Warumi 16 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Warumi 16:1-27

Salamu Kwa Watu Binafsi

116:1 2Kor 3:1; Mdo 18:18Napenda kumtambulisha kwenu dada yetu Foibe, mtumishi katika kanisa la Kenkrea. 216:2 Flp 2:29; 3Yn 5, 6; Mdo 9:13Naomba mpokeeni katika Bwana ipasavyo watakatifu na kumpa msaada wowote atakaohitaji kutoka kwenu, kwa maana yeye amekuwa msaada kwa watu wengi, mimi nikiwa miongoni mwao.

316:3 Mdo 18:2; Gal 5:6; Rum 8:1Wasalimuni Prisila16:3 Prisila kwa Kiyunani ni Priska, hivyo tafsiri nyingine zimemuita Priska. na Akila, watumishi wenzangu katika Kristo Yesu. 4Wao walihatarisha maisha yao kwa ajili yangu; wala si mimi tu ninayewashukuru bali pia makanisa yote ya watu wa Mataifa.

516:5 Kol 4:15; 1Kor 16:15Lisalimuni pia kanisa linalokutana nyumbani mwao.

Msalimuni rafiki yangu mpendwa Epaineto, aliyekuwa mtu wa kwanza kumwamini Kristo huko Asia.

6Msalimuni Maria, aliyefanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu.

716:7 Gal 1:22Wasalimuni Androniko na Yunia, jamaa zangu ambao wamekuwa gerezani pamoja nami. Wao ni maarufu miongoni mwa mitume, nao walikuwa katika Kristo kabla yangu.

8Msalimuni Ampliato, yeye nimpendaye katika Bwana.

916:9 Rum 16:3Msalimuni Urbano, mtendakazi mwenzetu katika Kristo, pamoja na rafiki yangu mpendwa Stakisi.

1016:10 Mdo 11:14Msalimuni Apele aliyejaribiwa na akaithibitisha imani yake katika Kristo.

Wasalimuni wote walio nyumbani mwa Aristobulo.

1116:11 Rum 16:7, 21; Mdo 11:14Msalimuni ndugu yangu Herodioni.

Wasalimuni wote walio nyumbani mwa Narkisi walio katika Bwana.

12Wasalimuni Trifaina na Trifosa, wale wanawake wanaofanya kazi kwa bidii katika Bwana.

Msalimuni rafiki yangu mpendwa Persisi, mwanamke mwingine aliyefanya kazi kwa bidii katika Bwana.

1316:13 Mk 15:21Msalimuni Rufo, mteule katika Bwana, pamoja na mama yake, ambaye amekuwa mama kwangu pia.

14Wasalimuni Asinkrito, Flegoni, Herme, Patroba, Herma na ndugu wote walio pamoja nao.

1516:15 Mdo 9:13; 16; 2Wasalimuni Filologo, Yulia, Nerea na dada yake, na Olimpa na watakatifu wote walio pamoja nao.

1616:16 1The 5:26; 1Pet 5:14Salimianeni ninyi kwa ninyi kwa busu takatifu.

Makanisa yote ya Kristo yanawasalimu.

Maelekezo Ya Mwisho

1716:17 1Tim 1:3; 6:3; Mt 18:15-17; 1Kor 14:20Ndugu zangu, nawasihi mjihadhari na kujiepusha na wale watu waletao matengano na kuweka vikwazo mbele yenu dhidi ya mafundisho mliyojifunza. 1816:18 Flp 3:19; Kol 2:4Kwa maana watu kama hao hawamtumikii Bwana Kristo, bali wanatumikia tamaa zao wenyewe. Kwa kutumia maneno laini na ya kubembeleza, hupotosha mioyo ya watu wajinga. 1916:19 Rum 1:8; Mt 10:16; 1Kor 14:20Kila mtu amesikia juu ya utii wenu, nami nimejawa na furaha tele kwa ajili yenu. Lakini nataka mwe na hekima katika mambo mema na bila hatia katika mambo maovu.

2016:20 Rum 15:33; Mwa 3:15Mungu wa amani atamponda Shetani chini ya miguu yenu upesi.

Neema ya Bwana wetu Yesu iwe nanyi. Amen.

2116:21 Mdo 16:1; 13:1; 17:6Timotheo, mtendakazi mwenzangu anawasalimu. Vivyo hivyo Lukio, Yasoni, na Sosipatro, ndugu zangu.

22Mimi, Tertio, niliye mwandishi wa waraka huu, nawasalimu katika Bwana.

2316:23 Mdo 19:22Gayo, ambaye ni mwenyeji wangu na wa kanisa lote, anawasalimu.

Erasto, mweka hazina wa mji huu, pamoja na Kwarto ndugu yetu pia wanawasalimu.

[ 2416:24 Rum 16:20; 1The 5:28Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe pamoja nanyi nyote. Amen.]

Maneno Ya Mwisho Ya Kumsifu Mungu

2516:25 Flp 3:20; Rum 2:16; Isa 48:6; 1Tim 3:16Sasa atukuzwe yeye awezaye kuwafanya ninyi imara kwa Injili yangu na kuhubiriwa kwa Yesu Kristo, kutokana na kufunuliwa siri zilizofichika tangu zamani za kale. 2616:26 Efe 1:9; 2Tim 1:10; Tit 1:2, 3; 1Pet 1:20; Mdo 6:7Lakini sasa siri hiyo imefunuliwa na kujulikana kupitia maandiko ya kinabii kutokana na amri ya Mungu wa milele, ili mataifa yote yaweze kumwamini na kumtii 2716:27 Rum 11:36; 1Tim 1:17; 6:16; Yud 25Mungu aliye pekee, mwenye hekima, ambaye kwa njia ya Yesu Kristo utukufu ni wake milele na milele! Amen.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

羅馬書 16:1-27

介紹菲比

1現在我給你們推薦我們的姊妹菲比,她是堅革哩教會的女執事。 2請你們因為在主裡的關係,照著做聖徒的本分接待她。無論她有什麼需要,請你們幫助她,因為她幫助過许多人,也幫助過我。

問候聖徒

3請代我問候百基拉亞居拉夫婦,他們是我在基督耶穌裡的同工, 4為了救我將生死置之度外。不但我感謝他們,就是外族人的教會也感謝他們。 5請問候在他們家中聚會的教會。請問候我所愛的以拜尼土,他在亞細亞最先信主。 6請問候瑪麗亞。她為你們受盡了勞苦。 7請問候安多尼古猶尼亞,他們是我的親人,曾與我一同坐牢,同受患難,在使徒中很有名望,比我先信基督。 8請問候我在主裡所愛的暗伯利9請問候在基督裡與我同工的耳巴奴和我所愛的士大古10請問候亞比利,他在基督裡曾受過考驗。請問候亞利多布全家。 11請問候我的親戚希羅天。請問候拿其數家中的信徒。 12請問候土非娜土富撒,她們都為主勞苦。請問候我所愛的彼息,她為主多受勞苦。 13請問候主所揀選的魯孚,也問候他的母親,他的母親就是我的母親。 14請問候亞遜其土弗勒干黑米八羅巴黑馬和他們當中的其他弟兄姊妹。 15請問候非羅羅古猶利亞尼利亞和他的妹妹、阿林巴和他們那裡的眾聖徒。 16你們要以聖潔的吻彼此問候。基督的眾教會都問候你們。

提防悖逆者

17弟兄姊妹,我勸你們要留意那些製造分裂、設置障礙、背離你們所學之道的人,你們要避開他們。 18他們並不是在事奉我們的主基督,只是為了滿足自己的慾望,用花言巧語欺騙單純善良的人。 19你們對主的順服已人人皆知,我為你們高興,我希望你們在好事上聰明,在壞事上無知。 20賜平安的上帝快要把撒旦踐踏在你們腳下了。願我們主耶穌的恩典常與你們同在!

其他人的問候

21我的同工提摩太和我的親屬路求耶孫所西巴德問候你們。 22我這為保羅代筆寫信的德特在主裡問候你們。 23接待我也接待全教會的該猶問候你們。 24主管本城財政的以拉都問候你們,括土弟兄也問候你們。

25感謝上帝!祂能使你們剛強,正如我所傳講的福音和耶穌基督的教導。這福音是自古隱藏、從未顯明的奧祕, 26如今按著永恆上帝的命令,藉著先知們所寫的經書公諸於世,讓世人都信從耶穌基督。 27願榮耀藉著耶穌基督歸於獨一全智的上帝,直到永遠。阿們!