Wagalatia 4 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Wagalatia 4:1-31

1Lile nisemalo ni kwamba wakati wote mrithi bado ni mtoto, hana tofauti na mtumwa, ingawa ndiye mmiliki wa mali yote. 2Yeye huwa yuko chini ya uangalizi wa walezi na wadhamini mpaka ufike wakati uliowekwa na baba yake. 34:3 Gal 4:9; 5:1; Kol 2:8, 20; Ebr 9:10Vivyo hivyo na sisi, tulipokuwa bado watoto wadogo, tulikuwa utumwani chini ya taratibu za kawaida za ulimwengu. 44:4 Mk 1:15; Rum 5:6; Efe 1:10; Yn 3:17; 1:14; Lk 2:27Lakini ulipowadia utimilifu wa wakati, Mungu alimtuma Mwanawe, ambaye alizaliwa na mwanamke, akazaliwa chini ya sheria, 54:5 Rum 3:24; Yn 1:12; Rum 8:14kusudi awakomboe wale waliokuwa chini ya sheria, ili tupate kupokea zile haki kamili za kufanywa watoto wa Mungu. 64:6 Mdo 16:7; Rum 5:5; 8:15, 16Kwa sababu ninyi ni watoto wa Mungu, Mungu amemtuma Roho wa Mwanawe mioyoni mwetu, anayelia, “Abba,4:6 Abba ni neno la Kiaramu ambalo maana yake ni Baba; lingeweza kutumiwa tu na mtoto wa kuzaa. Baba.” 74:7 Rum 8:17; Gal 3:29Kwa hiyo, wewe si mtumwa tena, bali ni mtoto, kwa kuwa wewe ni mtoto, Mungu amekufanya wewe pia kuwa mrithi kwa kupitia Kristo.

Paulo Awashawishi Wagalatia

84:8 Rum 1:28; 1Kor 1:21; 15:34; 1The 4:5; 2The 1:8; Gal 4:3Zamani, mlipokuwa hammjui Mungu, mlikuwa watumwa wa viumbe ambavyo kwa asili si Mungu. 94:9 1Kor 8:3; Gal 4:3; Kol 2:20Lakini sasa kwa kuwa mmemjua Mungu, au zaidi mmejulikana na Mungu, inakuwaje mnarejea tena katika zile kanuni za kwanza zenye udhaifu na upungufu? Mnataka ziwafanye tena watumwa? 104:10 Rum 14:5; Kol 2:16Mnaadhimisha siku maalum, miezi, nyakati na miaka! 114:11 1The 3:5; Gal 2:2; 5:2, 4Nina hofu juu yenu, kwamba kazi niliyofanya kwa ajili yenu inaweza kuwa nimejitaabisha bure.

124:12 Rum 7:1; Gal 6:18; 2Kor 2:5Ndugu zangu, nawasihi mwe kama mimi, kwa sababu mimi nimekuwa kama ninyi. Hamkunitendea jambo lolote baya. 134:13 1Kor 2:3; 2Kor 11:30; 12:7, 9; Gal 1:6Ninyi mwajua kwamba ni kwa ajili ya udhaifu wangu niliwahubiria Injili. 144:14 Mt 10:40; 2Sam 19:27; Mal 2:7; Zek 12:8; Mt 10:40; Lk 10:16Ingawa hali yangu iliwatia majaribuni, hamkunidharau wala kunidhihaki, bali mlinikaribisha kama malaika wa Mungu, kama vile Kristo Yesu. 15Ile hali ya furaha mliyokuwa nayo imekwenda wapi? Naweza kushuhudia kwamba, kama ingewezekana mngengʼoa macho yenu na kunipa mimi. 164:16 Gal 2:5, 14; Amo 5:10Je, sasa nimekuwa adui yenu kwa kuwaambia kweli?

174:17 Gal 2:4, 12; Rum 10:12; 1Kor 11:2Hao wana shauku ya kuwapata lakini si kwa kusudi zuri. Wanachotaka ni kuwatenga mbali nasi, ili ninyi mpate kuwaonea wao shauku. 184:18 Gal 4:13, 14Ni vizuri wakati wote kuwa na shauku kwa ajili ya kusudi zuri, si wakati nikiwa pamoja nanyi tu. 194:19 1The 2:11; Rum 8:29; Efe 4:13Watoto wangu wapendwa, ambao kwa mara nyingine ninawaonea utungu, ninatamani kwamba Kristo aumbike ndani yenu. 20Natamani kama ningekuwa pamoja nanyi sasa, pengine ningebadilisha sauti yangu. Kwa maana nina wasiwasi kwa ajili yenu.

Mfano Wa Hagari Na Sara

214:21 Rum 2:12Niambieni, ninyi mnaotaka kuwa chini ya sheria, je, hamjui sheria inavyosema? 22Kwa maana imeandikwa kwamba Abrahamu alikuwa na wana wawili, mmoja wa mwanamke mtumwa na wa pili wa mwanamke huru. 234:23 Gal 4:28, 29; Rum 9:7, 8; Mwa 17:16-21; 18:10-14; 4:24Lakini, mtoto wa mwanamke mtumwa alizaliwa kwa mapenzi ya mwili, na yule mwingine wa mwanamke huru alizaliwa kutokana na ahadi ya Mungu.

24Mambo haya yanaweza kuchukuliwa kama mfano. Kwa maana hao wanawake wawili ni mfano wa maagano mawili: Agano la kwanza, ni lile lililofanyika katika Mlima Sinai, lizaalo watoto wa utumwa. Hili ndilo huyo Hagari. 25Basi Hagari anawakilisha Mlima Sinai ulioko Arabuni, na unafanana na Yerusalemu ya sasa ambayo iko utumwani pamoja na watoto wake. 264:26 Flp 2:3; Ebr 12:22; Isa 2:2; Ufu 3:12; 21:2, 10Lakini Yerusalemu wa juu ni huru, nayo ndiye mama yetu. 274:27 Isa 54:1Kwa maana imeandikwa:

“Furahi, ewe mwanamke tasa,

wewe usiyezaa;

paza sauti, na kuimba kwa furaha,

wewe usiyepatwa na utungu wa kuzaa;

kwa maana watoto wa mwanamke aliyeachwa ukiwa ni wengi

kuliko wa mwanamke mwenye mume.”

284:28 Mdo 3:25; Rum 9:8; Gal 3:29Basi, sisi ndugu zangu, ni kama Isaki, tu watoto wa ahadi. 294:29 Mwa 21:9; Gal 5:11; 6:12Lakini, kama vile ilivyokuwa siku zile yule aliyezaliwa kwa mwili alivyomchokoza yule aliyezaliwa kwa Roho, ndivyo ilivyo hata sasa. 304:30 Mwa 21:10Lakini Maandiko yasemaje? “Mwondoe mwanamke mtumwa pamoja na mwanawe, kwa sababu mwana wa mwanamke mtumwa kamwe hatarithi pamoja na mwana wa aliye huru.” 314:31 Rum 7:4; Gal 4:22Kwa hiyo ndugu zangu, sisi si watoto wa mwanamke mtumwa, bali wa yule aliye huru.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

加拉太書 4:1-31

兒子與奴僕

1然而,產業繼承人還年幼時,雖然身為產業的主人,實際上和奴僕沒有分別。 2他一樣要受監護人和管家的約束,一直到他父親指定他繼承產業的日子為止。 3我們也一樣,當我們還是孩童的時候,我們受世界基本規條的轄制。 4然而,時候一到,上帝就差遣自己的兒子藉著一位女子降生,並受律法的約束, 5為要救贖一切受律法約束的人,使我們成為祂的兒女。

6我們4·6 我們」希臘文是「你們」。既然成為兒女,上帝就差遣祂兒子的靈進入我們的心裡,使我們可以稱呼上帝為「阿爸,父親」。 7由此可見,你們從今以後不再是奴僕,而是兒女。既然身為兒女,就可以靠著上帝成為產業繼承人。

保羅對加拉太人的關懷

8從前,你們不認識上帝,做那些假神的奴隸。 9現在,你們既然認識了上帝,或者更應該說是上帝認識了你們,為什麼還要回到那些無意義的基本規條之下,甘願再做它們的奴隸呢? 10為什麼還拘守什麼日子、月分、節期和年分呢? 11我真擔心我在你們身上的一番心血都枉費了!

12弟兄姊妹,我勸你們現在要像我一樣,因為我已經像你們一樣。你們向來沒有虧待過我。 13你們知道,當初是因為我生病才首次有機會向你們傳福音。 14那時,你們雖然因為我生病而受累,卻沒有輕視我、嫌棄我,反而接待我,就像接待上帝的天使,接待基督耶穌一樣。 15我可以為你們作證,如果可能的話,你們那時就是把眼睛剜出來給我,也心甘情願。你們當初的喜樂哪裡去了? 16現在我因為告訴你們真理,就成了你們的仇人嗎?

17那些人非常熱心地對待你們,其實他們心懷不軌,想要離間我們的關係,使你們熱心地對待他們。 18有人熱心待你們當然很好,但總要動機純正、始終如一,不應該只是我和你們在一起時才熱心待你們。 19孩子們,為了你們,我像一位母親再次經歷生產的痛苦,一直到基督的生命在你們裡面成形。 20我恨不得立刻趕到你們身邊,換種口氣說話,因為我為你們焦慮不安。

夏甲與撒拉的例子

21你們這些甘受律法約束的人啊!告訴我,你們沒聽過律法怎麼說嗎? 22律法書上說:亞伯拉罕有兩個兒子,一個是婢女生的,一個是主母生的。 23婢女的兒子是按著人的意願生的,主母的兒子是按著上帝的應許生的。 24這些事都有更深的含義,兩個婦人是指兩個約。夏甲代表頒佈於西奈山的約,她所生的孩子是奴僕。 25夏甲指的是阿拉伯西奈山,相當於現今的耶路撒冷,她和她的兒女都是奴僕。 26那天上的耶路撒冷則是自由的,是我們的母親。 27因為聖經上說:

「不生育、未生養的婦人啊,

要快樂;

未曾生產的女子啊,

要高聲歡呼,

因為沒有丈夫的比有丈夫的兒女更多。」

28弟兄姊妹,你們都像以撒一樣是照著上帝的應許出生的。 29當時,那按著人的意願生的兒子迫害那靠著聖靈生的兒子,現在的情況也和當時一樣。 30但聖經上怎麼說呢?聖經上說:「趕走婢女和她的兒子,因為婢女的兒子不能與主母的兒子一同承受產業。」 31弟兄姊妹,這樣看來,我們不是婢女的兒女,而是主母的兒女。