Wakolosai 3 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Wakolosai 3:1-25

Kanuni Za Kuishi Maisha Matakatifu

13:1 Rum 6:5; Mk 16:19Basi, kwa kuwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu, Kristo alikoketi mkono wa kuume wa Mungu. 23:2 Flp 3:19, 20Yafikirini mambo yaliyo juu, wala si ya duniani. 33:3 Rum 6:2; 2Kor 5:14Kwa maana ninyi mlikufa, nao uhai wenu sasa umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu. 43:4 1Kor 1:7; 1Pet 1:13; 1Yn 3:2; Gal 2:20; 1Kor 1:7; 1Pet 1:13; Yn 3:2Wakati Kristo, aliye uzima wenu, atakapotokea, ndipo nanyi mtakapotokea pamoja naye katika utukufu.

53:5 Efe 5:3-5; Rum 6:2; Efe 4:22; Gal 5:24; 1Kor 6:18; Efe 5:3; Gal 5:19-21Kwa hiyo, ueni kabisa chochote kilicho ndani yenu cha asili ya kidunia: yaani uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya na ulafi, ambayo ndiyo ibada ya sanamu. 63:6 Rum 1:18Kwa sababu ya mambo haya, ghadhabu ya Mungu inakuja. 73:7 Efe 2:2Ninyi pia zamani mlienenda katika mambo haya mlipoishi maisha hayo. 83:8 Efe 4:22-31Lakini sasa yawekeni mbali nanyi mambo kama haya yote: yaani hasira, ghadhabu, uovu, masingizio na lugha chafu kutoka midomoni mwenu. 93:9 Efe 4:22-25Msiambiane uongo, kwa maana mmevua kabisa utu wenu wa kale pamoja na matendo yake, 103:10 Rum 1:22; 2Kor 4:16; Efe 2:10nanyi mmevaa utu mpya, unaofanywa upya katika ufahamu sawasawa na mfano wa Muumba wake. 113:11 Rum 10:12; 1Kor 7:19; Gal 3:28; Efe 1:23Hapa hakuna Myunani wala Myahudi, aliyetahiriwa wala asiyetahiriwa, asiyestaarabika wala aliyestaarabika, mtumwa wala mtu huru, bali Kristo ni yote, na ndani ya wote.

123:12 Flp 2:3; 2Kor 6:6; Gal 5:22, 23; Efe 4:2Kwa hiyo, kwa kuwa ninyi mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao sana, jivikeni moyo wa huruma, utu wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu. 133:13 Efe 4:2, 32; 4:32Vumilianeni na kusameheana mtu akiwa na lalamiko lolote dhidi ya mwenzake. Sameheaneni kama vile Bwana alivyowasamehe ninyi. 143:14 1Kor 13:1-13; Efe 4:3Zaidi ya maadili haya yote jivikeni upendo, ambao ndio unaofunga kila kitu pamoja katika umoja mkamilifu.

153:15 Yn 14:27Amani ya Kristo na itawale mioyoni mwenu, kwa kuwa ninyi kama viungo vya mwili mmoja mmeitiwa amani. Tena kuweni watu wa shukrani. 163:16 Rum 10:17; Kol 1:28; Efe 5:19Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu, mkifundishana na kuonyana katika hekima yote, mkimwimbia Mungu zaburi, nyimbo na tenzi za rohoni, huku mkiwa na shukrani mioyoni mwenu. 173:17 Efe 5:20-22Lolote mfanyalo, ikiwa ni kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba katika yeye.

Kanuni Katika Madaraka Ya Nyumbani

18Ninyi wake, watiini waume zenu, kama inavyostahili katika Bwana.

193:19 Efe 5:25, 28, 33; 1Pet 3:7; Efe 4:31Ninyi waume, wapendeni wake zenu, wala msiwe na uchungu dhidi yao.

203:20 Efe 6:1; 5:24; Tit 2:9Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote, kwa maana hivi ndivyo inavyompendeza Bwana.

213:21 Efe 6:4Ninyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu, wasije wakakata tamaa.

223:22 Efe 6:5; 1Tim 6:1; Tit 2:9; 1Pet 2:18Ninyi watumwa, watiini mabwana zenu wa hapa duniani katika mambo yote. Fanyeni hivyo si wakiwepo tu, wala si kwa kutafuta upendeleo wao, bali kwa moyo mnyofu na kumcha Bwana. 233:23 Efe 6:6, 7Lolote mfanyalo, fanyeni kwa moyo kama watu wanaomtumikia Bwana, na si wanadamu, 243:24 Mdo 20:32kwa kuwa mnajua kwamba mtapokea urithi wenu kutoka kwa Bwana ukiwa thawabu yenu. Ni Bwana Yesu Kristo mnayemtumikia. 253:25 Mdo 10:34Yeyote atendaye mabaya atalipwa kwa ajili ya mabaya yake, wala hakuna upendeleo.

New International Version – UK

Colossians 3:1-25

Living as those made alive in Christ

1Since, then, you have been raised with Christ, set your hearts on things above, where Christ is, seated at the right hand of God. 2Set your minds on things above, not on earthly things. 3For you died, and your life is now hidden with Christ in God. 4When Christ, who is your3:4 Some manuscripts our life, appears, then you also will appear with him in glory.

5Put to death, therefore, whatever belongs to your earthly nature: sexual immorality, impurity, lust, evil desires and greed, which is idolatry. 6Because of these, the wrath of God is coming.3:6 Some early manuscripts coming on those who are disobedient 7You used to walk in these ways, in the life you once lived. 8But now you must also rid yourselves of all such things as these: anger, rage, malice, slander, and filthy language from your lips. 9Do not lie to each other, since you have taken off your old self with its practices 10and have put on the new self, which is being renewed in knowledge in the image of its Creator. 11Here there is no Gentile or Jew, circumcised or uncircumcised, barbarian, Scythian, slave or free, but Christ is all, and is in all.

12Therefore, as God’s chosen people, holy and dearly loved, clothe yourselves with compassion, kindness, humility, gentleness and patience. 13Bear with each other and forgive one another if any of you has a grievance against someone. Forgive as the Lord forgave you. 14And over all these virtues put on love, which binds them all together in perfect unity.

15Let the peace of Christ rule in your hearts, since as members of one body you were called to peace. And be thankful. 16Let the message of Christ dwell among you richly as you teach and admonish one another with all wisdom through psalms, hymns, and songs from the Spirit, singing to God with gratitude in your hearts. 17And whatever you do, whether in word or deed, do it all in the name of the Lord Jesus, giving thanks to God the Father through him.

Instructions for Christian households

18Wives, submit yourselves to your husbands, as is fitting in the Lord.

19Husbands, love your wives and do not be harsh with them.

20Children, obey your parents in everything, for this pleases the Lord.

21Fathers,3:21 Or Parents do not embitter your children, or they will become discouraged.

22Slaves, obey your earthly masters in everything; and do it, not only when their eye is on you and to curry their favour, but with sincerity of heart and reverence for the Lord. 23Whatever you do, work at it with all your heart, as working for the Lord, not for human masters, 24since you know that you will receive an inheritance from the Lord as a reward. It is the Lord Christ you are serving. 25Anyone who does wrong will be repaid for their wrongs, and there is no favouritism.