Wimbo 5 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Wimbo 5:1-16

Mpenzi

15:1 Yoe 3:18; Wim 4:12; 4:16; Isa 55:1Nimekuja kwenye bustani yangu, dada yangu,

bibi arusi wangu;

nimekusanya manemane yangu pamoja

na kikolezo changu.

Nimekula sega langu la asali na asali yangu;

nimekunywa divai yangu na maziwa yangu.

Marafiki

Kuleni, enyi marafiki, mnywe;

kunyweni ya kutosha, ee wapenzi.

Shairi La Nne

Mpendwa

25:2 Efe 5:275:2 Mit 8:4; Wim 6:9; 4:7; 1:15Nililala lakini moyo wangu ulikuwa macho.

Sikiliza! Mpenzi wangu anabisha:

“Nifungulie, dada yangu, mpenzi wangu,

hua wangu, asiye na hitilafu.

Kichwa changu kimeloa umande,

na nywele zangu manyunyu ya usiku.”

3Nimevua joho langu:

je, ni lazima nivae tena?

Nimenawa miguu yangu:

je, ni lazima niichafue tena?

4Mpenzi wangu aliweka mkono wake kwenye tundu la komeo;

moyo wangu ulianza kugonga kwa ajili yake.

5Niliinuka kumfungulia mpenzi wangu,

mikono yangu ikidondosha manemane,

vidole vyangu vikitiririka manemane,

penye vipini vya komeo.

65:6 Wim 6:1-2; 3:15:6 Hos 5:15; Mao 3:8Nilimfungulia mpenzi wangu,

lakini mpenzi wangu alishaondoka;

alikuwa amekwenda zake.

Moyo wangu ulishuka kwa kuondoka kwake.

Nilimtafuta lakini sikumpata.

Nilimwita lakini hakunijibu.

75:7 Wim 3:3Walinzi walinikuta

walipokuwa wakifanya zamu za ulinzi mjini.

Walinipiga, wakanijeruhi,

wakaninyangʼanya joho langu,

hao walinzi wa kuta!

85:8 Wim 2:7; 1:14; 2:5Enyi binti za Yerusalemu, ninawaagiza:

kama mkimpata mpenzi wangu,

mtamwambia nini?

Mwambieni ninazimia kwa mapenzi.

Marafiki

9Je, mpendwa wako ni bora kuliko wengine namna gani,

wewe uliye mzuri kupita wanawake wote?

Je, mpendwa wako ni mzuri kuliko wengine, namna gani,

hata unatuagiza hivyo?

Mpendwa

105:10 Za 45:2Mpenzi wangu anangʼaa, tena ni mwekundu,

wa kuvutia miongoni mwa wanaume kumi elfu.

11Kichwa chake ni dhahabu safi kuliko zote,

nywele zake ni za mawimbi

na ni nyeusi kama kunguru.

125:12 Mwa 49:12; Wim 1:15Macho yake ni kama ya hua

kandokando ya vijito vya maji,

aliyeogeshwa kwenye maziwa,

yaliyopangwa kama vito vya thamani.

13Mashavu yake ni kama matuta ya vikolezo

yakitoa manukato.

Midomo yake ni kama yungiyungi

inayodondosha manemane.

145:14 Ay 28:6Mikono yake ni fimbo za dhahabu

iliyopambwa kwa krisolitho.

Mwili wake ni kama pembe ya ndovu iliyongʼarishwa

iliyopambwa na yakuti samawi.

155:15 1Fal 4:33; Wim 7:4Miguu yake ni nguzo za marmar

zilizosimikwa katika vitako vya dhahabu safi.

Sura yake ni kama Lebanoni,

bora kama miti yake ya mierezi.

165:16 Wim 4:3; 7:9; Yer 31:3; Rum 8:35Kinywa chake chenyewe ni utamu,

kwa ujumla yeye ni wa kupendeza.

Huyu ndiye mpenzi wangu, huyu ndiye rafiki yangu,

ee binti za Yerusalemu.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

雅歌 5:1-16

男子:

1我的妹妹,我的新娘啊,

我已经来到自己的园中,

采了我的没药和香料,

品尝了我的蜂房和蜂蜜,

也享用了我的美酒和鲜奶。

耶路撒冷的少女:

朋友们,尽情吃喝吧。

相爱的人啊,沉醉在爱中吧!

女子:

2我虽然躺在床上,心却清醒。

我听见我的良人在叩门,说:“开门吧!

我的妹妹,我的爱人,

我完美无瑕的小鸽子啊,

我的头上沾满了露水,

头发被夜间的露珠弄湿了。”

3可是我已经脱了衣裳,难道要再穿上吗?

我已经洗了脚,怎能再沾土呢?

4我的良人从门孔伸进手来,

我心神为之荡漾,

5就起来为他开门;

我的双手滴下没药,

甚至门闩也沾了我指头滴下的没药。

6我为良人开了门,

他却已经离开了。

他的离去使我心中失落。5:6 他的离去使我心中失落”或译“他说话时,我神不守舍”。

我到处找他,却找不着;

我呼唤他,却得不到回答。

7城中巡逻的卫兵遇见我,

把我打伤了,

看守城墙的人还抢走了我的披肩。

8耶路撒冷的少女啊,

我恳求你们,

倘若遇见我的良人,

请告诉他我思爱成病。

耶路撒冷的少女:

9绝色的佳人啊!

你的良人与别的男子比较,

究竟有什么长处,

以致你这样恳求我们呢?

女子:

10他红光满面,

超越万人。

11他头如纯金,

乌黑发亮的卷发像波浪。

12他的眼睛清澈明亮,

如同溪旁用奶洗净的白鸽,

又像镶嵌合适的宝石。

13他的双颊芬芳,

犹如种满香草的花圃。

他的嘴唇好像百合花,

滴下没药汁。

14他的双臂如同镶着水苍玉的金杖,

身体如同镶嵌蓝宝石的象牙。

15他的双腿好像纯金座上的白玉石柱,

体格如黎巴嫩挺拔的香柏树。

16他的嘴甘甜如蜜,

整个人都令人爱慕。

耶路撒冷的少女啊,

这就是我的良人,

我的朋友。