Yeremia 16 – NEN & CST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 16:1-21

Siku Ya Maafa

1Kisha neno la Bwana likanijia: 216:2 Mwa 19:14; Mt 19:12; 1Kor 7:26-27“Kamwe usioe na kuwa na wana wala binti mahali hapa.” 316:3 Yer 6:21Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana kuhusu wana na binti wazaliwao katika nchi hii, na kuhusu wale wanawake ambao ni mama zao, na wale wanaume ambao ni baba zao: 416:4 Yer 25:33; 9:22; Za 83:10; Kum 28:26; Za 79:1-3; Yer 14:15; 19:7“Watakufa kwa magonjwa ya kufisha. Hawataombolezewa wala kuzikwa, lakini watakuwa kama mavi yaliyosambaa juu ya ardhi. Watakufa kwa upanga na kwa njaa, nazo maiti zao zitakuwa chakula cha ndege wa angani, na cha wanyama wa nchi.”

5Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana: “Usiingie katika nyumba ambayo kuna chakula cha matanga, usiende kuwaombolezea wala kuwahurumia, kwa sababu nimeziondoa baraka zangu, upendo wangu na huruma zangu kutoka kwa watu hawa,” asema Bwana. 616:6 Yer 9:21; Eze 9:5-6; Law 19:28; 21:5; Isa 22:12; 1:20“Wakubwa na wadogo watakufa katika nchi hii. Hawatazikwa wala kuombolezewa, na hakuna atakayejikatakata au kunyoa nywele za kichwa chake kwa ajili yao. 716:7 Mit 3:6; Eze 24:17; Hos 9:4; 2Sam 3:35; Yer 22:10; Mao 1:9, 16Hakuna yeyote atakayewapa chakula ili kuwafariji wale waombolezao kwa ajili ya wale waliokufa, hata akiwa amefiwa na baba au mama, wala hakuna yeyote atakayewapa kinywaji ili kuwafariji.

816:8 Kut 32:6; Mhu 7:2-4; Yer 15:17“Usiingie katika nyumba ambayo kuna karamu, na kuketi humo ili kula na kunywa. 916:9 Isa 51:3; Amo 6:4-7; Yer 7:34; Isa 22:12-14; Ufu 18:23; Eze 26:13Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliye Mungu wa Israeli: ‘Mbele ya macho yako na katika siku zako, nitakomesha sauti zote za shangwe na za furaha, na pia sauti za bibi arusi na bwana arusi mahali hapa.’

1016:10 Kum 29:24; Yer 5:19“Utakapowaambia watu hawa mambo haya yote na wakakuuliza, ‘Kwa nini Bwana ameamuru maafa makubwa kama haya dhidi yetu? Tumefanya kosa gani? Tumetenda dhambi gani dhidi ya Bwana, Mungu wetu?’ 1116:11 Amu 2:12-13; Za 106:35-43; 1Fal 9:9; Neh 9:26-29; Ay 31:27; Kum 29:25-26Basi waambie, ‘Ni kwa sababu baba zenu waliniacha mimi, wakafuata miungu mingine ili kuitumikia na kuiabudu. Waliniacha mimi na hawakuishika sheria yangu,’ asema Bwana. 1216:12 Kut 32:8; Amo 2:4; Mhu 9:3; Yer 13:10; 2Tim 3:13; Yer 7:26; Eze 20:30‘Lakini ninyi mmetenda uovu zaidi kuliko baba zenu. Tazama jinsi ambavyo kila mmoja wenu anafuata ukaidi wa moyo wake mbaya, badala ya kunitii mimi. 1316:13 Kum 4:26-28; Yer 15:4-5; 2Nya 20:7; Yer 5:19; Kum 28:36Kwa hiyo nitawaondoa katika nchi hii na kuwatupa katika nchi ambayo ninyi wala baba zenu hamkuijua, nako huko mtaitumikia miungu mingine usiku na mchana, kwa maana sitawapa fadhili zangu huko.’

1416:14 Kum 15:15; Yer 23:7-8; 29:10; 31:27, 38; 30:3“Hata hivyo, siku zinakuja,” asema Bwana, “wakati ambapo watu hawatasema tena, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewapandisha Waisraeli kutoka Misri,’ 1516:15 Isa 11:11-12; Za 53:6; Yer 3:18; 23:8; 30:3; Eze 38:14; Yoe 3:1; Kum 30:3bali watasema, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewatoa wana wa Israeli kutoka nchi ya kaskazini na nchi zote alizokuwa amewafukuzia.’ Maana nitawarudisha katika nchi niliyowapa baba zao.

1616:16 Amo 4:2; Hab 1:14-15; Amo 9:3; Mik 7:2; 1Sam 26:20“Lakini sasa nitawaagiza wavuvi wengi,” asema Bwana, “nao watawavua. Baada ya hilo, nitawaagizia wawindaji wengi, nao watawawinda kwenye kila mlima na kilima, na katika nyufa za miamba. 1716:17 Mhu 12:14; Mk 4:22; Mit 5:21; Sef 1:12; Yer 32:19; Mwa 3:8; Ebr 4:13Macho yangu yanaziona njia zao zote, hazikufichika kwangu, wala dhambi yao haikusitirika. 1816:18 Hes 35:34; Isa 40:2; Eze 43:7; Ufu 18:6; Isa 65:6; Yer 12:3; Za 101:3Nitawalipiza maradufu kwa ajili ya uovu wao na dhambi yao, kwa sababu wameinajisi nchi yangu kwa maumbo yasiyo na uhai ya vinyago vyao vibaya, na kuujaza urithi wangu na sanamu za kuchukiza.”

1916:19 Yer 3:17; Za 4:2; Isa 2:2; Za 18:2; 2Sam 22:3; Yer 14:22; Isa 40:19; 1Sam 12:21Ee Bwana, nguvu zangu na ngome yangu,

kimbilio langu wakati wa taabu,

kwako mataifa yatakujia

kutoka miisho ya dunia na kusema,

“Baba zetu hawakuwa na chochote zaidi ya miungu ya uongo,

sanamu zisizofaa kitu

ambazo hazikuwafaidia lolote.

2016:20 Isa 37:19; Rum 1:23; Gal 4:8; Za 115:4-7; Yer 2:11Je, watu hujitengenezea miungu yao wenyewe?

Naam, lakini hao si miungu!”

2116:21 Kut 3:15“Kwa hiyo nitawafundisha:

wakati huu nitawafundisha

nguvu zangu na uwezo wangu.

Ndipo watakapojua

kuwa Jina langu ndimi Bwana.

Nueva Versión Internacional (Castilian)

Jeremías 16:1-21

Mensaje de juicio

1La palabra del Señor vino a mí, y me dijo: 2«No te cases, ni tengas hijos ni hijas en este lugar». 3Porque así dice el Señor en cuanto a los hijos y las hijas que han nacido en este lugar, y en cuanto a las madres que los dieron a luz y los padres que los engendraron en este país: 4«Morirán de enfermedades horribles. Nadie llorará por ellos ni los sepultará; se quedarán sobre la faz de la tierra, como el estiércol. La espada y el hambre acabarán con ellos, y sus cadáveres servirán de alimento para las aves del cielo y para las bestias de la tierra».

5Así dice el Señor: «No entres en una casa donde estén de luto, ni vayas a llorar, ni los consueles, porque a este pueblo le he retirado mi paz, mi amor y mi compasión —afirma el Señor—. 6En este país morirán grandes y pequeños; nadie llorará por ellos ni los sepultará; nadie se hará heridas en el cuerpo ni se rapará la cabeza por ellos. 7Nadie ofrecerá un banquete fúnebre a los que estén de duelo para consolarlos por el muerto ni a nadie se le dará a beber la copa del consuelo, aun cuando quien haya muerto sea su padre o su madre.

8»No entres en una casa donde haya una celebración, ni te sientes con ellos a comer y beber. 9Porque así dice el Señor Todopoderoso, el Dios de Israel: Voy a poner fin en este lugar a toda expresión de alegría y de regocijo, y al cántico del novio y de la novia. Esto sucederá en vuestros propios días, y vosotros lo veréis.

10»Cuando anuncies a este pueblo todas estas cosas, ellos te preguntarán: “¿Por qué ha decretado el Señor contra nosotros esta calamidad tan grande? ¿Cuál es nuestra iniquidad? ¿Qué pecado hemos cometido contra el Señor nuestro Dios?” 11Entonces les responderás: “Esto es porque vuestros antepasados me abandonaron y se fueron tras otros dioses, y los sirvieron y los adoraron. Me abandonaron, y no cumplieron mi ley —afirma el Señor—. 12Pero vosotros os habéis comportado peor que vuestros antepasados. Cada uno sigue la terquedad de su corazón malvado, y no me ha obedecido. 13Por eso os voy a arrojar de esta tierra, a un país que ni vosotros ni vuestros antepasados habéis conocido, y allí serviréis a otros dioses día y noche. No os tendré clemencia”.

14»Por eso —afirma el Señor—, vienen días en que ya no se dirá: “Por la vida del Señor, que hizo salir a los israelitas de la tierra de Egipto”, 15sino: “Por la vida del Señor, que hizo salir a los israelitas de la tierra del norte, y de todos los países adonde los había expulsado”. Yo los haré volver a su tierra, la que antes di a sus antepasados.

16»Voy a enviar a muchos pescadores —afirma el Señor—, y ellos los pescarán. Después, enviaré a muchos cazadores, y ellos los cazarán por todas las montañas y colinas, y por las grietas de las rocas. 17Ciertamente mis ojos ven todas sus acciones; ninguna de ellas me es oculta. Su iniquidad no puede esconderse de mi vista. 18Primero les pagaré el doble por su iniquidad y su pecado, porque con los cadáveres de sus ídolos detestables han profanado mi tierra, y han llenado mi herencia con sus abominaciones».

19Señor, fuerza y fortaleza mía,

mi refugio en el día de la angustia:

desde los confines de la tierra

vendrán a ti las naciones, y dirán:

«Solo mentira heredaron nuestros antepasados;

heredaron lo absurdo,

lo que no sirve para nada.

20¿Acaso puede el hombre hacer sus propios dioses?

¡Pero si no son dioses!»

21«Por eso, esta vez les daré una lección;

les daré a conocer mi mano poderosa.

¡Así sabrán que mi nombre es el Señor!