Yakobo 5 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yakobo 5:1-20

Onyo Kwa Matajiri

15:1 1Tim 6:9; Mit 11:28; Lk 6:24Basi sikilizeni, ninyi matajiri, lieni na kuomboleza kwa ajili ya hali mbaya sana inayowajia. 25:2 Za 39:11; Ay 13:22; Mt 6:20; Yak 2:2Utajiri wenu umeoza na mavazi yenu yameliwa na nondo. 3Dhahabu yenu na fedha yenu vimeliwa na kutu. Kutu yake itashuhudia dhidi yenu nayo itaila miili yenu kama vile moto. Mmejiwekea hazina kwa ajili ya siku za mwisho. 45:4 Mt 3:5; Kum 24:15; Rum 9:29Angalieni! Ule ujira wa vibarua waliolima mashamba yenu mliouzuia kwa hila unapiga kelele dhidi yenu na vilio vya wavunaji vimefika masikioni mwa Bwana Mwenye Nguvu Zote. 55:5 Yer 12:3; 25:34Mmeishi duniani kwa anasa na kwa starehe, mmejinenepesha tayari kwa siku ya kuchinjwa. 65:6 Mit 3:34; Yak 2:6; Ebr 10:38; Yak 4:2Mmewahukumu na kuwaua watu wenye haki, waliokuwa hawapingani nanyi.

Uvumilivu Katika Mateso

75:7 Yer 5:24; Yoe 2:23Kwa hiyo, ndugu zangu, vumilieni hadi kuja kwake Bwana. Angalieni jinsi mkulima angojavyo ardhi itoe mavuno yake yaliyo ya thamani na jinsi anavyovumilia kwa ajili ya kupata mvua za kwanza na za mwisho. 85:8 Rum 13:11; 1Pet 4:7Ninyi nanyi vumilieni, tena simameni imara, kwa sababu kuja kwa Bwana kumekaribia. 95:9 Yak 4:11; Za 94:2; 1Kor 4:5; Mt 24:33Ndugu zangu, msinungʼunikiane msije mkahukumiwa. Hakimu amesimama mlangoni!

105:10 Mt 5:12; Ebr 11:25Ndugu zangu, waangalieni manabii walionena kwa Jina la Bwana, ili kuwa mfano wa uvumilivu katika kukabiliana na mateso. 115:11 Mt 5:10; Ay 2:10; Ebr 10:36; Ay 42:10; 12:17; Kut 34:6Kama mnavyojua, tunawahesabu kuwa wabarikiwa wale waliovumilia. Mmesikia habari za uvumilivu wake Ayubu na mmeona kile ambacho hatimaye Bwana alimtendea. Bwana ni mwingi wa huruma, na amejaa rehema.

125:12 Mt 5:31-34; Yak 1:25Zaidi ya yote, ndugu zangu, msiape, iwe kwa mbingu au kwa dunia, au kwa kitu kingine chochote. “Ndiyo” yenu na iwe ndiyo, na “Hapana” yenu iwe hapana, la sivyo mtahukumiwa.

Maombi Ya Imani

135:13 Za 50:15; Kol 3:16Je, mtu yeyote miongoni mwenu amepatwa na taabu? Basi inampasa aombe. Je, kuna yeyote mwenye furaha? Basi na aimbe nyimbo za kusifu. 145:14 Za 23:5; Mdo 11:30; Isa 1:6; Mk 6:13; 16:18; Lk 10:38Je, kuna yeyote miongoni mwenu aliye mgonjwa? Basi inampasa awaite wazee wa kanisa wamwombee na kumpaka mafuta kwa Jina la Bwana. 155:15 Yak 1:6; Isa 33:24; Mt 9:2Kule kuomba kwa imani kutamwokoa huyo mgonjwa, naye Bwana atamwinua na kama ametenda dhambi, atasamehewa. 165:16 Mdo 19:18; Ebr 12:13; Mt 7:7Kwa hiyo ungamianeni dhambi zenu ninyi kwa ninyi na kuombeana ili mpate kuponywa. Maombi ya mwenye haki yana nguvu tena yanafaa sana.

175:17 Mdo 14:15; 1Fal 17:1; Lk 4:25Eliya alikuwa mwanadamu kama sisi. Akaomba kwa bidii kwamba mvua isinyeshe, nayo haikunyesha juu ya nchi kwa muda wa miaka mitatu na miezi sita. 185:18 1Fal 18:41-45Kisha akaomba tena, nazo mbingu zikatoa mvua nayo ardhi ikatoa mazao yake.

195:19 Yak 3:14; Mt 18:15Ndugu zangu, yeyote miongoni mwenu akipotoka na kuicha kweli, naye akarejezwa na mtu mwingine, 205:20 Rum 11:14; 1Pet 4:8hamna budi kujua kwamba yeyote amrejezaye mwenye dhambi kutoka upotovu wake, ataiokoa roho ya huyo mwenye dhambi kutoka mauti na kusitiri wingi wa dhambi.

New International Reader’s Version

James 5:1-20

A Warning to Rich People

1You rich people, listen to me. Cry and weep, because you will soon be suffering. 2Your riches have rotted. Moths have eaten your clothes. 3Your gold and silver have lost their brightness. Their dullness will be a witness against you. Your wanting more and more will eat your body like fire. You have stored up riches in these last days. 4You have even failed to pay the workers who mowed your fields. Their pay is crying out against you. The cries of those who gathered the harvest have reached the ears of the Lord. He rules over all. 5You have lived an easy life on earth. You have given yourselves everything you wanted. You have made yourselves fat like cattle that will soon be butchered. 6You have judged and murdered people who aren’t guilty. And they weren’t even opposing you.

Be Patient When You Suffer

7Brothers and sisters, be patient until the Lord comes. See how the farmer waits for the land to produce its rich crop. See how patient the farmer is for the fall and spring rains. 8You too must be patient. You must remain strong. The Lord will soon come back. 9Brothers and sisters, don’t find fault with one another. If you do, you will be judged. And the Judge is standing at the door!

10Brothers and sisters, think about the prophets who spoke in the name of the Lord. They are an example of how to be patient when you suffer. 11As you know, we think that people who don’t give up are blessed. You have heard that Job was patient. And you have seen what the Lord finally did for him. The Lord is full of tender mercy and loving concern.

12My brothers and sisters, here is what is most important. Don’t make a promise by giving your word. Don’t promise by heaven or earth. And don’t promise by anything else to back up what you say. All you need to say is a simple “Yes” or “No.” If you do more than this, you will be judged.

The Prayer of Faith

13Is anyone among you in trouble? Then that person should pray. Is anyone among you happy? Then that person should sing songs of praise. 14Is anyone among you sick? Then that person should send for the elders of the church to pray over them. They should ask the elders to anoint them with olive oil in the name of the Lord. 15The prayer offered by those who have faith will make the sick person well. The Lord will heal them. If they have sinned, they will be forgiven. 16So confess your sins to one another. Pray for one another so that you might be healed. The prayer of a godly person is powerful. Things happen because of it.

17Elijah was a human being, just as we are. He prayed hard that it wouldn’t rain. And it didn’t rain on the land for three and a half years. 18Then he prayed again. That time it rained. And the earth produced its crops.

19My brothers and sisters, suppose one of you wanders away from the truth. And suppose someone brings that person back. 20Then here is what I want you to remember. Anyone who keeps a sinner from going astray will save them from death. God will erase many sins by forgiving them.