Yeremia 14 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 14:1-22

Ukame, Njaa Na Upanga

1Hili ndilo neno la Bwana kwa Yeremia kuhusu ukame:

214:2 Isa 3:26; Yer 8:21; Mit 21:13“Yuda anaomboleza,

miji yake inayodhoofika;

wanaomboleza kwa ajili ya nchi,

nacho kilio kinapanda kutoka Yerusalemu.

314:3 Kum 28:48; 2Fal 18:31; 2Sam 15:30; Es 6:12; Ay 6:19-20Wakuu wanawatuma watumishi wao maji;

wanakwenda visimani

lakini humo hakuna maji.

Wanarudi na vyombo bila maji;

wakiwa na hofu na kukata tamaa,

wanafunika vichwa vyao.

414:4 Amo 4:8; Zek 14:17; Yer 3:3; 12:11Ardhi imepasuka nyufa

kwa sababu hakuna mvua katika nchi;

wakulima wana hofu

na wanafunika vichwa vyao.

514:5 Isa 15:6Hata kulungu mashambani

anamwacha mtoto wake aliyezaliwa wakati huo huo

kwa sababu hakuna majani.

614:6 Ay 39:5-6; Yer 2:24; Za 104:11; Mwa 47:4Punda-mwitu wanasimama juu ya miinuko iliyo kame

na kutweta kama mbweha;

macho yao yanakosa nguvu za kuona

kwa ajili ya kukosa malisho.”

714:7 Isa 3:9; Hos 5:5; Yer 2:19; 8:14; Za 25:11; 79:9; 1Sam 12:22Ingawa dhambi zetu zinashuhudia juu yetu,

Ee Bwana, tenda jambo kwa ajili ya jina lako.

Kwa kuwa kukengeuka kwetu ni kukubwa,

nasi tumetenda dhambi dhidi yako.

814:8 Za 9:18; Mdo 28:20; Yer 17:13; 50:7; Za 18:46; Isa 25:9Ee Tumaini la Israeli,

Mwokozi wake wakati wa taabu,

kwa nini unakuwa kama mgeni katika nchi,

kama msafiri anayekaa kwa usiku mmoja tu?

914:9 Isa 50:2; Mwa 17:7; Yer 8:19; 15:16; Kut 29:45; Isa 63:19; Za 27:9Mbona unakuwa kama mtu aliyeshtukizwa,

kama shujaa asiye na uwezo wa kuokoa?

Wewe uko katikati yetu, Ee Bwana,

nasi tunaitwa kwa jina lako;

usituache!

1014:10 Yer 2:25; Za 119:101; Yer 6:20; Hes 8:13; Ebr 8:12; Amo 5:22; Hos 7:2; 9:9; Yer 44:21Hili ndilo Bwana asemalo kuhusu watu hawa:

“Wanapenda sana kutangatanga,

hawaizuii miguu yao.

Hivyo Bwana hawakubali;

sasa ataukumbuka uovu wao

na kuwaadhibu kwa ajili ya dhambi zao.”

1114:11 Kut 32:10; 1Sam 2:25Kisha Bwana akaniambia, “Usiombe kwa ajili ya mafanikio ya watu hawa. 1214:12 Kum 1:45; 1Sam 8:18; Yer 7:21; Law 1:1-17; Yer 11:11; Amo 5:22; Isa 51:19; Yer 9:16Ingawa wanafunga, sitasikiliza kilio chao; hata wakitoa dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za nafaka, sitazikubali. Badala yake, nitawaangamiza kwa upanga, njaa na tauni.”

13Lakini nikasema, “Aa, Bwana Mwenyezi, manabii wanaendelea kuwaambia, ‘Hamtaona upanga wala kukabiliwa na njaa. Naam, nitawapa amani ya kudumu mahali hapa.’ ”

1414:14 Yer 23:25; 2The 2:9-11; Eze 13:2-6; Yer 23:16; Mao 2:9; Eze 12:24; Yer 27:14Ndipo Bwana akaniambia, “Manabii wanatabiri uongo kwa jina langu. Sikuwatuma, wala sikuwaweka, wala sikusema nao. Wanawatabiria maono ya uongo, maaguzi, maono ya sanamu zisizofaa kitu, na madanganyo ya mawazo yao wenyewe. 1514:15 Yer 20:6; Eze 14:9; Yer 16:4; Mao 1:19; Yer 23:15; 5:12-13Kwa hiyo, hili ndilo Bwana asemalo kuhusu manabii wanaotabiri kwa jina langu: Mimi sikuwatuma, lakini wanasema, ‘Hakuna upanga wala njaa itakayoigusa nchi hii.’ Manabii hao hao watakufa kwa upanga na njaa. 1614:16 Yer 17:10; Mit 1:31; Yer 7:33; Za 79:3; Mt 15:14Nao watu hao wanaowatabiria watatupwa nje katika barabara za Yerusalemu kwa sababu ya njaa na upanga. Hapatakuwepo yeyote wa kuwazika wao au wake zao, wana wao au binti zao. Nitawamwagia maafa wanayostahili.

1714:17 Za 119:136; Yer 8:21; Mao 1:16; 2Fal 19:21; Yer 23:12“Nena nao neno hili:

“ ‘Macho yangu na yatiririkwe na machozi

usiku na mchana bila kukoma;

kwa kuwa binti yangu aliye bikira, yaani watu wangu,

amepata jeraha baya,

pigo la kuangamiza.

1814:18 Eze 7:14-15; 2Nya 36:10; Yer 13:17Kama nikienda mashambani,

ninaona wale waliouawa kwa upanga;

kama nikienda mjini,

ninaona maangamizi ya njaa.

Nabii na kuhani kwa pamoja

wamekwenda katika nchi wasiyoijua.’ ”

1914:19 Yer 7:29; 30:12-13; 8:15; Isa 1:6Je, umemkataa Yuda kabisa?

Umemchukia Sayuni kabisa?

Kwa nini umetuumiza

hata hatuwezi kuponyeka?

Tulitarajia amani,

lakini hakuna jema lililotujia;

tulitarajia wakati wa kupona

lakini kuna hofu kuu tu.

2014:20 Amu 10:10; Dan 9:7-8; Yer 3:13; Law 26:40; 1Fal 8:47; Ezr 9:6Ee Bwana, tunatambua uovu wetu

na kosa la baba zetu;

kweli tumetenda dhambi dhidi yako.

2114:21 Yer 17:12; Yos 7:9; Isa 62:7; Yer 3:17; Kut 2:24Kwa ajili ya jina lako usituchukie kabisa;

usikidharau kiti chako cha enzi kilichotukuka.

Kumbuka agano lako nasi

na usilivunje.

2214:22 1Fal 8:36; Isa 30:23; Za 135:7; Isa 41:24; 44:10; Yer 10:15Je, kuna sanamu yoyote isiyofaa kitu ya mataifa

iwezayo kuleta mvua?

Je, anga peke yake zaweza kutoa mvua?

La hasha, ni wewe peke yako,

Ee Bwana, Mungu wetu.

Kwa hiyo tumaini letu liko kwako,

kwa kuwa wewe ndiwe ufanyaye haya yote.

Swedish Contemporary Bible

Jeremia 14:1-22

Den svåra torkan, klagan och bön

1Det här är Herrens ord till Jeremia om torkan:

2”Juda sörjer.

Dess stadsportar sjunker ihop,

de böjer sig sörjande mot jorden.

Ett klagorop stiger upp från Jerusalem.

3De mäktiga skickar sina tjänare

för att hämta vatten,

men när de kommer till dammarna

finner de inget vatten.

De kommer tillbaka med tomma kärl,

besvikna och nedstämda,

och täcker sina huvuden.

4Marken är sprucken

av brist på regn i landet.

Bönderna är besvikna

och täcker sina huvuden.

5Också hinden på fältet överger

sin nyfödda kalv

därför att det inte finns något gräs.

6Vildåsnorna står på de kala höjderna

och flämtar som schakaler.

Deras ögon är matta,

för det finns inget gräs.”

7Våra missgärningar vittnar mot oss,

men grip ändå in, Herre,

för ditt eget ryktes skull!

Många gånger har vi fallit

och syndat mot dig.

8Du Israels hopp,

dess räddare i tider av nöd,

varför är du som en främling i landet,

som en vandrare som bara stannar över natten?

9Varför står du som en handfallen,

som en krigare som inte kan rädda?

Herre, du finns ju mitt ibland oss,

och vi bär ditt namn.

Överge oss inte!

10Så säger Herren om detta folk:

”De älskar att vandra omkring,

de håller inte sina fötter i styr.

Därför accepterar Herren dem inte mer.

Han minns nu deras skuld

och ska straffa dem för deras synder.”

11Herren sa till mig: ”Be inte om något gott för det här folket. 12Även om de fastar, ska jag inte lyssna till deras rop. När de offrar brännoffer och matoffer kommer jag inte att ta emot dem. I stället ska jag göra slut på dem med svärd, hungersnöd och pest.”

13Då sa jag: ”Min Herre, Herre, profeterna säger till dem att inget svärd eller någon hungersnöd ska drabba dem, utan du kommer att ge dem bestående fred på denna plats.”

14Då sa Herren till mig: ”Profeterna profeterar lögner i mitt namn. Jag har inte sänt dem eller befallt dem att tala eller gett dem några budskap. De profeterar för er falska syner, meningslösa spådomar och sina egna påhitt. 15Därför säger Herren om dessa profeter, som profeterar i mitt namn fastän jag inte har sänt dem, de som säger att varken svärd eller hungersnöd ska drabba detta land: Genom svärd och hungersnöd kommer dessa profeter själva att gå under. 16De som de profeterade för ska bli liggande på Jerusalems gator som offer för svält och svärd, och ingen ska begrava dem, varken dem själva, deras hustrur, söner eller döttrar. Jag ska låta deras egen ondska drabba dem.

17Säg detta till dem:

’Natt och dag

strömmar tårar från mina ögon,

oupphörligt.

Mitt folk, min arma dotter,

har drabbats av ett förkrossande slag,

av ett helt obotligt sår.

18Om jag går ut på fälten

ser jag dem som fallit för svärd.

Kommer jag in i staden

ser jag svältens härjningar.

Även präster och profeter

irrar rådlösa omkring i landet.14:18 Grundtextens innebörd är osäker.’ ”

19Har du fullkomligt förkastat Juda?

Avskyr du Sion?

Varför har du slagit oss så

att inget helande finns?

Vi hoppas på fred,

men inget gott kommer,

på en tid av helande,

men det råder förskräckelse.

20Herre, vi bekänner vår ondska

och våra förfäders skuld.

Vi har syndat mot dig.

21För ditt eget namns skull,

förkasta oss inte!

Låt inte din härlighets tron bli vanärad.

Kom ihåg ditt förbund med oss

och bryt det inte!

22Vilka av de andra folkens meningslösa gudar

skulle kunna ge oss regn?

Skulle himlen av sig själv

kunna sända regn?

Nej, det gör endast du,

Herre, vår Gud.

Därför är du vårt hopp,

för du har gjort allt detta.