Warumi 6 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Warumi 6:1-23

Kufa Na Kufufuka Pamoja Na Kristo

16:1 Rum 3:5, 6Tuseme nini basi? Je, tuendelee kutenda dhambi ili neema ipate kuongezeka? 26:2 Kol 3:5, 8La hasha! Sisi tulioifia dhambi, tutawezaje kuendelea kuishi tena katika dhambi? 36:3 Mt 28:19Au hamjui ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake? 46:4 Mdo 2:24; Kol 2:12; 2Kor 5:17; Gal 6:15Kwa hiyo tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti, ili kama vile Kristo alivyofufuliwa kutoka kwa wafu kwa utukufu wa Baba, vivyo hivyo sisi nasi pia tupate kuenenda katika upya wa uzima.

56:5 Efe 2:6; 2Tim 2:11Kwa maana ikiwa tumeungana naye katika mauti yake, bila shaka tutaungana naye katika ufufuo wake. 66:6 Gal 5:24; Kol 3:9; 2Kor 4:10; Gal 2:20; Rum 7:24Kwa maana twajua kwamba utu wetu wa kale ulisulubiwa pamoja naye ili ule mwili wa dhambi upate kuangamizwa, nasi tusiendelee kuwa tena watumwa wa dhambi. 76:7 1Pet 4:1; Rum 6:18Kwa maana mtu yeyote aliyekufa amehesabiwa haki mbali na dhambi.

86:8 Rum 6:5; 2Tim 2:11Basi ikiwa tulikufa pamoja na Kristo, tunaamini kwamba pia tutaishi pamoja naye. 96:9 Mdo 2:24; Ufu 1:18Kwa maana tunajua kwamba Kristo, kwa sababu alifufuliwa kutoka kwa wafu, hawezi kufa tena; mauti haina tena mamlaka juu yake. 106:10 Rum 6:2; Ebr 7:27; 9:26-28; Gal 2:19; 1Pet 3:18Kifo alichokufa, aliifia dhambi mara moja tu, lakini uzima alio nao anamwishia Mungu.

116:11 Rum 6:2; 2Kor 5:15; 1Pet 2:24Vivyo hivyo, jihesabuni wafu katika dhambi lakini mlio hai kwa Mungu katika Kristo Yesu. 126:12 Rum 6:16; Mwa 4:7; Za 19:13; 119:133Kwa hiyo, msiruhusu dhambi itawale ndani ya miili yenu, ipatikanayo na kufa, ili kuwafanya mzitii tamaa mbaya. 136:13 Rum 7:5; 2Kor 5:156:13 1Pet 2:24Wala msivitoe viungo vya miili yenu vitumike kama vyombo vya uovu vya kutenda dhambi, bali jitoeni kwa Mungu, kama watu waliotolewa kutoka mautini kuingia uzimani. Nanyi vitoeni viungo vya miili yenu kwake kama vyombo vya haki. 146:14 Rum 2:12; Gal 5:18; Rum 3:24Kwa maana dhambi haitakuwa na mamlaka juu yenu, kwa sababu hampo chini ya sheria, bali chini ya neema.

Watumwa Wa Haki

156:15 1Kor 9:21Ni nini basi? Je, tutende dhambi kwa kuwa hatuko chini ya sheria bali chini ya neema? La, hasha! 166:16 Za 51:5; 2Pet 2:19Je, hamjui kwamba mnapojitoa kwa mtu yeyote kama watumwa watiifu, ninyi ni watumwa wa yule mnayemtii, aidha watumwa wa dhambi, ambayo matokeo yake ni mauti, au watumwa wa utii ambao matokeo yake ni haki? 176:17 Rum 1:18; 2Kor 2:14; 2Tim 1:13Lakini Mungu ashukuriwe kwa kuwa ninyi ambao kwanza mlikuwa watumwa wa dhambi, mmekuwa watii kutoka moyoni kwa mafundisho mliyopewa. 186:18 Rum 8:2; 1Pet 4:1Nanyi, mkiisha kuwekwa huru mbali na dhambi, mmekuwa watumwa wa haki.

196:19 Rum 3:5; Gal 3:15Ninasema kwa namna ya kibinadamu kwa sababu ya udhaifu wenu wa hali ya asili. Kama vile mlivyokuwa mkivitoa viungo vya miili yenu kama watumwa wa mambo machafu na uovu uliokuwa ukiongezeka zaidi, hivyo sasa vitoeni viungo vyenu kama watumwa wa haki inayowaelekeza mpate kutakaswa. 206:20 Rum 6:16; Yn 8:34Mlipokuwa watumwa wa dhambi, mlikuwa hamtawaliwi na haki. 216:21 Rum 6:23; Eze 16:61, 63; Rum 8:6, 13Lakini mlipata faida gani kwa mambo hayo ambayo sasa mnayaonea aibu? Mwisho wa mambo hayo ni mauti. 226:22 1Pet 2:16Lakini sasa kwa kuwa mmewekwa huru mbali na dhambi na mmekuwa watumwa wa Mungu, faida mnayopata ni utakatifu, ambao mwisho wake ni uzima wa milele. 236:23 Mit 10:16; Yak 1:15; Mt 25:46Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti, bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

罗马书 6:1-23

与基督同死同活

1那么,我们该怎么说呢?我们可以继续犯罪,使恩典显得更丰富吗? 2绝不可以!我们既然向罪死了,岂可继续活在罪中? 3难道你们不知道,我们受洗归属基督耶稣是和祂一同死吗? 4我们借着洗礼和祂一同死了,埋葬了,这样我们的一举一动可以有新生命的样式,正如基督借着父的荣耀从死里复活一样。

5如果我们和基督一同死了,也必和祂一同复活。 6我们知道,我们的旧人已经和祂一同钉在十字架上,使辖制我们身体的罪失去力量,使我们不再做罪的奴隶。 7因为人一旦死了,便脱离了罪。

8如果我们与基督同死,相信也必与祂同活。 9因为我们知道,基督既然从死里复活了,就不会再死,死亡也不能再控制祂。 10祂死,是向罪死,只死一次;祂活,却是向上帝永远活着。 11这样,你们应当看自己是向罪死了,但向上帝则看自己是活在基督耶稣里。

12所以,不要让罪辖制你们必死的身体,使你们顺从身体的私欲; 13也不要将你们的身体献给罪作不义的工具,而是要像一个从死里复活的人将自己奉献给上帝,把身体献给上帝作义的工具。 14罪不能再主宰你们,因为你们已经不在律法之下,而是在恩典之中。

做义的奴仆

15那么,我们在恩典之中,不在律法之下,就可以任意犯罪吗?绝不可以! 16你们难道不明白吗?你们献身给谁、服从谁,就是谁的奴隶。做罪的奴隶,结局是死亡;做上帝的奴仆,就被称为义人。 17感谢上帝!你们从前虽然做过罪的奴隶,现在却衷心服从了所传给你们的教导, 18从罪中得到释放,成为义的奴仆。

19因为你们有人性的软弱,我就从人的立场向你们解释。以前你们将身体献给肮脏不法的事,任其奴役,助长不法。现在你们要将身体奉献给义,为义效劳,成为圣洁的人。 20你们做罪的奴隶时,不受义的约束, 21做了现在想起来也觉得羞耻的事,得到了什么益处呢?那些事只能导致死亡! 22但现在你们已从罪中得到释放,做了上帝的奴仆,这样会使你们圣洁,最终得到永生。 23因为罪的代价就是死亡,而上帝借着主基督耶稣赐下的礼物则是永生。