Walawi 19 – NEN & NVI

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Walawi 19:1-37

Sheria Mbalimbali

1Bwana akamwambia Mose, 2“Sema na kusanyiko lote la Israeli na uwaambie: ‘Kuweni watakatifu, kwa kuwa mimi, Bwana Mungu wenu, ni mtakatifu.

319:3 Kut 20:8, 12; Law 11:44; Neh 9:14; 13:15-21; Isa 58:13; Mk 2:27“ ‘Kila mmoja wenu ni lazima amheshimu mama yake na baba yake, na pia ni lazima kuzishika Sabato zangu. Mimi ndimi Bwana Mungu wenu.

419:4 Kut 20:4; Amu 17:3; Za 96:5; 115:4-7; 135:15; 1Kor 10:14“ ‘Msiabudu sanamu, wala msijitengenezee miungu ya shaba. Mimi ndimi Bwana Mungu wenu.

5“ ‘Mnapotoa dhabihu ya sadaka ya amani kwa Bwana, toeni kwa namna ambayo itakubaliwa kwa niaba yenu. 619:6 Law 7:16-18Sadaka hiyo italiwa siku iyo hiyo mnayoitoa, au kesho yake; chochote kitakachobaki hadi siku ya tatu lazima kiteketezwe kwa moto. 7Kama sehemu yoyote ya sadaka hiyo italiwa siku ya tatu, itakuwa si safi, nayo haitakubaliwa. 819:8 Law 22:2, 15-16; Hes 18:32; Mwa 17:14Yeyote atakayekula atawajibishwa, kwa sababu amenajisi kitu kilicho kitakatifu kwa Bwana; mtu huyo lazima akatiliwe mbali na watu wake.

919:9 Rut 2:2-7; Law 23:10, 22; Kum 24:19-22; Ay 24:10; Kut 23:11; Kum 15:1-18“ ‘Wakati uvunapo mavuno ya nchi yako, usivune hadi kwenye mipaka ya shamba lako, wala usikusanye mabaki ya mavuno yako. 1019:10 Kum 24:19-22; Za 140:12; Mit 14:31; Isa 3:12-15; Mhu 5:8Usirudi mara ya pili katika shamba lako la mizabibu, wala usiokote zabibu zilizoanguka chini. Ziache kwa ajili ya maskini na mgeni. Mimi ndimi Bwana Mungu wako.

1119:11 Kut 20:15-16; 23:4; Lk 3:14; Efe 4:25; Law 6:2; 1Fal 13:18; Yer 9:3-5; Mdo 5:3-4“ ‘Usiibe.

“ ‘Usiseme uongo.

“ ‘Msidanganyane.

1219:12 Yer 5:2; 7:9; 34:16; 44:16, 26; Mal 3:5; Kut 3:13; 20:7; Kum 18:19; Mit 18:10; Isa 42:8; Mt 5:33“ ‘Usiape kwa uongo kwa Jina langu, na hivyo kulinajisi jina la Mungu wako. Mimi ndimi Bwana.

1319:13 Law 25:14, 17; Kut 20:15; 22:15, 25-27; Ay 7:2; 24:12; 31:39; Isa 16:14; Mal 3:5; Kum 24:15; Yer 22:13; Mt 20:8; 1Tim 5:18; Yak 5:4“ ‘Usimdhulumu wala kumwibia jirani yako.

“ ‘Usishikilie mshahara wa kibarua usiku kucha hadi asubuhi.

1419:14 Kut 4:11; Law 21:18; 25:17, 36; Kum 27:18; Rum 14:13; 1Pet 2:17“ ‘Usimlaani kiziwi, wala usiweke kikwazo mbele ya kipofu, lakini umche Mungu wako. Mimi ndimi Bwana.

1519:15 Kut 13:2; 23:8; Kum 24:17; Ay 13:8, 10; 32:21; 34:19; Mit 24:23; 28:21; Mal 2:9; Yak 2:1-4“ ‘Usipotoshe haki; usionyeshe kumpendelea maskini, wala upendeleo kwa mwenye cheo, bali mwamulie jirani yako kwa haki.

1619:16 Za 15:3, 5; 31:13; 41:6; 101:5; Yer 6:28; 9:4; Eze 22:9, 12; Kut 23:7; Kum 10:17; 27:25“ ‘Usieneze uchochezi miongoni mwa watu wako.

“ ‘Usifanye kitu chochote kile kinachohatarisha maisha ya jirani yako. Mimi ndimi Bwana.

1719:17 1Yn 2:9; Mt 18:15; Lk 17:3; Mwa 27:41“ ‘Usimchukie ndugu yako moyoni mwako. Karipia jirani yako kwa uwazi ili usishiriki hatia yake.

1819:18 Mwa 4:23; Rum 12:19; 13:9; Ebr 10:30; Za 103:9; Kut 20:16; Mt 5:43; 19:16; 22:39; Mk 12:31; Lk 10:27; Yn 13:34; Gal 5:14; Yak 2:8“ ‘Usijilipizie kisasi wala kuwa na kinyongo dhidi ya mmoja wa jamaa yako, lakini mpende jirani yako kama unavyojipenda wewe mwenyewe. Mimi ndimi Bwana.

1919:19 Mwa 26:5; Kum 22:9, 11“ ‘Mtazishika amri zangu.

“ ‘Usiwaache wanyama wako wa kufugwa wakazaana na wengine wa aina tofauti.

“ ‘Usipande mbegu za aina mbili katika shamba lako.

“ ‘Usivae nguo iliyofumwa kwa nyuzi za aina mbili tofauti.

2019:20 Kum 22:23-27“ ‘Kama mwanaume anakutana kimwili na mwanamke ambaye ni msichana mtumwa aliyeposwa na mwanaume mwingine, lakini ambaye hajakombolewa wala hajapewa uhuru, lazima iwepo adhabu inayofaa. Hata hivyo hawatauawa, kwa sababu msichana alikuwa bado hajaachwa huru. 2119:21 Law 5:15Lakini huyo mtu lazima alete kondoo dume kwenye ingilio la Hema la Kukutania kwa ajili ya sadaka ya hatia kwa Bwana. 22Kupitia kwa huyo kondoo dume wa sadaka ya hatia, kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana kwa ajili ya dhambi aliyotenda, naye atasamehewa dhambi yake.

23“ ‘Mtakapoingia katika hiyo nchi na kupanda aina yoyote ya mti wa matunda, hesabuni matunda yake kama yaliyokatazwa. Kwa miaka mitatu mtayahesabu kwamba yamekatazwa; hayaruhusiwi kuliwa. 2419:24 Kut 22:29; Mit 3:9; Kum 12:17-18Katika mwaka wa nne matunda yote ya mti huo yatakuwa matakatifu, sadaka ya sifa kwa Bwana. 25Bali katika mwaka wa tano mnaweza kula matunda ya mti huo. Kwa njia hii mavuno yenu yataongezewa. Mimi ndimi Bwana Mungu wako.

2619:26 Mwa 9:4; 30:27; Isa 44:25; Eze 22:18; 2Fal 17:17“ ‘Msile nyama yoyote yenye damu ndani yake.

“ ‘Msifanye uaguzi wala uchawi.

2719:27 Law 21:5; 2Sam 10:4-5; Yer 41:5; 48:37; Eze 5:1-5; Yer 9:26“ ‘Msikate nywele za kichwa denge, wala kunyoa pembe za ndevu zenu.

2819:28 Law 21:5; 1Fal 18:28; Yer 16:6; 41:5; 47:5“ ‘Msichanje chale miili yenu kwa ajili ya mfu, wala msijichore alama juu ya miili yenu. Mimi ndimi Bwana.

2919:29 Law 21:9; Kum 23:18; Mwa 34:7“ ‘Usimdhalilishe binti yako kwa kumfanya kahaba, la sivyo nchi itageukia ukahaba na kujaa uovu.

3019:30 Kut 20:8; Law 26:2“ ‘Shika Sabato zangu na kuheshimu mahali pangu patakatifu. Mimi ndimi Bwana.

3119:31 Kut 22:18; 1Sam 28:7-20; 1Nya 10:13; Law 20:6; 2Fal 21:6; 23:24; Isa 8:19; 19:3; 29:4; 47:12; 65:4“ ‘Msiende kwa waaguzi, wala msitafute wapunga pepo, kwa maana watawanajisi. Mimi ndimi Bwana Mungu wako.

3219:32 1Fal 12:8; Ay 29:8; 32:4; Mit 23:22; Mao 5:12; 1Tim 5:1; Law 11:44“ ‘Uwapo mbele ya mzee, simama ili kuonyesha heshima kwa wazee, nawe umche Mungu wako. Mimi ndimi Bwana.

33“ ‘Wakati mgeni anaishi pamoja nawe katika nchi yako, usimnyanyase. 3419:34 Kut 12:48; 22:21; 23:9; Kum 10:19; 23:7; Za 146:9Mgeni anayeishi pamoja nawe ni lazima umtendee kama mmoja wa wazawa wa nchi yako. Mpende kama unavyojipenda mwenyewe, kwa maana ulikuwa mgeni katika nchi ya Misri. Mimi ndimi Bwana Mungu wako.

3519:35 Kum 25:13-16“ ‘Usitumie vipimo vya udanganyifu unapopima urefu, kupima uzito, wala kupima wingi. 3619:36 Ay 31:6; Mit 11:1; 20:10; Hes 12:7; Mik 6:11; Amu 6:19; Rut 2:17; 1Sam 1:24; 17:17; Eze 45:10-11; Kum 25:13-15; Kut 12:17Tumia mizani halali, mawe ya kupimia uzito halali, efa19:36 Efa kilikuwa kipimo cha vitu vikavu. halali, na hini19:36 Hini kilikuwa kipimo cha vitu vimiminika. halali. Mimi ndimi Bwana Mungu wako, ambaye alikutoa katika nchi ya Misri.

3719:37 2Fal 17:37; 2Nya 7:17; Za 119:5; Eze 18:9; Mwa 26:5; Kum 6:25; Law 18:4-5“ ‘Shika amri zangu zote na sheria zangu zote, nawe uzifuate. Mimi ndimi Bwana.’ ”

Nueva Versión Internacional

Levítico 19:1-37

Llamado a la santidad

1El Señor ordenó a Moisés 2que hablara con toda la asamblea de los israelitas y dijera: «Sean santos, porque yo, el Señor su Dios, soy santo.

3»Respeten todos ustedes a su madre y a su padre, y observen mis sábados. Yo soy el Señor su Dios.

4»No se vuelvan a los ídolos inútiles, ni se hagan dioses de metal fundido. Yo soy el Señor su Dios.

5»Cuando ofrezcan al Señor un sacrificio de comunión, háganlo de tal manera que el Señor lo acepte de buen grado. 6Cómanselo el día en que lo sacrifiquen o al día siguiente. Lo que sobre para el tercer día deberán quemarlo. 7Si alguien lo come al tercer día, tal sacrificio no será válido, pues la carne ya se habrá vuelto impura. 8Cualquiera que lo coma sufrirá las consecuencias de su pecado por profanar lo que ha sido consagrado al Señor. Tal persona será eliminada de su pueblo.

Relaciones sociales

9»Cuando llegue el tiempo de la cosecha, no sieguen hasta el último rincón de sus campos ni recojan todas las espigas que allí queden. 10No rebusquen hasta el último racimo de sus viñas, ni recojan las uvas que se hayan caído. Déjenlas para los pobres y los extranjeros. Yo soy el Señor su Dios.

11»No roben.

»No mientan.

»No engañen a su prójimo.

12»No juren en mi nombre falsamente, ni profanen el nombre de su Dios. Yo soy el Señor.

13»No defraudes a tu prójimo ni lo despojes de nada.

»No retengas la paga de tu jornalero hasta el día siguiente.

14»No maldigas al sordo ni pongas tropiezos al ciego, sino teme a tu Dios. Yo soy el Señor.

15»No perviertas la justicia, ni te muestres parcial en favor del pobre o del rico, sino juzga a todos con justicia.

16»No andes difundiendo calumnias entre tu pueblo, ni expongas la vida de tu prójimo con falsos testimonios. Yo soy el Señor.

17»No alimentes en tu corazón odios contra tu hermano, sino reprende con franqueza a tu prójimo para que no sufras las consecuencias de su pecado.

18»No seas vengativo con tu prójimo ni le guardes rencor. Ama a tu prójimo como a ti mismo. Yo soy el Señor.

Otras exigencias de la santidad

19»Cumplan mis estatutos:

»No crucen animales de especies diferentes.

»No planten en su campo dos clases distintas de semilla.

»No usen ropa tejida con dos clases distintas de hilo.

20»Si un hombre se acuesta con una esclava prometida a otro en matrimonio, pero que aún no ha sido rescatada ni declarada libre, a los dos se les impondrá el castigo debido,19:20 a los dos … debido. Alt. los dos deberán ser investigados. pero no se les condenará a muerte porque ella aún no ha sido declarada libre. 21No obstante, el hombre deberá ofrecer al Señor un carnero como ofrenda por su culpa. Lo llevará a la entrada de la Tienda de reunión, 22y el sacerdote pedirá perdón ante el Señor por el pecado cometido. De este modo su pecado será perdonado.

23»Cuando ustedes entren en la tierra y planten cualquier clase de árboles frutales, durante tres años no comerán su fruto, sino que lo considerarán inmundo.19:23 inmundo. Lit. incircunciso. 24En el cuarto año todo su fruto será consagrado como una ofrenda de alabanza al Señor, 25y en el quinto año ya podrán comer de su fruto. De este modo aumentarán sus cosechas. Yo soy el Señor su Dios.

26»No coman nada que tenga sangre.

»No practiquen la agorería ni la adivinación.

27»No se corten el cabello en redondo ni se despunten la barba.

28»No se hagan heridas en el cuerpo por causa de los muertos, ni tatuajes en la piel. Yo soy el Señor.

29»No degraden a su hija haciendo de ella una prostituta, para que tampoco se prostituya la tierra ni se llene de perversidad.

Otros deberes

30»Observen mis sábados y muestren reverencia por mi santuario. Yo soy el Señor.

31»No acudan a los médiums, ni busquen a los espiritistas, porque se harán impuros por causa de ellos. Yo soy el Señor su Dios.

32»Ponte de pie en presencia de los mayores.

»Respeta a los ancianos.

»Teme a tu Dios. Yo soy el Señor.

33»Cuando algún extranjero se establezca en el país de ustedes, no lo traten mal. 34Al contrario, trátenlo como si fuera uno de ustedes. Ámenlo como a ustedes mismos, porque también ustedes fueron extranjeros en Egipto. Yo soy el Señor su Dios.

35»No sean deshonestos falseando las medidas de longitud, de peso y de capacidad. 36Usen balanzas, pesas y medidas justas. Un efa19:36 Es decir, aprox. 16 kg. exacto y un hin19:36 Es decir, aprox. 3.8 l. exacto. Yo soy el Señor su Dios, que los saqué de Egipto.

37»Cumplan todos mis estatutos y obedezcan todas mis leyes. Yo soy el Señor».