Wafilipi 4 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Wafilipi 4:1-23

14:1 Flp 1:8; 1Kor 16:13Kwa hiyo, ndugu zangu, ninaowapenda na ambao ninawaonea shauku, ninyi mlio furaha yangu na taji yangu, hivi ndivyo iwapasavyo kusimama imara katika Bwana, ninyi wapenzi wangu.

Mausia

24:2 Flp 2:2; 3:16Nawasihi Euodia na Sintike wawe na nia moja katika Bwana. 34:3 Flp 2:25; Ufu 20:12Naam, nakusihi wewe pia, mwenzangu mwaminifu, uwasaidie hawa wanawake, kwa sababu walijitaabisha katika kazi ya Injili pamoja nami bega kwa bega, wakiwa pamoja na Klementi na watendakazi wenzangu ambao majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima.

44:4 Za 85:6; 97:12; Hab 3:18; Mt 5:12; Rum 12:12; Flp 3:1Furahini katika Bwana siku zote, tena nasema furahini! 54:5 Za 119:151; 145:18; Ebr 10:37; Yak 5:8, 9Upole wenu na ujulikane na watu wote. Bwana yu karibu. 64:6 Mt 6:25-34; Kol 4:2; 1Pet 5:7; Za 145:18; Efe 6:18; 1Tim 2:1Msijisumbue kwa jambo lolote, bali katika kila jambo kwa kuomba na kusihi pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu. 74:7 Isa 26:3; Yn 14:27; Efe 3:19Nayo amani ya Mungu, inayopita fahamu zote, itailinda mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.

84:8 1The 5:22; Rum 12:17Hatimaye, ndugu zangu, mambo yote yaliyo ya kweli, yoyote yaliyo na sifa njema, yoyote yaliyo ya haki, yoyote yaliyo safi, yoyote ya kupendeza, yoyote yenye staha, ukiwepo uzuri wowote, pakiwepo chochote kinachostahili kusifiwa, tafakarini mambo hayo. 94:9 1Kor 4:16; Rum 12:17Mambo yote mliyojifunza au kuyapokea au kuyasikia kutoka kwangu, au kuyaona kwangu, yatendeni hayo. Naye Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi.

Shukrani Kwa Matoleo Yenu

104:10 2Kor 11:9Nina furaha kubwa katika Bwana kwamba hatimaye mmeanza upya kushughulika tena na maisha yangu. Kweli mmekuwa mkinifikiria lakini mlikuwa hamjapata nafasi ya kufanya hivyo. 114:11 1Tim 6:6, 8; Ebr 13:5Sisemi hivyo kwa vile nina mahitaji, la! Kwa maana nimejifunza kuridhika katika hali yoyote. 124:12 1Kor 4:11; 2Kor 11:9Ninajua kupungukiwa, pia ninajua kuwa na vingi. Nimejifunza siri ya kuridhika katika kila hali, wakati wa kushiba na wakati wa kuona njaa, wakati wa kuwa na vingi na wakati wa kupungukiwa. 134:13 2Kor 12:9; Efe 3:16; Kol 1:11; 1Tim 1:12; 2Tim 4:17Naweza kuyafanya mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.

144:14 Flp 1:7Lakini, mlifanya vyema kushiriki nami katika taabu zangu. 154:15 Flp 1:5; Mdo 16:9; 2Kor 11:8, 9Zaidi ya hayo, ninyi Wafilipi mnajua kwamba siku za kwanza nilipoanza kuhubiri Injili, nilipoondoka Makedonia, hakuna kanisa jingine lililoshiriki nami katika masuala ya kutoa na kupokea isipokuwa ninyi. 164:16 Mdo 17:1; 1The 2:9Kwa maana hata nilipokuwa huko Thesalonike, mliniletea msaada kwa ajili ya mahitaji yangu zaidi ya mara moja. 174:17 1Kor 9:11, 12Si kwamba natafuta sana yale matoleo, bali natafuta sana ile faida itakayozidi sana kwa upande wenu. 184:18 Flp 2:25; 2Kor 2:14Nimelipwa kikamilifu hata na zaidi; nimetoshelezwa kabisa sasa, kwa kuwa nimepokea kutoka kwa Epafrodito vile vitu mlivyonitumia, sadaka yenye harufu nzuri, dhabihu inayokubalika na ya kumpendeza Mungu. 194:19 Za 23:1; 2Kor 9:8; Rum 2:4Naye Mungu wangu atawajaza ninyi na kila mnachohitaji kwa kadiri ya utajiri wake katika utukufu ndani ya Kristo Yesu.

204:20 Gal 1:4; 1The 1:3; 3:11, 13; Rum 11:36Mungu wetu aliye Baba yetu apewe utukufu milele na milele. Amen.

Salamu Za Mwisho

214:21 Gal 1:2Msalimuni kila mtakatifu katika Kristo Yesu. Ndugu walioko pamoja nami wanawasalimu. 224:22 Mdo 9:13Watakatifu wote wanawasalimu, hasa wale watu wa nyumbani mwa Kaisari.

234:23 Rum 16:20; Gal 6:18Neema ya Bwana Yesu Kristo iwe pamoja na roho zenu. Amen.

New International Reader’s Version

Philippians 4:1-23

Remain Strong in the Lord

1My brothers and sisters, in this way remain strong in the Lord. I love you and long for you. Dear friends, you are my joy and my crown.

2Here is what I’m asking Euodia and Syntyche to do. I’m asking them to work together in the Lord. That’s because they both belong to the Lord. 3My true companion, here is what I ask you to do. Help these women, because they have served at my side. They have worked with me to spread the good news. So have Clement and the rest of those who have worked together with me. Their names are all written in the book of life.

Final Commands

4Always be joyful because you belong to the Lord. I will say it again. Be joyful! 5Let everyone know how gentle you are. The Lord is coming soon. 6Don’t worry about anything. No matter what happens, tell God about everything. Ask and pray, and give thanks to him. 7Then God’s peace will watch over your hearts and your minds. He will do this because you belong to Christ Jesus. God’s peace can never be completely understood.

8Finally, my brothers and sisters, always think about what is true. Think about what is noble, right and pure. Think about what is lovely and worthy of respect. If anything is excellent or worthy of praise, think about those kinds of things. 9Do what you have learned or received or heard from me. Follow my example. The God who gives peace will be with you.

Paul Gives Thanks for the Philippians’ Gifts

10At last you are concerned about me again. That makes me very happy. We belong to the Lord. I know that you were concerned. But you had no chance to show it. 11I’m not saying this because I need anything. I have learned to be content no matter what happens to me. 12I know what it’s like not to have what I need. I also know what it’s like to have more than I need. I have learned the secret of being content no matter what happens. I am content whether I am well fed or hungry. I am content whether I have more than enough or not enough. 13I can do all this by the power of Christ. He gives me strength.

14But it was good of you to share in my troubles. 15And you believers at Philippi know what happened when I left Macedonia. Not one church helped me in the matter of giving and receiving. You were the only one that did. That was in the early days when you first heard the good news. 16Even when I was in Thessalonica, you sent me help when I needed it. And you did it more than once. 17It is not that I want your gifts. What I really want is what is best for you. 18I have received my full pay and have more than enough. I have everything I need. That’s because Epaphroditus brought me the gifts you sent. They are a sweet-smelling offering. They are a gift that God accepts. He is pleased with it. 19My God will meet all your needs. He will meet them in keeping with his wonderful riches. These riches come to you because you belong to Christ Jesus.

20Give glory to our God and Father for ever and ever. Amen.

Final Greetings

21Greet all God’s people. They belong to Christ Jesus.

The brothers and sisters who are with me send greetings.

22All God’s people here send you greetings. Most of all, those who live in the palace of Caesar send you greetings.

23May the grace of the Lord Jesus Christ be with your spirit. Amen.