Wakolosai 3 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Wakolosai 3:1-25

Kanuni Za Kuishi Maisha Matakatifu

13:1 Rum 6:5; Mk 16:19Basi, kwa kuwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu, Kristo alikoketi mkono wa kuume wa Mungu. 23:2 Flp 3:19, 20Yafikirini mambo yaliyo juu, wala si ya duniani. 33:3 Rum 6:2; 2Kor 5:14Kwa maana ninyi mlikufa, nao uhai wenu sasa umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu. 43:4 1Kor 1:7; 1Pet 1:13; 1Yn 3:2; Gal 2:20; 1Kor 1:7; 1Pet 1:13; Yn 3:2Wakati Kristo, aliye uzima wenu, atakapotokea, ndipo nanyi mtakapotokea pamoja naye katika utukufu.

53:5 Efe 5:3-5; Rum 6:2; Efe 4:22; Gal 5:24; 1Kor 6:18; Efe 5:3; Gal 5:19-21Kwa hiyo, ueni kabisa chochote kilicho ndani yenu cha asili ya kidunia: yaani uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya na ulafi, ambayo ndiyo ibada ya sanamu. 63:6 Rum 1:18Kwa sababu ya mambo haya, ghadhabu ya Mungu inakuja. 73:7 Efe 2:2Ninyi pia zamani mlienenda katika mambo haya mlipoishi maisha hayo. 83:8 Efe 4:22-31Lakini sasa yawekeni mbali nanyi mambo kama haya yote: yaani hasira, ghadhabu, uovu, masingizio na lugha chafu kutoka midomoni mwenu. 93:9 Efe 4:22-25Msiambiane uongo, kwa maana mmevua kabisa utu wenu wa kale pamoja na matendo yake, 103:10 Rum 1:22; 2Kor 4:16; Efe 2:10nanyi mmevaa utu mpya, unaofanywa upya katika ufahamu sawasawa na mfano wa Muumba wake. 113:11 Rum 10:12; 1Kor 7:19; Gal 3:28; Efe 1:23Hapa hakuna Myunani wala Myahudi, aliyetahiriwa wala asiyetahiriwa, asiyestaarabika wala aliyestaarabika, mtumwa wala mtu huru, bali Kristo ni yote, na ndani ya wote.

123:12 Flp 2:3; 2Kor 6:6; Gal 5:22, 23; Efe 4:2Kwa hiyo, kwa kuwa ninyi mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao sana, jivikeni moyo wa huruma, utu wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu. 133:13 Efe 4:2, 32; 4:32Vumilianeni na kusameheana mtu akiwa na lalamiko lolote dhidi ya mwenzake. Sameheaneni kama vile Bwana alivyowasamehe ninyi. 143:14 1Kor 13:1-13; Efe 4:3Zaidi ya maadili haya yote jivikeni upendo, ambao ndio unaofunga kila kitu pamoja katika umoja mkamilifu.

153:15 Yn 14:27Amani ya Kristo na itawale mioyoni mwenu, kwa kuwa ninyi kama viungo vya mwili mmoja mmeitiwa amani. Tena kuweni watu wa shukrani. 163:16 Rum 10:17; Kol 1:28; Efe 5:19Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu, mkifundishana na kuonyana katika hekima yote, mkimwimbia Mungu zaburi, nyimbo na tenzi za rohoni, huku mkiwa na shukrani mioyoni mwenu. 173:17 Efe 5:20-22Lolote mfanyalo, ikiwa ni kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba katika yeye.

Kanuni Katika Madaraka Ya Nyumbani

18Ninyi wake, watiini waume zenu, kama inavyostahili katika Bwana.

193:19 Efe 5:25, 28, 33; 1Pet 3:7; Efe 4:31Ninyi waume, wapendeni wake zenu, wala msiwe na uchungu dhidi yao.

203:20 Efe 6:1; 5:24; Tit 2:9Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote, kwa maana hivi ndivyo inavyompendeza Bwana.

213:21 Efe 6:4Ninyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu, wasije wakakata tamaa.

223:22 Efe 6:5; 1Tim 6:1; Tit 2:9; 1Pet 2:18Ninyi watumwa, watiini mabwana zenu wa hapa duniani katika mambo yote. Fanyeni hivyo si wakiwepo tu, wala si kwa kutafuta upendeleo wao, bali kwa moyo mnyofu na kumcha Bwana. 233:23 Efe 6:6, 7Lolote mfanyalo, fanyeni kwa moyo kama watu wanaomtumikia Bwana, na si wanadamu, 243:24 Mdo 20:32kwa kuwa mnajua kwamba mtapokea urithi wenu kutoka kwa Bwana ukiwa thawabu yenu. Ni Bwana Yesu Kristo mnayemtumikia. 253:25 Mdo 10:34Yeyote atendaye mabaya atalipwa kwa ajili ya mabaya yake, wala hakuna upendeleo.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

歌罗西书 3:1-25

追求属天的事

1你们既然和基督一同复活了,就应当追求天上的事,那里有坐在上帝右边的基督。 2你们要思想天上的事,而不是地上的事, 3因为你们的旧生命已经死了,你们的新生命与基督一同藏在上帝里面。 4基督就是你们的新生命,祂显现的时候,你们也必和祂一起在荣耀中显现。

5所以,你们要治死身上属世的罪恶,如淫乱、污秽、邪情、恶欲和贪心,贪心就是拜偶像, 6因为上帝的烈怒必临到做这些事的悖逆之人。 7你们过去也和他们一样过着罪恶的生活, 8但现在必须杜绝这一切的恶事,如怒气、愤恨、恶毒、毁谤和污言秽语。 9不要彼此说谎,因为你们已经脱去了旧人和旧的行为, 10穿上了新人。这新人在知识上不断更新,更像他的造物主。 11从此,不再分希腊人、犹太人,受割礼的、未受割礼的,野蛮人、未开化的人3:11 未开化的人”希腊文是“西古提人”。,奴隶和自由人,基督就是一切,并且贯穿一切。

12所以,你们既然是上帝所拣选的,是圣洁、蒙爱的人,就要心存怜悯、恩慈、谦虚、温柔和忍耐。 13倘若彼此之间有怨言,总要互相宽容,彼此饶恕,主怎样饶恕你们,你们也要照样饶恕他人。 14最重要的是要有爱,爱能把一切完美地联合在一起。 15要让基督的平安掌管你们的心,你们就是为此而蒙召成为一个身体。要常存感恩的心。 16要将基督的话丰丰富富地存在心里,用各样智慧彼此教导,互相劝诫,以感恩的心用诗篇、圣乐、灵歌颂赞上帝。 17你们无论做什么事、说什么话,都要奉主耶稣的名而行,并借着祂感谢父上帝。

和谐家庭

18你们做妻子的,要顺服丈夫,信主的人应当这样做。 19你们做丈夫的,要爱妻子,不可恶待她们。 20你们做儿女的,凡事要听从父母,因为这是主所喜悦的。 21你们做父亲的,不要激怒儿女,免得他们灰心丧志。 22你们做奴仆的,凡事要听从你们世上的主人,不要只做讨好人的表面工夫,要以敬畏主的心真诚服侍。 23无论做什么事,都要发自内心,像是为主做的,而不是为人做的, 24因为你们知道自己一定会从主那里得到基业为奖赏。你们事奉的是主基督, 25凡作恶的人终必自食恶果,因为上帝不偏待人。