Wimbo 3 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Wimbo 3:1-11

13:1 Isa 26:9; Wim 5:6Usiku kucha kwenye kitanda changu

nilimtafuta yule moyo wangu umpendaye;

nilimtafuta, lakini sikumpata.

2Sasa nitaondoka na kuzunguka mjini,

katika barabara zake na viwanja;

nitamtafuta yule moyo wangu umpendaye.

Kwa hiyo nilimtafuta lakini sikumpata.

33:3 Wim 5:7; Isa 21:6-11Walinzi walinikuta

walipokuwa wakizunguka mji.

Nikawauliza, “Je, mmemwona

yule moyo wangu umpendaye?”

43:4 Wim 8:2; 6:9; 8:5; Rum 8:35-39; Mit 8:17; 4:13Kitambo kidogo tu baada ya kuwapita

nilimpata yule moyo wangu umpendaye.

Nilimshika na sikumwachia aende

mpaka nilipomleta katika nyumba ya mama yangu,

katika chumba cha yule aliyenichukua mimba.

53:5 Wim 2:7; 8:4Binti za Yerusalemu, ninawaagiza

kwa paa na kwa ayala wa shambani:

Msichochee wala kuamsha mapenzi

hata yatakapotaka yenyewe.

Shairi La Tatu

Mpenzi

63:6 Wim 8:6; 4:6, 14; Kut 30:34; Yer 2:2Ni nani huyu anayekuja kutoka jangwani

kama nguzo ya moshi,

anayenukia manemane na uvumba

iliyotengenezwa kwa vikolezo vyote

vya mfanyabiashara?

73:7 1Sam 8:11Tazama! Ni gari la Solomoni

lisindikizwalo na mashujaa sitini,

walio wakuu sana wa Israeli,

83:8 Ay 15:22; Za 91:5wote wamevaa panga,

wote wazoefu katika vita,

kila mmoja na upanga wake pajani,

wamejiandaa kwa ajili ya hofu za usiku.

9Mfalme Solomoni alijitengenezea gari;

alilitengeneza kwa mbao kutoka Lebanoni.

103:10 Mt 22:37; Efe 3:19; Rum 5:8Nguzo zake alizitengeneza kwa fedha,

kitako chake kwa dhahabu.

Kiti chake kilipambwa kwa zambarau,

gari lake likanakshiwa njumu kwa upendo

na binti za Yerusalemu.

113:11 Isa 3:16; 54:5; 32:9-13; 62:5; Yer 3:14Tokeni nje, ninyi binti za Sayuni,

mkamtazame Mfalme Solomoni akiwa amevaa taji,

taji ambalo mama yake alimvika

siku ya arusi yake,

siku ambayo moyo wake ulishangilia.

New International Version – UK

Song of Songs 3:1-11

1All night long on my bed

I looked for the one my heart loves;

I looked for him but did not find him.

2I will get up now and go about the city,

through its streets and squares;

I will search for the one my heart loves.

So I looked for him but did not find him.

3The watchmen found me

as they made their rounds in the city.

‘Have you seen the one my heart loves?’

4Scarcely had I passed them

when I found the one my heart loves.

I held him and would not let him go

till I had brought him to my mother’s house,

to the room of the one who conceived me.

5Daughters of Jerusalem, I charge you

by the gazelles and by the does of the field:

do not arouse or awaken love

until it so desires.

6Who is this coming up from the wilderness

like a column of smoke,

perfumed with myrrh and incense

made from all the spices of the merchant?

7Look! It is Solomon’s carriage,

escorted by sixty warriors,

the noblest of Israel,

8all of them wearing the sword,

all experienced in battle,

each with his sword at his side,

prepared for the terrors of the night.

9King Solomon made for himself the carriage;

he made it of wood from Lebanon.

10Its posts he made of silver,

its base of gold.

Its seat was upholstered with purple,

its interior inlaid with love.

Daughters of Jerusalem, 11come out,

and look, you daughters of Zion.

Look3:10,11 Or interior lovingly inlaid / by the daughters of Jerusalem. / 11 Come out, you daughters of Zion, / and look on King Solomon wearing a crown,

the crown with which his mother crowned him

on the day of his wedding,

the day his heart rejoiced.