Walawi 20 – NEN & KLB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Walawi 20:1-27

Adhabu Kwa Ajili Ya Dhambi

1Bwana akamwambia Mose, 220:2 Mwa 26:11; Kut 19:21; Law 24:14; Hes 15:35-36; Kum 21:21; Yos 7:25; 2Fal 17:17; 23:10; 2Nya 33:6“Sema na wana wa Israeli: ‘Mwisraeli yeyote au mgeni anayeishi katika Israeli ambaye atamtoa yeyote miongoni mwa watoto wake kuwa sadaka kwa mungu Moleki, mtu huyo lazima auawe. Watu wa jumuiya hiyo watampiga kwa mawe. 320:3 Law 23:30; 15:31; 18:21; Za 74:7; 79:1; Yer 7:30; Eze 5:11; Hes 19:20Mimi nitauelekeza uso wangu dhidi ya mtu huyo, nami nitamkatilia mbali na watu wake. Kwa maana kwa kumtoa mmoja wa watoto wake kwa mungu Moleki, amenajisi madhabahu yangu na kulinajisi Jina langu takatifu. 420:4 Kum 17:2-5Ikiwa watu wa jumuiya watafumba macho wakati mtu huyo anapomtoa mmoja wa watoto wake kwa mungu Moleki, nao wakaacha kumuua, 520:5 Kut 20:5; Law 17:7mimi nitauelekeza uso wangu dhidi ya mtu huyo pamoja na jamaa yake, nami nitawakatilia mbali yeye na watu wote waliofanya ukahaba na Moleki.

620:6 Law 19:31“ ‘Mimi nitauelekeza uso wangu dhidi ya mtu anayeenda kwa waaguzi na wenye pepo, na hivyo kujifanyia ukahaba kwa kuwafuata, nami nitamkatilia mbali na watu wake.

720:7 Law 11:44, 45; Kut 29:1; 31:13; Efe 1:4; 1Pet 1:16; Kut 6:2; 20:2“ ‘Jitakaseni basi, nanyi kuweni watakatifu, kwa sababu mimi ndimi Bwana Mungu wenu. 820:8 Mwa 26:5; Kut 31:13; Eze 20:12Shikeni amri zangu na kuzifuata. Mimi ndimi Bwana, niwafanyaye ninyi watakatifu.

920:9 Kut 20:12; 21:17; Yer 35:16; Mal 1:6; 2:10; Kum 21:21; 22:30; 27:16; Eze 18:13; 22:7; 33:4-5; Mt 15:4; Mk 7:10; Yos 2:19; 2Sam 1:16; 3:29; 1Fal 2:37“ ‘Ikiwa mtu yeyote atamlaani baba yake au mama yake, lazima auawe. Amemlaani baba yake au mama yake, nayo damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe.

1020:10 Kut 20:14; 21:12; Kum 5:18; 22:22; Yn 8:5; Mwa 38:24“ ‘Ikiwa mtu atazini na mke wa mtu mwingine, yaani mke wa jirani yake, wazinzi hao wawili lazima wauawe.

1120:11 Law 18:7-8; Kum 27:23“ ‘Kama mtu atakutana kimwili na mke wa baba yake, hakumheshimu baba yake. Mwanaume huyo na mwanamke huyo wote wauawe; damu yao itakuwa juu ya vichwa vyao wenyewe.

1220:12 Mwa 11:31; 38:16; Law 18:15“ ‘Ikiwa mtu atakutana kimwili na mke wa mwanawe, lazima wote wawili wauawe. Walichokifanya ni upotovu; damu yao itakuwa juu ya vichwa vyao wenyewe.

1320:13 Law 18:22“ ‘Kama mwanaume akikutana kimwili na mwanaume mwenzake kama vile mwanaume afanyavyo na mwanamke, wanaume hao wawili wamefanya lililo chukizo sana. Lazima wauawe; nayo damu yao itakuwa juu ya vichwa vyao wenyewe.

1420:14 Law 18:8, 17; 21:9; Hes 16:39; Amu 14:15; 15:6; Kum 27:23“ ‘Ikiwa mwanaume ataoa binti pamoja na mama yake, huo ni uovu. Wote watatu ni lazima wachomwe moto, ili kwamba pasiwepo na uovu katikati yenu.

1520:15 Kut 20:10; 22:19; Law 18:23; 18:9; 5:1; Mwa 17:14; 20:12“ ‘Kama mwanaume akikutana kimwili na mnyama, ni lazima auawe, na pia ni lazima mnyama huyo auawe.

16“ ‘Kama mwanamke atamsogelea mnyama kukutana naye kimwili, muueni mwanamke huyo pamoja na mnyama pia. Lazima wauawe; damu yao itakuwa juu ya vichwa vyao wenyewe.

1720:17 Mwa 26:5; Kut 31:13; Eze 20:12; Mwa 26:5; Kut 31:13; Eze 20:12“ ‘Ikiwa mtu anamwoa dada yake, binti aliyezaliwa na baba yake au mama yake, nao wakakutana kimwili, ni aibu. Lazima wakatiliwe mbali machoni pa watu wao. Huyo mwanaume amemwaibisha dada yake, hivyo atawajibika kwa ajili ya uovu huo.

1820:18 Law 15:24; Eze 18:6; 20:19; Law 18:2, 12“ ‘Ikiwa mwanaume atalala na mwanamke aliye katika hedhi yake na kukutana naye kimwili, amefunua mtiririko wa hedhi yake, naye huyo mwanamke amejifunua uchi wake. Wote wawili lazima wakatiliwe mbali na watu wao.

19“ ‘Usikutane kimwili na dada wa mama yako wala wa baba yako, kwa maana hilo litamwaibisha jamaa wa karibu; ninyi wawili mtawajibika kwa ajili ya uovu huo.

2020:20 Law 18:13-14; Mwa 15:2“ ‘Ikiwa mwanaume atakutana kimwili na shangazi yake, amemwaibisha mjomba wake. Nao watawajibika kwa ajili ya uovu huo; watakufa bila kuzaa mtoto.

2120:21 Law 18:16; Mt 14:4; Mk 6:18“ ‘Ikiwa mwanaume ataoa mke wa ndugu yake, hili ni tendo chafu; amemwaibisha ndugu yake. Nao hawatazaa mtoto.

2220:22 Mwa 26:5; Law 18:25-28“ ‘Zishikeni amri na sheria zangu zote na kuzifuata, ili nchi ninayowaleta kuishi isiwatapike. 2320:23 Law 18:3, 24-25, 27-30Kamwe msiishi kwa kufuata desturi za mataifa nitakayoyafukuza mbele yenu. Kwa sababu walifanya mambo haya yote, nami nikachukizwa sana nao. 2420:24 Kut 3:8; 13:5; 33:16; Hes 14:8; 16:14; 1Fal 8:53; Za 135Lakini niliwaambia ninyi, “Mtaimiliki nchi yao; nitawapa ninyi kuwa urithi, nchi inayotiririka maziwa na asali.” Mimi ndimi Bwana Mungu wenu, ambaye amewatenga kutoka mataifa.

2520:25 Law 10:10; Kum 14:3-21; Mdo 10:14; Law 11:47“ ‘Kwa hiyo, ninyi lazima mweze kutofautisha kati ya wanyama walio safi na wasio safi, pia kati ya ndege wasio safi na walio safi. Msijitie unajisi kutokana na mnyama yeyote, au ndege, wala kitu chochote kitambaacho juu ya ardhi, vile ambavyo nimevitenga kuwa najisi kwa ajili yenu. 2620:26 Kum 14:2; Law 19:2; Yos 24:19; 2Fal 19:22Mtakuwa watakatifu kwangu, kwa sababu Mimi, Bwana, ni mtakatifu, nami nimewatenga kutoka mataifa kuwa wangu mwenyewe.

2720:27 Kut 22:18; Law 19:31; 24:14; Kum 18:10; 1Sam 28:7“ ‘Mwanaume au mwanamke ambaye ni mchawi, mwaguzi au mwenye kupunga pepo miongoni mwenu lazima auawe. Mtawapiga kwa mawe; nayo damu yao itakuwa juu ya vichwa vyao wenyewe.’ ”

Korean Living Bible

레위기 20:1-27

죄에 대한 형벌

1여호와께서 모세를 통하여 이스라엘 백성에게 이렇게 말씀하셨다.

2“이스라엘 자손이든 너희 가운데 사는 외국인이든 누구든지 자기 자식을 이방 신 몰렉에게 제물로 바치는 자는 그 지방 사람이 돌로 쳐죽여야 한다.

3그가 자기 자식을 몰렉에게 바쳐서 내 성소를 더럽히고 나의 거룩한 이름을 욕되게 하였으므로 나도 그를 심판하여 내 백성 가운데서 그를 제거하겠다.

4만일 그 지방 사람이 자식을 몰렉에게 바친 그의 소행을 못 본 척하고 그를 죽이지 않으면

5내가 그 사람과 그의 가족과 그리고 그를 본받아 나를 저버리고 몰렉을 섬기는 모든 자들을 심판하여 그들을 내 백성 가운데서 제거하겠다.

6“그리고 영매나 무당을 따르는 자도 내가 심판하여 그들을 내 백성 가운데서 제거하겠다.

7그러므로 너희는 자신을 구별하여 거룩하게 하여라. 나는 너희 하나님 여호와이다.

8너희는 나의 모든 명령을 준수하라. 나는 너희를 거룩하게 하는 여호와이다.

9“누구든지 자기 아버지나 어머니를 저주하는 자는 반드시 죽여라. 그는 자기를 낳아 준 부모를 저주하였으므로 죽어야 마땅하다.

10“누구든지 남의 아내와 간통하면 남녀를 다 같이 처형하라.

11누가 계모와 잠자리를 같이하여 자기 아버지를 욕되게 하였으면 두 사람을 모두 죽여라. 20:11 또는 ‘그 피가 자기에게 돌아가리라’그들은 죽어 마땅하다.

12누가 자기 며느리와 잠자리를 같이하면 둘 다 죽여라. 그들은 서로 더럽혔으므로 죽어 마땅하다.

13누구든지 동성 연애를 하면 둘 다 죽여라. 그들은 추잡한 짓을 하였으므로 죽어 마땅하다.

14누구든지 어떤 여인과 그 여인의 어머니를 함께 데리고 살면서 더러운 짓을 하면 세 사람을 모두 불태워 죽이고 너희 가운데 다시는 그런 악한 일이 없도록 하라.

15만일 남자가 짐승과 더러운 짓을 하면 그를 반드시 죽이고 그 짐승도 죽일 것이며

16또 여자가 짐승과 음란한 짓을 해도 그 여자와 짐승을 모두 죽여라. 그들은 죽어 마땅하다.

17“의붓 누이이든 이복 누이이든 누구든지 자기 누이와 성관계를 하면 그들을 대중 앞에 끌어내어 처형하라. 그들은 부끄러운 짓을 하였으므로 벌을 받아 마땅하다.

18만일 누가 생리 기간 중의 여자와 성관계를 하면 그들은 20:18 또는 ‘피 근원’부정한 곳을 드러내었으므로 두 사람을 모두 그 백성 가운데서 제거해 버려라.

19“누구든지 자기 이모나 고모와 부끄러운 짓을 해서는 안 된다. 그들은 가까운 친척이므로 그 죄의 대가를 받아야 할 것이다.

20누구든지 자기 백모나 숙모와 부끄러운 짓을 하면 그들은 다 같이 벌을 받아 자식 없이 죽을 것이다.

21그리고 누가 자기 형제의 아내를 데리고 살면 그는 더러운 짓을 하여 자기 형제를 부끄럽게 하였으므로 그들도 자식이 없을 것이다.

22“너희는 나의 모든 법과 규정을 준수하라. 그러면 너희가 가나안 땅에 들어가도 내가 너희를 쫓아내지 않을 것이다.

23너희는 내가 너희 앞에서 쫓아낼 민족의 풍습을 좇지 말아라. 그들은 내가 너희에게 경고한 이런 일을 그대로 행하고 있으므로 내가 그들을 몹시 싫어하고 있다.

24그러나 나는 전에 너희에게 약속한 대로 기름지고 비옥한 그들의 땅을 너희 소유로 주겠다. 나는 많은 민족 가운데서 특별히 너희를 구별하여 세운 너희 하나님 여호와이다.

25그러므로 너희는 새나 짐승이나 무엇이든지 부정한 것과 깨끗한 것을 구별하고 내가 너희에게 부정하다고 일러 준 새나 짐승이나 곤충을 먹지 말아라. 너희는 이런 것으로 자신을 더럽혀서는 안 된다.

26나 여호와가 거룩한 것처럼 너희도 나에게 거룩하여라. 이것은 내가 많은 민족 가운데서 특별히 너희를 구별하여 내 백성으로 삼았기 때문이다.

27“영매나 무당은 남자이건 여자이건 반드시 돌로 쳐죽여라. 이런 사람은 죽어도 마땅하다.”