Yeremia 29 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 29:1-32

Barua Kwa Watu Wa Uhamisho

129:1 2Nya 36:10; Yer 13:1729:1 Eze 39:25; Rum 10:20; Sef 3:20; Yer 46:27; Eze 37:21; Kum 30:3; Yer 30:3Haya ndiyo maneno ya ile barua ambayo nabii Yeremia aliituma kutoka Yerusalemu kwenda kwa wazee waliobaki miongoni mwa wale waliohamishwa, na kwa makuhani, manabii na watu wengine wote ambao Nebukadneza alikuwa amewachukua kwenda uhamishoni Babeli kutoka Yerusalemu. 229:2 2Fal 24:12; Yer 22:24-28; 2Fal 24:8(Hii ilikuwa ni baada ya Mfalme Yekonia29:2 Yekonia au Konia ni jina jingine la Yehoyakini. na malkia mamaye, maafisa wa mahakama, viongozi wa Yuda na wa Yerusalemu, mafundi na wahunzi kwenda uhamishoni kutoka Yerusalemu.) 3Barua ilikabidhiwa kwa Elasa mwana wa Shafani, na kwa Gemaria mwana wa Hilkia, ambao Sedekia mfalme wa Yuda aliwatuma kwa Mfalme Nebukadneza huko Babeli. Barua yenyewe ilisema:

429:4 Yer 24:5Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, awaambialo wale wote niliowapeleka kutoka Yerusalemu kwenda uhamishoni Babeli: 5“Jengeni nyumba na mstarehe, pandeni bustani na mle mazao yake. 629:6 Yer 30:19Oeni wake na mzae wana na binti, waozeni wana wenu wake, nanyi watoeni binti zenu waolewe, ili nao pia wazae wana na binti. Ongezekeni idadi yenu huko, wala msipungue. 729:7 Ebr 6:10; 1Tim 2:1-2; Rum 13:1-5; Es 3:8Pia tafuteni amani na mafanikio ya mji ambamo nimewapeleka uhamishoni. Mwombeni Bwana kwa ajili ya mji huo, kwa sababu ukistawi, ninyi pia mtastawi.”

829:8 Yer 37:9; 23:21-27; 1Yn 4:1; Kum 13:1Naam, hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Msikubali manabii na wabashiri walioko miongoni mwenu wawadanganye. Msisikilize ndoto ambazo mmewatia moyo kuota. 929:9 Mao 2:14; Eze 13:6; Yer 27:15; 23:21Wanawatabiria ninyi uongo kwa jina langu. Sikuwatuma,” asema Bwana.

1029:10 2Nya 36:21; Dan 9:2; Yer 16:14; 24:6; 32:42; 1Fal 8:56Hili ndilo asemalo Bwana: “Miaka sabini itakapotimia kwa ajili ya Babeli, nitakuja kwenu na kutimiza ahadi yangu ya rehema ya kuwarudisha mahali hapa. 1129:11 Za 40:5; Zek 8:15; Isa 55:12Kwa maana ninajua mipango niliyo nayo kwa ajili yenu,” asema Bwana, “ni mipango ya kuwafanikisha na wala si ya kuwadhuru, ni mipango ya kuwapa tumaini katika siku zijazo. 1229:12 Za 145:19; Isa 55:6; Dan 9:3; Hos 2:23; Sef 3:12; Zek 13:9Kisha mtaniita, na mtakuja na kuniomba, nami nitawasikiliza. 1329:13 Mt 7:7; Kum 4:29; 2Nya 6:37; Yer 24:7Mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote. 14Nitaonekana kwenu,” asema Bwana, “nami nitawarudisha watu wenu waliotekwa. Nitawakusanya kutoka mataifa yote na mahali pote nilipokuwa nimewafukuzia, nami nitawarudisha mahali ambapo nilikuwa nimewatoa walipochukuliwa uhamishoni,” asema Bwana.

15Mnaweza mkasema, “Bwana ameinua manabii kwa ajili yetu huku Babeli,” 16lakini hili ndilo asemalo Bwana kuhusu mfalme aketiaye kiti cha enzi cha Daudi, na watu wa kwenu wote wanaobaki katika mji huu, ndugu zenu ambao hawakwenda pamoja nanyi uhamishoni. 1729:17 Yer 24:8-10; 27:8; Isa 5:4Naam, hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Nitatuma upanga, njaa na tauni dhidi yao, nami nitawafanya kuwa kama tini dhaifu zile ambazo ni mbovu sana zisizofaa kuliwa. 1829:18 Yer 15:4; Kum 28:25; Yer 42:18; Mao 2:18-19; Hes 5:27; Yer 18:16; Isa 28:22Nitawafukuza kwa upanga, kwa njaa na kwa tauni, nami nitawafanya kitu cha kuchukiza sana kwa falme zote za dunia, na kuwa kitu cha laana na cha kuogofya, cha dharau na kukemewa, miongoni mwa mataifa yote nitakakowafukuzia. 1929:19 Yer 6:19; 32:33; 25:4; 7:25Kwa kuwa hawakuyasikiliza maneno yangu,” asema Bwana, “maneno ambayo niliwatumia tena na tena kupitia watumishi wangu manabii. Wala ninyi watu wa uhamisho hamkusikiliza pia,” asema Bwana.

2029:20 Yer 24:5; Amo 3:6; Mik 4:10Kwa hiyo, sikieni neno la Bwana, enyi nyote mlio uhamishoni, niliowapeleka Babeli kutoka Yerusalemu. 2129:21 Yer 14:14Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo kuhusu Ahabu mwana wa Kolaya, na Sedekia mwana wa Maaseya, wanaowatabiria uongo kwa jina langu: “Nitawatia mikononi mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli, naye atawaua mbele ya macho yenu hasa. 2229:22 Dan 3:6; Isa 65:15Kwa ajili yao, watu wote wa uhamisho kutoka Yuda walioko Babeli watatumia laana hii: ‘Bwana na akutendee kama Sedekia na Ahabu, ambao mfalme wa Babeli aliwachoma kwa moto.’ 2329:23 Yer 23:14; Ebr 4:13; Yer 13:27; Sef 3:4; Mwa 31:48; Yer 7:11Kwa kuwa wamefanya mambo maovu kabisa katika Israeli, wamezini na wake za majirani zao, tena kwa Jina langu wamesema uongo, mambo ambayo sikuwaambia kuyafanya. Nami nayajua haya, na ni shahidi wa jambo hilo,” asema Bwana.

Ujumbe Kwa Shemaya

24Mwambie Shemaya Mnehelami, 2529:25 2Fal 25:18; Yer 21:1“Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Ulituma barua kwa jina lako mwenyewe kwa watu wote wa Yerusalemu, kwa Sefania mwana wa kuhani Maaseya na kwa makuhani wengine wote. Ulimwambia Sefania, 2629:26 Kum 13:1-5; 1Sam 10:11; 2Fal 9:11; Yer 20:2; Yn 10:20; Hos 9:7Bwana amekuweka wewe uwe kuhani badala ya Yehoyada ili uwe msimamizi wa nyumba ya Bwana. Unapaswa kufunga kwa mikatale na mnyororo wa shingoni mwendawazimu yeyote anayejifanya nabii. 27Kwa nini basi hukumkemea Yeremia Mwanathothi, aliyejifanya kama nabii miongoni mwenu? 28Ametutumia ujumbe huu huku Babeli: Mtakuwako huko muda mrefu. Kwa hiyo jengeni nyumba mkakae; pandeni mashamba na mle mazao yake.’ ”

29Kuhani Sefania, hata hivyo, akamsomea nabii Yeremia ile barua. 30Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia kusema: 3129:31 Yer 14:14; 28:15“Tuma ujumbe huu kwa watu wote walio uhamishoni: ‘Hili ndilo Bwana asemalo kuhusu Shemaya Mnehelami: Kwa sababu Shemaya amewatabiria ninyi, hata ingawa sikumtuma, naye amewafanya kuamini uongo, 3229:32 1Sam 2:30-33; Yer 28:16; Rum 2:8hili ndilo Bwana asemalo: Hakika nitamwadhibu Shemaya Mnehelami pamoja na uzao wake. Hapatakuwa na yeyote atakayebaki miongoni mwa watu hawa, wala hataona mema nitakayowatendea watu wangu, asema Bwana, kwa sababu ametangaza uasi dhidi yangu.’ ”

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

耶利米書 29:1-32

致信給被擄的人

1-2耶哥尼雅王、太后、宮廷侍臣、猶大耶路撒冷的官員、技工和工匠被尼布甲尼撒王擄到巴比倫後,耶利米先知從耶路撒冷寄信給被擄之人中倖存的長老、先知和眾民。 3猶大西底迦沙番的兒子以利亞薩希勒迦的兒子基瑪利把這封信送給巴比倫尼布甲尼撒。以下是信的內容:

4以色列的上帝——萬軍之耶和華對所有從耶路撒冷被擄到巴比倫的人說: 5「你們要建造房子住下來,要耕種田園,吃田中的出產。 6你們要娶妻生子,也要給你們的兒女娶妻選夫,使他們生兒育女,你們好在那裡人丁興旺,不致人口減少。 7你們要為所住的城市謀求福祉,向耶和華禱告,因為你們的福祉有賴於那城的福祉。」 8以色列的上帝——萬軍之耶和華說:「不要被你們中間的先知和占卜者欺騙,不要聽信他們做的夢。 9他們以我的名義對你們說假預言,其實我並沒有差遣他們。這是耶和華說的。」

10耶和華說:「你們被擄到巴比倫七十年期滿後,我就要眷顧你們,成就我充滿恩典的應許,把你們帶回這地方。 11因為我知道我為你們安排的計劃。我的計劃不是要降禍給你們,而是要賜福給你們,使你們的未來充滿希望。這是耶和華說的。 12那時,你們必呼求我,向我禱告,我也必垂聽。 13你們尋求我,就必尋見。只要你們全心尋求我, 14我必讓你們尋見。這是耶和華說的。我必把你們從流放之地招聚起來,使你們回到故土。這是耶和華說的。

15「你們說耶和華在巴比倫為你們選立了先知, 16但論到坐在大衛寶座上的君王和這城裡的百姓,就是沒有與你們一同被擄的同胞, 17萬軍之耶和華這樣說,『看啊,我必使戰爭、饑荒和瘟疫臨到他們,使他們像爛得不能吃的無花果。 18我要使他們飽受戰爭、饑荒和瘟疫之災,使他們的遭遇令天下萬國驚懼。在我流放他們去的地方,他們必受凌辱、嘲笑、譏諷和咒詛。 19這都是因為他們不聽我的話。這是耶和華說的。我曾屢次差遣我的僕人——眾先知去警告他們,他們卻不肯聽。』這是耶和華說的。 20因此,你們這些從耶路撒冷被擄到巴比倫的人啊!要聽耶和華的話。 21以色列的上帝——萬軍之耶和華說:『哥賴雅的兒子亞哈瑪西雅的兒子西底迦以我的名義說假預言,我要把他們交在巴比倫尼布甲尼撒的手中,讓他當著你們的面處死他們。 22被擄到巴比倫猶大人咒詛人的時候會說,「願耶和華使你的下場像被巴比倫王燒死的西底迦亞哈一樣!」 23因為他們二人在以色列做了惡事,與他人的妻子通姦。我沒有差派他們,他們卻奉我的名說假預言。我知道他們的所作所為,我對這一切瞭若指掌。』這是耶和華說的。」

24耶和華吩咐我對尼希蘭示瑪雅說: 25以色列的上帝——萬軍之耶和華說,你曾以自己的名義寫信給住在耶路撒冷的眾民、瑪西雅的兒子西番雅祭司及其他祭司。你在信中對西番雅說, 26『耶和華已立你為祭司代替耶何耶大,管理耶和華的殿,負責拘捕妄自發預言的狂人,給他們戴上鐵鏈枷鎖。 27現在,亞拿突耶利米在你們當中自稱為先知,你為什麼不斥責他呢? 28他甚至寄信給我們這些在巴比倫的人,說被擄的日子還很長久,要我們建房子住下來,耕種田園,吃田中的出產。』」

29西番雅祭司就把示瑪雅的信讀給耶利米先知聽。 30耶和華對耶利米說: 31「你派人送信給所有被擄的人,說,『耶和華說祂沒有差遣尼希蘭示瑪雅,他卻說預言,誘使你們聽信謊言, 32所以耶和華必懲罰他和他的後代,使他斷子絕孫,看不到耶和華賜給祂子民的福祉,因為他說了悖逆耶和華的話。這是耶和華說的。』」