi mwenyewe nitakaa Mispa ili kuwawakilisha mbele ya Wakaldayo wanaotujia, lakini ninyi mtavuna divai, matunda ya kiangazi na mafuta, nanyi mtaweka katika vyombo vyenu vya kuhifadhia, na kuishi katika miji mliyojitwalia.”

1140:11 Hes 21:11; 25:1; Isa 16:4; Mao 1:14; Yer 24:9; Mwa 25:30; Yer 12:14Wayahudi wote waliokuwa Moabu, Amoni, Edomu na nchi nyingine zote waliposikia kwamba mfalme wa Babeli ameacha mabaki ya watu katika Yuda na amemweka Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani kuwa mtawala wao, 1240:12 Yer 43:5wakarudi wote katika nchi ya Yuda kwa Gedalia huko Mispa, kutoka nchi zote ambazo walikuwa wametawanywa. Nao wakavuna divai na matunda tele wakati wa kiangazi.

13Yohanani mwana wa Karea pamoja na maafisa wote wa jeshi waliokuwa bado wapo kwenye eneo la wazi wakamjia Gedalia huko Mispa 1440:14 Mwa 19:38; 2Sam 10:1-19; Amo 1:13; Yer 41:10; 25:21; 49:1na kumwambia, “Je, hujui kwamba Baalisi mfalme wa Waamoni amemtuma Ishmaeli mwana wa Nethania akuue?” Lakini Gedalia mwana wa Ahikamu hakuwaamini.

1540:15 Kum 5:17; Mt 5:21-22; Mwa 11:4; Mt 26:31; Yn 11:52; Rum 11:5; 2Fal 21:15Kisha Yohanani mwana wa Karea akamwambia Gedalia kwa siri huko Mispa, “Acha niende nikamuue Ishmaeli mwana wa Nethania, wala hakuna atakayejua. Kwa nini akuue na kusababisha Wayahudi wote waliokuzunguka watawanyike, na mabaki wa Yuda waangamie?”

1640:16 Yer 43:2Lakini Gedalia mwana wa Ahikamu akamwambia Yohanani mwana wa Karea, “Usifanye jambo kama hilo! Unalosema kuhusu Ishmaeli si kweli.”

New Russian Translation

Иеремия 40:1-16

Иеремия освобожден

1Слово Господа, которое было к Иеремии, после того как Невузарадан, начальник царской охраны, освободил его в Раме. Тот нашел Иеремию, закованного в цепи, среди всех пленников из Иерусалима и Иудеи, которых угоняли в плен в Вавилон. 2Разыскав Иеремию, начальник охраны сказал ему:

– Господь, твой Бог, сулил такую беду этой стране. 3А ныне она разразилась: как Господь говорил, так Он и сделал. Это случилось потому, что вы грешили против Господа и не слушались Его. 4Но сегодня я освобождаю тебя от цепей, что на твоих руках. Если хочешь, пойдем со мной в Вавилон, и я позабочусь о тебе, а не хочешь, так и не ходи. Смотри, вся земля перед тобой: ступай, куда хочешь.

5Не успел Иеремия отойти, как Невузарадан добавил:

– Возвращайся к Гедалии, сыну Ахикама, внуку Шафана, которого царь Вавилона назначил начальником над городами Иудеи, и живи у него среди народа. Или ступай, куда хочешь.

Затем начальник охраны дал ему припасов и подарок и отпустил его. 6И Иеремия пошел к Гедалии, сыну Ахикама, в Мицпу и поселился там у него среди народа, который был оставлен в стране.

Убийство Гедалии

(4 Цар. 25:22-26)

7Когда все военачальники и их люди, оставшиеся в этой стране, услышали, что царь Вавилона назначил Гедалию, сына Ахикама, наместником над страной, и что ему поручили заботы о мужчинах, женщинах и детях, которые были самыми бедными в стране и не были угнаны в плен в Вавилон, 8они пришли к Гедалии в Мицпу. Это были Исмаил, сын Нефании, Иоханан и Ионафан, сыновья Кареаха, Серая, сын Танхумета, сыновья Ефая из Нетофы, Иезания, сын маахитянина, со своими людьми. 9Гедалия, сын Ахикама, внук Шафана, поклялся им, чтобы успокоить их и их людей:

– Не бойтесь халдейских вельмож, – сказал он. – Селитесь в стране, служите царю Вавилона, и вам будет хорошо. 10Сам я буду жить в Мицпе, чтобы представлять вас перед халдеями, которые будут приходить к нам, а вы собирайте и запасайте вино, летние плоды и оливковое масло в кувшины и живите себе в городах, которые заняли.

11Когда все иудеи в Моаве, Аммоне, Эдоме и во всех других странах услышали, что халдейский царь оставил в Иудее часть народа и назначил Гедалию, сына Ахикама, внука Шафана, их наместником, 12все они вернулись в землю Иудеи к Гедалии, в Мицпу, из всех стран, куда были изгнаны. Они собрали в изобилии вина и летних плодов. 13Иоханан, сын Кареаха, и все военачальники, все еще пребывавшие в поле, явились к Гедалии в Мицпу 14и сказали ему:

– Неужели ты не знаешь, что Баалис, царь аммонитян, подослал Исмаила, сына Нефании, чтобы убить тебя?

Но Гедалия, сын Ахикама, не поверил им. 15Тогда Иоханан, сын Кареаха, тайно сказал Гедалии в Мицпе:

– Давай я пойду и убью Исмаила, сына Нефании, так, что никто об этом не узнает. Зачем позволять ему лишать тебя жизни, чтобы все иудеи, которые собрались вокруг тебя, были рассеяны, чтобы оставшиеся из народа Иудеи погибли?!

16Но Гедалия, сын Ахикама, сказал Иоханану, сыну Кареаха:

– Не делай этого! То, что ты говоришь об Исмаиле, неправда.