Walawi 7 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Walawi 7:1-38

Sadaka Ya Hatia

17:1 Law 5:15; Eze 40:39; Kut 29:27; Law 6:17; 21:22“ ‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya hatia, ambayo ni takatifu sana: 2Sadaka ya hatia itachinjiwa mahali pale ambapo sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa, nayo damu yake itanyunyizwa pande zote za madhabahu. 37:3 Kut 29:13; Law 3:4-9Mafuta yake yote yatatolewa sadaka: mafuta ya mkia na mafuta yale yanayofunika sehemu za ndani, 47:4 Law 3:15figo zote mbili pamoja na mafuta yanayozizunguka yaliyo karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo yataondolewa pamoja na hizo figo. 57:5 Kut 29:13; Tit 2:14; Ebr 9:28Kuhani atayateketeza juu ya madhabahu kuwa sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto. Hii ni sadaka ya hatia. 67:6 Law 6:18; Eze 42:13; Law 3:3; Za 93:5; Law 14:13Mwanaume yeyote katika jamaa ya kuhani aweza kuila, lakini lazima iliwe mahali patakatifu; ni takatifu sana.

77:7 Kut 30:10; Law 5:15; 2:3; 6:17; 14:13; 2Fal 12:16; 1Kor 9:13; 10:18; Hes 5:8“ ‘Sheria hii ya sadaka ya hatia ni sawasawa na ile ya sadaka ya dhambi: Nyama ya yule mnyama aliyetolewa sadaka ni ya yule kuhani anayesimamia ibada ya upatanisho. 8Kuhani anayetoa sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya mtu yeyote anaweza kuichukua ngozi ya mnyama yule aliyetolewa iwe yake. 97:9 Law 2:4-7; Hes 18:9; Eze 44:29Kila sadaka ya nafaka iliyookwa jikoni au kupikwa katika sufuria au katika kikaangio itakuwa ya kuhani anayeitoa. 10Nayo kila sadaka ya nafaka, iwe imechanganywa na mafuta au iko kavu, itakuwa ya wana wa Aroni, nayo itagawanywa sawa kati yao.

Sadaka Ya Amani

11“ ‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya amani ambayo mtu aweza kuileta kwa Bwana:

127:12 Law 2:1-4; 22:29; Za 50:14; 54:6; 107:22; 116:17; Yer 33:11; 44:19; Hes 6:19“ ‘Ikiwa mtu atatoa sadaka ya amani kwa ajili ya kuonyesha shukrani, pamoja na sadaka hii ya shukrani, atatoa maandazi yasiyotiwa chachu yaliyochanganywa na mafuta, mikate myembamba isiyotiwa chachu iliyopakwa mafuta, maandazi ya unga laini uliokandwa vizuri na kuchanganywa na mafuta. 137:13 Kut 34:22; Law 23:17; Amo 4:5Pamoja na sadaka hii ya amani ya shukrani ataleta sadaka ya maandazi yaliyotengenezwa kwa chachu. 147:14 Hes 18:8Ataleta moja ya kila aina ya andazi kama sadaka, matoleo kwa Bwana; hii ni ya kuhani anayenyunyiza damu ya sadaka ya amani. 157:15 Kut 12:10; Law 22:30; Ebr 3:13-15Nyama ya sadaka ya amani kwa ajili ya shukrani lazima iliwe siku iyo hiyo inapotolewa; hutabakiza kitu chochote mpaka asubuhi.

167:16 Mwa 28:20; Kum 12:6; 23:21-23; Kut 35:29; Law 19:5-9; 22:18-21; 23:38; Hes 15:3; 29:39; Za 54:6; Eze 46:12“ ‘Lakini kama sadaka yake ni kwa ajili ya nadhiri au ni sadaka ya hiari, sadaka hiyo italiwa siku hiyo inapotolewa, lakini chochote kinachobakia kinaweza kuliwa kesho yake. 177:17 Kut 12:10; Law 19:6Nyama yoyote ya sadaka inayobaki mpaka siku ya tatu lazima iteketezwe kwa moto. 187:18 2Nya 33:16; Law 5:1; 19:7; Hes 18:27; Mwa 4:4-5; Mit 15:8; 21:27; Yer 6:20; Amo 5:22Kama nyama yoyote ya sadaka ya amani italiwa siku ya tatu, Bwana hataikubali. Haitahesabiwa kwake huyo aliyeitoa, kwa kuwa ni najisi. Mtu atakayekula sehemu yake yoyote atahesabiwa hatia.

19“ ‘Nyama ile inayogusa chochote ambacho ni najisi kwa kawaida ya ibada kamwe haitaliwa, ni lazima iteketezwe kwa moto. Kuhusu nyama nyingine, mtu yeyote aliye safi kwa kawaida ya ibada anaweza kuila. 207:20 Law 5:3; 22:3-7; Mwa 17:14; Law 15:3Lakini kama mtu yeyote najisi akila nyama yoyote ya sadaka ya amani iliyotolewa kwa Bwana, huyo mtu lazima akatiliwe mbali na watu wake. 217:21 Law 5:2; 11:24-28; 11:10-13; Kum 14:3; Eze 4:14Kama mtu yeyote akigusa kitu kilicho najisi, iwe ni uchafu wa mwanadamu, au mnyama najisi, au kitu chochote kilicho najisi, kitu cha kuchukiza, kisha akala nyama yoyote ya sadaka ya amani iliyotolewa kwa Bwana, mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.’ ”

Kula Mafuta Na Kunywa Damu Kwakatazwa

22Bwana akamwambia Mose, 237:23 Law 17:13; Kum 14:4; 1Sam 2:29“Waambie Waisraeli: ‘Msile mafuta yoyote ya ngʼombe, kondoo wala mbuzi. 247:24 Kut 22:31Mafuta ya mnyama aliyekutwa amekufa au ameraruliwa na mnyama pori yanaweza kutumika kwa kazi nyingine yoyote, lakini kamwe msiyale. 25Mtu yeyote alaye mafuta ya mnyama ambaye ametolewa sadaka kwa Bwana kwa moto ni lazima akatiliwe mbali na watu wake. 267:26 Mwa 9:4; Law 3:17; 17:10-14; Kum 12:16; 1Sam 14:33; Eze 44:15; Mdo 15:20Popote mtakapoishi, kamwe msinywe damu ya ndege yeyote wala ya mnyama. 277:27 Mwa 9:4; Mdo 15:20-29Ikiwa mtu yeyote atakunywa damu, mtu huyo lazima akatiliwe mbali na watu wake.’ ”

Fungu La Makuhani

28Bwana akamwambia Mose, 29“Waambie Waisraeli: ‘Mtu yeyote aletaye sadaka ya amani kwa Bwana ataleta sehemu ya sadaka hiyo kama dhabihu yake kwa Bwana. 307:30 Kut 29:24; Hes 6:20; Law 8:27; 9:21Ataleta sadaka kwa mikono yake mwenyewe iliyotolewa kwa Bwana kwa moto; ataleta mafuta ya huyo mnyama pamoja na kidari, naye atainua hicho kidari mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa. 317:31 Kut 29:27, 31Kuhani atayateketeza hayo mafuta juu ya madhabahu, lakini kidari kitakuwa cha Aroni na wanawe. 327:32 Kut 29:27; Law 10:14-15; Hes 5:9; 6:20; 18:18Paja la kulia la sadaka zako za amani utampa kuhani kama matoleo. 33Mwana wa Aroni atoaye damu na mafuta ya sadaka ya amani ndiye atakayepewa paja hilo la kulia kuwa fungu lake. 347:34 Kut 29:22, 27; Law 10:15; Hes 6:20; 18:18-19; 1Sam 9:24Kutoka kwenye sadaka za amani za Waisraeli, mimi Mungu nimepokea kidari kile kilichoinuliwa pamoja na lile paja lililotolewa, nami nimevitoa kwa kuhani Aroni na wanawe kuwa fungu lao la kawaida kutoka kwa Waisraeli.’ ”

35Hii ndiyo sehemu ya sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto, ambazo zilitengwa kwa ajili ya Aroni na wanawe siku ile walipowekwa wakfu ili kumtumikia Bwana katika kazi ya ukuhani. 367:36 Law 8:12, 30; Kut 40:13-15; Ebr 7:18-28; 8:1-13Siku ile walipotiwa mafuta, Bwana aliagiza kwamba Waisraeli wawape hili kama fungu lao la kawaida kwa vizazi vijavyo.

377:37 Law 6:9, 14; Kut 29:31; Law 6:20Basi haya ndiyo masharti kuhusu sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya nafaka, sadaka ya dhambi, sadaka ya hatia, sadaka ya kuwekwa wakfu, na sadaka ya amani, 387:38 Law 26:46; Hes 36:13; Kum 4:5; 29:1-3; Kut 19:11ambayo Bwana alimpa Mose juu ya Mlima Sinai siku ile alipowaagiza Waisraeli walete sadaka zao kwa Bwana, katika Jangwa la Sinai.

New International Version

Leviticus 7:1-38

The Guilt Offering

1“ ‘These are the regulations for the guilt offering, which is most holy: 2The guilt offering is to be slaughtered in the place where the burnt offering is slaughtered, and its blood is to be splashed against the sides of the altar. 3All its fat shall be offered: the fat tail and the fat that covers the internal organs, 4both kidneys with the fat on them near the loins, and the long lobe of the liver, which is to be removed with the kidneys. 5The priest shall burn them on the altar as a food offering presented to the Lord. It is a guilt offering. 6Any male in a priest’s family may eat it, but it must be eaten in the sanctuary area; it is most holy.

7“ ‘The same law applies to both the sin offering7:7 Or purification offering; also in verse 37 and the guilt offering: They belong to the priest who makes atonement with them. 8The priest who offers a burnt offering for anyone may keep its hide for himself. 9Every grain offering baked in an oven or cooked in a pan or on a griddle belongs to the priest who offers it, 10and every grain offering, whether mixed with olive oil or dry, belongs equally to all the sons of Aaron.

The Fellowship Offering

11“ ‘These are the regulations for the fellowship offering anyone may present to the Lord:

12“ ‘If they offer it as an expression of thankfulness, then along with this thank offering they are to offer thick loaves made without yeast and with olive oil mixed in, thin loaves made without yeast and brushed with oil, and thick loaves of the finest flour well-kneaded and with oil mixed in. 13Along with their fellowship offering of thanksgiving they are to present an offering with thick loaves of bread made with yeast. 14They are to bring one of each kind as an offering, a contribution to the Lord; it belongs to the priest who splashes the blood of the fellowship offering against the altar. 15The meat of their fellowship offering of thanksgiving must be eaten on the day it is offered; they must leave none of it till morning.

16“ ‘If, however, their offering is the result of a vow or is a freewill offering, the sacrifice shall be eaten on the day they offer it, but anything left over may be eaten on the next day. 17Any meat of the sacrifice left over till the third day must be burned up. 18If any meat of the fellowship offering is eaten on the third day, the one who offered it will not be accepted. It will not be reckoned to their credit, for it has become impure; the person who eats any of it will be held responsible.

19“ ‘Meat that touches anything ceremonially unclean must not be eaten; it must be burned up. As for other meat, anyone ceremonially clean may eat it. 20But if anyone who is unclean eats any meat of the fellowship offering belonging to the Lord, they must be cut off from their people. 21Anyone who touches something unclean—whether human uncleanness or an unclean animal or any unclean creature that moves along the ground7:21 A few Hebrew manuscripts, Samaritan Pentateuch, Syriac and Targum (see 5:2); most Hebrew manuscripts any unclean, detestable thing—and then eats any of the meat of the fellowship offering belonging to the Lord must be cut off from their people.’ ”

Eating Fat and Blood Forbidden

22The Lord said to Moses, 23“Say to the Israelites: ‘Do not eat any of the fat of cattle, sheep or goats. 24The fat of an animal found dead or torn by wild animals may be used for any other purpose, but you must not eat it. 25Anyone who eats the fat of an animal from which a food offering may be7:25 Or offering is presented to the Lord must be cut off from their people. 26And wherever you live, you must not eat the blood of any bird or animal. 27Anyone who eats blood must be cut off from their people.’ ”

The Priests’ Share

28The Lord said to Moses, 29“Say to the Israelites: ‘Anyone who brings a fellowship offering to the Lord is to bring part of it as their sacrifice to the Lord. 30With their own hands they are to present the food offering to the Lord; they are to bring the fat, together with the breast, and wave the breast before the Lord as a wave offering. 31The priest shall burn the fat on the altar, but the breast belongs to Aaron and his sons. 32You are to give the right thigh of your fellowship offerings to the priest as a contribution. 33The son of Aaron who offers the blood and the fat of the fellowship offering shall have the right thigh as his share. 34From the fellowship offerings of the Israelites, I have taken the breast that is waved and the thigh that is presented and have given them to Aaron the priest and his sons as their perpetual share from the Israelites.’ ”

35This is the portion of the food offerings presented to the Lord that were allotted to Aaron and his sons on the day they were presented to serve the Lord as priests. 36On the day they were anointed, the Lord commanded that the Israelites give this to them as their perpetual share for the generations to come.

37These, then, are the regulations for the burnt offering, the grain offering, the sin offering, the guilt offering, the ordination offering and the fellowship offering, 38which the Lord gave Moses at Mount Sinai in the Desert of Sinai on the day he commanded the Israelites to bring their offerings to the Lord.