Walawi 4 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Walawi 4:1-35

Sadaka Ya Dhambi

1Bwana akamwambia Mose, 24:2 Law 5:15-18; 22:14; Hes 15:22, 24-29; 35:11-15; Yos 20:3-9; Ebr 9:4; 1Sam 14:27; Za 19:12“Waambie Waisraeli: ‘Mtu yeyote afanyapo dhambi bila kukusudia na akatenda lile lililokatazwa katika amri yoyote ya Bwana:

34:3 Kut 12:5; 28:41; 30:10; Mwa 18:23; Law 3:12; 5:6-13; 9:2-22; 8:14; 10:16; 16:3-5; Hes 15:27; Za 66:15; Eze 43:19-23; Ebr 9:13-14“ ‘Ikiwa kuhani aliyetiwa mafuta amefanya dhambi na kuwaletea watu hatia, lazima alete kwa Bwana fahali mchanga asiye na dosari, kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili ya dhambi aliyotenda. 44:4 Law 1:3; Hes 8:12; 19:4Atamkabidhi huyo fahali kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana. Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha huyo fahali na kumchinja mbele za Bwana. 54:5 Law 16:14Kisha kuhani huyo aliyetiwa mafuta atachukua sehemu ya damu ya huyo fahali na kuileta katika Hema la Kukutania. 64:6 Kut 24:8; 25:8; Law 16:14-19; Isa 42:21; Yn 8:20; Rum 3:24; 2Kor 5:19; Efe 2:13; Ufu 5:9Atachovya kidole chake katika hiyo damu na kuinyunyiza sehemu yake mara saba mbele za Bwana mbele ya pazia la mahali patakatifu. 74:7 Kut 27:2; 29:12; Law 8:15; 5:9; 9:9; 16:18; Ebr 9:21-25; Yos 7:11Kisha kuhani atatia sehemu ya hiyo damu juu ya pembe za madhabahu ya kufukizia uvumba wenye harufu nzuri iliyoko mbele za Bwana katika Hema la Kukutania. Damu iliyobaki ya huyo fahali ataimwaga chini ya hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka kwenye ingilio la Hema la Kukutania. 8Atayaondoa mafuta yote ya fahali huyo wa sadaka ya dhambi, mafuta yale yanayofunika sehemu za ndani au zile zinazounganika nazo, 94:9 Law 3:4figo zote mbili na mafuta yaliyo juu yake karibu na kiuno na yale yanayofunika ini ambayo atayaondoa pamoja na figo zote, 104:10 Kut 32:2; 29:13kama vile mafuta yanayoondolewa kutoka kwenye maksai aliyetolewa sadaka ya amani. Kisha kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa. 114:11 Kut 29:14; Law 8:17; 9:11; Hes 19:5; 4:12; Kut 29:14; Law 1:16; 6:11, 30; 8:17; 9:11; 10:14; Ebr 13:11; Hes 19:9Lakini ngozi ya huyo fahali na nyama zake zote, pamoja na kichwa na miguu yake, sehemu za ndani na matumbo, 12yaani sehemu nyingine zote zilizobaki za huyo fahali, lazima azitoe nje ya kambi mpaka mahali palipo safi kiibada, ambapo majivu hutupwa, naye atamchoma kwa moto juu ya kuni zilizoko juu ya lundo la majivu.

134:13 Hes 15:24-26“ ‘Ikiwa jumuiya yote ya Israeli watatenda dhambi pasipo kukusudia na kufanya lile lililokatazwa katika amri yoyote ya Bwana, hata kama jumuiya haifahamu juu ya jambo hilo, wana hatia. 144:14 Hes 15:24; 4:15; Kut 3:16; 19:7; 29:10; 2Nya 29:23; Hes 8:10; Isa 53:6; Mt 8:17; Ebr 9:2; 9:12-14Wanapotambua kuhusu dhambi waliyoitenda, lazima kusanyiko lilete fahali mchanga kuwa sadaka ya dhambi na kuikabidhi mbele ya Hema la Kukutania. 15Wazee wa jumuiya wataweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo fahali aliye mbele za Bwana, naye fahali atachinjwa mbele za Bwana. 16Kisha kuhani aliyetiwa mafuta ataiingiza sehemu ya damu ya huyo fahali ndani ya Hema la Kukutania. 174:17 Hes 19:4, 18Atachovya kidole chake kwenye damu na kuinyunyiza mara saba mbele za Bwana mbele ya hilo pazia. 184:18 Law 5:9; 6:30; 8:15; 10:18; 17:6; 2Nya 29:22Atatia sehemu ya hiyo damu juu ya pembe za madhabahu yaliyo mbele za Bwana katika Hema la Kukutania. Damu iliyobaki ataimwaga chini ya madhabahu ya kuteketezea sadaka, penye ingilio la Hema la Kukutania. 19Atayaondoa mafuta yote ya yule fahali na kuyateketeza juu ya madhabahu, 204:20 Kut 29:36; 32:30; Rum 3:25; Ebr 10:10-15; Hes 15:25; Dan 9:24naye atamfanyia fahali huyu kama alivyomfanyia yule fahali mwingine wa sadaka ya dhambi. Kwa njia hii kuhani atawafanyia watu upatanisho, nao watasamehewa. 214:21 Law 16:5, 15; 2Nya 29:21Kisha atamchukua yule fahali nje ya kambi na kumteketeza kama alivyomteketeza yule wa kwanza. Hii ni sadaka ya dhambi kwa ajili ya jumuiya.

224:22 Hes 31:13“ ‘Wakati kiongozi ametenda dhambi bila kukusudia na kufanya yaliyokatazwa katika amri yoyote ya Bwana Mungu wake, ana hatia. 234:23 Law 1:10; Kut 18:21; Hes 16:2; Ezr 9:2; Mdo 3:17; 2Sam 21:1-3Atakapofahamishwa dhambi aliyotenda, ni lazima alete mbuzi dume asiye na dosari kama sadaka yake. 244:24 Law 6:25Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha yule mbuzi na kumchinja mahali pale ambapo sadaka za kuteketezwa huchinjiwa mbele za Bwana. Hii ni sadaka ya dhambi. 254:25 Law 9:9; 16:18; Eze 43:20-22Kisha kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya dhambi kwa kidole chake na kuitia kwenye pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketeza, na kuimwaga damu iliyobaki chini ya madhabahu. 264:26 Kut 32:30; Law 5:10; 12:8; Hes 15:28Atayateketeza mafuta yote juu ya madhabahu, kama alivyoteketeza mafuta ya sadaka ya amani. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho wa dhambi kwa ajili ya yule mtu, naye atasamehewa.

274:27 Hes 15:27“ ‘Kama mtu katika jumuiya ametenda dhambi pasipo kukusudia na kufanya lile lililokatazwa katika amri yoyote ya Bwana, yeye ana hatia. 284:28 Eze 40:39; 44:27; Law 1:10Atakapofahamishwa dhambi yake aliyoitenda, ni lazima alete mbuzi jike asiye na dosari kama sadaka yake kwa ajili ya dhambi aliyotenda. 294:29 Law 1:4; Mwa 8:21Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka ya dhambi na kumchinjia mahali pa kuteketezea sadaka. 30Kisha kuhani atachukua sehemu ya ile damu kwa kidole chake na kuitia kwenye pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na kuimwaga damu iliyobaki chini ya madhabahu. 314:31 Mwa 8:21; Law 1:4; 3:14; Kut 29:18; Ezr 6:10Atayaondoa mafuta yote, kama vile mafuta yaondolewavyo kwenye sadaka ya amani, naye kuhani atayateketeza juu ya madhabahu kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake, naye atasamehewa.

324:32 Kut 29:38; Law 9:3; 14:10; 1:3-4; Isa 53:7; Yn 1:29; Mdo 8:32; Ufu 5:6-14“ ‘Ikiwa ataleta mwana-kondoo kama sadaka yake ya dhambi, atamleta jike asiye na dosari. 33Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha huyo mwana-kondoo na kumchinja kwa ajili ya sadaka ya dhambi mahali sadaka ya kuteketezwa huchinjiwa. 34Kisha kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya dhambi kwa kidole chake na kuitia juu ya pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa, na ile damu iliyobaki ataimwaga chini ya madhabahu. 35Ataondoa mafuta yote, kama vile mafuta yaondolewavyo kutoka kwenye mwana-kondoo wa sadaka ya amani, naye kuhani atayateketeza juu ya madhabahu juu ya zile sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake kwa dhambi aliyoitenda, naye atasamehewa.

La Bible du Semeur

Lévitique 4:1-35

Les sacrifices pour le péché

1L’Eternel s’adressa à Moïse en ces termes : 2Parle aux Israélites et dis-leur : Lorsque quelqu’un aura péché involontairement4.2 Par mégarde, ou par erreur. Pour les péchés commis délibérément, voir Nb 15.30. en commettant l’une quelconque des choses qui sont interdites par les commandements de l’Eternel, voici comment on procédera :

Pour le grand-prêtre

3Si c’est le prêtre qui a reçu l’onction4.3 Il s’agit du grand-prêtre, seul consacré par l’onction (Ex 29.7), les autres prêtres l’étant par aspersion (Ex 29.21). qui a péché et qui par là même a chargé le peuple de culpabilité, il offrira à l’Eternel pour le péché qu’il aura commis, un jeune taureau sans défaut, en sacrifice pour le péché. 4Il amènera le taureau à l’entrée de la tente de la Rencontre devant l’Eternel, il posera sa main sur la tête du taureau et l’égorgera devant l’Eternel. 5Le prêtre qui a reçu l’onction prendra du sang de la victime et l’apportera dans la tente de la Rencontre. 6Il trempera son doigt dans le sang et en aspergera sept fois le voile du sanctuaire devant l’Eternel. 7Puis il appliquera de ce sang sur les cornes de l’autel des parfums aromatiques, devant l’Eternel, dans la tente de la Rencontre. Il répandra tout le reste du sang du taureau sur le socle de l’autel des holocaustes situé à l’entrée de la tente de la Rencontre. 8Ensuite, il enlèvera toute la graisse du taureau du sacrifice pour le péché, celle qui recouvre les entrailles et toute celle qui y est attachée, 9les deux rognons et la graisse qui les enveloppe et qui couvre le dos, ainsi que le dessus du foie qu’il ôtera avec les rognons, 10comme on le fait pour le sacrifice de communion. Le prêtre les brûlera sur l’autel des holocaustes. 11Quant à la peau du taureau, toute sa viande, sa tête, ses pattes, ses entrailles avec leur contenu, 12soit tout le reste du taureau, il l’emportera hors du camp en un lieu rituellement pur, où sont déversées les cendres grasses, et il le brûlera sur un feu de bûches, à l’endroit où l’on déverse les cendres.

Pour l’ensemble du peuple

13Si c’est l’ensemble de la communauté d’Israël qui s’est rendue coupable d’un péché involontaire – si, sans le savoir, l’assemblée a fait l’une des choses que l’Eternel a défendues dans ses commandements et s’est ainsi rendue coupable – 14l’assemblée offrira, quand on découvrira la faute, un jeune taureau en sacrifice pour le péché. On l’amènera devant la tente de la Rencontre, 15les responsables de la communauté poseront leurs mains sur la tête du taureau devant l’Eternel, et on l’égorgera devant lui. 16Le prêtre ayant reçu l’onction apportera du sang de la victime dans la tente de la Rencontre. 17Il y trempera son doigt et en aspergera sept fois le voile devant l’Eternel. 18Il appliquera du sang sur les cornes de l’autel, devant l’Eternel dans la tente de la Rencontre. Il répandra tout le reste du sang sur le socle de l’autel des holocaustes situé à l’entrée de la tente. 19Ensuite, il enlèvera toute la graisse et la brûlera sur l’autel. 20Il suivra, pour le reste du taureau, la même procédure que pour le taureau sacrifié pour son péché. Le prêtre accomplira ainsi le rite d’expiation pour eux, et il leur sera pardonné. 21Il fera transporter le taureau hors du camp et le brûlera comme il a été ordonné pour le taureau précédent. Tel est le sacrifice pour le péché de la communauté.

Pour un chef

22Si c’est un chef qui a péché en faisant involontairement l’une des choses que l’Eternel son Dieu a défendues dans ses commandements, et s’il prend conscience de sa faute, 23ou si on lui fait connaître le péché qu’il a commis, il amènera comme sacrifice un bouc mâle sans défaut. 24Il posera sa main sur la tête de la victime avant de l’égorger à l’endroit où l’on égorge l’holocauste devant l’Eternel. C’est un sacrifice pour le péché. 25Le prêtre prendra avec son doigt du sang du sacrifice pour le péché et en appliquera sur les cornes de l’autel des holocaustes ; puis il répandra le reste du sang sur le socle de l’autel des holocaustes. 26Il brûlera toute la graisse sur l’autel, comme dans le cas du sacrifice de communion. Ainsi le prêtre accomplira pour ce chef le rite d’expiation de son péché, et il lui sera pardonné.

Pour un simple membre du peuple

27Si c’est un simple membre du peuple qui a péché en faisant involontairement quelque chose que l’Eternel a défendu dans ses commandements, et s’il prend conscience de sa faute4.27 Pour les v. 27-31, voir Nb 15.27-28., 28ou si on lui fait connaître le péché qu’il a commis, il apportera comme sacrifice une chèvre4.28 De moindre valeur que le bouc. Si le coupable était trop pauvre, il pouvait offrir un oiseau (5.7-8 ; 12.6, 8). sans défaut pour le péché qu’il a commis. 29Il posera sa main sur la tête de la victime sacrifiée pour le péché et l’égorgera dans le lieu où l’on offre l’holocauste. 30Puis le prêtre prendra avec son doigt du sang de la victime pour l’appliquer sur les cornes de l’autel des holocaustes, et il répandra tout le reste du sang sur le socle de l’autel. 31Il ôtera toute la graisse, comme on le fait pour le sacrifice de communion, et il la brûlera sur l’autel, produisant ainsi une odeur apaisante pour l’Eternel. Le prêtre accomplira ainsi le rite d’expiation pour cet homme, et il lui sera pardonné.

32Si c’est un agneau qu’il présente en sacrifice pour le péché, il amènera une femelle sans défaut. 33Il posera sa main sur la tête de la victime du sacrifice pour le péché et l’égorgera comme telle à l’endroit où l’on immole l’holocauste. 34Puis le prêtre prendra avec son doigt du sang de l’animal sacrifié pour le péché et le mettra sur les cornes de l’autel des holocaustes ; puis il répandra le reste du sang sur le socle de l’autel. 35Il enlèvera toute la graisse, comme on le fait pour l’agneau offert en sacrifice de communion ; ensuite le prêtre la brûlera sur l’autel, sur les sacrifices et offrandes consumés par le feu qui appartiennent à l’Eternel. Le prêtre accomplira ainsi le rite d’expiation pour le péché commis par cet homme, et il lui sera pardonné.