Kutakasa Kutoka Maambukizo Ya Magonjwa Ya Ngozi
1Bwana akamwambia Mose, 214:2 Law 13:57; Kum 24:8; Mt 8:2-4; Mk 1:40-44; Lk 5:12-14; 17:14“Haya ndiyo masharti yamhusuyo mtu mgonjwa wakati wa kufanyiwa ibada ya utakaso wakati aletwapo kwa kuhani: 3Kuhani atakwenda kumchunguza nje ya kambi. Kama mtu huyo atakuwa amepona ugonjwa wake wa ngozi wa kuambukiza, 414:4 Kut 12:22; Hes 19:6; Za 51:7; Ebr 9:19kuhani ataagiza vitu vifuatavyo viletwe kwa ajili ya mtu atakayetakaswa: ndege wawili safi walio hai, mti wa mwerezi, kitani nyekundu, na hisopo. 5Kisha kuhani ataagiza kwamba mmoja wa ndege wale achinjwe kwenye chungu chenye maji safi. 6Kisha kuhani atamchukua ndege aliye hai na kumtumbukiza pamoja na mti wa mwerezi, kitani nyekundu na hisopo ndani ya damu ya yule ndege aliyechinjiwa kwenye maji safi. 714:7 2Fal 5:10-14; Isa 52:15; Eze 36:25; Law 8:11; Ebr 10:22Atamnyunyizia yule mwenye ugonjwa wa kuambukiza maji hayo mara saba, na kumtangaza kuwa safi. Kisha atamwachia yule ndege aliye hai aende zake kwenye mashamba.
814:8 Law 11:25; 13:11; 15:5; 17:15; 22:6; Kut 29:4; Hes 5:2-3; 12:14-15; 19:7-8; 20; 31:24; 2Nya 26:21“Huyo mtu atakayetakaswa ni lazima afue nguo zake, anyoe nywele zake zote, na aoge kwa maji; ndipo atakapokuwa safi kwa desturi ya ibada. Baada ya hili anaweza kuingia kambini, lakini ni lazima akae nje ya hema lake kwa siku saba. 914:9 Law 13:5-6; Hes 6:9; Kum 21:12Siku ya saba ni lazima anyoe nywele zake zote; yaani anyoe nywele za kichwa, ndevu zake, kope zake na nywele nyingine zote. Ni lazima afue nguo zake, na aoge kwa maji, naye atakuwa safi.
1014:10 Hes 6:10; 15:9; 28:20; Mt 8:4; Mk 1:44; Lk 5:14; Law 2:1; 4:32“Siku ya nane, ni lazima alete kondoo dume wawili na kondoo jike mmoja, wote wa mwaka mmoja na wasio na dosari, pamoja na sehemu tatu za kumi za efa14:10 Sehemu tatu za kumi za efa ni sawa na kilo 3. za unga laini uliochanganywa na mafuta, kwa ajili ya sadaka ya nafaka, na logi moja14:10 Logi ni kipimo cha ujazo ambacho ni sawa na lita 0.3. ya mafuta. 1114:11 Hes 6:10, 16Kuhani atakayemtangaza kuwa safi atahitaji kumkabidhi mgonjwa aliyepona pamoja na sadaka zake zote mbele za Bwana katika ingilio la Hema la Kukutania.
1214:12 Law 5:18; 6:6-7; Kut 29:24“Kisha kuhani atamchukua mmoja wa wale kondoo dume na kumtoa kuwa sadaka ya hatia, pamoja na ile logi moja ya mafuta; ataviinua mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa. 1314:13 Kut 29:11; Law 6:24-30; 7:7; Isa 53:7; Yn 1:29; 1Pet 1:19; Ufu 5:6Atamchinja huyo kondoo katika mahali patakatifu ambapo sadaka ya dhambi na ile ya kuteketezwa huchinjiwa. Kama ilivyo sadaka ya dhambi, sadaka ya hatia ni ya kuhani; nayo ni takatifu sana. 1414:14 Kut 29:20; Law 8:23; Ufu 12:11; Ebr 9:9-14; Kol 1:14; 2Kor 7:1Kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya hatia na kuitia kwenye ncha ya sikio la kuume la yule atakayetakaswa, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume. 15Kuhani atachukua sehemu ya ile logi ya mafuta, ayamimine kwenye kiganja cha mkono wake mwenyewe wa kushoto, 16na achovye kidole chake cha shahada cha mkono wake wa kuume kwenye mafuta yaliyoko kwenye kiganja chake, na kwa kidole hicho anyunyize mafuta hayo mara saba mbele za Bwana. 1714:17 Rum 6:13-22; 1Kor 6:20Kuhani atampaka yule anayetakaswa sehemu ya mafuta yaliyobaki kiganjani kwenye ncha ya sikio lake la kuume, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume, mahali palepale alipompaka damu ya sadaka ya kuondoa hatia. 1814:18 Law 15:15; 4:26; Hes 15:28; Dan 9:24; Rum 3:23-25; 5:11; Efe 2:12-22; Kol 1:19-22Kuhani atayapaka mafuta yaliyobaki kwenye kiganja chake juu ya kichwa cha yule anayetakaswa, na kufanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana.
1914:19 Law 5:3; 15:15“Kisha kuhani atatoa dhabihu ya sadaka ya dhambi na kufanya upatanisho kwa ajili ya yule atakayetakaswa kutoka unajisi wake. Baada ya hayo, kuhani atachinja sadaka ya kuteketezwa 2014:20 Law 15:30na kuitoa juu ya madhabahu, pamoja na sadaka ya nafaka ili kumfanyia upatanisho, naye atakuwa safi.
2114:21 Law 5:7; 12:8; Ay 34:19; Mt 11:30; Lk 6:20; Mit 17:5; 1Yn 5:3“Hata hivyo, kama ni maskini na hawezi kupata vitu hivi, lazima achukue mwana-kondoo mmoja kama sadaka ya hatia ipate kuinuliwa ili kumfanyia upatanisho, pamoja na sehemu ya kumi ya efa14:21 Sehemu ya kumi ya efa ni sawa na lita 2. ya unga laini uliochanganywa na logi moja ya mafuta kwa ajili ya sadaka ya nafaka, 2214:22 Law 5:7; 15:30; 12:8; Lk 2:24na hua wawili au makinda mawili ya njiwa, kile atakachoweza kupata, mmoja kwa sadaka ya dhambi, na mwingine kwa sadaka ya kuteketezwa.
23“Katika siku ya nane, lazima avilete vitu hivyo kwa kuhani, kwa ajili ya kutakaswa kwake kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana. 2414:24 Hes 6:14; 1The 5:23; 1Yn 1:7; Ufu 7:14Kuhani atamchukua mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya hatia, pamoja na ile logi ya mafuta ya kuinuliwa mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa. 2514:25 Kut 29:20Atamchinja huyo mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya hatia. Pia ataichukua sehemu ya damu yake na kuipaka kwenye ncha ya sikio la kuume la yule anayetakaswa, na aipake pia kwenye kidole gumba cha mkono wa kuume wa huyo mtu, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume. 26Kuhani atamiminia sehemu ya mafuta kwenye kiganja chake cha mkono wa kushoto, 27na kwa kidole chake cha shahada cha mkono wa kuume, atamnyunyizia yule anayetakaswa yale mafuta yaliyo kwenye kiganja chake mara saba mbele za Bwana. 28Atampaka mafuta yaliyobaki kwenye kiganja chake katika sehemu zote, kama alivyompaka damu ya sadaka ya hatia: yaani, kwenye ncha ya sikio la kuume la yule anayetakaswa, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume. 29Kuhani atayapaka mafuta yaliyobaki katika kiganja chake kwenye kichwa cha yule anayetakaswa, na kufanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana. 3014:30 Rum 8:3Kisha atatoa dhabihu wale hua ama yale makinda ya njiwa ambayo mtu ataweza kuwapata, 3114:31 Law 5:7; 15:15, 30mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na mwingine kuwa sadaka ya kuteketezwa, pamoja na sadaka ya nafaka. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya yule anayetakaswa.”
3214:32 Law 13:2; 14:34; Mwa 12:5; 17:8; 48:4; Kut 6:4; Hes 13:2; 27:12; 32:22; Kum 3:27; 32:49; Isa 45:7; Amo 3:6Haya ndiyo masharti kwa mtu yeyote mwenye ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, na ambaye hana uwezo wa kutoa sadaka za kawaida kwa ajili ya kutakaswa kwake.
Kutakaswa Upele
33Bwana akawaambia Mose na Aroni, 34“Mtakapoingia katika nchi ya Kanaani ambayo ninawapa kuwa milki yenu, nami nikaweka upele ueneao kwenye nyumba katika nchi ile, 3514:35 Za 91:10; Mit 3:33; Zek 5:4ni lazima mwenye nyumba hiyo akamwambie kuhani, ‘Nimeona kitu fulani kinachofanana na upele kwenye nyumba yangu.’ 3614:36 Hes 19:18; Za 51:7; Isa 52:11; 1Tim 5:22; Ufu 18:4Kuhani ataagiza vitu vyote vitolewe ndani ya nyumba, kabla hajaenda kuchunguza kama ina ugonjwa huo, ili kitu chochote ndani ya nyumba kisitangazwe kuwa najisi. Baada ya hili, kuhani ataingia ndani na kuikagua hiyo nyumba. 3714:37 Law 13:19; 14:38; 13:4-5Atachunguza upele huo katika kuta za nyumba hiyo, nazo kama zina rangi ya kijani kibichi au wekundu, na kuna mibonyeo ndani ya ukuta, 38kuhani atatoka na kufunga mlango wa nyumba hiyo kwa siku saba. 39Siku ya saba, kuhani atarudi kuikagua nyumba. Kama upele umeenea juu ya kuta, 40ataagiza kwamba mawe yote yaliyoambukizwa yaondolewe na kutupwa katika eneo lililo najisi nje ya mji. 41Kuta zote za ndani ya nyumba hiyo ni lazima zikwanguliwe, na kifusi chake kitupwe mahali najisi nje ya mji. 42Kisha watachukua mawe mengine na kujenga palipobomolewa kwa udongo mpya wa mfinyanzi, na kuipiga nyumba hiyo lipu mpya.
43“Ikiwa upele huo utatokea tena ndani ya ile nyumba baada ya mawe kuondolewa na nyumba kukwanguliwa na kuwekwa lipu mpya, 4414:44 Law 13:51kuhani atakwenda kuikagua, na kama upele umeenea ndani ya nyumba, basi ni upele uharibuo; nyumba hiyo ni najisi. 45Ni lazima ibomolewe: mawe yake, mbao na lipu yake, vyote vikatupwe nje ya mji mahali palipo najisi.
4614:46 Law 11:24; 17:15; 22:6; Hes 19:7-10; 1Kor 15:33“Yeyote atakayeingia katika nyumba hiyo ikiwa imefungwa, atakuwa najisi mpaka jioni. 4714:47 Law 11:25Yeyote atakayelala au kula ndani ya nyumba hiyo ni lazima afue nguo zake.
4814:48 Law 13:6; Kum 32:29; Ay 5:18; Hos 6:1; Mk 5:29; Lk 7:21“Lakini ikiwa kuhani atakuja kuikagua na kukuta kuwa upele haujaenea tena baada ya nyumba kupigwa lipu, ataitangaza nyumba ile kuwa safi, kwa sababu upele umekwisha. 4914:49 1Fal 4:33Ili kuitakasa nyumba hiyo, mwenye nyumba ataleta ndege wawili, mti wa mwerezi, kitani nyekundu na hisopo. 50Atamchinja mmoja wa wale ndege kwenye chungu chenye maji safi. 5114:51 Za 51:7; 1Fal 4:33Kisha atachukua mti wa mwerezi, hisopo, kitani nyekundu na ndege aliye hai, na kuvitumbukiza ndani ya damu ya ndege aliyechinjwa pamoja na maji safi, na kuinyunyizia nyumba ile mara saba. 52Ataitakasa nyumba kwa damu ya yule ndege, maji safi, ndege aliye hai, mti wa mwerezi, hisopo na kitani nyekundu. 53Kisha atamwachia yule ndege aliye hai huru mashambani nje ya mji. Kwa njia hii atafanya upatanisho kwa ajili ya nyumba ile, nayo itakuwa safi.”
5414:54 Law 13:2Haya ndiyo masharti kuhusu aina yoyote ya ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, mwasho wowote, 5514:55 Law 13:47-52upele ndani ya nguo au ndani ya nyumba, 5614:56 Law 13:2; 14:57; 10:10; Kut 15:26; Kum 24:8; Za 78:5; 119:96; Mit 6:23kwa uvimbe, vipele au kipaku kingʼaacho, 57kupambanua wakati kitu fulani ni safi au najisi.
Haya ndiyo masharti kuhusu magonjwa ya ngozi ya kuambukiza na upele.
Regler for renselse efter en smitsom sygdom
1-2Herren gav derefter Moses følgende anvisninger for, hvordan urene personer kan blive erklæret rene igen:
3„Præsten skal gå uden for lejren for at undersøge dem, som er erklæret urene. Hvis præsten kan se, at sygdommen er forsvundet, 4skal han bede om to levende fugle af den slags, der må spises, noget cedertræ, en purpurrød snor og isopgrene. Tingene skal bruges i renselsesceremonien for dem, som er blevet helbredt. 5Præsten skal beordre den ene af fuglene slagtet over et lerkar med frisk kildevand. 6Den anden fugl, som stadig er i live, skal sammen med cedertræet, den purpurrøde snor og isopgrenen dyppes i det opsamlede blod. 7Så skal præsten syv gange stænke blod over dem, som er blevet helbredt, og erklære dem for raske, idet han slipper den levende fugl løs.
8Derefter skal de, som er blevet helbredt, vaske deres tøj, barbere håret af og bade, hvorefter de kan vende tilbage til lejren, men de skal holde sig uden for deres families telt i syv dage. 9På den syvende dag skal de igen barbere håret af og også øjenbrynene, samt skægget for mændenes vedkommende, og de skal bade og vaske deres tøj igen, før de endelig kan erklæres for fuldkommen helbredt for deres sygdom.
10Næste dag, altså på den ottende dag, skal de hver tage to vædderlam uden fysiske skavanker, et etårs gimmerlam, også uden fysiske skavanker, seks liter fint mel rørt op i olivenolie og en tredjedel liter olivenolie. 11Så skal præsten, som har foretaget undersøgelsen, bringe de helbredte og deres offergaver frem for Herren ved indgangen til åbenbaringsteltet. 12Han skal tage det ene af vædderlammene, det, der skal bruges til skyldoffer, sammen med olivenolien og svinge det foran alteret. 13Så skal han slagte lammet på det indviede sted, hvor syndoffer- og brændofferdyrene slagtes, og kødet fra dette skyldoffer tilfalder præsten, så han kan spise det. Det er jo indviet til Herren. 14Derefter skal han tage noget af blodet fra skyldofferet og smøre det på de helbredtes højre øreflip, højre tommelfinger og højre storetå. 15Så skal han hælde noget af olivenolien i sin venstre hånd, 16dyppe sin højre finger i det og stænke det syv gange foran Herren, 17og dernæst smøre noget af olien på de helbredtes højre øreflip, tommelfinger og storetå oven på skyldofferdyrets blod. 18Når det er gjort, skal han hælde resten af olien i sin hånd over deres hoved. På den måde skal han skaffe dem soning hos Herren.
19Derefter skal præsten ofre gimmerlammet som syndoffer og udføre forsoningsritualet på de helbredtes vegne. Til sidst skal han bringe det andet vædderlam som brændoffer 20og ofre det på alteret sammen med afgrødeofferet, så han skaffer dem soning. Da kan de endelig erklæres for rene.
21Hvis de pågældende imidlertid er fattige og ikke har råd til tre lam, kan de nøjes med at bringe et enkelt vædderlam som skyldoffer. Lammet skal svinges foran Herrens alter som soning for dem. Som afgrødeoffer kan de nøjes med at ofre tre liter fint mel rørt op i olivenolie samt en tredjedel liter olivenolie.
22De skal så i stedet bringe to turtelduer eller to unge duer, afhængigt af hvad de har råd til. Den ene due skal bruges som syndoffer og den anden som brændoffer. 23På den ottende dag, efter at de er erklæret rene, skal de bringe dyrene til præsten ved indgangen til åbenbaringsteltet. 24Han skal så tage lammet og svinge det foran Herrens alter sammen med olivenolien, 25hvorpå han skal slagte lammet og bringe det som skyldoffer og smøre noget af blodet på de helbredtes højre øreflip, tommelfinger og storetå.
26Præsten skal nu hælde olivenolie i sin venstre hånd, 27dyppe sin højre finger i det og stænke det syv gange på Herrens alter. 28Derefter skal han smøre noget af den tiloversblevne olivenolie på deres højre øreflip, tommelfinger og storetå oven på skyldofferdyrets blod. 29Den resterende olie i hans hånd skal han hælde ud over hovedet på dem, på hvis vegne renselsesceremonien udføres, og derved skaffe soning for dem hos Herren.
30Derpå skal han ofre de to turtelduer eller de to unge duer, hvad nu de helbredte kom med. 31Den ene af duerne skal bruges til syndoffer og den anden til brændoffer sammen med afgrødeofferet. På den måde skal præsten skaffe dem soning hos Herren.”
32Disse regler gælder for dem, som ikke er i stand til at bringe de ofre, der normalt kræves i forbindelse med renselsesceremonien.
33Derefter sagde Herren til Moses og Aron: 34„Når I ankommer til Kana’ans land, som jeg har givet jer lovning på, kan det ske, at der kommer mug eller svamp i et hus. 35I så fald skal husets ejer henvende sig til præsten og ikke lægge skjul på sin mistanke om, at der er noget smitsomt i hans hus. 36Så skal præsten beordre huset ryddet, før han går i gang med at undersøge det, så ikke hele indboet bliver urent. 37Hvis han i husets vægge opdager grønlige eller rødlige pletter, der går dybere end selve overfladen, 38skal han afspærre huset i syv dage 39og derefter komme og inspicere det igen. Viser det sig nu, at pletterne på væggen har bredt sig, 40skal præsten beordre den del af væggen fjernet og materialerne anbragt på en dertil indrettet losseplads uden for byen. 41Derefter skal han sørge for, at husets indervægge bliver skrabet grundigt, og at al det afskrabede materiale bliver smidt på lossepladsen uden for byen. 42Så skal der sættes nye sten ind i stedet for de gamle, og væggen skal pudses med ny mørtel.
43Hvis pletterne nu viser sig igen, 44skal præsten komme tilbage og undersøge huset på ny. Hvis han ser, at pletterne har bredt sig, er der tale om noget smitsomt, og huset er urent. 45Derfor skal han beordre huset revet ned, og han skal sørge for, at både sten, tømmer og puds bliver fjernet og smidt på lossepladsen.
46Enhver, der overtræder forbudet om at gå ind i det afspærrede hus, skal regnes for uren indtil aften, 47og enhver, som sover eller spiser i huset, skal vaske sit tøj bagefter.
48Men hvis præsten ved den næste undersøgelse kan se, at der ikke er nye pletter, skal han foretage den ceremonielle renselse, for huset er nu uden for smittefare. 49Renselsen foregår ved, at han tager to fugle, et stykke cedertræ, en purpurrød snor og en isopgren. 50Den ene fugl skal han slagte over et lerkar med frisk kildevand 51-52og derefter dyppe cedertræet, isopgrenen, den purpurrøde snor og den levende fugl i det opsamlede blod. Så skal han bestænke huset syv gange, for at huset kan blive renset, 53og lade den levende fugl slippe fri uden for byen. Det er den fremgangsmåde, som må følges, når et hus er urent, og der skal skaffes soning for det, så det kan blive renset.”
54Det var reglerne for, hvordan man kan fastslå angreb af smitsomme sygdomme 55på tøj og i huse 56og i forbindelse med pletter på huden, udslæt og sår. 57Ved at følge de her regler, kan I afgøre, om der er tale om angreb af en smitsom sygdom eller ej. Derfor blev denne lov givet.