Walawi 21 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Walawi 21:1-24

Sheria Kwa Ajili Ya Makuhani

121:1 Kut 28:1; Law 5:3; 13:3; Hes 5:2; 6:6; 19:11; 31:19; Eze 44:25Bwana akamwambia Mose, “Sema na makuhani, wana wa Aroni, uwaambie: ‘Kamwe kuhani asijitie unajisi kwa utaratibu wa kiibada kwa ajili ya mtu wake yeyote anayekufa, 2isipokuwa jamaa wake wa karibu, kama vile mama yake au baba yake, mwanawe au binti yake, ndugu yake, 321:3 Hes 6:6; 21:5; Law 13:40; 19:28; Yer 7:29; 16:6; Eze 5:1; 44:20au dada yake asiyeolewa ambaye anamtegemea kwa kuwa hana mume, kwa ajili ya hao aweza kujitia unajisi. 4Kamwe asijitie unajisi mwenyewe kutokana na wale watu ambao anahusiana nao kwa kuoana, na hivyo kujitia unajisi.

5“ ‘Kamwe makuhani wasinyoe nywele za vichwa vyao wala wasinyoe pembeni mwa ndevu zao, au kuweka chale kwenye miili yao. 621:6 Ezr 8:28; Law 18:21; 3:11; 22:25; 10:3; Kut 19:22; Law 20:7; Za 15:4; Mt 5:33-37; Yak 5:12Lazima wawe watakatifu kwa Mungu wao, na kamwe wasilinajisi jina la Mungu wao. Kwa sababu ndio wanaotoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa Bwana, chakula cha Mungu wao, hivyo lazima wawe watakatifu.

721:7 Eze 44:22; 21:8; Law 3:11; Kut 31:13; 21:9; Mwa 38:24; Law 19:29; Kut 29:29; Hes 35:25; Kut 28:2“ ‘Kamwe wasioe wanawake waliojinajisi kwa ukahaba, au waliopewa talaka na waume wao, kwa sababu makuhani ni watakatifu kwa Mungu wao. 8Waoneni kuwa watakatifu, kwa sababu ndio wanaotoa chakula cha Mungu wenu. Kumbukeni kuwa ni watakatifu, kwa sababu Mimi Bwana ni mtakatifu, Mimi niwafanyaye ninyi kuwa watakatifu.

9“ ‘Ikiwa binti wa kuhani anajitia unajisi kwa kufanya ukahaba, anamwaibisha baba yake; lazima achomwe kwa moto.

1021:10 Kut 29:7; Law 8:7-13; 16:4; 10:6“ ‘Kuhani mkuu, yule miongoni mwa ndugu zake ambaye amekwisha kutiwa mafuta kwa kumiminiwa juu ya kichwa chake, na ambaye amewekwa wakfu kuvaa mavazi ya ukuhani, kamwe asiache nywele zake bila kufunikwa, wala asirarue nguo zake. 1121:11 Hes 5:2; 6:6; 9:6; 19:11-14; 31:19; Law 19:28Kamwe asiingie mahali palipo maiti ndani. Kamwe asijitie unajisi, hata kwa ajili ya baba yake au mama yake, 1221:12 Kut 25:8; 28:41; Law 10:7wala asiondoke mahali patakatifu pa Mungu wake au kupanajisi, kwa sababu amewekwa wakfu kwa mafuta ya Mungu wake. Mimi ndimi Bwana.

1321:13 Eze 44:22“ ‘Mwanamke kuhani atakayemwoa lazima awe bikira. 14Kamwe asimwoe mjane, au mwanamke aliyepewa talaka, wala mwanamke aliyejinajisi kwa ukahaba, bali atamwoa tu bikira kutoka miongoni mwa watu wake, 1521:15 Rum 12:1; 1Kor 3:16; Efe 5:17; 1The 4:1-8na hivyo hatawatia unajisi watoto wake miongoni mwa watu wake. Mimi ndimi Bwana, nimfanyaye mtakatifu.’ ”

16Bwana akamwambia Mose, 1721:17 Hes 16:5; Za 64:4“Mwambie Aroni: ‘Kwa vizazi vijavyo, hakuna mzao wako mwenye dosari atakayekaribia kutoa chakula cha Mungu wake. 1821:18 Law 22:19-25; 19:14; 2Sam 4:4; 9:3; 19:26Hakuna mtu mwenye dosari yoyote awezaye kukaribia: hakuna mtu aliye kipofu au kiwete, au aliyeharibika uso au asiye na viungo kamili, 19hakuna mtu mwenye mguu au mkono uliolemaa, 2021:20 Law 22:24; Kum 23:1; Isa 56:3au mwenye kibiongo au aliyedumaa, au aliye na tatizo la macho, au aliye na uvimbe wenye usaha au majipu, au aliyehasiwa. 2121:21 Law 3:11; 22:19Hakuna mzao wa kuhani Aroni mwenye kilema chochote atakayekaribia kutoa sadaka kwa Bwana ya kuteketezwa kwa moto. Kama ana kilema, kamwe asikaribie kutoa chakula cha Mungu wake. 2221:22 1Kor 9:13Anaweza kula chakula kitakatifu sana cha Mungu wake, pia hata chakula kitakatifu. 2321:23 Kut 25:8; Law 20:8; Hes 18:19Lakini kwa sababu ya kilema chake, kamwe asikaribie karibu na pazia wala kukaribia madhabahu, asije akanajisi mahali patakatifu pangu. Mimi ndimi Bwana, niwafanyaye watakatifu.’ ”

24Basi Mose akamwambia Aroni jambo hili na wanawe, pamoja na Waisraeli wote.

King James Version

Leviticus 21:1-24

1And the LORD said unto Moses, Speak unto the priests the sons of Aaron, and say unto them, There shall none be defiled for the dead among his people: 2But for his kin, that is near unto him, that is, for his mother, and for his father, and for his son, and for his daughter, and for his brother, 3And for his sister a virgin, that is nigh unto him, which hath had no husband; for her may he be defiled. 4But he shall not defile himself, being a chief man among his people, to profane himself.21.4 he…: or, being an husband among his people, he shall not defile himself for his wife, etc 5They shall not make baldness upon their head, neither shall they shave off the corner of their beard, nor make any cuttings in their flesh. 6They shall be holy unto their God, and not profane the name of their God: for the offerings of the LORD made by fire, and the bread of their God, they do offer: therefore they shall be holy. 7They shall not take a wife that is a whore, or profane; neither shall they take a woman put away from her husband: for he is holy unto his God. 8Thou shalt sanctify him therefore; for he offereth the bread of thy God: he shall be holy unto thee: for I the LORD, which sanctify you, am holy.

9¶ And the daughter of any priest, if she profane herself by playing the whore, she profaneth her father: she shall be burnt with fire.

10And he that is the high priest among his brethren, upon whose head the anointing oil was poured, and that is consecrated to put on the garments, shall not uncover his head, nor rend his clothes; 11Neither shall he go in to any dead body, nor defile himself for his father, or for his mother; 12Neither shall he go out of the sanctuary, nor profane the sanctuary of his God; for the crown of the anointing oil of his God is upon him: I am the LORD. 13And he shall take a wife in her virginity. 14A widow, or a divorced woman, or profane, or an harlot, these shall he not take: but he shall take a virgin of his own people to wife. 15Neither shall he profane his seed among his people: for I the LORD do sanctify him.

16¶ And the LORD spake unto Moses, saying, 17Speak unto Aaron, saying, Whosoever he be of thy seed in their generations that hath any blemish, let him not approach to offer the bread of his God.21.17 bread: or, food 18For whatsoever man he be that hath a blemish, he shall not approach: a blind man, or a lame, or he that hath a flat nose, or any thing superfluous, 19Or a man that is brokenfooted, or brokenhanded, 20Or crookbackt, or a dwarf, or that hath a blemish in his eye, or be scurvy, or scabbed, or hath his stones broken;21.20 a dwarf: or, too slender 21No man that hath a blemish of the seed of Aaron the priest shall come nigh to offer the offerings of the LORD made by fire: he hath a blemish; he shall not come nigh to offer the bread of his God. 22He shall eat the bread of his God, both of the most holy, and of the holy. 23Only he shall not go in unto the vail, nor come nigh unto the altar, because he hath a blemish; that he profane not my sanctuaries: for I the LORD do sanctify them. 24And Moses told it unto Aaron, and to his sons, and unto all the children of Israel.