Walawi 13 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Walawi 13:1-59

Masharti Kuhusu Magonjwa Ya Ngozi Yaambukizayo

1Bwana akawaambia Mose na Aroni, 213:2 Law 14:3, 32, 56; Kut 4:6; Hes 5:2; Kum 24:8; 28:27; Isa 3:17; Eze 22:26; Mt 8:2-4; 10:8; Lk 17:1-16; Yn 13:8-10“Iwapo mtu yeyote atakuwa na uvimbe au upele au alama nyeupe juu ya ngozi yake ambayo yaweza kuwa ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza,13:2 Ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, yaani ukoma, ni neno lililotumika kwa Kiebrania kueleza magonjwa mbalimbali ya ngozi ambayo si lazima yawe ni ukoma halisi. ni lazima aletwe kwa Aroni kuhani ama kwa wanawe, kuhani mmojawapo. 313:3 Law 21:1; Hes 9:6; 13:4; Law 14:38; Hes 12:14-15; Kum 24:9Kuhani atachunguza hicho kidonda kilichopo juu ya ngozi yake, na kama nywele za mahali palipo na kidonda zimebadilika kuwa nyeupe, na ikiwa kidonda kimeingia ndani ya ngozi, basi ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, yaani ukoma. Kuhani atakapomchunguza, atamtangaza mtu huyo kuwa ni najisi kwa kawaida ya ibada. 4Kama alama juu ya ngozi yake ni nyeupe, lakini haionekani kuwa imeingia ndani zaidi ya ngozi, na nywele kwenye alama hiyo hazijageuka kuwa nyeupe, kuhani atamtenga mtu huyo mahali pa pekee kwa siku saba. 513:5 Law 14:9Siku ya saba, kuhani atamchunguza, na kama hakuona badiliko kwenye kile kidonda na hakijaenea juu ya ngozi, atamtenga kwa siku nyingine saba. 613:6 Mt 8:3; Lk 5:12-14; Law 11:25; 14:8, 9, 20; 15:8; Hes 8:7Siku ya saba kuhani atamchunguza tena, na kama kidonda kimepungua na hakijaenea juu ya ngozi, kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa ni safi, ni upele tu. Ni lazima mtu huyo afue mavazi yake, naye atakuwa safi. 713:7 Lk 5:14; 13:8Lakini ikiwa ule upele utaenea juu ya ngozi yake baada ya yeye kujionyesha kwa kuhani na kutangazwa kuwa safi, ni lazima aende tena kwa kuhani. 8Kuhani atamchunguza, na kama upele umeenea kwenye ngozi, atamtangaza kuwa najisi, kwani ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, yaani ukoma.

9“Wakati mtu yeyote ana ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, ni lazima aletwe kwa kuhani. 1013:10 Mk 1:44; Lk 17:14; Hes 12:10; 2Nya 26:19-20Kuhani atamchunguza na kama kuna uvimbe mweupe juu ya ngozi ambao umefanya nywele kuwa nyeupe, na kama kuna nyama mbichi ndani ya uvimbe, 1113:11 Kut 4:6; Law 14:8; Hes 12:10; Mt 8:2ni ugonjwa sugu wa ngozi, na kuhani atamtangaza kuwa najisi. Hatamtenga tena kwa sababu ni najisi tayari.

12“Ikiwa ugonjwa utakuwa umeenea kwenye ngozi yake yote kwa kadiri kuhani atakavyoweza kuona, kwamba umeenea kwenye ngozi yote ya huyo mgonjwa kutoka kichwani mpaka wayo, 13kuhani atamchunguza, na kama ugonjwa umeenea mwili mzima, atamtangaza huyo mtu kuwa safi. Kwa kuwa mwili wote umekuwa mweupe, yeye ni safi. 1413:14 Lk 5:12-14Lakini itokeapo nyama mbichi kwenye ngozi yake, atakuwa najisi. 1513:15 Kum 32:29; Za 147:3Kuhani atakapoiona hiyo nyama mbichi, atamtangaza mtu huyo kuwa najisi. Hiyo nyama mbichi ni najisi, ana ugonjwa wa kuambukiza. 16Hiyo nyama mbichi ikigeuka na kuwa nyeupe, ni lazima amwendee kuhani. 17Kuhani atamchunguza, na kama vidonda vimekuwa vyeupe, kuhani atamtangaza mgonjwa huyo kuwa safi; kisha atakuwa safi.

1813:18 Kut 9:9; 15:26; Za 38:3-7; Isa 38:21; Kum 28:27; 2Fal 20:7; 13:19; Law 14:37“Wakati mtu ana jipu juu ya ngozi yake nalo likapona, 19napo mahali palipokuwa na jipu pakatokea uvimbe mweupe, au alama yenye wekundu na weupe, ni lazima akajionyeshe kwa kuhani. 20Kuhani atapachunguza, na kama uvimbe umezama ndani ya ngozi, na nywele zimegeuka kuwa nyeupe, kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa najisi. Ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza uliojitokeza pale jipu lilipokuwa. 21Lakini ikiwa wakati kuhani anapopachunguza pakawa hapana nywele nyeupe ndani yake, wala hakuna shimo bali pamepungua, basi kuhani atamtenga mtu huyo kwa siku saba. 22Kama unaenea kwenye ngozi, kuhani atamtangaza kuwa najisi; ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza. 2313:23 Mit 28:13; Lk 5:14; 1Pet 4:2-4Lakini ikiwa ile alama haijabadilika wala kuenea, ni kovu tu kutokana na jipu, kuhani atamtangaza kuwa safi.

24“Wakati mtu ameungua kwenye ngozi yake, pakatokea alama yenye wekundu na weupe, au alama nyeupe ikaonekana penye nyama mbichi pale palipoungua, 25kuhani ataichunguza ile alama, na kama nywele zilizoko juu yake zimegeuka kuwa nyeupe, napo pametokea shimo, basi huo ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza ambao umetokea juu ya jeraha la moto. Kuhani atamtangaza kuwa najisi; ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza. 26Lakini kama kuhani akichunguza na kuona kwamba hakuna nywele nyeupe kwenye alama ile, wala hakuna shimo napo pameanza kupungua, basi kuhani atamtenga kwa siku saba. 27Siku ya saba kuhani atamchunguza tena, na kama unaenea kwenye ngozi, kuhani atamtangaza kuwa najisi; ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza. 2813:28 Kum 24:8; Mal 2:7; 1Kor 12:9; Isa 3:17Lakini, kama alama ile haikubadilika na wala haijaenea kwenye ngozi, napo pamepungua, ni uvimbe kutokana na jeraha la moto, na kuhani atamtangaza kuwa safi; ni kovu tu kutokana na kuungua.

29“Ikiwa mwanaume au mwanamke ana kidonda juu ya kichwa au juu ya kidevu, 30kuhani atakichunguza kile kidonda, na kama ataona kuwa kimeingia ndani, na nywele zilizoko juu yake ni njano na nyembamba, kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa najisi, kwani ni upele; ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza wa kichwa au kidevu. 31Lakini kama kuhani akichunguza aina hii ya kidonda, kionekane kuwa hakina shimo na hakuna nywele nyeusi juu yake, basi atamtenga mtu huyo kwa siku saba. 32Siku ya saba kuhani atachunguza kidonda kile, na kama upele haujaenea, na hakuna nywele za manjano juu yake, wala hakuna shimo lolote, 33mtu huyo ni lazima anyolewe, isipokuwa mahali palipo na ugonjwa, naye kuhani atamtenga kwa siku nyingine saba. 3413:34 Law 11:25Siku ya saba kuhani atachunguza tena ule upele; ikiwa haujaenea kwenye ngozi na hakuna shimo mahali pale, kuhani atamtangaza kuwa safi. Lazima afue nguo zake, naye atakuwa safi. 35Lakini ikiwa upele utaenea juu ya ngozi baada ya kutangazwa kuwa safi, 36kuhani atamchunguza, na kama upele umeenea kwenye ngozi, kuhani hana haja ya kutazama kama kuna nywele za manjano, mtu huyo ni najisi. 37Hata hivyo, katika uchunguzi wake akiona hapajabadilika, na nywele nyeusi zimeota juu yake, upele umepona. Yeye si najisi, kuhani atamtangaza kuwa safi.

38“Ikiwa mwanaume au mwanamke ana alama nyeupe juu ya ngozi yake, 39kuhani atamchunguza, na kama alama hizo zina weupe uliofifia, ni vipele visivyo na madhara vilivyojitokeza kwenye ngozi; mtu huyo ni safi.

4013:40 Law 21:5; 2Fal 2:23; Isa 3:24; 15:2; 22:12; Eze 27:31; 29:18; Amo 8:10; Mik 1:16“Wakati mwanaume hana nywele naye ana upaa, yeye ni safi. 41Ikiwa hana nywele kwenye ngozi ya kichwa chake, na ana upaa tangu kwenye paji, ni safi. 42Lakini kama ana kidonda chenye wekundu na weupe kwenye kichwa chake chenye upaa, au kwenye paji la uso, ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza unaojitokeza kichwani au kwenye paji lake la uso. 43Kuhani atamchunguza, na kama kidonda kilichovimba juu ya kichwa chake au kwenye paji la uso ni chekundu au cheupe kama ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, 44mtu huyo ni mgonjwa, na ni najisi. Kuhani atamtangaza kuwa najisi kwa sababu ya kidonda kwenye kichwa chake.

4513:45 Law 5:2; 10:6; Eze 24:17, 22; Mik 3:7; Mao 4:15; Lk 17:12“Mtu mwenye ugonjwa kama huo wa kuambukiza ni lazima avae nguo zilizoraruka, awachilie nywele zake bila kuzichana, afunike sehemu ya chini ya uso wake, na apige kelele, ‘Najisi! Najisi!’ 4613:46 Hes 5:1-4; 12:14; 2Fal 7:3; 15:5; 1Kor 5:5; 2The 3:6; Ebr 12:15Kwa muda wote atakaokuwa na ugonjwa huo wa kuambukiza atabaki kuwa najisi. Ni lazima aishi peke yake; ni lazima aishi nje ya kambi.

Masharti Kuhusu Upele

47“Kama vazi lolote lina maambukizo ya upele: likiwa ni vazi la sufu au kitani, 48lolote lililofumwa au kusokotwa likiwa la kitani au la sufu, ngozi yoyote au chochote kilichotengenezwa kwa ngozi, 49tena kama maambukizo kwenye vazi, au ngozi, au lililofumwa au kusokotwa, au kifaa chochote cha ngozi, ni rangi ya kijani au nyekundu, huo ni upele unaoenea na ni lazima kuhani aonyeshwe. 50Kuhani atachunguza upele huo na kukitenga kifaa hicho kwa siku saba. 5113:51 Law 14:44; Eze 16:42Siku ya saba atakichunguza, na kama upele umeenea kwenye nguo, au kifaa kilichofumwa au kusokotwa, au ngozi, kwa vyovyote vile itumikavyo, ni upele uangamizao, kifaa hicho ni najisi. 52Ni lazima aichome hiyo nguo, ikiwa ni ya sufu ama kitani iliyofumwa ama kusokotwa, ama chombo chochote cha ngozi chenye maambukizo, kwa kuwa ni upele unaoangamiza; chombo chote ni lazima kichomwe moto.

53“Lakini wakati kuhani atakapokichunguza na kuona kuwa ule upele haujaenea kwenye nguo iliyofumwa au kusokotwa, au vifaa vya ngozi, 54ataagiza kwamba kifaa chenye maambukizo kisafishwe. Kisha atakitenga kwa siku saba. 55Baada ya kifaa chenye maambukizo kusafishwa, kuhani atakichunguza, na kama upele haujaonyesha badiliko lolote, hata kama haujaenea, ni najisi. Kichome kwa moto, iwe upele umeenea upande mmoja au mwingine. 56Kama kuhani ataona kuwa ile alama imefifia baada ya kuoshwa, basi atararua sehemu iliyo ambukizwa ya nguo au ngozi au kifaa kilichofumwa au kusokotwa. 57Lakini kama ikijitokeza tena kwenye nguo au kitu kilichofumwa au kusokotwa, ama kifaa cha ngozi, kwamba ule upele unaenea, chochote chenye upele ni lazima kichomwe kwa moto. 58Nguo, au kitu kilichofumwa au kusokotwa, au kifaa chochote cha ngozi ambacho kimesafishwa na kuondolewa upele, ni lazima kioshwe tena, nacho kitakuwa safi.”

59Haya ni masharti kuhusu maambukizo ya upele kwenye mavazi ya sufu au kitani, yaliyofumwa ama kusokotwa, ama kifaa chochote cha ngozi, kwa ajili ya kuvitangaza kuwa safi au najisi.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

利未記 13:1-59

有關痲瘋病的條例

1耶和華對摩西亞倫說:

2「如果有人皮膚上長腫包、皮疹或白斑,出現痲瘋病13·2 痲瘋病」此處為傳統譯法,希伯來文的意思指包括痲瘋病在內的各種嚴重皮膚病。症狀,要將他帶到祭司亞倫亞倫做祭司的子孫那裡。 3祭司要檢查患處,如果患處凹陷,患處的毛髮變白,就是痲瘋病,要宣佈他是不潔淨的。 4如果那人的患處有白斑,沒有凹陷,患處的毛髮也沒有變白,祭司要把他隔離七天。 5第七天,祭司要再次檢查患處,如果患處沒有惡化,沒有擴散,祭司要把他再隔離七天。 6第七天,祭司要再次檢查,如果患處顏色變淡,也沒有擴散,祭司要宣佈他是潔淨的。他患的不過是皮疹,他要洗淨衣物,便會潔淨。 7如果祭司已查看並宣佈他是潔淨的,但皮疹又擴散,他必須再去見祭司。 8祭司檢查時,如果發現皮疹已擴散,就要宣佈他是不潔淨的,患了痲瘋病。

9「如果有人患痲瘋病,必須將他帶到祭司面前。 10祭司檢查時,如果發現他皮膚上有白色腫包,毛髮變白,患處出現瘡口, 11他就是患了慢性痲瘋病,祭司要宣佈他是不潔淨的。他無須被隔離,因他已經不潔淨。 12如果他的痲瘋病已擴散,頭上腳上到處可見, 13祭司就要檢查。如果發現痲瘋病已擴散到他全身,全身的皮膚變白,祭司就要宣佈他是潔淨的。 14但如果他身上出現潰爛之處,他便不潔淨。 15祭司看到他身上的潰爛之處,就要宣佈他是不潔淨的,因為那潰爛之處表明他患了痲瘋病。 16如果潰爛之處痊癒並變白,他就要去見祭司。 17祭司檢查時,若發現潰爛之處確已變白,就要宣佈他是潔淨的,他便潔淨了。

18「如果有人身上長瘡,又痊癒了, 19但原患處出現白色腫包或白裡帶紅的斑,他就要去讓祭司檢查。 20祭司檢查時,若發現患處凹陷,患處的毛髮變白,就要宣佈他是不潔淨的。這是瘡變成了痲瘋病。 21但祭司檢查時,若發現患處沒有白毛,沒有凹陷,肉色變淡,就要把他隔離七天。 22隔離期間,若患處擴散,祭司要宣佈他是不潔淨的,是患了痲瘋病。 23如果患處的斑原樣未變,沒有擴散,便是瘡疤,祭司要宣佈他是潔淨的。

24「如果有人被火燒傷,患處變白或白中帶紅, 25祭司要檢查他的患處。如果患處的毛髮變白,傷口凹陷,他的燒傷已變成痲瘋病,祭司要宣佈他是不潔淨的,因為他患了痲瘋病。 26祭司檢查時,若發現患處沒有白毛,傷口沒有凹陷,顏色變淡,就要把他隔離七天。 27第七天,祭司要再次檢查,若發現患處擴散,就要宣佈他是不潔淨的,因為他患了痲瘋病。 28如果患處沒有擴散,顏色變淡,就是燒傷引起的腫包,祭司要宣佈他是潔淨的,因為那不過是燒傷的疤痕。

29「如果有男女頭上或下巴長瘡, 30祭司要檢查患處,若發現患處凹陷,上面有黃色細毛,就要宣佈那人是不潔淨的,因為那是疥癬,是痲瘋病。 31祭司檢查時,若發現患處沒有凹陷,沒有黑毛,就要將那人隔離七天。 32第七天,祭司要檢查患處,若發現疥癬沒有擴散,上面沒有黃毛,患處沒有凹陷, 33那人要剃去頭髮和鬍鬚,但不可剃患處的毛髮。祭司要將他再隔離七天。 34第七天,祭司要再次檢查,若發現疥癬沒有擴散,患處沒有凹陷,就要宣佈那人是潔淨的。那人要洗淨衣服,便潔淨了。 35那人潔淨以後,疥癬若再次擴散, 36祭司就要再次檢查。如果疥癬確已擴散,祭司不必再找黃毛,那人是不潔淨的。 37如果祭司看到疥癬原樣未變,患處長出黑毛,那人就已經痊癒,是潔淨的。祭司要宣佈那人是潔淨的。

38「如果有男女身上長白斑, 39祭司要檢查患處,若發現斑呈灰白色,就是皮疹,那人是潔淨的。

40「如果有人脫髮,成了禿頭,他是潔淨的。 41如果有人前額脫髮,他只是前額光禿,仍是潔淨的。 42如果在光禿的頭上或前額上長出白裡帶紅的瘡,那就是痲瘋病。 43祭司要檢查患處,若發現瘡周圍腫脹,看起來像痲瘋病, 44就是得了痲瘋病,那人是不潔淨的。祭司要宣佈那人是不潔淨的。

45「患痲瘋病的人必須撕裂衣服,披頭散髮,遮住臉的下半部,高喊『不潔淨!不潔淨!』 46只要病不痊癒,他就不潔淨,要獨自住在營外。

黴變衣物的條例

47「如果衣物出現黴斑,不論是羊毛衣、細麻衣、 48羊毛織品、細麻織品,還是皮革或皮革製品, 49只要發現黴斑是綠色或紅色的,那就是黴變,要拿給祭司檢查。 50祭司檢查後,要把那衣物隔離七天。 51第七天,祭司要再次檢查,若發現衣物、編織品或皮革上的黴斑蔓延,那衣物就是不潔淨的。 52不論那是衣服、羊毛或細麻織品,還是皮革製品,祭司都必須把它燒掉,因為那是黴變。必須燒掉黴變的衣物。 53如果祭司發現衣服、編織品或皮革上的黴斑沒有蔓延, 54就要吩咐人洗淨衣物,再隔離七天。 55之後,祭司要再次檢查洗過的衣物,若發現黴斑原樣未變,即使沒有蔓延,那衣物也是不潔淨的。無論衣物裡面還是外面黴變,都必須把它燒掉。 56如果祭司發現洗過後黴斑退色,就要把黴變的部分從衣服、皮革、編織品上撕下來。 57以後衣物、編織品或皮革上若再次出現黴斑,便是舊患復發,要把它燒掉。 58如果洗過衣服、編織品或皮革後,黴斑消失了,要再洗一次就潔淨了。

59「羊毛衣、細麻衣、編織品或皮革製品出現黴變時,以上條例可用來鑒定這些衣物是否潔淨。」