Yeremia 31 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 31:1-40

Mahamisho Kurudi Kwa Shangwe

131:1 Law 26:12; Yer 30:22“Wakati huo, nitakuwa Mungu wa koo zote za Israeli nao watakuwa watu wangu,” asema Bwana.

231:2 Hes 14:20; Kut 33:14; Kum 12:9Hili ndilo asemalo Bwana:

“Watu watakaopona upanga

watapata upendeleo jangwani;

nitakuja niwape Israeli pumziko.”

331:3 Rum 11:28; Kum 4:37; Hos 11:4; Yn 6:44Bwana alitutokea wakati uliopita, akisema:

“Nimekupenda kwa upendo wa milele,

nimekuvuta kwa wema.

431:4 Yer 30:18-19; 2Fal 19:21; Mwa 31:27; Kut 15:20; Yer 30:19Nitakujenga tena nawe utajengeka upya,

ewe Bikira Israeli.

Utachukua tena matari yako

na kwenda kucheza na wenye furaha.

531:5 Yer 33:13; Oba 1:19; Isa 65:12; Amo 9:14; Kum 20:6; Yer 50:19; Isa 37:30Utapanda tena shamba la mizabibu

juu ya vilima vya Samaria,

wakulima watapanda

na kufurahia matunda yake.

631:6 Kum 33:19; Mik 4:2; Isa 52:8; 56:10; Yer 50:4-5Itakuja siku wakati walinzi watakapowapigia kelele

juu ya vilima vya Efraimu wakisema,

‘Njooni, twendeni juu Sayuni,

kwake Bwana Mungu wetu.’ ”

731:7 Kum 28:13; Isa 61:9; Za 14:7; 28:9; Isa 37:31; 12:6Hili ndilo asemalo Bwana:

“Mwimbieni Yakobo kwa furaha,

mpigieni kelele aliye mkuu wa mataifa.

Zifanyeni sifa zenu zisikike, nanyi mseme,

‘Ee Bwana, okoa watu wako,

mabaki ya Israeli.’

831:8 Yer 3:18; Mwa 33:13; Za 106:47; Isa 42:16; Eze 34:16; 34:12-14Tazama, nitawaleta kutoka nchi ya kaskazini

na kuwakusanya kutoka miisho ya dunia.

Miongoni mwao watakuwepo vipofu na viwete,

mama wajawazito na wenye utungu wa kuzaa.

Umati mkubwa wa watu utarudi.

931:9 Ezr 3:12; Za 126:5; Isa 63:13; Za 126:5; Isa 63:13; 40:4; 49:11; Kut 4:22; Hes 20:8Watakuja wakilia;

wataomba wakati ninawarudisha.

Nitawaongoza kando ya vijito vya maji

katika mapito yaliyo tambarare ambapo hawatajikwaa,

kwa sababu mimi ndimi baba wa Israeli,

naye Efraimu ni mzaliwa wangu wa kwanza.

1031:10 Isa 66:19; Kum 30:4; Isa 11:12; 40:11; Eze 34:12; Yer 25:22; Law 26:33“Sikieni neno la Bwana, enyi mataifa,

litangazeni katika nchi za pwani ya mbali:

‘Yeye aliyewatawanya Israeli atawakusanya

na atalichunga kundi lake la kondoo kama mchungaji.’

1131:11 Kut 6:6; Isa 44:23; Za 142:6; 9:16Kwa kuwa Bwana atamlipia fidia Yakobo

na kuwakomboa mkononi mwa walio na nguvu kuliko wao.

1231:12 Eze 40:2; Mik 4:1; Yoe 3:18; Hes 18:12; Hos 2:21-22; Wim 4:15; Yn 16:22; Isa 58:11; Wim 4:15; Isa 30:19Watakuja na kupiga kelele kwa furaha katika miinuko ya Sayuni;

watashangilia ukarimu wa Bwana:

nafaka, divai mpya na mafuta,

wana-kondoo wachanga

na ndama wa makundi ya ngʼombe nitakaowapa.

Watakuwa kama bustani iliyonyeshewa vizuri,

wala hawatahuzunika tena.

1331:13 Isa 61:3; Za 30:11; Isa 51:11Kisha wanawali watacheza na kufurahi,

vijana waume na wazee pia.

Nitageuza maombolezo yao kuwa furaha,

nitawapa faraja na furaha badala ya huzuni.

1431:14 Law 7:35-36; Za 36:8; Isa 30:23Nitawashibisha makuhani kwa wingi,

nao watu wangu watajazwa kwa ukarimu wangu,”

asema Bwana.

1531:15 Yos 18:25; Mwa 37:35; Yer 10:20; Mt 2:17-18; Ay 7:21Hili ndilo asemalo Bwana:

“Sauti imesikika huko Rama,

maombolezo na kilio kikubwa,

Raheli akiwalilia watoto wake

na anakataa kufarijiwa,

kwa sababu watoto wake hawako tena.”

1631:16 Za 30:5; Isa 25:8; Rut 2:12; Eze 11:17-18; 2Nya 15:7; Yer 30:3; Isa 30:19Hili ndilo asemalo Bwana:

“Izuie sauti yako kulia,

na macho yako yasitoe machozi,

kwa kuwa kazi yako itapata thawabu,”

asema Bwana.

“Watarudi kutoka nchi ya adui.

17Kwa hiyo kuna tumaini kwa siku zijazo,”

asema Bwana.

“Watoto wako watarudi nchi yao yenyewe.

1831:18 Ay 5:17; Hos 4:16; 10:11; Za 80:3-4; Mao 5:21; Yer 50:11“Hakika nimeyasikia maombolezo ya Efraimu:

‘Ulinirudi kama ndama mkaidi,

nami nimekubali kutii.

Unirudishe, nami nitarudi,

kwa sababu wewe ndiwe Bwana, Mungu wangu.

1931:19 Za 95:10; Eze 36:31; 21:12; Lk 18:13; Yer 8:4; Ezr 9:6; Za 25:7Baada ya kupotea, nilitubu;

baada ya kuelewa, nilijipiga kifua.

Niliaibika na kuona haya

kwa sababu niliibeba aibu ya ujana wangu.’

2031:20 Isa 44:21; Hos 4:4; Mik 7:18; 1Fal 3:26; Mao 3:33; Isa 55:7Je, Efraimu si mwanangu mpendwa,

mtoto ninayependezwa naye?

Ingawa mara kwa mara ninanena dhidi yake,

bado ninamkumbuka.

Kwa hiyo moyo wangu unamwonea shauku,

nina huruma kubwa kwa ajili yake,”

asema Bwana.

2131:21 Isa 35:8; Yer 50:5; Isa 52:11; Yer 3:12; Eze 21:19“Weka alama za barabara,

weka vibao vya kuelekeza.

Zingatia vyema njia kuu,

barabara ile unayoipita.

Rudi, ee Bikira Israeli,

rudi kwenye miji yako.

2231:22 Yer 2:23; Hos 4:16; Isa 43:19; Kum 32:10Utatangatanga hata lini,

ee binti usiye mwaminifu?

Bwana ameumba kitu kipya duniani:

mwanamke atamlinda mwanaume.”

2331:23 Yer 30:18; Isa 1:26; Zek 8:3; Mwa 28:3; Hes 6:24; Isa 2:2; Za 48:1Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo, “Nitakapowarudisha toka nchi ya kutekwa kwenu, watu walio katika nchi ya Yuda na miji yake kwa mara nyingine tena watatumia maneno haya: ‘Bwana akubariki, ee makao ya haki, ee mlima mtakatifu.’ 2431:24 Yer 33:12, 18; Zek 8:4-8; Yer 30:18Watu wataishi pamoja katika Yuda na miji yake yote, wakulima na wote wanaohamahama na mifugo yao. 2531:25 Yn 4:14; Isa 40:29Nitawaburudisha waliochoka na kuwatuliza walio na huzuni.”

26Kwa jambo hili niliamka na kuangalia pande zote. Usingizi wangu ulikuwa mtamu kwangu.

2731:27 Eze 36:9-11; Hos 2:23; Yer 16:14Bwana asema, “Siku zinakuja, nitakapoongeza idadi ya watu, na kuzidisha hesabu ya mifugo katika nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda. 2831:28 Yer 18:8; 44:27; Kum 30; 9; Amo 9:14; Ay 29:2; Eze 36:10-11; Yer 1:10Kama vile nilivyowaangalia ili kungʼoa na kubomoa, kuharibu, kuangamiza na kuleta maafa juu yao, vivyo hivyo nitawaangalia ili kujenga na kupanda,” asema Bwana. 2931:29 Mwa 9:25; Kum 24:16; Eze 18:2; Mao 5:7“Katika siku hizo, watu hawatasema tena,

“ ‘Baba wamekula zabibu chachu,

nayo meno ya watoto yakatiwa ganzi.’

3031:30 2Fal 14:6; Gal 6:7; Isa 3:11Badala yake, kila mmoja atakufa kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe; yeyote alaye zabibu chachu, meno yake mwenyewe yatatiwa ganzi.

3131:31 Kum 29:14; Ebr 8:8-12; Yer 33:14; Lk 22:20; Isa 42:6; 54:10; Ebr 10:16-17“Siku zinakuja,” asema Bwana,

“nitakapofanya agano jipya

na nyumba ya Israeli

na nyumba ya Yuda.

3231:32 Kut 24:8; Kum 5:3; 1:31; Yer 11:4; Isa 54:5Halitafanana na agano

nililofanya na baba zao

wakati nilipowashika mkono

kuwaongoza watoke Misri,

kwa sababu walivunja agano langu,

ijapokuwa nilikuwa mume kwao,”

asema Bwana.

3331:33 Kum 6:6; 2Kor 3:3; Yer 24:7; Ebr 10:16; Za 40:8; Kut 4:15“Hili ndilo agano nitakalofanya na nyumba ya Israeli

baada ya siku zile,” asema Bwana.

“Nitaweka sheria yangu katika nia zao,

na kuiandika mioyoni mwao.

Nitakuwa Mungu wao,

nao watakuwa watu wangu.

3431:34 1Yn 2:27; Yn 6:45; Isa 54:13; Za 85:2; Mik 7:19; Rum 11:27; Isa 11:9Mtu hatamfundisha tena jirani yake,

wala mtu kumfundisha ndugu yake akisema, ‘Mjue Bwana Mungu,’

kwa sababu wote watanijua mimi,

tangu aliye mdogo kabisa kwao, hadi aliye mkuu sana,”

asema Bwana.

“Kwa sababu nitasamehe uovu wao,

wala sitazikumbuka dhambi zao tena.”

3531:35 Za 136:7-9; Mwa 1; 16; Yer 10:16; Kut 14:21; Za 93:3Hili ndilo asemalo Bwana,

yeye aliyeweka jua

liwake mchana,

yeye anayeamuru mwezi na nyota

kungʼaa usiku,

yeye aichafuaye bahari

ili mawimbi yake yangurume;

Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake:

3631:36 Ay 38:33; Isa 54:9-10; Za 89:36-37; Yer 33:20-26“Ikiwa amri hizi zitaondoka machoni pangu,”

asema Bwana,

“ndipo wazao wa Israeli watakoma

kuwa taifa mbele yangu daima.”

3731:37 Ay 38:5; Yer 33:22, 24, 26; Rum 11:1-5Hili ndilo asemalo Bwana:

“Ikiwa mbingu zilizo juu zitaweza kupimika

na misingi ya dunia chini

ikaweza kuchunguzwa,

ndipo nitakapowakataa wazao wote wa Israeli

kwa sababu ya yote waliyoyatenda,”

asema Bwana.

3831:38 Yer 30:18; Neh 3:1; 2Nya 25:23; Zek 14:10; Yer 24:6; 2Fal 14:13“Siku zinakuja,” asema Bwana, “wakati mji huu utajengwa upya kwa ajili yangu, kuanzia mnara wa Hananeli hadi Lango la Pembeni. 3931:39 1Fal 7:23Kamba ya kupimia itaanzia hapo kuendelea hadi kwenye kilima cha Garebu, na kisha kugeuka kuelekea Goa. 4031:40 Yer 2:23; 7:31-32; 1Sam 15:23; Yn 18:1; 2Fal 11:16; Yoe 3:17; Zek 14:21Bonde lote watupwapo maiti na majivu pia na matuta yote kutoka Bonde la Kidroni upande wa mashariki hadi pembe ya Lango la Farasi, itakuwa takatifu kwa Bwana. Kamwe mji huu hautangʼolewa tena wala kubomolewa.”

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

耶利米書 31:1-40

以色列人必回歸

1耶和華說:「那時,我要做以色列各宗族的上帝,他們必做我的子民。

2「逃脫刀兵之災的以色列人必在曠野蒙恩,

找到安息之所。

這是耶和華說的。」

3從前,耶和華向以色列顯現,說:

「我以永遠不變的愛愛你,

我以慈愛吸引你到我身邊。

4以色列人啊,

我要重建你們的家園,

你們要再次拿起鈴鼓與歡樂的人一同跳舞。

5你們將在撒瑪利亞的山上重新栽種葡萄園,

享受園中的果實。

6有一天,看守園子的人要在以法蓮的山上呼喊,

『我們上錫安朝見我們的上帝耶和華吧!』」

7耶和華說:

「你們要為雅各歡呼歌唱,

向列國之首喝采。

你們要傳揚頌讚,說,

『耶和華啊,

求你拯救以色列剩餘的子民!』

8看啊,我要從北方,

從地極招聚他們,

其中有瞎子、跛子、孕婦和產婦,

他們要成群結隊地回到這裡。

9我必引領他們回來,

他們必一路含淚禱告。

我要使他們走在溪水邊,

行在平坦的路上,

他們必不會跌倒,

因為我是以色列的父親,

以法蓮是我的長子。

10「列國啊,你們要聽耶和華的話,

要在遠方的海島宣揚,

『祂從前驅散以色列人,

如今必再聚集、保護他們,

好像牧人看守自己的羊群一樣。』

11耶和華必拯救雅各的子孫,

從強敵手中救出他們。

12他們必來到錫安山上歡呼,

為耶和華所賜的五穀、新酒、

油、羔羊和牛犢而歡欣。

他們就像水源充足的田園,

一無所缺。

13那時,少女要歡然起舞,

老人和青年要一起快樂。

我要使他們轉憂為喜,

我要安慰他們,使他們歡喜,

不再憂愁。

14我要使祭司有充足的供應,

使我的子民飽享美物。

這是耶和華說的。」

15耶和華說:

「在拉瑪有痛哭哀號的聲音,

拉結在為兒女哀痛,

不肯接受安慰,

因為他們都死了。」

16耶和華說:

「不要哭泣,不要流淚,

因為你的勞苦必有回報,

你的兒女必從敵國回來。

這是耶和華說的。

17你將來必有盼望,

你的兒女必重返家園。

這是耶和華說的。

18我聽見以法蓮31·18 以法蓮」是北國以色列的主要支派,常用來代指北國以色列。在為自己悲歎,

『我們就像未經馴服的牛犢,

你管教我們,使我們順服,

求你使我們回到你身邊,

重新復興,

因為你是我們的上帝耶和華。

19我們曾經離開你,

但我們後悔了;

我們醒悟之後捶胸頓足,

痛悔不已,

因早年的所作所為而羞愧難當。』」

20耶和華說:「以法蓮不是我的愛子嗎?

他不是我喜悅的孩子嗎?

我雖然常常責備他,

但仍然惦記著他。

我深深地想念他,

我必憐憫他。

21以色列人啊,

你們要為自己設置路標,

豎起路牌,

牢記你們走過的大道。

以色列人啊,

回來吧!回到你們的城邑吧!

22不忠貞的子民啊!

你們四處流浪要到何時呢?

耶和華在地上行了一件新事——女子將要護衛男子。」

23以色列的上帝——萬軍之耶和華說:「我使被擄的猶大人回到故鄉後,他們要在猶大各城邑再次呼喊,

『公義的居所啊,

聖山啊,願耶和華賜福給你!』

24「農夫和牧人必住在猶大的各城邑。 25我要使疲乏的人振作起來,使苦悶的人快樂起來。」

26這時,我醒過來,覺得這一覺實在香甜。

27耶和華說:「看啊,時候將到,我要使以色列猶大人丁興旺,牲畜繁多。 28我曾決意剷除、拆毀、推翻、剿滅他們,降災給他們,將來我必塑造、栽培他們。這是耶和華說的。 29那時,人再不會說,

『父親吃酸葡萄,

兒子的牙酸倒了。』

30因為各人都要承擔自己的罪,誰吃酸葡萄,誰的牙酸倒。」 31耶和華說:「看啊,時候將到,我要與以色列家和猶大家另立新約, 32這約不同於我與他們祖先所立的約,就是我牽著他們祖先的手領他們離開埃及時所立的。雖然我是他們的丈夫,他們卻違背了我的約。這是耶和華說的。」

33耶和華說:「那些日子以後,我將與以色列家立這樣的約,我要把我的律法放在他們腦中,寫在他們心上。我要做他們的上帝,他們要做我的子民。 34誰都無需再教導他的鄰居和弟兄,說,『你要認識耶和華』,因為他們無論尊卑都必認識我。我要赦免他們的過犯,忘掉他們的罪惡。這是耶和華說的。」

35使陽光白天照耀、

星月晚上發光、

大海波濤洶湧的萬軍之耶和華說:

36「只要天地之律還在,

以色列邦國必永續不斷。

這是耶和華說的。」

37耶和華說:

「正如無人能量度高天,

探測大地的根基,

同樣我也決不會因以色列人的所作所為而棄絕他們。

這是耶和華說的。」

38耶和華說:「看啊,時候將到,從哈楠業樓直到角門,整個耶路撒冷城要重建起來歸給耶和華。 39城界要向外延伸到迦立山,再轉到歌亞40甚至拋屍、倒灰的整個山谷,以及從汲淪溪到東邊馬門拐角的所有田地都要歸給耶和華作聖地,永不再被傾覆、毀滅。」