Yeremia 37 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 37:1-21

Yeremia Gerezani

137:1 2Fal 14:17; 1Nya 3:16; Eze 17:13; 2Nya 36:10; 24:8, 12; Yer 22:24Sedekia mwana wa Yosia akafanywa kuwa mfalme wa Yuda na Nebukadneza mfalme wa Babeli, naye akatawala mahali pa Yehoyakini37:1 Yehoyakini ni jina jingine la Yekonia au Konia. mwana wa Yehoyakimu. 237:2 2Fal 24:19; 2Nya 36:12-14; Mit 29:12Lakini sio Sedekia, wala watumishi wake, wala watu wa nchi walisikiliza maneno ya Bwana aliyonena kupitia kwa nabii Yeremia.

337:3 2Fal 25:18; Yer 52:24; Hes 21:7; 1Sam 12:19; Yer 38:14; Kut 8:28; 1Fal 13:6Hata hivyo, Mfalme Sedekia akamtuma Yehukali mwana wa Shelemia, pamoja na kuhani Sefania mwana wa Maaseya kwa nabii Yeremia na ujumbe huu: “Tafadhali utuombee kwa Bwana, Mungu wetu.”

437:4 Yer 32:2Wakati huu Yeremia alikuwa huru kuingia na kutoka katikati ya watu, kwa sababu alikuwa bado hajatiwa gerezani. 537:5 Mwa 15; 18; Yer 34:21; 31:1; Isa 30:5; 2Fal 24:7; Eze 17:15Jeshi la Farao lilikuwa limetoka Misri, nao Wakaldayo waliokuwa wameuzunguka Yerusalemu kwa majeshi waliposikia taarifa kuhusu jeshi hilo walijiondoa Yerusalemu.

6Ndipo neno la Bwana likamjia nabii Yeremia kusema: 737:7 Mwa 25:22; 2Fal 22:18; 18:21; Yer 2:12; 36; Mao 4:17“Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Mwambie mfalme wa Yuda aliyekutuma uniulize mimi, ‘Jeshi la Farao lililotoka kuja kukusaidia litarudi katika nchi yake yenyewe, yaani Misri. 837:8 Yer 21:10; 39; 8; Mit 21:30; Yer 38:3, 8Kisha Wakaldayo watarudi na kushambulia mji huu, watauteka na kuuchoma moto.’

937:9 Yer 29:8; Mk 13:5“Hili ndilo Bwana asemalo: Msijidanganye wenyewe mkifikiri, ‘Hakika Wakaldayo watatuacha na kwenda zao.’ Hakika hawatawaacha! 1037:10 Law 26:36-38; Isa 30:17; Yer 21:4-5, 10Hata kama mngelishinda jeshi lote la Wakaldayo linalowashambulia ninyi, na wakawa ni watu waliojeruhiwa tu waliobaki kwenye mahema yao, wangetoka na kuuchoma mji huu moto.”

11Baada ya jeshi la Wakaldayo kujiondoa kutoka Yerusalemu kwa sababu ya jeshi la Farao, 1237:12 Yer 32:9Yeremia akaanza kuondoka mjini ili kwenda nchi ya Benyamini ili akapate sehemu yake ya milki miongoni mwa watu huko. 1337:13 Yer 20:2; 21:9Lakini alipofika kwenye Lango la Benyamini, mkuu wa walinzi, ambaye jina lake lilikuwa Iriya mwana wa Shelemia mwana wa Hanania, akamkamata Yeremia na kusema, “Wewe unakwenda kujiunga na Wakaldayo!”

1437:14 Isa 58:6; Yer 40:4Yeremia akasema, “Hiyo si kweli, mimi sijiungi na Wakaldayo.” Lakini Iriya hakumsikiliza; badala yake, akamkamata Yeremia na kumpeleka kwa maafisa. 1537:15 Yer 20:2; 38:26; Ebr 11:36; Mdo 5:40; 12:6; 1Fal 22:27Wakamkasirikia Yeremia, wakaamuru apigwe, na akafungwa katika nyumba ya Yonathani mwandishi waliyokuwa wameifanya gereza.

16Yeremia akawekwa kwenye chumba kilichofukuliwa chini, kilichojengwa kwa zege ndani ya gereza chini ya ngome, akakaa huko kwa muda mrefu. 1737:17 Yer 15:11; 38:16; 21:7; Mwa 25:22Kisha Mfalme Sedekia akatumana aletwe katika jumba la kifalme, mahali alipomuuliza kwa siri, “Je, kuna neno lolote kutoka kwa Bwana?”

Yeremia akajibu, “Ndiyo, utatiwa mikononi mwa mfalme wa Babeli.”

1837:18 1Sam 16:18; Yn 10:32; Mdo 25:8Kisha Yeremia akamwambia Mfalme Sedekia, “Nimefanya kosa gani dhidi yako na maafisa wako au watu hawa, hata ukanitia gerezani? 1937:19 Yer 14:13; Eze 13:2Wako wapi manabii wako waliokutabiria wakisema, ‘Mfalme wa Babeli hatakushambulia wewe wala nchi hii?’ 20Lakini sasa, bwana wangu mfalme, tafadhali sikiliza. Niruhusu nilete maombi yangu mbele yako, usinirudishe kwenye nyumba ya Yonathani mwandishi, nisije nikafia humo.”

2137:21 Law 26:26; 2Kor 4; 6; Isa 33:16; 2Fal 25:3; Yer 52:6; 39:13-14Ndipo Mfalme Sedekia akatoa maagizo Yeremia awekwe katika ua wa walinzi, na apewe mkate kutoka mitaa ya waokaji kila siku mpaka mikate yote katika mji itakapokwisha. Kwa hiyo Yeremia akabaki katika ua wa walinzi.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

耶利米书 37:1-21

西底迦求耶利米代祷

1巴比伦尼布甲尼撒约西亚的儿子西底迦代替约雅敬的儿子哥尼雅做犹大王。 2西底迦和他的臣仆及人民却没有听从耶和华借耶利米先知说的话。 3西底迦王派示利米雅的儿子犹甲玛西雅的儿子祭司西番雅来对耶利米先知说:“求你为我们向我们的上帝耶和华祷告。” 4当时,耶利米还可以自由来往,没有被他们囚在狱中。 5那时,法老的军队已从埃及出发,正在围攻耶路撒冷迦勒底人听见消息就退兵了。

6耶和华对耶利米先知说: 7“这是以色列的上帝耶和华的话,‘犹大王派你们来求问我,你们告诉他,前来支援你们的法老军队必中途返回埃及8迦勒底人必卷土重来,攻占这城,将它付之一炬。 9耶和华说,你们不要自欺,以为迦勒底人必撤军。其实他们不会撤军。 10即使你们能打败迦勒底全军,他们营中受伤的残兵也必起来烧毁这城。’”

11迦勒底人因害怕法老的军队而撤军的时候, 12耶利米起身离开耶路撒冷,前往便雅悯境内去接收他在同族中应得的地业。 13耶利米先知来到便雅悯门时,哈拿尼亚的孙子、示利米雅的儿子守门官伊利雅逮捕了他,说:“你想去投奔迦勒底人!” 14耶利米说:“不,我不是去投奔迦勒底人。”但伊利雅不信,把他押到众官长那里。 15官长们大怒,命人鞭打耶利米,把他囚禁在书记约拿单的房子里,因为他们已把这房子改作监牢。 16耶利米被囚禁在地牢中许多天。

17后来,西底迦王派人把他带到自己的宫中,私下问他:“耶和华有什么话给你吗?”耶利米说:“有,你要被交在巴比伦王手中。” 18耶利米又问他:“我在什么事上得罪了你、你的臣仆或人民,以致你们把我囚在监牢中? 19那些曾向你们预言‘巴比伦王绝不会来这里攻打你们’的先知如今在哪里呢? 20现在,我主我王啊,请听我说!求你不要把我送回书记约拿单的房子,免得我死在那里。”

21于是,西底迦王下令把耶利米囚在护卫兵的院子里,派人每天从饼铺取一个饼给他,直到城中绝粮。耶利米就这样住在护卫兵的院子里。