Yakobo 5 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yakobo 5:1-20

Onyo Kwa Matajiri

15:1 1Tim 6:9; Mit 11:28; Lk 6:24Basi sikilizeni, ninyi matajiri, lieni na kuomboleza kwa ajili ya hali mbaya sana inayowajia. 25:2 Za 39:11; Ay 13:22; Mt 6:20; Yak 2:2Utajiri wenu umeoza na mavazi yenu yameliwa na nondo. 3Dhahabu yenu na fedha yenu vimeliwa na kutu. Kutu yake itashuhudia dhidi yenu nayo itaila miili yenu kama vile moto. Mmejiwekea hazina kwa ajili ya siku za mwisho. 45:4 Mt 3:5; Kum 24:15; Rum 9:29Angalieni! Ule ujira wa vibarua waliolima mashamba yenu mliouzuia kwa hila unapiga kelele dhidi yenu na vilio vya wavunaji vimefika masikioni mwa Bwana Mwenye Nguvu Zote. 55:5 Yer 12:3; 25:34Mmeishi duniani kwa anasa na kwa starehe, mmejinenepesha tayari kwa siku ya kuchinjwa. 65:6 Mit 3:34; Yak 2:6; Ebr 10:38; Yak 4:2Mmewahukumu na kuwaua watu wenye haki, waliokuwa hawapingani nanyi.

Uvumilivu Katika Mateso

75:7 Yer 5:24; Yoe 2:23Kwa hiyo, ndugu zangu, vumilieni hadi kuja kwake Bwana. Angalieni jinsi mkulima angojavyo ardhi itoe mavuno yake yaliyo ya thamani na jinsi anavyovumilia kwa ajili ya kupata mvua za kwanza na za mwisho. 85:8 Rum 13:11; 1Pet 4:7Ninyi nanyi vumilieni, tena simameni imara, kwa sababu kuja kwa Bwana kumekaribia. 95:9 Yak 4:11; Za 94:2; 1Kor 4:5; Mt 24:33Ndugu zangu, msinungʼunikiane msije mkahukumiwa. Hakimu amesimama mlangoni!

105:10 Mt 5:12; Ebr 11:25Ndugu zangu, waangalieni manabii walionena kwa Jina la Bwana, ili kuwa mfano wa uvumilivu katika kukabiliana na mateso. 115:11 Mt 5:10; Ay 2:10; Ebr 10:36; Ay 42:10; 12:17; Kut 34:6Kama mnavyojua, tunawahesabu kuwa wabarikiwa wale waliovumilia. Mmesikia habari za uvumilivu wake Ayubu na mmeona kile ambacho hatimaye Bwana alimtendea. Bwana ni mwingi wa huruma, na amejaa rehema.

125:12 Mt 5:31-34; Yak 1:25Zaidi ya yote, ndugu zangu, msiape, iwe kwa mbingu au kwa dunia, au kwa kitu kingine chochote. “Ndiyo” yenu na iwe ndiyo, na “Hapana” yenu iwe hapana, la sivyo mtahukumiwa.

Maombi Ya Imani

135:13 Za 50:15; Kol 3:16Je, mtu yeyote miongoni mwenu amepatwa na taabu? Basi inampasa aombe. Je, kuna yeyote mwenye furaha? Basi na aimbe nyimbo za kusifu. 145:14 Za 23:5; Mdo 11:30; Isa 1:6; Mk 6:13; 16:18; Lk 10:38Je, kuna yeyote miongoni mwenu aliye mgonjwa? Basi inampasa awaite wazee wa kanisa wamwombee na kumpaka mafuta kwa Jina la Bwana. 155:15 Yak 1:6; Isa 33:24; Mt 9:2Kule kuomba kwa imani kutamwokoa huyo mgonjwa, naye Bwana atamwinua na kama ametenda dhambi, atasamehewa. 165:16 Mdo 19:18; Ebr 12:13; Mt 7:7Kwa hiyo ungamianeni dhambi zenu ninyi kwa ninyi na kuombeana ili mpate kuponywa. Maombi ya mwenye haki yana nguvu tena yanafaa sana.

175:17 Mdo 14:15; 1Fal 17:1; Lk 4:25Eliya alikuwa mwanadamu kama sisi. Akaomba kwa bidii kwamba mvua isinyeshe, nayo haikunyesha juu ya nchi kwa muda wa miaka mitatu na miezi sita. 185:18 1Fal 18:41-45Kisha akaomba tena, nazo mbingu zikatoa mvua nayo ardhi ikatoa mazao yake.

195:19 Yak 3:14; Mt 18:15Ndugu zangu, yeyote miongoni mwenu akipotoka na kuicha kweli, naye akarejezwa na mtu mwingine, 205:20 Rum 11:14; 1Pet 4:8hamna budi kujua kwamba yeyote amrejezaye mwenye dhambi kutoka upotovu wake, ataiokoa roho ya huyo mwenye dhambi kutoka mauti na kusitiri wingi wa dhambi.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

雅各書 5:1-20

警告為富不仁者

1你們這些富有的人啊!為那將要臨到你們身上的災難痛哭哀號吧! 2你們的財物朽壞了,衣服也被蟲蛀了。 3你們的金銀生了鏽,那鏽必要指控你們,像火一樣吞噬你們的身體。在末世的日子裡,你們只知道積攢財寶。 4工人替你們收割莊稼,你們卻剋扣他們的工錢。那工錢發出不平的呼喊,工人的冤聲已經傳到萬軍之主的耳中了。 5你們在世上奢侈享樂,在被宰殺的日子裡,把自己養得肥肥胖胖。 6你們冤枉好人、殘害無辜,他們也沒有反抗。

要忍耐到底

7弟兄姊妹,你們要一直忍耐到主來。你們看農夫怎樣耐心等候地裡寶貴的出產,等候秋雨和春雨的降臨。 8同樣,你們也要忍耐,心志堅定,因為主快來了。 9弟兄姊妹,不要互相埋怨,免得受審判。你們看,審判的主已經站在門外了。 10弟兄姊妹,你們要效法從前奉主的名說話的先知,以他們的受苦和忍耐為榜樣。 11我們認為那些忍耐到底的人是有福的。你們都知道約伯的忍耐,也知道主最終怎樣待他,因為主充滿憐憫和慈悲。

12我的弟兄姊妹,最重要的是不可起誓,不可指著天起誓,也不可指著地起誓,不可指著任何東西起誓。你們說話,是就說是,不是就說不是,免得你們受審判。

禱告的力量

13你們中間正在受苦的人應該禱告,喜樂的人應該唱歌讚美, 14生病的人應該請教會的長老來,奉主的名用油抹他的身體並為他禱告。 15出於信心的禱告必能使病人痊癒,主必使他康復。倘若他犯了罪,也必得到赦免。 16所以你們要彼此認罪,互相代禱,好得到醫治。義人的禱告有極大的力量和功效。 17以利亞先知和我們一樣同是血肉之軀,他懇切地祈求不要下雨,結果三年半沒有下雨。 18後來他再禱告求雨,天就降雨,地也長出了莊稼。

19我的弟兄姊妹,如果有人領一個偏離真道的人歸回正路, 20他該知道:使一個迷途中的罪人歸回正路就是救一個靈魂脫離死亡,並且會遮蓋許多罪。