Wakolosai 2 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Wakolosai 2:1-23

12:1 Kol 1:29; 4:12; 4:13, 15, 16; Ufu 1:11Nataka mjue jinsi ninavyojitaabisha kwa ajili yenu na kwa ajili ya wale walioko Laodikia, na pia kwa ajili ya wote ambao hawajapata kuniona mimi binafsi. 22:2 Efe 6:22; Kol 4:8; Rum 16:25Kusudi langu ni watiwe moyo na kuunganishwa katika upendo, ili wapate ule utajiri wa ufahamu mkamilifu, ili waijue siri ya Mungu, yaani, Kristo mwenyewe, 32:3 Isa 11:2; Yer 23:5; Rum 11:33; 1Kor 1:24, 30ambaye ndani yake kumefichwa hazina zote za hekima na maarifa. 42:4 Rum 16:18Nawaambia mambo haya ili mtu yeyote asiwadanganye kwa maneno ya kuwashawishi. 52:5 1Kor 5:4; 1The 2:17Kwa kuwa ingawa mimi siko pamoja nanyi kimwili, lakini niko pamoja nanyi kiroho, nami nafurahi kuuona utaratibu wenu na jinsi uthabiti wa imani yenu katika Kristo ulivyo.

Ukamilifu Wa Maisha Katika Kristo

62:6 Yn 13:13; Kol 1:10Hivyo basi, kama vile mlivyompokea Kristo Yesu kuwa Bwana, endeleeni kukaa ndani yake, 72:7 Efe 3:17; 4:22mkiwa na mizizi, na mmejengwa ndani yake, mkiimarishwa katika imani kama mlivyofundishwa, na kufurika kwa wingi wa shukrani.

82:8 1Tim 6:20; Kol 2:20; Gal 4:2Angalieni mtu yeyote asiwafanye ninyi mateka kwa elimu batili na madanganyo matupu yanayotegemea mapokeo ya wanadamu na mafundisho ya ulimwengu badala ya Kristo.

92:9 Yn 1:16Maana ukamilifu wote wa Uungu umo ndani ya Kristo katika umbile la mwili wa kibinadamu, 102:10 Efe 1:22; Mt 28:18nanyi mmepewa ukamilifu ndani ya Kristo, ambaye ndiye mkuu juu ya kila enzi na kila mamlaka. 112:11 Rum 2:29; Flp 3:3; Gal 5:24Katika Kristo pia mlitahiriwa kwa kutengwa mbali na asili ya dhambi, si kwa tohara inayofanywa kwa mikono ya wanadamu, bali kwa ile tohara iliyofanywa na Kristo, 122:12 Mt 28:19; Rum 6:5; Mdo 2:24mkiwa mmezikwa pamoja naye katika ubatizo, na kufufuliwa pamoja naye kwa njia ya imani yenu katika uweza wa Mungu, aliyemfufua kutoka kwa wafu.

132:13 Efe 2:15; 2:5; 4:32Mlipokuwa wafu katika dhambi zenu na kutokutahiriwa katika asili yenu ya dhambi, Mungu aliwafanya mwe hai pamoja na Kristo. Alitusamehe dhambi zetu zote, 142:14 Efe 2:15; 1Pet 2:24akiisha kuifuta ile hati yenye mashtaka yaliyokuwa yanatukabili, pamoja na maagizo yake. Aliiondoa isiwepo tena, akiigongomea kwenye msalaba wake. 152:15 Kol 2:10; Efe 6:12; Mt 12:29; Lk 10:18; Yn 12:31Mungu akiisha kuzivua enzi na mamlaka, alizifanya kuwa kitu cha fedheha hadharani kwa kuziburura kwa ujasiri, akizishinda katika msalaba wa Kristo.

162:16 Rum 14:3, 4; Mk 7:19; Rum 14:17; Law 23:2; Rum 14:5Kwa hiyo mtu asiwahukumu ninyi kuhusu vyakula au vinywaji, au kuhusu kuadhimisha sikukuu za dini, au Sikukuu za Mwezi Mwandamo au siku ya Sabato. 172:17 Ebr 8:5; 10:1Hizi zilikuwa kivuli cha mambo ambayo yangekuja, lakini ile iliyo halisi imo ndani ya Kristo. 182:18 Kol 2:23; 1Kor 9:24; Flp 3:14Mtu yeyote asiwaondolee thawabu yenu kwa kusisitiza kunyenyekea kwake na kuabudu malaika. Mtu kama huyo hudumu katika maono yake, akijivuna bila sababu katika mawazo ya kibinadamu. 192:19 Efe 1:22; 1Kor 2:8; Gal 4:3, 9, 14, 16Yeye amepoteza ushirikiano na Kichwa, ambaye kutoka kwake mwili wote unalishwa na kushikamanishwa pamoja kwa viungo na mishipa, nao hukua kwa ukuaji utokao kwa Mungu.

Maonyo Dhidi Ya Walimu Wa Uongo

20Kwa kuwa mlikufa pamoja na Kristo, mkayaacha yale mafundisho ya msingi ya ulimwengu huu, kwa nini bado mnaishi kama ninyi ni wa ulimwengu? Kwa nini mnajitia chini ya amri: 212:21 1Tim 4:3“Msishike! Msionje! Msiguse!”? 222:22 1Kor 6:13; Isa 29:13; Mt 15:9; Tit 1:14Haya yote mwisho wake ni kuharibika yanapotumiwa, kwa sababu msingi wake ni katika maagizo na mafundisho ya wanadamu. 232:23 Kol 2:18Kwa kweli amri kama hizo huonekana kama zina hekima, katika namna za ibada walizojitungia wenyewe, na unyenyekevu wa uongo na kuutawala mwili kwa ukali, lakini hayafai kitu katika kuzuia tamaa za mwili.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

歌羅西書 2:1-23

1我希望你們知道,為了你們和老底嘉人,以及許多從未和我見過面的人,我是怎樣努力奮鬥的, 2為要使你們眾人心受鼓勵,聯結在愛裡,有豐富篤定的真知灼見,可以認識上帝的奧祕。這奧祕就是基督, 3一切智慧和知識都蘊藏在祂裡面。 4我講這番話是為了防止有人用花言巧語迷惑你們。 5現在,我人雖不在你們那裡,心卻和你們在一起,看到你們生活井然有序,對基督堅信不移,我很喜樂。

生活以基督為中心

6你們既然接受了基督耶穌為主,就當繼續遵從祂, 7按照你們所受的教導在祂裡面扎根成長,信心堅固,滿懷感恩。

8你們要謹慎,免得有人用空洞虛假的哲學把你們擄去。這些哲學不是出於基督,而是出於人的傳統和世俗的玄學。 9因為上帝完全的神性有形有體地蘊藏在基督裡, 10你們在基督裡得到了豐盛的生命。祂是一切執政者和掌權者的元首。

11你們也在基督裡受了非人手所行的割禮,是基督為除掉你們的罪惡本性而行的割禮。 12你們接受洗禮時已經與基督一同埋葬了,並藉著相信上帝使基督從死裡復活的大能,與基督一同復活了。 13你們從前死在過犯和未被割除的罪惡本性中,但現在上帝卻使你們與基督一同活了過來。上帝赦免了我們一切的過犯, 14撤銷了指控我們違背律法的罪狀,將它和基督一同釘在了十字架上, 15打敗了一切在靈界執政、掌權的邪惡勢力,用基督在十字架上的勝利公開羞辱牠們。

16所以,不可讓人在飲食、節期、朔日2·16 朔日」即每月初一。或安息日的事上批評你們。 17這些都不過是將來之事的影子,那真實的本體是基督。 18有些人喜歡故作謙虛,敬拜天使,沉迷於所看見的幻象,你們不要因他們而失去得獎賞的資格。他們隨從墮落的思想無故自高自大, 19沒有與身體的頭——基督聯結。全身是靠關節和筋絡維繫,從基督得到供應,按上帝的旨意漸漸成長。

20你們既然和基督一同死了,擺脫了世俗的玄學,為什麼仍像活在世俗中, 21服從「不可拿、不可嚐、不可摸」之類的規條呢? 22這些規條不過是人的戒律和說教,經不起實踐的考驗, 23看似充滿智慧,其實只不過是自創的宗教、自表謙卑、苦待己身,對於克制邪情私慾毫無用處。