Walawi 14 – NEN & CARS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Walawi 14:1-57

Kutakasa Kutoka Maambukizo Ya Magonjwa Ya Ngozi

1Bwana akamwambia Mose, 214:2 Law 13:57; Kum 24:8; Mt 8:2-4; Mk 1:40-44; Lk 5:12-14; 17:14“Haya ndiyo masharti yamhusuyo mtu mgonjwa wakati wa kufanyiwa ibada ya utakaso wakati aletwapo kwa kuhani: 3Kuhani atakwenda kumchunguza nje ya kambi. Kama mtu huyo atakuwa amepona ugonjwa wake wa ngozi wa kuambukiza, 414:4 Kut 12:22; Hes 19:6; Za 51:7; Ebr 9:19kuhani ataagiza vitu vifuatavyo viletwe kwa ajili ya mtu atakayetakaswa: ndege wawili safi walio hai, mti wa mwerezi, kitani nyekundu, na hisopo. 5Kisha kuhani ataagiza kwamba mmoja wa ndege wale achinjwe kwenye chungu chenye maji safi. 6Kisha kuhani atamchukua ndege aliye hai na kumtumbukiza pamoja na mti wa mwerezi, kitani nyekundu na hisopo ndani ya damu ya yule ndege aliyechinjiwa kwenye maji safi. 714:7 2Fal 5:10-14; Isa 52:15; Eze 36:25; Law 8:11; Ebr 10:22Atamnyunyizia yule mwenye ugonjwa wa kuambukiza maji hayo mara saba, na kumtangaza kuwa safi. Kisha atamwachia yule ndege aliye hai aende zake kwenye mashamba.

814:8 Law 11:25; 13:11; 15:5; 17:15; 22:6; Kut 29:4; Hes 5:2-3; 12:14-15; 19:7-8; 20; 31:24; 2Nya 26:21“Huyo mtu atakayetakaswa ni lazima afue nguo zake, anyoe nywele zake zote, na aoge kwa maji; ndipo atakapokuwa safi kwa desturi ya ibada. Baada ya hili anaweza kuingia kambini, lakini ni lazima akae nje ya hema lake kwa siku saba. 914:9 Law 13:5-6; Hes 6:9; Kum 21:12Siku ya saba ni lazima anyoe nywele zake zote; yaani anyoe nywele za kichwa, ndevu zake, kope zake na nywele nyingine zote. Ni lazima afue nguo zake, na aoge kwa maji, naye atakuwa safi.

1014:10 Hes 6:10; 15:9; 28:20; Mt 8:4; Mk 1:44; Lk 5:14; Law 2:1; 4:32“Siku ya nane, ni lazima alete kondoo dume wawili na kondoo jike mmoja, wote wa mwaka mmoja na wasio na dosari, pamoja na sehemu tatu za kumi za efa14:10 Sehemu tatu za kumi za efa ni sawa na kilo 3. za unga laini uliochanganywa na mafuta, kwa ajili ya sadaka ya nafaka, na logi moja14:10 Logi ni kipimo cha ujazo ambacho ni sawa na lita 0.3. ya mafuta. 1114:11 Hes 6:10, 16Kuhani atakayemtangaza kuwa safi atahitaji kumkabidhi mgonjwa aliyepona pamoja na sadaka zake zote mbele za Bwana katika ingilio la Hema la Kukutania.

1214:12 Law 5:18; 6:6-7; Kut 29:24“Kisha kuhani atamchukua mmoja wa wale kondoo dume na kumtoa kuwa sadaka ya hatia, pamoja na ile logi moja ya mafuta; ataviinua mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa. 1314:13 Kut 29:11; Law 6:24-30; 7:7; Isa 53:7; Yn 1:29; 1Pet 1:19; Ufu 5:6Atamchinja huyo kondoo katika mahali patakatifu ambapo sadaka ya dhambi na ile ya kuteketezwa huchinjiwa. Kama ilivyo sadaka ya dhambi, sadaka ya hatia ni ya kuhani; nayo ni takatifu sana. 1414:14 Kut 29:20; Law 8:23; Ufu 12:11; Ebr 9:9-14; Kol 1:14; 2Kor 7:1Kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya hatia na kuitia kwenye ncha ya sikio la kuume la yule atakayetakaswa, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume. 15Kuhani atachukua sehemu ya ile logi ya mafuta, ayamimine kwenye kiganja cha mkono wake mwenyewe wa kushoto, 16na achovye kidole chake cha shahada cha mkono wake wa kuume kwenye mafuta yaliyoko kwenye kiganja chake, na kwa kidole hicho anyunyize mafuta hayo mara saba mbele za Bwana. 1714:17 Rum 6:13-22; 1Kor 6:20Kuhani atampaka yule anayetakaswa sehemu ya mafuta yaliyobaki kiganjani kwenye ncha ya sikio lake la kuume, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume, mahali palepale alipompaka damu ya sadaka ya kuondoa hatia. 1814:18 Law 15:15; 4:26; Hes 15:28; Dan 9:24; Rum 3:23-25; 5:11; Efe 2:12-22; Kol 1:19-22Kuhani atayapaka mafuta yaliyobaki kwenye kiganja chake juu ya kichwa cha yule anayetakaswa, na kufanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana.

1914:19 Law 5:3; 15:15“Kisha kuhani atatoa dhabihu ya sadaka ya dhambi na kufanya upatanisho kwa ajili ya yule atakayetakaswa kutoka unajisi wake. Baada ya hayo, kuhani atachinja sadaka ya kuteketezwa 2014:20 Law 15:30na kuitoa juu ya madhabahu, pamoja na sadaka ya nafaka ili kumfanyia upatanisho, naye atakuwa safi.

2114:21 Law 5:7; 12:8; Ay 34:19; Mt 11:30; Lk 6:20; Mit 17:5; 1Yn 5:3“Hata hivyo, kama ni maskini na hawezi kupata vitu hivi, lazima achukue mwana-kondoo mmoja kama sadaka ya hatia ipate kuinuliwa ili kumfanyia upatanisho, pamoja na sehemu ya kumi ya efa14:21 Sehemu ya kumi ya efa ni sawa na lita 2. ya unga laini uliochanganywa na logi moja ya mafuta kwa ajili ya sadaka ya nafaka, 2214:22 Law 5:7; 15:30; 12:8; Lk 2:24na hua wawili au makinda mawili ya njiwa, kile atakachoweza kupata, mmoja kwa sadaka ya dhambi, na mwingine kwa sadaka ya kuteketezwa.

23“Katika siku ya nane, lazima avilete vitu hivyo kwa kuhani, kwa ajili ya kutakaswa kwake kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana. 2414:24 Hes 6:14; 1The 5:23; 1Yn 1:7; Ufu 7:14Kuhani atamchukua mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya hatia, pamoja na ile logi ya mafuta ya kuinuliwa mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa. 2514:25 Kut 29:20Atamchinja huyo mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya hatia. Pia ataichukua sehemu ya damu yake na kuipaka kwenye ncha ya sikio la kuume la yule anayetakaswa, na aipake pia kwenye kidole gumba cha mkono wa kuume wa huyo mtu, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume. 26Kuhani atamiminia sehemu ya mafuta kwenye kiganja chake cha mkono wa kushoto, 27na kwa kidole chake cha shahada cha mkono wa kuume, atamnyunyizia yule anayetakaswa yale mafuta yaliyo kwenye kiganja chake mara saba mbele za Bwana. 28Atampaka mafuta yaliyobaki kwenye kiganja chake katika sehemu zote, kama alivyompaka damu ya sadaka ya hatia: yaani, kwenye ncha ya sikio la kuume la yule anayetakaswa, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume. 29Kuhani atayapaka mafuta yaliyobaki katika kiganja chake kwenye kichwa cha yule anayetakaswa, na kufanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana. 3014:30 Rum 8:3Kisha atatoa dhabihu wale hua ama yale makinda ya njiwa ambayo mtu ataweza kuwapata, 3114:31 Law 5:7; 15:15, 30mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na mwingine kuwa sadaka ya kuteketezwa, pamoja na sadaka ya nafaka. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya yule anayetakaswa.”

3214:32 Law 13:2; 14:34; Mwa 12:5; 17:8; 48:4; Kut 6:4; Hes 13:2; 27:12; 32:22; Kum 3:27; 32:49; Isa 45:7; Amo 3:6Haya ndiyo masharti kwa mtu yeyote mwenye ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, na ambaye hana uwezo wa kutoa sadaka za kawaida kwa ajili ya kutakaswa kwake.

Kutakaswa Upele

33Bwana akawaambia Mose na Aroni, 34“Mtakapoingia katika nchi ya Kanaani ambayo ninawapa kuwa milki yenu, nami nikaweka upele ueneao kwenye nyumba katika nchi ile, 3514:35 Za 91:10; Mit 3:33; Zek 5:4ni lazima mwenye nyumba hiyo akamwambie kuhani, ‘Nimeona kitu fulani kinachofanana na upele kwenye nyumba yangu.’ 3614:36 Hes 19:18; Za 51:7; Isa 52:11; 1Tim 5:22; Ufu 18:4Kuhani ataagiza vitu vyote vitolewe ndani ya nyumba, kabla hajaenda kuchunguza kama ina ugonjwa huo, ili kitu chochote ndani ya nyumba kisitangazwe kuwa najisi. Baada ya hili, kuhani ataingia ndani na kuikagua hiyo nyumba. 3714:37 Law 13:19; 14:38; 13:4-5Atachunguza upele huo katika kuta za nyumba hiyo, nazo kama zina rangi ya kijani kibichi au wekundu, na kuna mibonyeo ndani ya ukuta, 38kuhani atatoka na kufunga mlango wa nyumba hiyo kwa siku saba. 39Siku ya saba, kuhani atarudi kuikagua nyumba. Kama upele umeenea juu ya kuta, 40ataagiza kwamba mawe yote yaliyoambukizwa yaondolewe na kutupwa katika eneo lililo najisi nje ya mji. 41Kuta zote za ndani ya nyumba hiyo ni lazima zikwanguliwe, na kifusi chake kitupwe mahali najisi nje ya mji. 42Kisha watachukua mawe mengine na kujenga palipobomolewa kwa udongo mpya wa mfinyanzi, na kuipiga nyumba hiyo lipu mpya.

43“Ikiwa upele huo utatokea tena ndani ya ile nyumba baada ya mawe kuondolewa na nyumba kukwanguliwa na kuwekwa lipu mpya, 4414:44 Law 13:51kuhani atakwenda kuikagua, na kama upele umeenea ndani ya nyumba, basi ni upele uharibuo; nyumba hiyo ni najisi. 45Ni lazima ibomolewe: mawe yake, mbao na lipu yake, vyote vikatupwe nje ya mji mahali palipo najisi.

4614:46 Law 11:24; 17:15; 22:6; Hes 19:7-10; 1Kor 15:33“Yeyote atakayeingia katika nyumba hiyo ikiwa imefungwa, atakuwa najisi mpaka jioni. 4714:47 Law 11:25Yeyote atakayelala au kula ndani ya nyumba hiyo ni lazima afue nguo zake.

4814:48 Law 13:6; Kum 32:29; Ay 5:18; Hos 6:1; Mk 5:29; Lk 7:21“Lakini ikiwa kuhani atakuja kuikagua na kukuta kuwa upele haujaenea tena baada ya nyumba kupigwa lipu, ataitangaza nyumba ile kuwa safi, kwa sababu upele umekwisha. 4914:49 1Fal 4:33Ili kuitakasa nyumba hiyo, mwenye nyumba ataleta ndege wawili, mti wa mwerezi, kitani nyekundu na hisopo. 50Atamchinja mmoja wa wale ndege kwenye chungu chenye maji safi. 5114:51 Za 51:7; 1Fal 4:33Kisha atachukua mti wa mwerezi, hisopo, kitani nyekundu na ndege aliye hai, na kuvitumbukiza ndani ya damu ya ndege aliyechinjwa pamoja na maji safi, na kuinyunyizia nyumba ile mara saba. 52Ataitakasa nyumba kwa damu ya yule ndege, maji safi, ndege aliye hai, mti wa mwerezi, hisopo na kitani nyekundu. 53Kisha atamwachia yule ndege aliye hai huru mashambani nje ya mji. Kwa njia hii atafanya upatanisho kwa ajili ya nyumba ile, nayo itakuwa safi.”

5414:54 Law 13:2Haya ndiyo masharti kuhusu aina yoyote ya ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, mwasho wowote, 5514:55 Law 13:47-52upele ndani ya nguo au ndani ya nyumba, 5614:56 Law 13:2; 14:57; 10:10; Kut 15:26; Kum 24:8; Za 78:5; 119:96; Mit 6:23kwa uvimbe, vipele au kipaku kingʼaacho, 57kupambanua wakati kitu fulani ni safi au najisi.

Haya ndiyo masharti kuhusu magonjwa ya ngozi ya kuambukiza na upele.

Священное Писание

Левит 14:1-56

Очищение от заразных кожных болезней

1Вечный сказал Мусе:

2– Вот правила о больном во время его очищения. Когда его приведут к священнослужителю, 3пусть священнослужитель выйдет за лагерь и осмотрит его. Если больной исцелился от заразной кожной болезни, 4то пусть священнослужитель велит взять для очищаемого двух живых чистых птиц и кедрового дерева, алой пряжи и иссопа14:4 Иссоп – по всей вероятности, это не собственно иссоп, а один из видов майорана, распространённый в Исраиле. Кедровое дерево, алая шерсть и иссоп были символами очищения от греха в иудейской культуре.. 5Пусть священнослужитель велит убить одну из птиц над глиняным горшком со свежей водой. 6Пусть он возьмёт живую птицу и погрузит её вместе с кедровым деревом, алой пряжей и иссопом в кровь птицы, убитой над свежей водой. 7Пусть он семь раз окропит очищаемого от заразной болезни, объявит его чистым и выпустит живую птицу в открытое поле.

8Пусть очищаемый выстирает одежду, сбреет все волосы, вымоется – и будет чист. Теперь он может войти в лагерь, но должен семь дней жить вне шатра. 9На седьмой день пусть он сбреет все волосы: голову, бороду, брови и остальные волосы. Пусть он выстирает одежду и вымоется – и будет чист.

10На восьмой день он должен принести двух ягнят-самцов и одну годовалую самку – всех без изъяна – с двадцатью четырьмя чашками14:10 Букв.: «три десятых ефы». лучшей муки, смешанной с маслом, для хлебного приношения и одну треть литра14:10 Букв.: «один лог». Также в ст. 12, 15, 21, 24. масла. 11Пусть священнослужитель, совершающий очищение, поставит очищаемого с его приношениями перед Вечным у входа в шатёр встречи.

12Пусть священнослужитель возьмёт одного из ягнят и принесёт его в жертву повинности вместе с одной третью литра масла. Он потрясёт их перед Вечным как приношение потрясания. 13Пусть он заколет ягнёнка в святом месте, где закалывают жертву за грех и жертву всесожжения. Подобно жертве за грех, жертва повинности принадлежит священнослужителю – это великая святыня. 14Пусть священнослужитель возьмёт кровь жертвы повинности и помажет ею мочку правого уха очищаемого, большой палец его правой руки и большой палец правой ноги. 15Пусть священнослужитель возьмёт одну треть литра масла, нальёт в ладонь левой руки, 16погрузит правый указательный палец в масло на ладони и с пальца окропит маслом перед Вечным семь раз. 17Маслом, оставшимся в ладони, священнослужитель помажет мочку правого уха очищаемого, большой палец его правой руки и большой палец правой ноги поверх крови жертвы повинности. 18Оставшееся в ладони масло священнослужитель выльет на голову очищаемого и очистит его перед Вечным.

19Пусть священнослужитель принесёт жертву за грех и очистит очищаемого от нечистоты. После этого священнослужитель заколет жертву всесожжения, 20принесёт её на жертвеннике вместе с хлебным приношением, очистит его, и он будет чист.

21Но если он беден, и такое приношение ему не по средствам, то пусть он возьмёт одного ягнёнка в жертву повинности для потрясания, чтобы очистить себя, и полтора килограмма14:21 Букв.: «одну десятую ефы». лучшей муки, смешанной с маслом, для хлебного приношения, одну треть литра масла 22и двух горлиц или двух молодых голубей, какие будут ему по средствам: одного – в жертву за грех, а другого – для всесожжения.

23На восьмой день пусть он принесёт их, чтобы очиститься, к священнослужителю, к входу в шатёр встречи, перед Вечным. 24Пусть священнослужитель возьмёт ягнёнка жертвы повинности вместе с одной третью литра масла и потрясёт их перед Вечным как приношение потрясания. 25Пусть он заколет ягнёнка жертвы повинности, возьмёт его кровь и помажет ею мочку правого уха очищаемого, большой палец его правой руки и большой палец правой ноги. 26Пусть священнослужитель нальёт масло в ладонь левой руки 27и указательным пальцем правой руки окропит маслом из ладони перед Вечным семь раз. 28Пусть он помажет маслом из ладони те же места, которые он помазал кровью жертвы повинности: мочку правого уха очищаемого, большой палец его правой руки и большой палец правой ноги. 29Остальное масло из ладони пусть священнослужитель выльет на голову очищаемого, чтобы очистить его перед Вечным. 30Пусть он принесёт в жертву горлиц или молодых голубей, какие жертвующему по средствам: 31одного – в жертву за грех, а другого – во всесожжение вместе с хлебным приношением. Так священнослужитель очистит очищаемого перед Вечным.

32Вот правила для любого, кто болел заразной кожной болезнью и кому не по средствам принести для своего очищения обычные приношения.

О плесени в домах

33Вечный сказал Мусе и Харуну:

34– Когда вы войдёте в землю Ханаана, которую Я отдаю вам во владение, и Я наведу растущую плесень на какой-нибудь дом в той земле, 35то пусть хозяин дома пойдёт и скажет священнослужителю: «В моём доме я видел что-то похожее на плесень». 36Пусть священнослужитель велит вынести всё из дома, прежде чем войдёт осмотреть плесень, иначе всё в доме будет объявлено нечистым. После этого пусть священнослужитель войдёт и осмотрит дом. 37Пусть он осмотрит плесень на стенах: если на них будут зеленоватые или красноватые пятна, на вид углубляющиеся в поверхность стены, 38то пусть священнослужитель выйдет наружу и запрёт его на семь дней. 39На седьмой день священнослужитель вернётся снова обследовать дом. Если плесень распространилась по стенам, 40то пусть он велит выворотить заражённые камни и бросить их на нечистое место за пределами города. 41Изнутри пусть стены дома выскоблят, а отскоблённую обмазку высыпят на нечистое место за пределами города. 42Пусть старые камни заменят новыми и обмажут дом новой обмазкой.

43Если после того, как камни были выворочены, а дом выскоблили и обмазали, плесень появится в доме снова, 44священнослужитель должен пойти и осмотреть его. Если плесень распространилась по дому – это растущая плесень; дом нечист. 45Пусть дом разрушат, а его камни, строительное дерево и всю обмазку вынесут из города на нечистое место.

46Любой, кто войдёт в дом, когда он заперт, будет нечист до вечера. 47Любой, кто будет в этом доме спать или есть, должен выстирать одежду.

48Но если священнослужитель, который придёт осмотреть его, увидит, что плесень не распространилась после того, как дом был обмазан, то он объявит дом чистым, так как плесень сошла. 49Чтобы очистить дом, пусть он возьмёт двух птиц и кедровое дерево, алую пряжу и иссоп. 50Пусть он заколет одну из птиц над свежей водой в глиняном горшке. 51Пусть он возьмёт кедровое дерево, иссоп, алую пряжу и живую птицу, погрузит их в кровь убитой птицы и в свежую воду и окропит дом семь раз. 52Так он очистит дом кровью птицы, свежей водой, живой птицей, кедровым деревом, иссопом и алой пряжей. 53Пусть он выпустит живую птицу в открытое поле за пределами города. Так он очистит дом, и дом станет чист.

54Таковы правила о любой заразной кожной болезни: о лишае, 55о плесени на одежде и на доме, об опухоли, сыпи и воспалении, 56чтобы определить чистоту чего-либо.

Таковы правила о заразных кожных болезнях и плесени.