Wimbo 5 – NEN & HOF

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Wimbo 5:1-16

Mpenzi

15:1 Yoe 3:18; Wim 4:12; 4:16; Isa 55:1Nimekuja kwenye bustani yangu, dada yangu,

bibi arusi wangu;

nimekusanya manemane yangu pamoja

na kikolezo changu.

Nimekula sega langu la asali na asali yangu;

nimekunywa divai yangu na maziwa yangu.

Marafiki

Kuleni, enyi marafiki, mnywe;

kunyweni ya kutosha, ee wapenzi.

Shairi La Nne

Mpendwa

25:2 Efe 5:275:2 Mit 8:4; Wim 6:9; 4:7; 1:15Nililala lakini moyo wangu ulikuwa macho.

Sikiliza! Mpenzi wangu anabisha:

“Nifungulie, dada yangu, mpenzi wangu,

hua wangu, asiye na hitilafu.

Kichwa changu kimeloa umande,

na nywele zangu manyunyu ya usiku.”

3Nimevua joho langu:

je, ni lazima nivae tena?

Nimenawa miguu yangu:

je, ni lazima niichafue tena?

4Mpenzi wangu aliweka mkono wake kwenye tundu la komeo;

moyo wangu ulianza kugonga kwa ajili yake.

5Niliinuka kumfungulia mpenzi wangu,

mikono yangu ikidondosha manemane,

vidole vyangu vikitiririka manemane,

penye vipini vya komeo.

65:6 Wim 6:1-2; 3:15:6 Hos 5:15; Mao 3:8Nilimfungulia mpenzi wangu,

lakini mpenzi wangu alishaondoka;

alikuwa amekwenda zake.

Moyo wangu ulishuka kwa kuondoka kwake.

Nilimtafuta lakini sikumpata.

Nilimwita lakini hakunijibu.

75:7 Wim 3:3Walinzi walinikuta

walipokuwa wakifanya zamu za ulinzi mjini.

Walinipiga, wakanijeruhi,

wakaninyangʼanya joho langu,

hao walinzi wa kuta!

85:8 Wim 2:7; 1:14; 2:5Enyi binti za Yerusalemu, ninawaagiza:

kama mkimpata mpenzi wangu,

mtamwambia nini?

Mwambieni ninazimia kwa mapenzi.

Marafiki

9Je, mpendwa wako ni bora kuliko wengine namna gani,

wewe uliye mzuri kupita wanawake wote?

Je, mpendwa wako ni mzuri kuliko wengine, namna gani,

hata unatuagiza hivyo?

Mpendwa

105:10 Za 45:2Mpenzi wangu anangʼaa, tena ni mwekundu,

wa kuvutia miongoni mwa wanaume kumi elfu.

11Kichwa chake ni dhahabu safi kuliko zote,

nywele zake ni za mawimbi

na ni nyeusi kama kunguru.

125:12 Mwa 49:12; Wim 1:15Macho yake ni kama ya hua

kandokando ya vijito vya maji,

aliyeogeshwa kwenye maziwa,

yaliyopangwa kama vito vya thamani.

13Mashavu yake ni kama matuta ya vikolezo

yakitoa manukato.

Midomo yake ni kama yungiyungi

inayodondosha manemane.

145:14 Ay 28:6Mikono yake ni fimbo za dhahabu

iliyopambwa kwa krisolitho.

Mwili wake ni kama pembe ya ndovu iliyongʼarishwa

iliyopambwa na yakuti samawi.

155:15 1Fal 4:33; Wim 7:4Miguu yake ni nguzo za marmar

zilizosimikwa katika vitako vya dhahabu safi.

Sura yake ni kama Lebanoni,

bora kama miti yake ya mierezi.

165:16 Wim 4:3; 7:9; Yer 31:3; Rum 8:35Kinywa chake chenyewe ni utamu,

kwa ujumla yeye ni wa kupendeza.

Huyu ndiye mpenzi wangu, huyu ndiye rafiki yangu,

ee binti za Yerusalemu.

Hoffnung für Alle

Hoheslied 5:1-16

Er:

1Ich betrete den Garten,

mein Mädchen, meine Braut.

Ich pflücke die Myrrhe

und ernte den Balsam.

Ich öffne die Wabe

und esse den Honig.

Ich trinke den Wein

und genieße die Milch.

Esst auch ihr, Freunde,

trinkt euren Wein!

Berauscht euch an der Liebe!

Suche in der Nacht

Sie:

2Ich schlief, doch mein Herz war wach.

Da, es klopft! Mein Liebster kommt!

Er:

Mach auf, mein Mädchen, meine Freundin!

Mein Täubchen, meine Vollkommene, lass mich herein!

Mein Haar ist vom Tau der Nacht ganz durchnässt.

Sie:

3Ich habe mein Kleid schon ausgezogen,

soll ich es deinetwegen wieder anziehn?

Meine Füße habe ich schon gewaschen,

ich würde sie nur wieder schmutzig machen.

4Jetzt streckt er seine Hand

durch die Öffnung in der Tür.

Mein Herz schlägt bis zum Hals,

weil er in meiner Nähe ist.

5Ich springe auf und will dem Liebsten öffnen;

meine Hände greifen nach dem Riegel,

sie sind voll von Myrrhenöl.

6Schnell öffne ich die Tür für meinen Liebsten,

doch weg ist er, spurlos verschwunden.

Entsetzen packt mich: Er ist fortgegangen!

Ich suche ihn, doch ich kann ihn nirgends finden;

ich rufe laut nach ihm, doch er gibt keine Antwort.

7Bei ihrem Rundgang greifen die Wächter mich auf.

Sie schlagen und verwunden mich,

ohne Mitleid reißen sie mir den Umhang weg.

8Ihr Mädchen von Jerusalem,

ich beschwöre euch:

Wenn ihr meinen Liebsten findet, dann sagt ihm,

dass ich krank vor Liebe bin.

Die Mädchen:

9Warum beschwörst du uns,

du schönste aller Frauen?

Was hat denn dein Liebster anderen voraus?

Was unterscheidet ihn von den anderen Männern?

Sie:

10Mein Liebster strahlt vor Schönheit und Kraft5,10 Wörtlich: ist strahlend und rötlich. – Gemeint ist eine schöne, gesunde Hautfarbe.,

unter Tausenden ist keiner so wie er!

11Sein Gesicht schimmert wie Gold,

sein Haar ist rabenschwarz,

seine Locken erinnern an die Blütenrispen einer Dattelpalme.

12Seine Augen sind von vollkommener Schönheit,

so wie Tauben, die in Milch baden

und aus vollen Bächen trinken.

13Seine Wangen duften nach Balsamkräutern,

nach kostbaren Salben.

Seine Lippen leuchten wie rote Lilien,

sie sind mit Myrrhenöl benetzt.

14Seine Arme sind wie Barren aus Gold,

mit Türkissteinen verziert.

Sein Leib gleicht einer Statue aus Elfenbein,

über und über mit Saphiren bedeckt.

15Seine Beine sind Alabastersäulen,

die auf goldenen Sockeln stehn.

Eindrucksvoll wie der Libanon ist seine Gestalt,

stattlich wie mächtige Zedern.

16Seine Küsse sind zärtlich,

alles an ihm ist begehrenswert.

So ist mein Liebster, mein Freund,

ihr Mädchen von Jerusalem.