Walawi 6 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Walawi 6:1-30

Kurudisha Kilichochukuliwa

1Bwana akamwambia Mose: 26:2 Hes 5:6; Za 73:27; Mdo 5:4; Kol 3:9; Law 19:11; Yer 9:4-5; Kut 22:7; Mwa 31:7; Mit 24:28“Kama mtu yeyote akitenda dhambi, naye si mwaminifu kwa Bwana kwa kumdanganya jirani yake kuhusu kitu fulani alichokabidhiwa, au kimeachwa chini ya utunzaji wake, au kimeibwa, au kama akimdanganya, 36:3 Kut 23:4; 22:11; Kum 22:1-3; Law 19:12; Yer 7:9; Zek 5:4au akiokota mali iliyopotea na akadanganya, au kuapa kwa uongo, au kama akitenda dhambi yoyote ambayo watu waweza kuitenda; 46:4 Law 5:16; Eze 33:15; Lk 19:8wakati akitenda dhambi hizo na kuwa mwenye hatia, ni lazima arudishe kile alichokuwa amekiiba au amekichukua kwa dhuluma, au alichokuwa amekabidhiwa, au mali iliyokuwa imepotea akaipata, 56:5 Hes 5:7; Law 5:15; 2Sam 12:6; Lk 19:8au chochote alichokuwa amekiapia kwa uongo. Lazima akirudishe kikamilifu, na aongeze sehemu ya tano ya thamani yake, vyote ampe mwenye mali siku ile anapeleka sadaka yake ya hatia. 66:6 Law 5:15; Hes 5:8; Kut 12:5; Kum 15:21; Efe 5:27; Ebr 9:14; 10:1-17Kisha kama adhabu lazima amletee kuhani, yaani kwa Bwana, kama sadaka yake ya hatia, kondoo dume asiye na dosari na mwenye thamani kamili kutoka kundi lake. 76:7 Kut 32:30; Law 4:26Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana, naye atasamehewa kwa kosa lolote katika mambo hayo aliyoyatenda yaliyomfanya kuwa na hatia.”

Sadaka Ya Kuteketezwa

8Bwana akamwambia Mose: 96:9 Law 7:37“Mpe Aroni na wanawe agizo hili: ‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa: Sadaka ya kuteketezwa itabaki kwenye moto juu ya madhabahu usiku kucha, mpaka asubuhi, nao moto lazima uwe unaendelea kuwaka juu ya madhabahu. 106:10 Kut 39:27, 28; 28:39-43; Law 1:16; Eze 44:17Kisha kuhani atavaa mavazi yake ya kitani, pamoja na nguo za ndani za kitani mwilini wake, na aondoe majivu ya sadaka ya kuteketezwa ambayo moto umeteketeza juu ya madhabahu, na kuyaweka kando ya madhabahu. 116:11 Law 4:12Kisha atayavua mavazi haya na kuvaa mengine, naye achukue yale majivu nje ya kambi na kuyapeleka mahali palipo safi kwa kawaida ya ibada. 126:12 Law 1:7; Kut 29:13; 32:6Moto ulio juu ya madhabahu lazima uwe unaendelea kuwaka, kamwe usizimike. Kila asubuhi kuhani ataongeza kuni na kupanga sadaka ya kuteketezwa juu ya moto, na kuteketeza mafuta ya sadaka za amani juu yake. 136:13 Isa 33:14; Dan 7:10; Mt 25:41Moto lazima uendelee kuwaka juu ya madhabahu mfululizo, kamwe usizimike.

Sadaka Ya Nafaka

146:14 Law 2:1; Hes 6:15; 15:4; 28:13“ ‘Haya ndiyo masharti ya sadaka ya nafaka: Wana wa Aroni wataileta mbele za Bwana, mbele za madhabahu. 156:15 Law 2:1, 9Kuhani atachukua konzi ya unga laini na mafuta, pamoja na uvumba wote ulioko juu ya sadaka ya nafaka, ateketeze sehemu ya kumbukumbu juu ya madhabahu kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana. 166:16 Law 2:2-3, 11; 8:31; 10:13; 16:24; 24:9; Eze 44:29; Kut 27:9; 29:11, 31; Hes 18:10Aroni na wanawe watakula sehemu iliyobaki, lakini italiwa bila kutiwa chachu mahali patakatifu, nao wataila kwenye ua wa Hema la Kukutania. 176:17 Hes 5:9; 18:9-10; Kut 29:28; 40:10; Law 7:7; 10:12; 21:22Kamwe haitaokwa na chachu; nimewapa kama fungu lao la sadaka iliyotolewa kwangu kwa moto. Ni takatifu sana, kama vile ilivyo sadaka ya dhambi na ya hatia. 186:18 Law 2:3; 7:6; Hes 18:9-10; 5:9; Mwa 9:12; Kut 30:29Kila mwanaume mzao wa Aroni aweza kuila. Ni fungu lake la kawaida la sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto kwa vizazi vijavyo. Chochote kinachozigusa kitakuwa kitakatifu.’ ”

19Tena Bwana akamwambia Mose, 206:20 Kut 28:41; 16:36; 29:2; Hes 4:16; 5:15; 28:5; Law 23:13“Hii ni sadaka ambayo Aroni na wanawe wanapaswa kuleta kwa Bwana siku atakapotiwa mafuta: sehemu ya kumi ya efa6:20 Sehemu ya kumi ya efa ni sawa na kilo moja. ya unga laini kama sadaka ya kawaida ya nafaka. Nusu yake ataitoa asubuhi na nusu nyingine jioni. 216:21 Law 2:5; 6:22; Kut 28:41; 29:30; Law 1:9; Isa 53:10; Mt 20:28; Dan 9:26Iandae kwa mafuta kwenye kikaango; ilete ikiwa imechanganywa vizuri, na utoe hiyo sadaka ya nafaka ikiwa imevunjwa vipande vipande kuwa harufu nzuri ya kumpendeza Bwana. 22Mwanawe atakayeingia mahali pake kama kuhani aliyetiwa mafuta ndiye atakayeiandaa. Ni fungu la kawaida la Bwana, nalo litateketezwa kabisa. 23Kila sadaka ya nafaka ya kuhani itateketezwa kabisa; kamwe haitaliwa.”

Sadaka Ya Dhambi

24Bwana akamwambia Mose, 256:25 Kut 29:11; 30:10; Law 4:24; 1:3; Za 93:5“Mwambie Aroni na wanawe: ‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya dhambi: Sadaka ya dhambi itachinjiwa mbele za Bwana mahali sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa, ni takatifu sana. 266:26 Kut 27:9, 21; 40:2; Hes 18:9; Eze 44:27-28Kuhani anayeitoa ndiye atakayeikula; itakuliwa katika mahali patakatifu, katika ua wa Hema la Kukutania. 276:27 Kut 29:37; Law 10:10; Eze 44:19; 46:20; Hag 2:12Chochote kitakachogusa nyama yoyote ya hiyo sadaka kitakuwa kitakatifu, na kama hiyo damu itadondokea juu ya vazi, lazima uifulie mahali patakatifu. 286:28 Law 11:33; 15:12; Hes 19:15Chungu cha udongo kitakachopikiwa nyama lazima kivunjwe, lakini kama imepikiwa kwenye chombo cha shaba, chombo hicho kitasuguliwa na kusuuzwa kwa maji. 296:29 Eze 42:13Kila mwanaume katika familia ya kuhani aweza kula nyama hiyo; ni takatifu sana. 306:30 Eze 45:15; Law 4:12, 18; 16:27; Ebr 13:11Lakini kila sadaka ya dhambi ambayo damu yake imeletwa ndani ya Hema la Kukutania kufanya upatanisho katika Mahali Patakatifu kamwe haitaliwa; lazima iteketezwe.

New International Reader’s Version

Leviticus 6:1-30

1The Lord spoke to Moses. He said, 2“Suppose someone sins by not being faithful to me. They do it by tricking their neighbors. They trick them in connection with something their neighbors have placed in their care. They steal from their neighbors. Or they cheat them. 3Or they find something their neighbors have lost and then tell a lie about it. Or they go to court. They promise to tell the truth. But instead they tell a lie when they are a witness about it. Or they lie when they are witnesses about any other sin like those sins. 4When they sin in any of these ways and realize their guilt, they must return what they stole. They must give back what they took by cheating their neighbors. They must return what their neighbors placed in their care. They must return the lost property they found. 5They must return anything they told a lie about when they were witnesses in court. They must pay back everything in full. They must add a fifth of its value to it. They must give all of it to the owner on the day they bring their guilt offering. 6He must bring their guilt offering to the priest to pay for their sin. It is an offering to me. They must bring a ram from the flock. It must not have any flaws. It must be worth the required amount of money. 7The priest will sacrifice the ram to pay for their sin. He will do it in my sight. And they will be forgiven for any of the things they did that made them guilty.”

More Rules for Burnt Offerings

8The Lord spoke to Moses. He said, 9“Give Aaron and the priests in his family line a command. Tell them, ‘Here are some more rules for burnt offerings. The burnt offering must remain on the altar through the whole night. The fire on the altar must be kept burning until morning. 10The priest must put on his linen clothes. He must put on linen underwear next to his body. He must remove the ashes of the burnt offering that the fire has burned up on the altar. He must place them beside the altar. 11Then he must take his clothes off and put others on. He must carry the ashes outside the camp to a “clean” place. 12The fire on the altar must be kept burning. It must not go out. Every morning the priest must add more wood to the fire. He must place the burnt offering on the fire. He must burn the fat of the friendship offerings on it. 13The fire must be kept burning on the altar all the time. It must not go out.

More Rules for Grain Offerings

14“ ‘Here are some more rules for grain offerings. The priests in Aaron’s family line must bring the grain offering to the Lord in front of the altar. 15The priest must take a handful of the finest flour and olive oil. He must add to it all the incense on the grain offering. He must burn that part on the altar. It will remind him that all good things come from the Lord. Its smell pleases the Lord. 16Aaron and the priests in his family line will eat the rest of it. But they must eat it without yeast in the holy area. They must eat it in the courtyard of the tent of meeting. 17It must not be baked with yeast added to it. The Lord has given it to the priests as their share of the food offerings presented to him. It is very holy, just like the sin offering and the guilt offering. 18Any priests in Aaron’s family line can eat it. It is their share of the food offerings presented to the Lord. It is their share for all time to come. Anyone who touches these offerings will become holy.’ ”

19The Lord spoke to Moses. He said, 20“On the day each high priest in Aaron’s family line is anointed, he must bring an offering to me. He must bring three and a half pounds of the finest flour as a regular grain offering. He must bring half of it in the morning. He must bring the other half in the evening. 21Mix it with olive oil. Cook it on a metal plate. Break it in pieces. Bring it as a grain offering. Its smell pleases the Lord. 22The son of Aaron who will become the next high priest after him will prepare the grain offering. It is the share that must be given to the Lord for all time to come. It must be completely burned up. 23Every grain offering a high priest offers must be completely burned up. It must not be eaten.”

More Rules for Sin Offerings

24The Lord spoke to Moses. He said, 25“Speak to Aaron and the priests in his family line. Tell them, ‘Here are some more rules for sin offerings. You must kill the animal for the sin offering in the sight of the Lord. Kill it in the place where the burnt offering is killed. It is very holy. 26The priest who offers it will eat it. He must eat it in the holy area. He must eat it in the courtyard of the tent of meeting. 27Anyone who touches any of its meat will become holy. Suppose some of the blood is spilled on someone’s clothes. Then you must wash them in the holy area. 28Break the clay pot the meat is cooked in. But suppose you cook it in a bronze pot. Then you must scrub the pot and rinse it with water. 29Any male in a priest’s family may eat the meat. It is very holy. 30But suppose some of the blood of a sin offering is brought into the tent of meeting. And that blood is brought into the Holy Room to pay for sin. Then that sin offering must not be eaten. It must be burned up.