Warumi 15 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Warumi 15:1-33

Usijipendeze Mwenyewe, Bali Wapendeze Wengine

115:1 Rum 14:1; 1The 5:14Sisi tulio na nguvu, hatuna budi kuchukuliana na kushindwa kwa wale walio dhaifu wala si kujipendeza nafsi zetu wenyewe. 215:2 1Kor 10:33Kila mmoja wetu inampasa kumpendeza jirani yake kwa mambo mema, ili kumjenga katika imani. 315:3 2Kor 8:9; Za 69:9Kwa maana hata Kristo hakujipendeza mwenyewe, bali kama ilivyoandikwa: “Matukano yao wale wanaokutukana wewe yalinipata mimi.” 415:4 Rum 4:23, 24; 1Kor 10:11; 9:9, 10; 10:11; 2Tim 3:16, 17Kwa maana kila kitu kilichoandikwa zamani, kiliandikwa kutufundisha, ili kwamba kwa saburi na faraja tunayopata katika Maandiko tuwe na tumaini.

515:5 2Kor 13:11; Efe 4:3Mungu atoaye saburi na faraja, awajalie ninyi roho ya umoja miongoni mwenu mnapomfuata Kristo Yesu, 615:6 Ufu 1; 6; Za 34:3; Mdo 4:24, 32ili kwa moyo mmoja mpate kumtukuza Mungu aliye Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo.

Injili Sawa Kwa Wayahudi Na Kwa Watu Wa Mataifa

715:7 Rum 14:1; 5:2Karibishaneni ninyi kwa ninyi kama Kristo alivyowakaribisha ninyi ili kumletea Mungu utukufu. 815:8 Mt 15:24; Mdo 3:25, 26; 2Kor 1:20Kwa maana nawaambia kwamba, Kristo amekuwa mtumishi kwa wale waliotahiriwa ili kuonyesha kweli ya Mungu na kuthibitisha zile ahadi walizopewa baba zetu wa zamani, 915:9 Rum 3:29; Mt 9:8; 2Sam 22:50; Za 18:49pia ili watu wa Mataifa wamtukuze Mungu kwa rehema zake. Kama ilivyoandikwa:

“Kwa hiyo nitakutukuza katikati ya watu wa Mataifa;

nitaliimbia sifa jina lako.”

1015:10 Kum 32:43Tena yasema,

“Enyi watu wa Mataifa, furahini

pamoja na watu wa Mungu.”

1115:11 Za 117:1Tena,

“Msifuni Bwana, ninyi watu wa Mataifa wote,

na kumwimbia sifa, enyi watu wote.”

1215:12 Ufu 5:5; Isa 11:10; Mt 12:21Tena Isaya anasema,

“Shina la Yese litachipuka,

yeye atakayeinuka ili kutawala juu ya mataifa.

Watu wa Mataifa watamtumaini.”

1315:13 Rum 14:17; 1Kor 4:20Mungu wa tumaini awajaze ninyi furaha yote na amani katika kumwamini, ili mpate kujawa na tumaini tele kwa nguvu ya Roho Mtakatifu.

Paulo Mhudumu Wa Watu Wa Mataifa

1415:14 Efe 5:9; 2Pet 1:12Ndugu zangu, mimi mwenyewe ninasadiki kwamba mmejaa wema na ufahamu wote, tena mnaweza kufundishana ninyi kwa ninyi. 1515:15 Rum 12:3; 1:5; 12:3; Gal 1:15; Efe 3:7, 8Nimewaandikia kwa ujasiri vipengele kadha wa kadha katika waraka huu kama kuwakumbusha tena kwa habari ya ile neema Mungu aliyonipa, 1615:16 Mdo 9:5; Rum 11:13; 1:1; Isa 66:20ili kuwa mhudumu wa Kristo Yesu kwa watu wa Mataifa nikiwa na huduma ya kikuhani ya kutangaza Injili ya Mungu, ili watu wa Mataifa wapate kuwa dhabihu inayokubaliwa na Mungu, iliyotakaswa na Roho Mtakatifu.

1715:17 Flp 3:3; Ebr 2:17Kwa hiyo ninajisifu katika Kristo Yesu, kwenye utumishi wangu kwa Mungu. 1815:18 Mdo 15:12; Rum 1:15; 16:26Kwa maana sitathubutu kusema kitu chochote zaidi ya kile ambacho Kristo amefanya kwa kunitumia mimi katika kuwaongoza watu wa Mataifa wamtii Mungu kwa yale niliyosema na kufanya, 1915:19 Yn 4:48; Mdo 19:11; 22:17-21kwa nguvu za ishara na miujiza, kwa uweza wa Roho wa Mungu, hivyo kuanzia Yerusalemu hadi maeneo yote ya kandokando yake mpaka Iliriko, nimekwisha kuihubiri Injili ya Kristo kwa ukamilifu. 2015:20 2Kor 10:15, 16Hivyo ni nia yangu kuhubiri Habari Njema, si pale ambapo Kristo amekwisha kujulikana, ili nisije nikajenga juu ya msingi wa mtu mwingine. 2115:21 Isa 52:15Lakini kama ilivyoandikwa:

“Wale ambao hawajahubiriwa habari zake wataona,

nao wale ambao hawajazisikia watafahamu.”

2215:22 Rum 1:13Hii ndiyo sababu nimezuiliwa mara nyingi nisiweze kuja kwenu.

Paulo Apanga Kwenda Rumi

2315:23 Mdo 19:21; 24:17Lakini sasa kwa kuwa hakuna nafasi zaidi kwa ajili yangu katika sehemu hii, ninatamani kuja kwenu kama ambavyo nimekuwa na shauku kwa miaka mingi. 2415:24 Rum 15:28; 1Kor 16:6; Tit 3:1Nimekusudia kufanya hivyo nitakapokuwa njiani kwenda Hispania. Natarajia kuwaona katika safari yangu na kusafirishwa nanyi mpaka huko, baada ya kufurahia ushirika wenu kwa kitambo kidogo. 2515:25 Mdo 19:21; 24:17Sasa, niko njiani kuelekea Yerusalemu kwa ajili ya kuwahudumia watakatifu huko. 2615:26 Rum 16:9; 2Kor 1:11; Kol 4:12Kwa kuwa imewapendeza watu wa Makedonia na Akaya kufanya changizo kwa ajili ya maskini walioko miongoni mwa watakatifu huko Yerusalemu. 2715:27 1Kor 9:11; Rum 9:4; 11:17; Gal 6:6Imewapendeza kufanya hivyo, naam, kwani ni wadeni wao. Kwa maana ikiwa watu wa Mataifa wameshiriki baraka za rohoni za Wayahudi, wao ni wadeni wa Wayahudi, ili Wayahudi nao washiriki baraka zao za mambo ya mwilini. 2815:28 Flp 4:17; Rum 15:24Kwa hiyo baada ya kukamilisha kazi hii na kuhakikisha kuwa wamepokea kila kitu kilichokusanywa, nitapitia kwenu nikiwa njiani kwenda Hispania. 2915:29 Rum 1:10; 1:11Ninajua kwamba nitakapokuja kwenu, nitakuja na wingi wa baraka za Kristo.

3015:30 Gal 5:22; 2Kor 1:11; Kol 4:12Basi, ndugu zangu, nawasihi kwa Jina la Bwana wetu Yesu Kristo na kwa upendo wa Roho Mtakatifu, kujiunga nami katika taabu zangu mkiniombea kwa Mungu. 3115:31 2Kor 1:10; 2Tim 3:11Ombeni ili nipate kuokolewa mikononi mwa wale wasioamini walioko Uyahudi, na kwamba utumishi wangu upate kukubaliwa na watakatifu wa huko Yerusalemu, 3215:32 Mdo 18:21; Rum 1:10, 13; 1Kor 16:18ili kwa mapenzi ya Mungu niweze kuja kwenu kwa furaha, nami niburudishwe pamoja nanyi. 3315:33 2The 3:16Mungu wa amani na awe pamoja nanyi nyote. Amen.

New International Version – UK

Romans 15:1-33

1We who are strong ought to bear with the failings of the weak and not to please ourselves. 2Each of us should please our neighbours for their good, to build them up. 3For even Christ did not please himself but, as it is written: ‘The insults of those who insult you have fallen on me.’15:3 Psalm 69:9 4For everything that was written in the past was written to teach us, so that through the endurance taught in the Scriptures and the encouragement they provide we might have hope.

5May the God who gives endurance and encouragement give you the same attitude of mind towards each other that Christ Jesus had, 6so that with one mind and one voice you may glorify the God and Father of our Lord Jesus Christ.

7Accept one another, then, just as Christ accepted you, in order to bring praise to God. 8For I tell you that Christ has become a servant of the Jews15:8 Greek circumcision on behalf of God’s truth, so that the promises made to the patriarchs might be confirmed 9and, moreover, that the Gentiles might glorify God for his mercy. As it is written:

‘Therefore I will praise you among the Gentiles;

I will sing the praises of your name.’15:9 2 Samuel 22:50; Psalm 18:49

10Again, it says,

‘Rejoice, you Gentiles, with his people.’15:10 Deut. 32:43

11And again,

‘Praise the Lord, all you Gentiles;

let all the peoples extol him.’15:11 Psalm 117:1

12And again, Isaiah says,

‘The Root of Jesse will spring up,

one who will arise to rule over the nations;

in him the Gentiles will hope.’15:12 Isaiah 11:10 (see Septuagint)

13May the God of hope fill you with all joy and peace as you trust in him, so that you may overflow with hope by the power of the Holy Spirit.

Paul the minister to the Gentiles

14I myself am convinced, my brothers and sisters, that you yourselves are full of goodness, filled with knowledge and competent to instruct one another. 15Yet I have written to you quite boldly on some points to remind you of them again, because of the grace God gave me 16to be a minister of Christ Jesus to the Gentiles. He gave me the priestly duty of proclaiming the gospel of God, so that the Gentiles might become an offering acceptable to God, sanctified by the Holy Spirit.

17Therefore I glory in Christ Jesus in my service to God. 18I will not venture to speak of anything except what Christ has accomplished through me in leading the Gentiles to obey God by what I have said and done – 19by the power of signs and wonders, through the power of the Spirit of God. So from Jerusalem all the way round to Illyricum, I have fully proclaimed the gospel of Christ. 20It has always been my ambition to preach the gospel where Christ was not known, so that I would not be building on someone else’s foundation. 21Rather, as it is written:

‘Those who were not told about him will see,

and those who have not heard will understand.’15:21 Isaiah 52:15 (see Septuagint)

22This is why I have often been hindered from coming to you.

Paul’s plan to visit Rome

23But now that there is no more place for me to work in these regions, and since I have been longing for many years to visit you, 24I plan to do so when I go to Spain. I hope to see you while passing through and that you will assist me on my journey there, after I have enjoyed your company for a while. 25Now, however, I am on my way to Jerusalem in the service of the Lord’s people there. 26For Macedonia and Achaia were pleased to make a contribution for the poor among the Lord’s people in Jerusalem. 27They were pleased to do it, and indeed they owe it to them. For if the Gentiles have shared in the Jews’ spiritual blessings, they owe it to the Jews to share with them their material blessings. 28So after I have completed this task and have made sure that they have received this contribution, I will go to Spain and visit you on the way. 29I know that when I come to you, I will come in the full measure of the blessing of Christ.

30I urge you, brothers and sisters, by our Lord Jesus Christ and by the love of the Spirit, to join me in my struggle by praying to God for me. 31Pray that I may be kept safe from the unbelievers in Judea and that the contribution I take to Jerusalem may be favourably received by the Lord’s people there, 32so that I may come to you with joy, by God’s will, and in your company be refreshed. 33The God of peace be with you all. Amen.