Wimbo 8 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Wimbo 8:1-14

18:1 Mit 9:2; Wim 3:4Laiti ungelikuwa kwangu kama ndugu wa kiume,

ambaye aliyanyonya matiti ya mama yangu!

Kisha, kama ningekukuta huko nje,

ningelikubusu,

wala hakuna mtu yeyote angelinidharau.

2Ningelikuongoza na kukuleta

katika nyumba ya mama yangu,

yeye ambaye amenifundisha.

Ningelikupa divai iliyokolezwa unywe,

asali ya maua ya mikomamanga yangu.

38:3 Wim 2:6Mkono wake wa kushoto uko chini ya kichwa changu,

na mkono wake wa kuume unanikumbatia.

48:4 Wim 2:7; 3:5Binti za Yerusalemu, ninawaagiza:

msichochee wala kuamsha mapenzi

hata yatakapotaka yenyewe.

Shairi La Sita

Marafiki

58:5 Wim 3:4-6; Yn 17:14Ni nani huyu anayekuja kutoka nyikani

akimwegemea mpenzi wake?

Mpendwa

Nilikuamsha chini ya mtofaa,

huko mama yako alipotunga mimba yako,

huko yeye alipata utungu akakuzaa.

68:6 Wim 1:2; Hes 5:14; Hag 2:23; Isa 49:16Nitie kama muhuri moyoni mwako,

kama muhuri kwenye mkono wako;

kwa maana upendo una nguvu kama mauti,

wivu wake ni mkatili kama kuzimu.

Unachoma kama mwali wa moto,

kama mwali mkubwa wa moto wa Bwana hasa.

78:7 Mit 6:35Maji mengi hayawezi kuuzimisha upendo,

mito haiwezi kuugharikisha.

Kama mtu angelitoa mali yote ya nyumbani mwake

kwa ajili ya upendo,

angelidharauliwa kabisa.

Marafiki

8Tunaye dada mdogo,

matiti yake hayajakua bado.

Tutafanya nini kwa ajili ya dada yetu

wakati atakapokuja kuposwa?

9Kama yeye ni ukuta,

tutajenga minara ya fedha juu yake.

Na kama yeye ni mlango,

tutamzungushia mbao za mierezi.

Mpendwa

108:10 Kol 2:7; Eze 16:7Mimi ni ukuta,

nayo matiti yangu ni kama minara.

Ndivyo ambavyo nimekuwa machoni pake

kama yule anayeleta utoshelevu.

118:11 Mhu 2:4; Mt 21:33; Isa 7:23Solomoni alikuwa na shamba la mizabibu huko Baal-Hamoni;

alikodisha shamba lake la mizabibu kwa wapangaji.

Kila mmoja angeleta kwa ajili ya matunda yake

shekeli 1,0008:11 Shekeli 1,000 ni kama kilo 11.5. za fedha.

12Lakini shamba langu la mizabibu

ambalo ni langu mwenyewe

ni langu kutoa;

hizo shekeli 1,000 ni kwa ajili yako, ee Solomoni,

na shekeli mia mbili8:12 Shekeli 200 ni kama kilo 2.3. ni kwa ajili

ya wale wanaotunza matunda yake.

Mpenzi

138:13 Wim 2:14Wewe ukaaye bustanini

pamoja na marafiki mliohudhuria,

hebu nisikie sauti yako!

Mpendwa

148:14 Mit 5:19; Wim 2:8-17Njoo, mpenzi wangu,

uwe kama swala

au kama ayala kijana

juu ya milima iliyojaa vikolezo.

New International Version

Song of Songs 8:1-14

1If only you were to me like a brother,

who was nursed at my mother’s breasts!

Then, if I found you outside,

I would kiss you,

and no one would despise me.

2I would lead you

and bring you to my mother’s house—

she who has taught me.

I would give you spiced wine to drink,

the nectar of my pomegranates.

3His left arm is under my head

and his right arm embraces me.

4Daughters of Jerusalem, I charge you:

Do not arouse or awaken love

until it so desires.

Friends

5Who is this coming up from the wilderness

leaning on her beloved?

She

Under the apple tree I roused you;

there your mother conceived you,

there she who was in labor gave you birth.

6Place me like a seal over your heart,

like a seal on your arm;

for love is as strong as death,

its jealousy8:6 Or ardor unyielding as the grave.

It burns like blazing fire,

like a mighty flame.8:6 Or fire, / like the very flame of the Lord

7Many waters cannot quench love;

rivers cannot sweep it away.

If one were to give

all the wealth of one’s house for love,

it8:7 Or he would be utterly scorned.

Friends

8We have a little sister,

and her breasts are not yet grown.

What shall we do for our sister

on the day she is spoken for?

9If she is a wall,

we will build towers of silver on her.

If she is a door,

we will enclose her with panels of cedar.

She

10I am a wall,

and my breasts are like towers.

Thus I have become in his eyes

like one bringing contentment.

11Solomon had a vineyard in Baal Hamon;

he let out his vineyard to tenants.

Each was to bring for its fruit

a thousand shekels8:11 That is, about 25 pounds or about 12 kilograms; also in verse 12 of silver.

12But my own vineyard is mine to give;

the thousand shekels are for you, Solomon,

and two hundred8:12 That is, about 5 pounds or about 2.3 kilograms are for those who tend its fruit.

He

13You who dwell in the gardens

with friends in attendance,

let me hear your voice!

She

14Come away, my beloved,

and be like a gazelle

or like a young stag

on the spice-laden mountains.