Walawi 6 – NEN & BPH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Walawi 6:1-30

Kurudisha Kilichochukuliwa

1Bwana akamwambia Mose: 26:2 Hes 5:6; Za 73:27; Mdo 5:4; Kol 3:9; Law 19:11; Yer 9:4-5; Kut 22:7; Mwa 31:7; Mit 24:28“Kama mtu yeyote akitenda dhambi, naye si mwaminifu kwa Bwana kwa kumdanganya jirani yake kuhusu kitu fulani alichokabidhiwa, au kimeachwa chini ya utunzaji wake, au kimeibwa, au kama akimdanganya, 36:3 Kut 23:4; 22:11; Kum 22:1-3; Law 19:12; Yer 7:9; Zek 5:4au akiokota mali iliyopotea na akadanganya, au kuapa kwa uongo, au kama akitenda dhambi yoyote ambayo watu waweza kuitenda; 46:4 Law 5:16; Eze 33:15; Lk 19:8wakati akitenda dhambi hizo na kuwa mwenye hatia, ni lazima arudishe kile alichokuwa amekiiba au amekichukua kwa dhuluma, au alichokuwa amekabidhiwa, au mali iliyokuwa imepotea akaipata, 56:5 Hes 5:7; Law 5:15; 2Sam 12:6; Lk 19:8au chochote alichokuwa amekiapia kwa uongo. Lazima akirudishe kikamilifu, na aongeze sehemu ya tano ya thamani yake, vyote ampe mwenye mali siku ile anapeleka sadaka yake ya hatia. 66:6 Law 5:15; Hes 5:8; Kut 12:5; Kum 15:21; Efe 5:27; Ebr 9:14; 10:1-17Kisha kama adhabu lazima amletee kuhani, yaani kwa Bwana, kama sadaka yake ya hatia, kondoo dume asiye na dosari na mwenye thamani kamili kutoka kundi lake. 76:7 Kut 32:30; Law 4:26Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana, naye atasamehewa kwa kosa lolote katika mambo hayo aliyoyatenda yaliyomfanya kuwa na hatia.”

Sadaka Ya Kuteketezwa

8Bwana akamwambia Mose: 96:9 Law 7:37“Mpe Aroni na wanawe agizo hili: ‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa: Sadaka ya kuteketezwa itabaki kwenye moto juu ya madhabahu usiku kucha, mpaka asubuhi, nao moto lazima uwe unaendelea kuwaka juu ya madhabahu. 106:10 Kut 39:27, 28; 28:39-43; Law 1:16; Eze 44:17Kisha kuhani atavaa mavazi yake ya kitani, pamoja na nguo za ndani za kitani mwilini wake, na aondoe majivu ya sadaka ya kuteketezwa ambayo moto umeteketeza juu ya madhabahu, na kuyaweka kando ya madhabahu. 116:11 Law 4:12Kisha atayavua mavazi haya na kuvaa mengine, naye achukue yale majivu nje ya kambi na kuyapeleka mahali palipo safi kwa kawaida ya ibada. 126:12 Law 1:7; Kut 29:13; 32:6Moto ulio juu ya madhabahu lazima uwe unaendelea kuwaka, kamwe usizimike. Kila asubuhi kuhani ataongeza kuni na kupanga sadaka ya kuteketezwa juu ya moto, na kuteketeza mafuta ya sadaka za amani juu yake. 136:13 Isa 33:14; Dan 7:10; Mt 25:41Moto lazima uendelee kuwaka juu ya madhabahu mfululizo, kamwe usizimike.

Sadaka Ya Nafaka

146:14 Law 2:1; Hes 6:15; 15:4; 28:13“ ‘Haya ndiyo masharti ya sadaka ya nafaka: Wana wa Aroni wataileta mbele za Bwana, mbele za madhabahu. 156:15 Law 2:1, 9Kuhani atachukua konzi ya unga laini na mafuta, pamoja na uvumba wote ulioko juu ya sadaka ya nafaka, ateketeze sehemu ya kumbukumbu juu ya madhabahu kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana. 166:16 Law 2:2-3, 11; 8:31; 10:13; 16:24; 24:9; Eze 44:29; Kut 27:9; 29:11, 31; Hes 18:10Aroni na wanawe watakula sehemu iliyobaki, lakini italiwa bila kutiwa chachu mahali patakatifu, nao wataila kwenye ua wa Hema la Kukutania. 176:17 Hes 5:9; 18:9-10; Kut 29:28; 40:10; Law 7:7; 10:12; 21:22Kamwe haitaokwa na chachu; nimewapa kama fungu lao la sadaka iliyotolewa kwangu kwa moto. Ni takatifu sana, kama vile ilivyo sadaka ya dhambi na ya hatia. 186:18 Law 2:3; 7:6; Hes 18:9-10; 5:9; Mwa 9:12; Kut 30:29Kila mwanaume mzao wa Aroni aweza kuila. Ni fungu lake la kawaida la sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto kwa vizazi vijavyo. Chochote kinachozigusa kitakuwa kitakatifu.’ ”

19Tena Bwana akamwambia Mose, 206:20 Kut 28:41; 16:36; 29:2; Hes 4:16; 5:15; 28:5; Law 23:13“Hii ni sadaka ambayo Aroni na wanawe wanapaswa kuleta kwa Bwana siku atakapotiwa mafuta: sehemu ya kumi ya efa6:20 Sehemu ya kumi ya efa ni sawa na kilo moja. ya unga laini kama sadaka ya kawaida ya nafaka. Nusu yake ataitoa asubuhi na nusu nyingine jioni. 216:21 Law 2:5; 6:22; Kut 28:41; 29:30; Law 1:9; Isa 53:10; Mt 20:28; Dan 9:26Iandae kwa mafuta kwenye kikaango; ilete ikiwa imechanganywa vizuri, na utoe hiyo sadaka ya nafaka ikiwa imevunjwa vipande vipande kuwa harufu nzuri ya kumpendeza Bwana. 22Mwanawe atakayeingia mahali pake kama kuhani aliyetiwa mafuta ndiye atakayeiandaa. Ni fungu la kawaida la Bwana, nalo litateketezwa kabisa. 23Kila sadaka ya nafaka ya kuhani itateketezwa kabisa; kamwe haitaliwa.”

Sadaka Ya Dhambi

24Bwana akamwambia Mose, 256:25 Kut 29:11; 30:10; Law 4:24; 1:3; Za 93:5“Mwambie Aroni na wanawe: ‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya sadaka ya dhambi: Sadaka ya dhambi itachinjiwa mbele za Bwana mahali sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa, ni takatifu sana. 266:26 Kut 27:9, 21; 40:2; Hes 18:9; Eze 44:27-28Kuhani anayeitoa ndiye atakayeikula; itakuliwa katika mahali patakatifu, katika ua wa Hema la Kukutania. 276:27 Kut 29:37; Law 10:10; Eze 44:19; 46:20; Hag 2:12Chochote kitakachogusa nyama yoyote ya hiyo sadaka kitakuwa kitakatifu, na kama hiyo damu itadondokea juu ya vazi, lazima uifulie mahali patakatifu. 286:28 Law 11:33; 15:12; Hes 19:15Chungu cha udongo kitakachopikiwa nyama lazima kivunjwe, lakini kama imepikiwa kwenye chombo cha shaba, chombo hicho kitasuguliwa na kusuuzwa kwa maji. 296:29 Eze 42:13Kila mwanaume katika familia ya kuhani aweza kula nyama hiyo; ni takatifu sana. 306:30 Eze 45:15; Law 4:12, 18; 16:27; Ebr 13:11Lakini kila sadaka ya dhambi ambayo damu yake imeletwa ndani ya Hema la Kukutania kufanya upatanisho katika Mahali Patakatifu kamwe haitaliwa; lazima iteketezwe.

Bibelen på hverdagsdansk

3. Mosebog 6:1-23

Regler om de forskellige ofre, henvendt til præsterne

1Herren sagde videre til Moses: 2„Gør Aron og hans sønner bekendt med følgende regler for brændofrene:

Ilden skal holdes ved lige, og brændofferet skal blive liggende på alteret hele natten. 3Næste morgen skal præsten tage sit linnedundertøj og sine linnedbukser på, hvorefter han skal tage asken fra alteret og lægge den i en bunke ved siden af alteret. 4Så skal han skifte tøj og bære asken uden for lejren til det indviede sted. 5Men alterilden skal brænde hele tiden, den må under ingen omstændigheder gå ud. Hver morgen skal præsten lægge nyt brænde på ilden og placere det daglige brændoffer ovenpå, og han skal brænde fedtet som et takoffer. 6Husk at ilden altid skal brænde på alteret, for den må aldrig slukkes.

7De følgende regler gælder afgrødeofferet:

Efter at præsterne har bragt offeret til Herrens alter, 8skal ypperstepræsten tage en håndfuld af det fintmalede mel med olivenolien og røgelsen i og brænde det på alteret som et lifligt afgrødeoffer. 9Resten af melet skal tilhøre Aron og hans sønner, og det brød, de tilbereder af melet, skal laves uden surdej, og det skal spises i åbenbaringsteltets forgård. 10Hvis det drejer sig om ovnbagt brød, gælder samme regel: Der må ikke bruges surdej til brødet. Det er præsternes andel af de ofre, der brændes for mig på alteret, men deres andel er for mig lige så hellig som den del, der brændes på alteret. Det samme gælder synd- og skyldofre. 11Deres del af brændofrene må dog kun spises af præsterne selv, de mandlige efterkommere af Aron, fra generation til generation. Kun de indviede må røre ved det.”

12Derpå sagde Herren til Moses: 13„Samme dag Aron og hans sønner bliver salvet og indsat i deres præsteembede, skal de bringe Herren et almindeligt afgrødeoffer: to liter fintmalet mel. Den ene halvdel skal ofres om morgenen, og den anden halvdel skal ofres om aftenen. 14Det skal tilberedes på bageplade med olivenolie, og efter at brødet er gennembagt, skal det brækkes i stykker og bringes som et lifligt afgrødeoffer. 15Den af Arons efterkommere, der er indsat som ypperstepræst, skal forestå ceremonien. Dette er en permanent lov. 16Og for disse afgrødeofre fra præsterne gælder det, at hele offeret skal brændes. Intet af det må spises.”

17Herren fortsatte: 18„Gør Aron og hans sønner bekendt med følgende regler for syndofrene:

Ethvert dyr, der bringes som syndoffer, er indviet til mig. Dyret skal slagtes samme sted, hvor I slagter brændofferdyrene. 19Den præst, som udfører offerceremonien, skal sørge for, at kødet kun bliver spist i åbenbaringsteltets forgård. 20Kun indviede præster må røre ved kødet, og hvis der kommer blodstænk på deres tøj, skal de vaske tøjet på det sted, der er indviet til det. 21Hvis kødet bliver kogt i en gryde af ler, skal gryden knuses bagefter. Men hvis det er en gryde af bronze, der bruges, skal den skures og skylles grundigt med vand bagefter. 22Kun mænd af præsteslægten må spise af offerkødet, for det er et helligt offer. 23Men hvis syndofferdyrets blod er blevet båret ind i åbenbaringsteltet og brugt som sonoffer i helligdommen, må dets kød ikke spises. I den slags tilfælde skal kødet brændes.