Walawi 12 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Walawi 12:1-8

Utakaso Baada Ya Kuzaa Mtoto

1Bwana akamwambia Mose, 212:2 Law 15:19; 18:19; Isa 64:6; Eze 18:6; 22:10; 36:17“Waambie Waisraeli: ‘Mwanamke ambaye atapata mimba na kuzaa mtoto wa kiume atakuwa najisi kwa kawaida ya ibada kwa siku saba, kama anavyokuwa najisi wakati wa siku zake za hedhi. 312:3 Kut 22:30; Mwa 17:10-12; Lk 1:59; 2:21; 2:2; Yn 7:22-23Mvulana atatahiriwa siku ya nane. 4Kisha ni lazima huyo mwanamke asubiri kwa siku thelathini na tatu, ndipo atakaswe kutoka damu kwake. Hataruhusiwa kugusa kitu chochote kilicho kitakatifu au kuingia mahali patakatifu, mpaka siku za kutakaswa kwake zimetimia. 5Kama akimzaa mtoto wa kike, mwanamke huyo atakuwa najisi kwa majuma mawili, kama wakati wake wa hedhi. Kisha atasubiri kwa siku sitini na sita, ndipo atatakaswa kutoka damu kwake.

612:6 Lk 2:22; Kut 29:38; Law 5:7; 23:12; Hes 6:12-14; 7:15; Ufu 5:6-8; 7:14“ ‘Siku zake za utakaso kwa ajili ya mwana au binti zitakapotimia, mwanamke huyo atamletea kuhani kwenye ingilio la Hema la Kukutania mwana-kondoo mwenye umri wa mwaka mmoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, na kinda la njiwa au hua kwa ajili ya sadaka ya dhambi. 712:7 Ebr 9:9-28; 10:1-12Atavitoa mbele za Bwana ili kufanya upatanisho kwa ajili yake, na kisha atakuwa safi kwa desturi ya ibada kutokana na kutokwa damu kwake.

“ ‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya mwanamke atakayezaa mtoto wa kiume au wa kike. 812:8 Mwa 15:9; Law 4:26; 14:22; 5:7; Lk 2:22-24; Law 4:26; 2Kor 8:9Kama huyo mwanamke hana uwezo wa kumpata mwana-kondoo, ataleta hua wawili au makinda mawili ya njiwa, moja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa na mwingine kwa ajili ya sadaka ya dhambi. Kwa njia hii, kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake, naye atakuwa safi.’ ”

New International Reader’s Version

Leviticus 12:1-8

Becoming “Clean” After Having a Baby

1The Lord spoke to Moses. He said, 2“Speak to the Israelites. Tell them, ‘Suppose a woman becomes pregnant and has a baby boy. Then she will be “unclean” for seven days. It is the same as when she is “unclean” during her monthly period. 3On the eighth day the boy must be circumcised. 4After that, the woman must wait for 33 days to be made pure from her bleeding. She must not touch anything sacred until the 33 days are over. During that time she must not go to the sacred tent. 5But suppose she has a baby girl. Then she will be “unclean” for two weeks. It is the same as during her period. After the two weeks, she must wait for 66 days to be made pure from her bleeding.

6“ ‘After she has waited the required number of days to be made pure, she must bring two offerings. She must take them to the priest at the entrance to the tent of meeting. She must bring a lamb a year old for a burnt offering. She must also bring a young pigeon or a dove for a sin offering. 7The priest must offer them to the Lord. They will pay for her sin. Then she will be “clean” from her bleeding.

“ ‘These are the rules for a woman who has a baby boy or girl. 8But suppose she can’t afford a lamb. Then she must bring two doves or two young pigeons. One is for a burnt offering. The other is for a sin offering. The priest will sacrifice those offerings. That will pay for her sin. And she will be “clean.” ’ ”