Walawi 18 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Walawi 18:1-30

Uhusiano Wa Kukutana Kimwili Kinyume Cha Sheria

1Bwana akamwambia Mose, 218:2 Mwa 17:7; Eze 20:5; Kut 6:7“Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mimi ndimi Bwana Mungu wenu. 318:3 Kut 23:24; Kum 18:9; 2Fal 16:3; 17:8; 1Nya 5:25; Eze 23:8Msifanye kama wafanyavyo huko Misri, mahali mlipokuwa mnaishi, wala msifanye kama wanavyofanya katika nchi ya Kanaani, mahali ninapowapeleka. Msifuate matendo yao. 418:4 Mwa 26:5; Kum 4:1; 1Fal 11:11; Yer 44:10, 23; Eze 11:12Ni lazima mzitii sheria zangu, na mwe waangalifu kuzifuata amri zangu. Mimi ndimi Bwana Mungu wenu. 518:5 Mwa 26:5; Neh 9:20; Isa 55:2; Eze 18:9; 20:11; Amo 5:4-6; Mt 19:17; Rum 10:5; Gal 3:12Zishikeni amri zangu na sheria zangu, kwa maana mtu anayezitii ataishi kwa hizo. Mimi ndimi Bwana.

6“ ‘Hakuna mtu awaye yote atakayemsogelea ndugu wa karibu ili kukutana naye kimwili. Mimi ndimi Bwana.

718:7 Law 20:11; Kum 27:20; Eze 22:10-11“ ‘Usimvunjie heshima baba yako kwa kukutana kimwili na mama yako. Yeye ni mama yako; usiwe na mahusiano kama hayo naye.

818:8 1Kor 5:11; Mwa 35:22; Law 20:11; Kum 22:30; 27:20“ ‘Usikutane kimwili na mke wa baba yako; hiyo itamvunjia heshima baba yako.

918:9 Law 20:17; Kum 27:22; 2Sam 13:13; Eze 22:11“ ‘Usikutane kimwili na dada yako, wala binti wa baba yako, au binti wa mama yako, awe amezaliwa katika nyumba hiyo au mahali pengine.

10“ ‘Usikutane kimwili na binti wa mwanao ama binti wa binti yako; utajivunjia heshima.

11“ ‘Usikutane kimwili na binti wa mke wa baba yako, aliyezaliwa na baba yako; huyo ni dada yako.

1218:12 Law 20:19“ ‘Usikutane kimwili na dada wa baba yako; ni ndugu wa karibu wa baba yako.

1318:13 Law 20:20“ ‘Usikutane kimwili na dada wa mama yako, kwa sababu ni ndugu wa mama yako wa karibu.

14“ ‘Usimvunjie heshima ndugu wa baba yako, kwa kukutana kimwili na mke wake; yeye ni shangazi yako.

1518:15 Mwa 11:31; 38:16; Eze 22:11; Law 20:12“ ‘Usikutane kimwili na mkwe wako, yeye ni mke wa mwanao; usiwe na mahusiano kama hayo naye.

1618:16 Law 20:21; Mt 14:4; Mk 6:18“ ‘Usikutane kimwili na mke wa kaka yako; utamvunjia heshima kaka yako.

1718:17 Law 20:14; Kum 27:23“ ‘Usikutane kimwili na mwanamke kisha na binti yake. Usikutane kimwili na binti wa mwanawe au binti wa binti yake; hao ni ndugu zake wa karibu. Huo ni uovu.

1818:18 Mwa 30:1; Mal 2:15“ ‘Usimchukue dada wa mke wako kuwa mke mwenza, na kukutana naye kimwili wakati bado mke wako anaishi.

1918:19 Law 15:24-30; 20:18; Eze 18:6“ ‘Usimsogelee mwanamke ili kukutana naye kimwili wakati wa unajisi wa siku zake za mwezi.

2018:20 Kut 20:14; Mt 5:27-28; 1Kor 6:9; Ebr 13:4; Mit 6:29“ ‘Usikutane kimwili na mke wa jirani yako na kujitia naye unajisi.

2118:21 Kum 9:4; 12:31; 18:10; 2Fal 16:3; 17:17; 21:6; 23:10; 2Nya 28:1-4; 33:6; Za 106:37-38; Isa 48:11; 57:5; Yer 7:30-31; 19:5; 32:35; Eze 16:20; 22:26; 36:20; Mik 6:7; Law 19:12; 20:2-5; 21:6; Amo 2:7; 1Fal 11:5, 7, 33; Sef 1:5; Mal 1:12; Kut 6:2“ ‘Usimtoe mtoto wako yeyote awe kafara kwa mungu Moleki, kwani hutalinajisi kamwe jina la Mungu wako. Mimi ndimi Bwana.

2218:22 Law 20:13; Kum 23:18; Rum 1:27; 1Kor 6:9; Mwa 19:5“ ‘Usikutane kimwili na mwanaume kama mtu akutanaye na mwanamke; hilo ni chukizo.

2318:23 Kut 22:19; Law 20:15; Kum 27:21“ ‘Usikutane kimwili na mnyama na kujitia unajisi kwake. Mwanamke asijipeleke kwa mnyama ili kukutana naye kimwili; huo ni upotovu.

2418:24 Law 20:23; Kum 9:4; 18:12; Mt 15:18; 1Kor 3:17“ ‘Msijitie unajisi kwa njia yoyote katika hizi, kwa sababu hivi ndivyo mataifa nitakayoyafukuza mbele yenu yalivyojitia unajisi. 2518:25 Hes 35:34; Kum 9:5; 12:31; 18:12; 21:23; Law 20:23; Ay 20:15; Yer 51:34Hata nchi ilitiwa unajisi, hivyo nikaiadhibu kwa dhambi zake, nayo nchi ikawatapika wakazi wake. 2618:26 Mwa 26:5; 18:28; Law 20:22; Ezr 9:11; Mao 1:17Lakini ni lazima uzitunze amri zangu na sheria zangu. Mzawa na wageni waishio miongoni mwenu kamwe wasifanye mambo yoyote ya machukizo haya, 27kwa kuwa mambo haya yote yalifanywa na watu walioishi katika nchi hii kabla yenu, na nchi ikawa najisi. 28Kama mkiinajisi nchi, itawatapika kama ilivyowatapika mataifa yaliyowatangulia.

29“ ‘Kila mtu atakayefanya mojawapo ya machukizo haya, watu hao ni lazima wakatiliwe mbali na watu wao. 3018:30 Law 8:35; Kum 11:1; 19:2; Hes 14:5; Za 68:26; Kut 20:2; 15:11; 1Pet 1:16; Law 11:44; 20:26Shikeni maagizo yangu, wala msifuate desturi za machukizo yoyote yaliyofanywa kabla hamjafika katika nchi hii, na kujitia unajisi kwa hayo. Mimi ndimi Bwana Mungu wako.’ ”

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

利未記 18:1-30

禁止淫亂的條例

1耶和華對摩西說: 2「你把以下條例告訴以色列人。

「我是你們的上帝耶和華。 3你們曾經住在埃及,但不可效法埃及人的行為。我要把你們帶到迦南,但你們不可效法迦南人的行為,不可隨從他們的風俗。 4你們必須遵行我的典章,持守我的律例。我是你們的上帝耶和華。 5你們要遵守我的典章和律例。遵行的人必存活。我是耶和華。

6「你們任何人不可與近親亂倫。我是耶和華。 7不可與你母親亂倫而羞辱你父親。她是你的母親,不可與她亂倫。 8不可與你父親的妻妾亂倫,那會羞辱你的父親。 9不可與你的姊妹亂倫。不論是同父異母的,還是同母異父的,成長在同一家庭,還是不同家庭,都不可與她亂倫。 10不可與孫女或外孫女亂倫,那會自取羞辱。 11不可與你父親妻妾的女兒亂倫。她是你的姊妹,不可與她亂倫。 12不可與姑母亂倫,她是你父親的親人。 13不可與姨母亂倫,她是你母親的親人。 14不可與伯母或嬸母亂倫而羞辱你伯父或叔父。 15不可與兒媳亂倫。她是你兒子的妻子,不可與她亂倫。 16不可與兄嫂或弟媳亂倫,她是你兄弟的妻子。

17「不可與一個女人性交,又與她女兒性交,也不可與她孫女或外孫女性交。她們是她的近親。這都是邪惡行為。 18妻子還在世時,不可娶她的姊妹,與她的姊妹性交,使她們彼此作對。 19女人在月經期間不潔淨,不可與她性交。 20不可與鄰居的妻子性交,那會玷污自己。 21不可把兒女當作祭物獻給假神摩洛,不可褻瀆你上帝的名。我是耶和華。 22男人不可與男人性交,像和女人一樣,這是可憎的。 23不可與獸類交合,玷污自己。女人也不可與獸類交合。這是變態行為。

24「你們不可做這些事玷污自己。因為我要在你們面前趕走的各國正是因為這些行為而玷污了自己。 25他們居住的土地也都被玷污了,所以我因他們的罪惡而懲罰那片土地,我要使那片土地吐出他們。 26你們必須遵守我的律例和典章。不論你們還是寄居在你們中間的外族人,都不可做這些可憎之事。 27因為在你們之前居住在那裡的人做了這些可憎之事,玷污了那片土地。 28如果你們玷污了那片土地,它也會像吐出從前的居民一樣把你們吐出去。 29凡做這些可憎之事的,要將他從民中剷除。 30你們要遵守我的命令,不要效法那片土地上居民的惡俗,以致玷污自己。我是你們的上帝耶和華。」