Warumi 10 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Warumi 10:1-21

110:1 Za 20:4; Mdo 22:23Ndugu zangu, shauku ya moyo wangu na maombi yangu kwa Mungu ni kwa ajili ya Waisraeli, kwamba waokolewe. 210:2 Mdo 21:20; 22:3; Gal 1:14; 4:17; Rum 9:32Kwa maana ninaweza nikashuhudia wazi kwamba wao wana juhudi kubwa kwa ajili ya Mungu, lakini juhudi yao haina maarifa. 310:3 Rum 1:17; 9:31; Flp 3:9Kwa kuwa hawakuijua haki itokayo kwa Mungu, wakatafuta kuweka haki yao wenyewe, hawakujitia chini ya haki ya Mungu. 4Kwa maana Kristo ni ukomo wa sheria ili kuwe na haki kwa kila mtu aaminiye.

Wokovu Ni Kwa Ajili Ya Wote

5Mose anaandika kuhusu haki ile itokanayo na sheria, kwamba, “Mtu atendaye matendo hayo ataishi kwa hayo.” 610:6 Rum 9:30; Kut 30:12Lakini ile haki itokanayo na imani husema hivi: “Usiseme moyoni mwako, ‘Ni nani atakayepanda mbinguni?’ ” (yaani ili kumleta Kristo chini) 710:7 Kum 30:13; Mdo 2:24“au ‘Ni nani atashuka kwenda kuzimu?’ ” (yaani ili kumleta Kristo kutoka kwa wafu.) 810:8 Kum 30:14Lakini andiko lasemaje? “Lile neno liko karibu nawe, liko kinywani mwako na moyoni mwako,” yaani, lile neno la imani tunalolihubiri. 910:9 Mt 10:32; Lk 12:8; Mdo 2:24Kwa sababu kama ukikiri kwa kinywa chako kwamba “Yesu ni Bwana,” na kuamini moyoni mwako kwamba Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, utaokoka. 10Kwa maana kwa moyo mtu huamini na hivyo kuhesabiwa haki, tena kwa kinywa mtu hukiri na hivyo kupata wokovu. 1110:11 Isa 28:16; Mt 28:18; Mdo 10:36Kama yasemavyo Maandiko, “Yeyote amwaminiye hataaibika kamwe.” 12Kwa maana hakuna tofauti kati ya Myahudi na Myunani, yeye ni Bwana wa wote, mwenye utajiri kwa wote wamwitao. 1310:13 Mdo 2:21; Yoe 2:32Kwa maana, “Kila mtu atakayeliitia Jina la Bwana, ataokolewa.”

1410:14 Tit 1:3Lakini watamwitaje yeye ambaye hawajamwamini? Nao watawezaje kumwamini yeye ambaye hawajamsikia? Tena watamsikiaje bila mtu kuwahubiria? 1510:15 Isa 52:7Nao watahubirije wasipopelekwa? Kama ilivyoandikwa, “Tazama jinsi ilivyo mizuri miguu yao wale wanaohubiri habari njema!”

1610:16 Isa 53:1Lakini si wote waliotii Habari Njema. Kwa maana Isaya asema, “Bwana, ni nani aliyeamini ujumbe wetu?” 1710:17 Gal 3:2, 5; Kol 3:16Basi, imani chanzo chake ni kusikia, na kusikia huja kwa neno la Kristo. 1810:18 Za 19:4; Mt 24:14Lakini nauliza: Je, wao hawakusikia? Naam, wamesikia, kwa maana:

“Sauti yao imeenea duniani pote,

nayo maneno yao yameenea

hadi miisho ya ulimwengu.”

1910:19 Rum 11:11, 14; Kut 32:21Nami nauliza tena: Je, Waisraeli hawakuelewa? Kwanza, Mose asema,

“Nitawafanya mwe na wivu

kwa watu wale ambao si taifa.

Nitawakasirisha kwa taifa

lile lisilo na ufahamu.”

2010:20 Isa 65:1; Rum 9:20Naye Isaya kwa ujasiri mwingi anasema,

“Nimeonekana na watu wale ambao hawakunitafuta.

Nilijifunua kwa watu

wale ambao hawakunitafuta.”

2110:21 Isa 65:2; Yer 35:17Lakini kuhusu Israeli anasema,

“Mchana kutwa nimewanyooshea

watu wakaidi na wasiotii mikono yangu.”

New International Version – UK

Romans 10:1-21

1Brothers and sisters, my heart’s desire and prayer to God for the Israelites is that they may be saved. 2For I can testify about them that they are zealous for God, but their zeal is not based on knowledge. 3Since they did not know the righteousness of God and sought to establish their own, they did not submit to God’s righteousness. 4Christ is the culmination of the law so that there may be righteousness for everyone who believes.

5Moses writes this about the righteousness that is by the law: ‘The person who does these things will live by them.’10:5 Lev. 18:5 6But the righteousness that is by faith says: ‘Do not say in your heart, “Who will ascend into heaven?” ’10:6 Deut. 30:12 (that is, to bring Christ down) 7‘or “Who will descend into the deep?” ’10:7 Deut. 30:13 (that is, to bring Christ up from the dead). 8But what does it say? ‘The word is near you; it is in your mouth and in your heart,’10:8 Deut. 30:14 that is, the message concerning faith that we proclaim: 9if you declare with your mouth, ‘Jesus is Lord,’ and believe in your heart that God raised him from the dead, you will be saved. 10For it is with your heart that you believe and are justified, and it is with your mouth that you profess your faith and are saved. 11As Scripture says, ‘Anyone who believes in him will never be put to shame.’10:11 Isaiah 28:16 (see Septuagint) 12For there is no difference between Jew and Gentile – the same Lord is Lord of all and richly blesses all who call on him, 13for, ‘Everyone who calls on the name of the Lord will be saved.’10:13 Joel 2:32

14How, then, can they call on the one they have not believed in? And how can they believe in the one of whom they have not heard? And how can they hear without someone preaching to them? 15And how can anyone preach unless they are sent? As it is written: ‘How beautiful are the feet of those who bring good news!’10:15 Isaiah 52:7

16But not all the Israelites accepted the good news. For Isaiah says, ‘Lord, who has believed our message?’10:16 Isaiah 53:1 17Consequently, faith comes from hearing the message, and the message is heard through the word about Christ. 18But I ask: did they not hear? Of course they did:

‘Their voice has gone out into all the earth,

their words to the ends of the world.’10:18 Psalm 19:4

19Again I ask: did Israel not understand? First, Moses says,

‘I will make you envious by those who are not a nation;

I will make you angry by a nation that has no understanding.’10:19 Deut. 32:21

20And Isaiah boldly says,

‘I was found by those who did not seek me;

I revealed myself to those who did not ask for me.’10:20 Isaiah 65:1

21But concerning Israel he says,

‘All day long I have held out my hands

to a disobedient and obstinate people.’10:21 Isaiah 65:2