Walawi 19 – NEN & HTB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Walawi 19:1-37

Sheria Mbalimbali

1Bwana akamwambia Mose, 2“Sema na kusanyiko lote la Israeli na uwaambie: ‘Kuweni watakatifu, kwa kuwa mimi, Bwana Mungu wenu, ni mtakatifu.

319:3 Kut 20:8, 12; Law 11:44; Neh 9:14; 13:15-21; Isa 58:13; Mk 2:27“ ‘Kila mmoja wenu ni lazima amheshimu mama yake na baba yake, na pia ni lazima kuzishika Sabato zangu. Mimi ndimi Bwana Mungu wenu.

419:4 Kut 20:4; Amu 17:3; Za 96:5; 115:4-7; 135:15; 1Kor 10:14“ ‘Msiabudu sanamu, wala msijitengenezee miungu ya shaba. Mimi ndimi Bwana Mungu wenu.

5“ ‘Mnapotoa dhabihu ya sadaka ya amani kwa Bwana, toeni kwa namna ambayo itakubaliwa kwa niaba yenu. 619:6 Law 7:16-18Sadaka hiyo italiwa siku iyo hiyo mnayoitoa, au kesho yake; chochote kitakachobaki hadi siku ya tatu lazima kiteketezwe kwa moto. 7Kama sehemu yoyote ya sadaka hiyo italiwa siku ya tatu, itakuwa si safi, nayo haitakubaliwa. 819:8 Law 22:2, 15-16; Hes 18:32; Mwa 17:14Yeyote atakayekula atawajibishwa, kwa sababu amenajisi kitu kilicho kitakatifu kwa Bwana; mtu huyo lazima akatiliwe mbali na watu wake.

919:9 Rut 2:2-7; Law 23:10, 22; Kum 24:19-22; Ay 24:10; Kut 23:11; Kum 15:1-18“ ‘Wakati uvunapo mavuno ya nchi yako, usivune hadi kwenye mipaka ya shamba lako, wala usikusanye mabaki ya mavuno yako. 1019:10 Kum 24:19-22; Za 140:12; Mit 14:31; Isa 3:12-15; Mhu 5:8Usirudi mara ya pili katika shamba lako la mizabibu, wala usiokote zabibu zilizoanguka chini. Ziache kwa ajili ya maskini na mgeni. Mimi ndimi Bwana Mungu wako.

1119:11 Kut 20:15-16; 23:4; Lk 3:14; Efe 4:25; Law 6:2; 1Fal 13:18; Yer 9:3-5; Mdo 5:3-4“ ‘Usiibe.

“ ‘Usiseme uongo.

“ ‘Msidanganyane.

1219:12 Yer 5:2; 7:9; 34:16; 44:16, 26; Mal 3:5; Kut 3:13; 20:7; Kum 18:19; Mit 18:10; Isa 42:8; Mt 5:33“ ‘Usiape kwa uongo kwa Jina langu, na hivyo kulinajisi jina la Mungu wako. Mimi ndimi Bwana.

1319:13 Law 25:14, 17; Kut 20:15; 22:15, 25-27; Ay 7:2; 24:12; 31:39; Isa 16:14; Mal 3:5; Kum 24:15; Yer 22:13; Mt 20:8; 1Tim 5:18; Yak 5:4“ ‘Usimdhulumu wala kumwibia jirani yako.

“ ‘Usishikilie mshahara wa kibarua usiku kucha hadi asubuhi.

1419:14 Kut 4:11; Law 21:18; 25:17, 36; Kum 27:18; Rum 14:13; 1Pet 2:17“ ‘Usimlaani kiziwi, wala usiweke kikwazo mbele ya kipofu, lakini umche Mungu wako. Mimi ndimi Bwana.

1519:15 Kut 13:2; 23:8; Kum 24:17; Ay 13:8, 10; 32:21; 34:19; Mit 24:23; 28:21; Mal 2:9; Yak 2:1-4“ ‘Usipotoshe haki; usionyeshe kumpendelea maskini, wala upendeleo kwa mwenye cheo, bali mwamulie jirani yako kwa haki.

1619:16 Za 15:3, 5; 31:13; 41:6; 101:5; Yer 6:28; 9:4; Eze 22:9, 12; Kut 23:7; Kum 10:17; 27:25“ ‘Usieneze uchochezi miongoni mwa watu wako.

“ ‘Usifanye kitu chochote kile kinachohatarisha maisha ya jirani yako. Mimi ndimi Bwana.

1719:17 1Yn 2:9; Mt 18:15; Lk 17:3; Mwa 27:41“ ‘Usimchukie ndugu yako moyoni mwako. Karipia jirani yako kwa uwazi ili usishiriki hatia yake.

1819:18 Mwa 4:23; Rum 12:19; 13:9; Ebr 10:30; Za 103:9; Kut 20:16; Mt 5:43; 19:16; 22:39; Mk 12:31; Lk 10:27; Yn 13:34; Gal 5:14; Yak 2:8“ ‘Usijilipizie kisasi wala kuwa na kinyongo dhidi ya mmoja wa jamaa yako, lakini mpende jirani yako kama unavyojipenda wewe mwenyewe. Mimi ndimi Bwana.

1919:19 Mwa 26:5; Kum 22:9, 11“ ‘Mtazishika amri zangu.

“ ‘Usiwaache wanyama wako wa kufugwa wakazaana na wengine wa aina tofauti.

“ ‘Usipande mbegu za aina mbili katika shamba lako.

“ ‘Usivae nguo iliyofumwa kwa nyuzi za aina mbili tofauti.

2019:20 Kum 22:23-27“ ‘Kama mwanaume anakutana kimwili na mwanamke ambaye ni msichana mtumwa aliyeposwa na mwanaume mwingine, lakini ambaye hajakombolewa wala hajapewa uhuru, lazima iwepo adhabu inayofaa. Hata hivyo hawatauawa, kwa sababu msichana alikuwa bado hajaachwa huru. 2119:21 Law 5:15Lakini huyo mtu lazima alete kondoo dume kwenye ingilio la Hema la Kukutania kwa ajili ya sadaka ya hatia kwa Bwana. 22Kupitia kwa huyo kondoo dume wa sadaka ya hatia, kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana kwa ajili ya dhambi aliyotenda, naye atasamehewa dhambi yake.

23“ ‘Mtakapoingia katika hiyo nchi na kupanda aina yoyote ya mti wa matunda, hesabuni matunda yake kama yaliyokatazwa. Kwa miaka mitatu mtayahesabu kwamba yamekatazwa; hayaruhusiwi kuliwa. 2419:24 Kut 22:29; Mit 3:9; Kum 12:17-18Katika mwaka wa nne matunda yote ya mti huo yatakuwa matakatifu, sadaka ya sifa kwa Bwana. 25Bali katika mwaka wa tano mnaweza kula matunda ya mti huo. Kwa njia hii mavuno yenu yataongezewa. Mimi ndimi Bwana Mungu wako.

2619:26 Mwa 9:4; 30:27; Isa 44:25; Eze 22:18; 2Fal 17:17“ ‘Msile nyama yoyote yenye damu ndani yake.

“ ‘Msifanye uaguzi wala uchawi.

2719:27 Law 21:5; 2Sam 10:4-5; Yer 41:5; 48:37; Eze 5:1-5; Yer 9:26“ ‘Msikate nywele za kichwa denge, wala kunyoa pembe za ndevu zenu.

2819:28 Law 21:5; 1Fal 18:28; Yer 16:6; 41:5; 47:5“ ‘Msichanje chale miili yenu kwa ajili ya mfu, wala msijichore alama juu ya miili yenu. Mimi ndimi Bwana.

2919:29 Law 21:9; Kum 23:18; Mwa 34:7“ ‘Usimdhalilishe binti yako kwa kumfanya kahaba, la sivyo nchi itageukia ukahaba na kujaa uovu.

3019:30 Kut 20:8; Law 26:2“ ‘Shika Sabato zangu na kuheshimu mahali pangu patakatifu. Mimi ndimi Bwana.

3119:31 Kut 22:18; 1Sam 28:7-20; 1Nya 10:13; Law 20:6; 2Fal 21:6; 23:24; Isa 8:19; 19:3; 29:4; 47:12; 65:4“ ‘Msiende kwa waaguzi, wala msitafute wapunga pepo, kwa maana watawanajisi. Mimi ndimi Bwana Mungu wako.

3219:32 1Fal 12:8; Ay 29:8; 32:4; Mit 23:22; Mao 5:12; 1Tim 5:1; Law 11:44“ ‘Uwapo mbele ya mzee, simama ili kuonyesha heshima kwa wazee, nawe umche Mungu wako. Mimi ndimi Bwana.

33“ ‘Wakati mgeni anaishi pamoja nawe katika nchi yako, usimnyanyase. 3419:34 Kut 12:48; 22:21; 23:9; Kum 10:19; 23:7; Za 146:9Mgeni anayeishi pamoja nawe ni lazima umtendee kama mmoja wa wazawa wa nchi yako. Mpende kama unavyojipenda mwenyewe, kwa maana ulikuwa mgeni katika nchi ya Misri. Mimi ndimi Bwana Mungu wako.

3519:35 Kum 25:13-16“ ‘Usitumie vipimo vya udanganyifu unapopima urefu, kupima uzito, wala kupima wingi. 3619:36 Ay 31:6; Mit 11:1; 20:10; Hes 12:7; Mik 6:11; Amu 6:19; Rut 2:17; 1Sam 1:24; 17:17; Eze 45:10-11; Kum 25:13-15; Kut 12:17Tumia mizani halali, mawe ya kupimia uzito halali, efa19:36 Efa kilikuwa kipimo cha vitu vikavu. halali, na hini19:36 Hini kilikuwa kipimo cha vitu vimiminika. halali. Mimi ndimi Bwana Mungu wako, ambaye alikutoa katika nchi ya Misri.

3719:37 2Fal 17:37; 2Nya 7:17; Za 119:5; Eze 18:9; Mwa 26:5; Kum 6:25; Law 18:4-5“ ‘Shika amri zangu zote na sheria zangu zote, nawe uzifuate. Mimi ndimi Bwana.’ ”

Het Boek

Leviticus 19:1-37

Wees heilig, want Ik ben heilig

1De Here droeg Mozes op ook de volgende woorden aan de Israëlieten over te brengen. 2‘U moet heilig zijn, want Ik, de Here, uw God, ben heilig. 3U moet uw vader en moeder eren en mijn sabbatswet gehoorzamen, want Ik ben de Here, uw God. 4Maak geen afgodsbeelden en aanbid ze niet, want Ik ben de Here, uw God. 5Wanneer u de Here een vredeoffer brengt, doe het zoals is voorgeschreven, zodat het wordt aanvaard. 6Eet het dezelfde dag dat u het offert of uiterlijk de volgende dag, wat overblijft tot de derde dag moet worden verbrand. 7Want als iets ervan op de derde dag wordt gegeten, zal Mij dat met afkeer vervullen en Ik zal het niet aanvaarden. 8Als u het op de derde dag eet, zult u schuldig zijn, want u schendt daarmee de heiligheid van de Here en u zult worden verstoten uit het volk van de Here.

9Wanneer u de oogst binnenhaalt, moet u de randen van het veld niet helemaal afmaaien en wat op de grond is gevallen, moet u naderhand niet bijeenrapen. 10Hetzelfde geldt voor de wijnoogst, haal niet alle druiven van de planten en laat wat op de grond is gevallen, gewoon liggen. Laat het liggen voor de armen en voor hongerige reizigers, want Ik ben de Here, uw God.

11U mag niet stelen, liegen of elkaar bedriegen. 12Zweer geen valse eed, want daarmee ontheiligt u de naam van uw God, want Ik ben de Here. 13U mag niet roven of iemand iets afpersen en u moet de arbeiders die u hebt gehuurd, op tijd betalen. Als u een van hen nog loon schuldig bent, laat er dan niet nog een nacht overheen gaan voordat u hem uitbetaalt. 14U mag niet vloeken tegen een dove. U mag een blinde niets in de weg leggen. Heb ontzag voor uw God, Ik ben de Here! 15Rechters moeten bij hun uitspraken altijd rechtvaardig blijven en zich niet laten leiden door het feit of iemand rijk of arm is, zij moeten altijd strikt rechtvaardig zijn. 16Roddel niet. Doe niets dat het leven van uw naaste in gevaar brengt, want Ik ben de Here. 17U mag uw broeder niet haten. Vermaan ieder die zondigt, want als u er niets van zegt, bent u even schuldig als hij. 18Wees niet haatdragend of wraakzuchtig, maar heb uw naaste net zo lief als uzelf, want Ik ben de Here. 19Gehoorzaam mijn wetten: laat van uw vee niet verschillende soorten met elkaar paren, zaai uw land niet in met twee verschillende soorten zaad, draag geen kleren van twee soorten stof.

20Als een man een slavin verleidt die aan een andere man als vrouw is gegeven, hoewel zij niet is vrijgekocht, moeten zij beiden door de rechter worden gestraft. Maar zij zullen niet worden gedood, want zij was nog niet vrij. 21De betrokken man zal een ram als zijn schuldoffer voor de Here brengen bij de ingang van de tabernakel. 22De priester zal met de ram verzoening doen voor de begane zonde en het zal de zondaar worden vergeven.

23Wanneer u het land binnenkomt en allerlei vruchtbomen plant, zult u de eerste drie oogsten niet binnenhalen, want die zijn onrein. 24In het vierde jaar zal de hele oogst tot lof van de Here zijn geheiligd. 25In het vijfde jaar mag u de oogst eten en gebruiken, zo krijgt u een grotere opbrengst.

26Ik ben de Here, uw God! U mag geen vlees eten waarin nog bloed zit, u mag zich niet bezighouden met waarzeggerij en toverij. 27U mag, als teken van rouw om een dode, uw hoofdhaar niet rond laten afknippen, uw baardhaar niet aan de zijden afscheren, 28niet in uw lichaam snijden en geen tatoeëringen op uw huid aanbrengen—Ik ben de Here. 29Ontheilig uw dochter niet door haar te laten prostitueren, anders zal het land worden vervuld met schanddaden. 30Handhaaf mijn sabbatswetten en eerbiedig mijn tabernakel, want Ik ben de Here. 31Geef u niet af met geesten of mensen die de geesten van doden kunnen raadplegen, want Ik ben de Here, uw God. 32Eer en respecteer de ouderen, in ontzag voor God, Ik ben de Here. 33Vreemdelingen in uw land mag u niet onderdrukken of uitbuiten. 34Zij moeten worden behandeld als iedere andere burger, houd van hen als van uzelf. Vergeet niet dat ook u zelf als vreemdelingen in Egypte hebt gewoond. Ik ben de Here, uw God. 35-36 Wees onpartijdig in de rechtspraak. Gebruik de juiste maten voor lengte, gewicht en inhoud en geef altijd de volledige hoeveelheden. Want Ik ben de Here, uw God, die u uit Egypte heeft bevrijd. 37Al mijn regels en verordeningen moet u nauwgezet naleven, Ik ben de Here.’