Warumi 9 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Warumi 9:1-33

Kuteuliwa Kwa Israeli Na Mungu

19:1 Gal 1:20; 1Tim 2:7; Rum 1:9Ninasema kweli katika Kristo, wala sisemi uongo, dhamiri yangu inanishuhudia katika Roho Mtakatifu. 29:2 Rum 10:1Nina huzuni kuu na uchungu usiokoma moyoni mwangu. 39:3 Kut 32:32; 1Kor 12:3; 16:22; Rum 11:14Kwa maana ningetamani hata mimi nilaaniwe na kutengwa na Kristo kwa ajili ya ndugu zangu hasa, wale walio wa kabila langu kwa jinsi ya mwili, 49:4 Kut 6:7; Kum 7:6; 4:13; Flp 1:12; Za 147:19; Ebr 9:1; Mdo 13:32; Gal 3:16yaani, watu wa Israeli, ambao ndio wenye kule kufanywa wana, ule utukufu wa Mungu, yale maagano, kule kupokea sheria, ibada ya kwenye Hekalu na zile ahadi. 59:5 Mt 1:1-16; Yn 1:1; Kol 2:9; Rum 1:3, 25; 2Kor 11:31Wao ni wa uzao wa mababa wakuu wa kwanza, ambao kutoka kwao Kristo alikuja kwa jinsi ya mwili kama mwanadamu, yeye ambaye ni Mungu aliye juu ya vyote, mwenye kuhimidiwa milele! Amen.

69:6 Rum 2:28, 29; Gal 6:16Si kwamba Neno la Mungu limeshindwa. Kwa maana si kila Mwisraeli ambaye ni wa uzao utokanao na Israeli ni Mwisraeli halisi. 79:7 Mwa 21:12; Ebr 11:18Wala hawakuwi wazao wa Abrahamu kwa sababu wao ni watoto wake, lakini: “Uzao wako utahesabiwa kupitia kwake Isaki.” 89:8 Rum 8:14; Gal 3:16; 4:23Hii ina maana kwamba, si watoto waliozaliwa kimwili walio watoto wa Mungu, bali ni watoto wa ahadi wanaohesabiwa kuwa uzao wa Abrahamu. 99:9 Mwa 18:10; 18:14Kwa maana ahadi yenyewe ilisema, “Nitakurudia tena wakati kama huu, naye Sara atapata mtoto wa kiume.”

109:10 Mwa 25:23; 25:21Wala si hivyo tu, bali pia watoto aliowazaa Rebeka walikuwa na baba huyo huyo mmoja, yaani, baba yetu Isaki. 119:11 Rum 8:28; 9:16; 8:28Lakini, hata kabla hao mapacha hawajazaliwa au kufanya jambo lolote jema au baya, ili kwamba kusudi la Mungu la kuchagua lipate kusimama, 129:12 Mwa 25:23si kwa matendo, bali kwa yeye mwenye kuita, Rebeka aliambiwa, “Yule mkubwa atamtumikia yule mdogo.” 139:13 Mal 1:2-3; Kum 21:15; Mit 13:24; Mt 10:37; Lk 14:26; Yn 12:25Kama vile ilivyoandikwa, “Nimempenda Yakobo, lakini nimemchukia Esau.”

Mungu Hana Upendeleo

149:14 2Nya 19:7; Kum 32:4; Ay 8:3; 34:10; Za 92:15Tuseme nini basi? Je, Mungu ni dhalimu? La, hasha! 159:15 Kut 33:19Kwa maana Mungu alimwambia Mose,

“Nitamrehemu yeye nimrehemuye,

na pia nitamhurumia yeye nimhurumiaye.”

169:16 Efe 2:8; Tit 3:5Kwa hiyo haitegemei kutaka kwa mwanadamu au jitihada, bali hutegemea huruma ya Mungu. 179:17 Kut 14:4; Za 76:10Kwa maana Maandiko yamwambia Farao, “Nilikuinua kwa kusudi hili hasa, ili nipate kuonyesha uweza wangu juu yako, na ili Jina langu lipate kutangazwa duniani yote.”

189:18 Yos 11:20; Rum 11:25Kwa hiyo basi, Mungu humhurumia yeye atakaye kumhurumia na humfanya mgumu yeye atakaye kumfanya mgumu.

199:19 1Kor 15:35; Yos 2:18; 2Sam 16:10; Dan 4:35Basi mtaniambia, “Kama ni hivyo, kwa nini basi bado Mungu anatulaumu? Kwa maana ni nani awezaye kupinga mapenzi yake?” 209:20 Isa 64:8; Yer 18:6; Isa 10:15Lakini, ewe mwanadamu, u nani wewe ushindane na Mungu? “Je, kilichoumbwa chaweza kumwambia yeye aliyekiumba, ‘Kwa nini umeniumba hivi?’ ” 219:21 2Tim 2:20Je, mfinyanzi hana haki ya kufinyanga kutoka bonge moja vyombo vya udongo, vingine kwa matumizi ya heshima na vingine kwa matumizi ya kawaida?

229:22 Rum 2:4Iweje basi, kama Mungu kwa kutaka kuonyesha ghadhabu yake na kufanya uweza wake ujulikane, amevumilia kwa uvumilivu mwingi vile vyombo vya ghadhabu vilivyoandaliwa kwa uharibifu? 239:23 Rum 8:28; 8:30Iweje basi, kama yeye alitenda hivi ili kufanya wingi wa utukufu wake ujulikane kwa vile vyombo vya rehema yake, alivyotangulia kuvitengeneza kwa ajili ya utukufu wake, 249:24 Rum 8:28; 3:29yaani pamoja na sisi, ambao pia alituita, si kutoka kwa Wayahudi peke yao, bali pia kutoka kwa watu wa Mataifa?

Yote Yalitabiriwa Katika Maandiko

259:25 Hos 2:23; 1Pet 2:10Kama vile Mungu asemavyo katika Hosea:

“Nitawaita ‘watu wangu’

wale ambao si watu wangu;

nami nitamwita ‘mpenzi wangu’

yeye ambaye si mpenzi wangu,”

269:26 Hos 1:10; Mt 16:16tena,

“Itakuwa hasa mahali pale walipoambiwa,

‘Ninyi si watu wangu,’

wao wataitwa ‘wana wa Mungu aliye hai.’ ”

279:27 Mwa 22:17; Isa 10:22-23; Hos 1:10; Yoe 2:32; Rum 11:5Isaya anapiga kelele kuhusu Israeli:

“Ingawa idadi ya wana wa Israeli

ni wengi kama mchanga wa pwani,

ni mabaki yao tu watakaookolewa.

28Kwa kuwa Bwana ataitekeleza

hukumu yake duniani kwa haraka

na kwa ukamilifu.”

299:29 Yak 5:4; Isa 1:9; 13:19; Yer 50; 40Ni kama vile alivyotabiri Isaya akisema:

“Kama Bwana Mwenye Nguvu Zote

asingelituachia uzao,

tungelikuwa kama Sodoma,

tungelifanana na Gomora.”

Kutokuamini Kwa Israeli

309:30 Flp 3:9; Ebr 11:17Kwa hiyo tuseme nini basi? Kwamba watu wa Mataifa ambao hawakutafuta haki, wamepata haki ile iliyo kwa njia ya imani. 319:31 Isa 51:11; Rum 11:7; Gal 5:4Lakini Israeli, ambao walijitahidi kupata haki kwa njia ya sheria, hawakuipata. 329:32 1Pet 2:8Kwa nini? Kwa sababu hawakuitafuta kwa njia ya imani bali kwa njia ya matendo. Wakajikwaa kwenye lile “jiwe la kukwaza.” 339:33 Isa 8:14; 1Pet 2:6, 8Kama ilivyoandikwa:

“Tazama naweka katika Sayuni jiwe la kukwaza watu

na mwamba wa kuwaangusha.

Yeyote atakayemwamini

hataaibika kamwe.”

King James Version

Romans 9:1-33

1I say the truth in Christ, I lie not, my conscience also bearing me witness in the Holy Ghost, 2That I have great heaviness and continual sorrow in my heart. 3For I could wish that myself were accursed from Christ for my brethren, my kinsmen according to the flesh: 4Who are Israelites; to whom pertaineth the adoption, and the glory, and the covenants, and the giving of the law, and the service of God, and the promises; 5Whose are the fathers, and of whom as concerning the flesh Christ came, who is over all, God blessed for ever. Amen.

6Not as though the word of God hath taken none effect. For they are not all Israel, which are of Israel: 7Neither, because they are the seed of Abraham, are they all children: but, In Isaac shall thy seed be called. 8That is, They which are the children of the flesh, these are not the children of God: but the children of the promise are counted for the seed. 9For this is the word of promise, At this time will I come, and Sara shall have a son. 10And not only this; but when Rebecca also had conceived by one, even by our father Isaac; 11(For the children being not yet born, neither having done any good or evil, that the purpose of God according to election might stand, not of works, but of him that calleth;) 12It was said unto her, The elder shall serve the younger. 13As it is written, Jacob have I loved, but Esau have I hated.

14What shall we say then? Is there unrighteousness with God? God forbid. 15For he saith to Moses, I will have mercy on whom I will have mercy, and I will have compassion on whom I will have compassion. 16So then it is not of him that willeth, nor of him that runneth, but of God that sheweth mercy. 17For the scripture saith unto Pharaoh, Even for this same purpose have I raised thee up, that I might shew my power in thee, and that my name might be declared throughout all the earth. 18Therefore hath he mercy on whom he will have mercy, and whom he will he hardeneth. 19Thou wilt say then unto me, Why doth he yet find fault? For who hath resisted his will? 20Nay but, O man, who art thou that repliest against God? Shall the thing formed say to him that formed it, Why hast thou made me thus? 21Hath not the potter power over the clay, of the same lump to make one vessel unto honour, and another unto dishonour? 22What if God, willing to shew his wrath, and to make his power known, endured with much longsuffering the vessels of wrath fitted to destruction: 23And that he might make known the riches of his glory on the vessels of mercy, which he had afore prepared unto glory, 24Even us, whom he hath called, not of the Jews only, but also of the Gentiles? 25As he saith also in Osee, I will call them my people, which were not my people; and her beloved, which was not beloved. 26And it shall come to pass, that in the place where it was said unto them, Ye are not my people; there shall they be called the children of the living God. 27Esaias also crieth concerning Israel, Though the number of the children of Israel be as the sand of the sea, a remnant shall be saved: 28For he will finish the work, and cut it short in righteousness: because a short work will the Lord make upon the earth. 29And as Esaias said before, Except the Lord of Sabaoth had left us a seed, we had been as Sodoma, and been made like unto Gomorrha. 30What shall we say then? That the Gentiles, which followed not after righteousness, have attained to righteousness, even the righteousness which is of faith. 31But Israel, which followed after the law of righteousness, hath not attained to the law of righteousness. 32Wherefore? Because they sought it not by faith, but as it were by the works of the law. For they stumbled at that stumblingstone; 33As it is written, Behold, I lay in Sion a stumblingstone and rock of offence: and whosoever believeth on him shall not be ashamed.