Yeremia 32 – NEN & NRT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 32:1-44

Yeremia Anunua Shamba

132:1 2Fal 25:1; Yer 25:1; 39:1Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana, katika mwaka wa kumi wa utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda, ambao ulikuwa mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Mfalme Nebukadneza. 232:2 Neh 3:25; Yer 37:21; Mt 5:12; Za 88:8Wakati huo jeshi la mfalme wa Babeli lilikuwa limeuzunguka mji wa Yerusalemu, naye nabii Yeremia alikuwa amezuiliwa katika ua wa walinzi katika jumba la kifalme la Yuda.

332:3 Yer 26:8-9; 21; 4; 34:2-4Basi Sedekia mfalme wa Yuda alikuwa amemfunga huko akisema, “Kwa nini unatabiri hivyo? Wewe unasema, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ninakaribia kuutia mji huu mkononi mwa mfalme wa Babeli, naye atauteka. 432:4 Yer 21:7; 52:9; 44:30; 34:21; 38:18, 23; 39:5-7Sedekia mfalme wa Yuda hataweza kuponyoka mikononi mwa Wakaldayo, lakini kwa hakika atatiwa mikononi mwa mfalme wa Babeli, naye atazungumza naye ana kwa ana na kumwona kwa macho yake mwenyewe. 532:5 Yer 39:7; Eze 12:13; Mao 1:14; Mit 21:30; Yer 21:4; 2Fal 25:7Atamchukua Sedekia hadi Babeli, mahali atakapoishi mpaka nitakapomshughulikia, asema Bwana. Kama utapigana dhidi ya Wakaldayo, hutashinda.’ ”

6Yeremia akasema, “Neno la Bwana lilinijia kusema: 732:7 Law 25:24-32; Rut 4:3-4; Mt 27:10; Yos 21:18Hanameli mwana wa Shalumu mjomba wako atakuja kwako na kusema, ‘Nunua shamba langu huko Anathothi, kwa sababu wewe kama jamaa ya karibu ni haki na wajibu wako kulinunua.’

8“Kisha, kama Bwana alivyosema, binamu yangu Hanameli alinijia katika ua wa walinzi na kusema: ‘Nunua shamba langu lililoko Anathothi katika nchi ya Benyamini. Kwa kuwa ni haki yako kulikomboa na kulimiliki, jinunulie.’

“Nilijua kwamba hili lilikuwa neno la Bwana. 932:9 Mwa 23:16; Yer 37:12Hivyo nikalinunua shamba hilo lililoko Anathothi kutoka kwa binamu yangu Hanameli, nami nikampimia shekeli kumi na saba32:9 Shekeli 17 za fedha ni sawa na gramu 200. za fedha. 1032:10 Rut 4:9; Isa 8:2; Mwa 23:20Nikatia sahihi na kuweka muhuri hati ya kumiliki, nikaweka mashahidi, na kupima ile fedha kwenye mizani. 11Nikachukua ile hati ya kununulia, nakala iliyotiwa muhuri yenye makubaliano na masharti, pia pamoja na ile nakala isiyo na muhuri, 1232:12 Yer 36:4; 43:3-6; 51:59nami nikampa Baruku mwana wa Neria, mwana wa Maaseya, hati hii mbele ya binamu yangu Hanameli, na mbele ya mashahidi waliokuwa wameweka sahihi kwenye hati hii na mbele ya Wayahudi wote waliokuwa wameketi katika ua wa walinzi.

13“Nilimpa Baruku maelezo haya mbele yao: 1432:14 Isa 8:16‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Chukua hati hizi, yaani nakala zote zenye muhuri na zisizo na muhuri za hati ya kununulia, na uziweke kwenye gudulia la udongo wa mfinyanzi ili zidumu kwa muda mrefu. 1532:15 Eze 28:26; Amo 9:14-15; Yer 30:18; Isa 44:26Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Nyumba, mashamba na mashamba ya mizabibu yatanunuliwa tena katika nchi hii.’

16“Baada ya kumkabidhi Baruku mwana wa Neria hii hati ya kununulia, nilimwomba Bwana:

1732:17 Kum 9:29; Kut 20:5; Za 102:25; 2Fal 3:18; Mwa 32:9-12; Mt 19:26; 2Fal 19:15“Ee Bwana Mwenyezi, umeumba mbingu na nchi kwa uwezo wako mkuu na kwa mkono ulionyooshwa. Hakuna jambo lililo gumu usiloliweza. 1832:18 Kum 5:9-10; Eze 20:5; Kut 20:6; Za 109:14; Yer 10:16; Za 79:12Wewe huonyesha upendo kwa maelfu, lakini huleta adhabu kwa ajili ya dhambi za baba mapajani mwa watoto wao baada yao. Ee Mungu mkuu na mwenye uweza, ambaye jina lako ni Bwana Mwenye Nguvu Zote, 1932:19 Isa 28:29; Ay 34:11, 21; Mit 5:21; Dan 2:20; Mt 16:27; Ay 12:13; 14:16makusudi yako ni makuu, na matendo yako ni yenye uwezo. Macho yako yanaona njia zote za wanadamu, nawe humlipa kila mmoja kulingana na mwenendo wake, na kama yanavyostahili matendo yake. 2032:20 Kut 9:16; Isa 63:12; Kut 3:20; Ay 9:10; Isa 55:13; Yer 13:11Ulitenda ishara za miujiza na maajabu huko Misri, na umeyaendeleza mpaka leo, katika Israeli na miongoni mwa wanadamu wote, nawe umejulikana na kufahamika hivyo mpaka leo. 2132:21 1Nya 17:21; Kut 6:6; Kum 26:8; 2Sam 7:23; Dan 9:15; Yer 6:12; Kum 5:15Uliwatoa watu wako Israeli kutoka Misri kwa ishara na maajabu, kwa mkono wenye nguvu na ulionyooshwa na kwa matisho makuu. 2232:22 Kut 3:8; Eze 20:6Uliwapa nchi hii uliyokuwa umeapa kuwapa baba zao, nchi inayotiririka maziwa na asali. 2332:23 Za 78:54-55; Neh 9:26; Dan 9:10-14; Kum 28:64; Za 44:2; Kut 16:28; Yer 11:8Waliingia na kuimiliki, lakini hawakukutii wala kuifuata sheria yako. Hawakufanya kile ulichowaamuru kufanya. Hivyo ukaleta maafa haya yote juu yao.

2432:24 Yer 14:12; Yos 23:15; Kum 4:25-26; 2Sam 20:15; Yer 6:6; Kum 28:2“Tazama jinsi tumezungukwa na jeshi ili kuuteka mji huu. Kwa sababu ya upanga, njaa na tauni, mji utatiwa mikononi mwa Wakaldayo ambao wanaushambulia. Ulilosema limetokea kama vile unavyoona sasa. 25Ingawa mji utatiwa mikononi mwa Wakaldayo, wewe, Ee Bwana Mwenyezi, uliniambia, ‘Nunua shamba kwa fedha, na jambo hilo lishuhudiwe.’ ”

26Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia kusema: 2732:27 Hes 16:22; Mwa 18:14; 2Fal 3:18“Mimi ndimi Bwana, Mungu wa wote wenye mwili. Je, kuna jambo lolote lililo gumu nisiloliweza? 2832:28 2Nya 36:17; Yer 21:10Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana: Ninakaribia kuutia mji huu mikononi mwa Wakaldayo, na mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli ambaye atauteka. 2932:29 Yer 19:13; 52:13; 44:18; 7:9Wakaldayo ambao wanaushambulia mji huu watakuja na kuuchoma moto na kuuteketeza, pamoja na nyumba ambamo watu wamenikasirisha kwa kumfukizia Baali uvumba katika mapaa na kumimina sadaka za vinywaji kwa miungu mingine.

3032:30 Za 25:7; Yer 22:21; 8:19; 25:7“Watu wa Israeli na wa Yuda hawakufanya kitu kingine ila uovu mbele zangu tangu ujana wao. Naam, watu wa Israeli hawakufanya kitu kingine ila kunikasirisha kwa kazi ambazo mikono yao imetengeneza, asema Bwana. 3132:31 2Fal 23:27; 24:3; Sef 3:1; Mt 23:37; 2Fal 21:4-5; 1Fal 11:7-8Tangu siku ulipojengwa hadi sasa, mji huu umenikasirisha na kunighadhibisha kiasi kwamba ni lazima niuondoe machoni pangu. 3232:32 Isa 1:4-6; Dan 9:8; 1Fal 14:9; Yer 2:26; 44:9Watu wa Israeli na wa Yuda wamenikasirisha kwa uovu wote waliofanya: wao, wafalme wao na maafisa wao, makuhani wao na manabii wao, watu wa Yuda na wakazi wa Yerusalemu. 3332:33 1Fal 14:9; Za 14:3; Kum 4:5; Isa 28:9; Yer 7:13, 28; 2:27; Eze 8:16; Zek 7:11Walinigeuzia visogo vyao, wala si nyuso zao. Ingawa niliwafundisha tena na tena, hawakupenda kusikiliza wala kuitikia adhabu. 3432:34 Yer 7:30; Eze 8:3-16Waliweka miungu yao ya kuchukiza sana katika nyumba iitwayo kwa Jina langu na kuinajisi. 3532:35 Law 18:21; Yer 7:31; 2Fal 23:10; Yer 19:5; 25:7Wakajenga mahali pa juu pa kuabudia miungu kwa ajili ya Baali katika Bonde la Ben-Hinomu, ambapo walitoa wana wao na binti zao kafara kwa Moleki, ingawa kamwe sikuamuru, wala halikuingia akilini mwangu, kwamba watafanya chukizo kama hilo na kumfanya Yuda atende dhambi.

36“Mnasema kuhusu mji huu, ‘Kwa upanga, njaa na tauni, mji utatiwa mkononi mwa mfalme wa Babeli,’ lakini hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli asemalo: 3732:37 Isa 11:12; Yer 23:3-6; Law 25:18; Kum 30:3; Eze 34:28; 39:26; Yer 21:5Hakika nitawakusanya kutoka nchi zote nilizowafukuzia katika hasira yangu kali na ghadhabu yangu kuu, nitawarudisha mahali hapa na kuwaruhusu waishi kwa salama. 3832:38 Yer 24:7; 2Kor 6:16Watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao. 3932:39 Eze 11:19; Yn 17:21; 2Nya 30:12; Mdo 4:32; Kum 6:24; 10:16; Za 86:11Nitawapa moyo mmoja na kutenda pamoja, ili kwamba waniche daima kwa mema yao wenyewe na kwa mema ya watoto wao baada yao. 4032:40 Mwa 9:16; Isa 55:3; Yer 24; 7; Isa 42:6; Kum 4:10Nitafanya nao agano la milele: Kamwe sitaacha kuwatendea mema, nami nitawavuvia kunicha mimi, ili kamwe wasigeukie mbali nami. 4132:41 Kum 28:3-12; Yer 24:6; Kum 30; 9; Amo 9:15; Yer 31:28; Isa 62:4; Mik 7:18Nitafurahia kuwatendea mema, na kwa hakika nitawapanda katika nchi hii kwa moyo wangu wote na roho yangu yote.

4232:42 Yer 29:10; 31:28; Mao 3:38“Hili ndilo asemalo Bwana: Kama nilivyoleta maafa haya makubwa kwa watu hawa, ndivyo nitakavyowapa mafanikio niliyowaahidi. 43Kwa mara nyingine tena mashamba yatanunuliwa katika nchi hii ambayo mlisema, ‘Imekuwa ukiwa, isiyofaa, isiyo na watu wala wanyama, kwa sababu imetiwa mikononi mwa Wakaldayo.’ 4432:44 Yer 17:26; Ezr 9:9; Yer 33:7, 11, 26; Rut 4:9; Isa 8:2; Za 14:7Mashamba yatanunuliwa kwa fedha, na hati zitatiwa sahihi, zitatiwa muhuri na kushuhudiwa katika nchi ya Benyamini, katika vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu, katika miji ya Yuda na katika miji ya nchi ya vilima, sehemu za magharibi katika miji ya tambarare na katika Negebu, kwa sababu nitarudisha tena mafanikio yao,32:44 Au: nitawarudisha tena kutoka utumwani. asema Bwana.”

New Russian Translation

Иеремия 32:1-44

Иеремия покупает поле во время осады

1Вот слово Господне, которое было к Иеремии в десятом году правления Цедекии32:1 В 587 г. до н. э., царя Иудеи – это был восемнадцатый год правления Навуходоносора. 2Войско вавилонского царя осаждало Иерусалим, а пророк Иеремия был заключен в темницу при дворце царя Иудеи.

3Цедекия, царь Иудеи, заключил его там, сказав:

– Зачем ты так пророчествуешь? Ты говоришь: «Так говорит Господь: Я отдам этот город царю Вавилона, и он захватит его. 4Цедекия, царь Иудеи, не спасется от рук халдеев; его непременно отдадут вавилонскому царю, и он увидит его собственными глазами и будет разговаривать с ним лицом к лицу. 5Он возьмет Цедекию в Вавилон, где тот останется, пока Я не позабочусь о нем. Если будешь воевать против халдеев, то не преуспеешь».

6Иеремия сказал:

– Ко мне было слово Господне: 7«Ханамел, сын твоего дяди Шаллума, придет к тебе и скажет: „Купи мое поле в Анатоте, потому что ты – ближайший родственник, и у тебя есть право и обязанность купить его“».

8Потом, как и сказал Господь, мой двоюродный брат Ханамел пришел ко мне в темницу и сказал:

– Купи мое поле в Анатоте, что в земле Вениамина. Ты имеешь право выкупить его и владеть им, так купи его себе.

Я знал, что таково было слово Господне, 9и купил поле в Анатоте у моего двоюродного брата Ханамела, отвесив ему семнадцать шекелей32:9 Около 200 граммов. серебра. 10Я подписал купчую, приложил к ней свою печать, пригласил свидетелей и отвесил серебро на весах. 11Я взял купчую – запечатанную копию с договором и его условиями и незапечатанную – 12и отдал эту купчую Баруху, сыну Нирии, сына Махсеи, в присутствии моего двоюродного брата Ханамела, свидетелей, которые ее подписали, и всех иудеев, которые находились во дворе темницы.

13В их присутствии Я дал Баруху такое повеление: 14«Так говорит Господь Сил, Бог Израиля: „Возьми эти грамоты – запечатанную копию купчей и незапечатанную – и положи их в глиняный кувшин, чтобы они могли храниться долго. 15Ведь так говорит Господь Сил, Бог Израиля: В этой стране будут снова покупать дома, поля и виноградники“».

16Отдав купчую Баруху, сыну Нирии, я помолился Господу:

17– О Владыка Господь! Ты создал небеса и землю Своей великой силой и простертой рукой. Нет ничего невозможного для Тебя. 18Ты являешь милость тысячам, но воздаешь за вину родителей их детям после них. О великий и могучий Бог, Чье имя – Господь Сил, 19Твои намерения величественны и Твои дела велики. Твои глаза раскрыты на все пути человека; Ты воздаешь каждому за его путь, по плодам дел его. 20Ты совершил знамения и чудеса в Египте и творил их доныне и в Израиле, и среди всего человеческого рода, и приобретал Себе славу, которая принадлежит Тебе и сегодня. 21Знамениями и чудесами, могучей дланью, простертой рукой и великим страхом Ты вывел Свой народ Израиль из египетской земли. 22Ты отдал им эту землю, которую клялся отдать их отцам, землю, где течет молоко и мед. 23Они вошли в нее и завладели ею, но не слушали Тебя и не жили по Твоему Закону; они не делали того, что Ты повелевал им. За это Ты наслал на них всю эту беду.

24Видишь, как насыпают осадные валы, чтобы взять город. Из-за меча, голода и мора город достанется халдеям, которые напали на нас. То, что Ты сказал, исполнилось, и вот, Ты видишь это. 25Ты, Владыка Господь, говорил мне: «Купи себе поле за серебро и пригласи для сделки свидетелей», но ведь город переходит в руки халдеев.

26И было слово Господне к Иеремии:

27– Я – Господь, Бог всех людей. Есть ли что-нибудь невозможное для Меня? 28Поэтому так говорит Господь: Я отдам этот город халдеям и Навуходоносору, царю Вавилона, который захватит его. 29Халдеи, которые воюют с этим городом, придут и предадут его огню; они сожгут его дотла с домами, на крышах которых народ возжигал благовония Баалу и совершал жертвенные возлияния чужим богам, вызывая Мой гнев.

30Народ Израиля и Иудеи с юности делал лишь зло в Моих глазах; да, народ Израиля лишь вызывал Мой гнев делами своих рук, – возвещает Господь. – 31Со дня его основания до сегодняшнего дня этот город вызвал у Меня такой гнев и негодование, что Я отвергну его от Себя. 32Народ Израиля и Иудеи вызывал Мой гнев всем злом, которое он делал – они сами, их цари и вельможи, их священники и пророки, жители Иудеи и горожане Иерусалима. 33Они повернулись ко Мне спиной, а не лицом; Я наставлял их снова и снова, но они не слушали и не принимали наставлений. 34Они поставили свои мерзости в доме, который называется Моим именем, и осквернили его. 35Они построили святилища Баалу на возвышенностях в долине Бен-Гинном, чтобы приносить своих сыновей и дочерей в огненную жертву Молоху32:35 Молох – аммонитский бог, в жертвы которому приносились дети. По Закону за поклонение Молоху израильтянам грозила смертная казнь (см. Лев. 18:21; 20:2-5)., хотя Я не повелевал этого; Мне даже на ум не приходило, что они должны делать такую мерзость и вводить Иудею в грех.

36Вы говорите об этом городе: «Из-за меча, голода и мора он достанется царю Вавилона», но так говорит Господь, Бог Израиля: 37Я непременно соберу их из всех земель, в которые Я изгнал их в гневе, ярости и страшном негодовании; Я приведу их обратно в этот край и дам им жить в безопасности. 38Они будут Моим народом, а Я буду их Богом. 39Я дам им одно сердце и один путь – всегда чтить Меня на благо себе и своим потомкам. 40Я заключу с ними вечный завет, по которому Я не перестану делать для них добро и вдохновлять их, чтобы они чтили Меня, чтобы они никогда больше не отвернулись от Меня. 41Я с радостью буду делать для них добро и непременно насажу их на этой земле от всего сердца и от всей души.

42Ведь так говорит Господь:

– Как Я навел на этот народ всю эту страшную беду, так Я пошлю им и все благоденствие, которое Я им обещал. 43И снова будут покупать поля в этой стране, о который вы говорите: «Это разоренный край без людей и животных; он был отдан в руки халдеев». 44Поля будут покупать за серебро и будут подписывать купчие, ставить на них печати и приглашать к ним свидетелей в землях Вениамина, в окрестностях Иерусалима и в городах нагорий, западных предгорий и Негева, потому что Я восстановлю их, – возвещает Господь.