Wafilipi 3 – NEN & NEN

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Wafilipi 3:1-21

Hakuna Tumaini Katika Mwili

13:1 Flp 2:18; 4:4Hatimaye, ndugu zangu, furahini katika Bwana! Mimi kuwaandikia mambo yale yale hakuniudhi, kwa maana ni kinga kwa ajili yenu.

23:2 Za 22:16, 20Jihadharini na mbwa, wale watenda maovu, jihadharini na wale wajikatao miili yao, wasemao ili kuokoka ni lazima kutahiriwa. 33:3 Gal 3:15; Kol 2:11Kwa maana sisi ndio tulio tohara, sisi tumwabuduo Mungu katika Roho, tunaona fahari katika Kristo Yesu, ambao hatuweki tumaini letu katika mwili, 43:4 2Kor 11:21; 11:8, 22ingawa mimi mwenyewe ninazo sababu za kuutumainia mwili.

Kama mtu yeyote akidhani anazo sababu za kuutumainia mwili, mimi zaidi. 53:5 Lk 1:59; 2Kor 11:22; Rum 11:1; Mdo 23:6Nilitahiriwa siku ya nane, mimi ni Mwisraeli wa kabila la Benyamini, Mwebrania wa Waebrania. Kwa habari ya sheria, ni Farisayo, 63:6 Mdo 8:3; Rum 10:5kwa habari ya juhudi, nilikuwa nalitesa kanisa, kuhusu haki ipatikanayo kwa sheria, mimi nilikuwa sina hatia.

73:7 Mt 13:44; Lk 14:33Lakini mambo yale yaliyokuwa faida kwangu, sasa nayahesabu kuwa hasara kwa ajili ya Kristo. 83:8 Yer 9:23, 24; Yn 17:3Zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara tupu nikiyalinganisha na faida kubwa ipitayo kiasi cha kumjua Kristo Yesu Bwana wangu, ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote, nikiyahesabu kuwa kama mavi ili nimpate Kristo. 93:9 Rum 10:5; 9:30Nami nionekane mbele zake bila kuwa na haki yangu mwenyewe ipatikanayo kwa sheria, bali ile ipatikanayo kwa imani katika Kristo, haki ile itokayo kwa Mungu kwa njia ya imani. 103:10 Rum 8:17; 6:3-5Nataka nimjue Kristo na uweza wa kufufuka kwake na ushirika wa mateso yake, ili nifanane naye katika mauti yake, 113:11 Yn 11:24; Rum 6:5; Ufu 20:5, 6ili kwa njia yoyote niweze kufikia ufufuo wa wafu.

Kukaza Mwendo Ili Kufikia Lengo

12Si kwamba nimekwisha kufikia, au kwamba nimekwisha kuwa mkamilifu, la hasha! Bali nakaza mwendo ili nipate kile ambacho kwa ajili yake, nimeshikwa na Kristo Yesu. 133:13 Lk 9:22Ndugu zangu, sijihesabu kuwa nimekwisha kushika. Lakini ninafanya jambo moja: Ninasahau mambo yale yaliyopita, nakaza mwendo kufikia yale yaliyo mbele. 143:14 Ebr 6:1; 1Kor 9:24; Rum 8:28Nakaza mwendo nifikie ile alama ya ushindi iliyowekwa ili nipate tuzo ya mwito mkuu wa Mungu ambao nimeitiwa huko juu mbinguni katika Kristo Yesu.

153:15 1Kor 2:6; Gal 5:10; Efe 1:17; 1The 4:9Hivyo sisi sote tuliokuwa kiroho tuwaze jambo hili, hata mkiwaza mengine katika jambo lolote, Mungu ataliweka wazi hilo nalo. 163:16 Gal 6:16; Rum 12:16; 15:15; Flp 2:2Lakini na tushike sana lile ambalo tumekwisha kulifikia.

173:17 1Kor 4:16; Tit 3:12Ndugu zangu, kwa pamoja fuateni mfano wangu na kuwatazama wale wanaofuata kielelezo tulichowawekea. 183:18 Mdo 20:31; Gal 6:12Kwa maana, kama nilivyokwisha kuwaambia mara nyingi kabla, nami sasa nasema tena hata kwa machozi, watu wengi wanaishi kama adui wa msalaba wa Kristo. 193:19 Za 73:17; Rum 16:18; 5:21; Yud 13; Rum 8:5, 6; Kol 3:2Mwisho wa watu hao ni maangamizi, Mungu wao ni tumbo, na utukufu wao ni aibu, na mawazo yao yamo katika mambo ya dunia. 203:20 Efe 2:19; Kol 3:1; Ebr 12:22; 1Kor 1:7Lakini uenyeji wetu uko mbinguni. Nasi tunamngoja kwa shauku Mwokozi kutoka huko, yaani, Bwana Yesu Kristo, 213:21 Efe 1:19; 1Kor 15:43-53; Rum 8:29; Kol 3:4atakayeubadili mwili wetu wa unyonge, ili upate kufanana na mwili wake wa utukufu, kwa uweza ule ambao kwa huo aweza hata kuvitiisha vitu vyote chini yake.

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Wafilipi 3:1-21

Hakuna Tumaini Katika Mwili

13:1 Flp 2:18; 4:4Hatimaye, ndugu zangu, furahini katika Bwana! Mimi kuwaandikia mambo yale yale hakuniudhi, kwa maana ni kinga kwa ajili yenu.

23:2 Za 22:16, 20Jihadharini na mbwa, wale watenda maovu, jihadharini na wale wajikatao miili yao, wasemao ili kuokoka ni lazima kutahiriwa. 33:3 Gal 3:15; Kol 2:11Kwa maana sisi ndio tulio tohara, sisi tumwabuduo Mungu katika Roho, tunaona fahari katika Kristo Yesu, ambao hatuweki tumaini letu katika mwili, 43:4 2Kor 11:21; 11:8, 22ingawa mimi mwenyewe ninazo sababu za kuutumainia mwili.

Kama mtu yeyote akidhani anazo sababu za kuutumainia mwili, mimi zaidi. 53:5 Lk 1:59; 2Kor 11:22; Rum 11:1; Mdo 23:6Nilitahiriwa siku ya nane, mimi ni Mwisraeli wa kabila la Benyamini, Mwebrania wa Waebrania. Kwa habari ya sheria, ni Farisayo, 63:6 Mdo 8:3; Rum 10:5kwa habari ya juhudi, nilikuwa nalitesa kanisa, kuhusu haki ipatikanayo kwa sheria, mimi nilikuwa sina hatia.

73:7 Mt 13:44; Lk 14:33Lakini mambo yale yaliyokuwa faida kwangu, sasa nayahesabu kuwa hasara kwa ajili ya Kristo. 83:8 Yer 9:23, 24; Yn 17:3Zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara tupu nikiyalinganisha na faida kubwa ipitayo kiasi cha kumjua Kristo Yesu Bwana wangu, ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote, nikiyahesabu kuwa kama mavi ili nimpate Kristo. 93:9 Rum 10:5; 9:30Nami nionekane mbele zake bila kuwa na haki yangu mwenyewe ipatikanayo kwa sheria, bali ile ipatikanayo kwa imani katika Kristo, haki ile itokayo kwa Mungu kwa njia ya imani. 103:10 Rum 8:17; 6:3-5Nataka nimjue Kristo na uweza wa kufufuka kwake na ushirika wa mateso yake, ili nifanane naye katika mauti yake, 113:11 Yn 11:24; Rum 6:5; Ufu 20:5, 6ili kwa njia yoyote niweze kufikia ufufuo wa wafu.

Kukaza Mwendo Ili Kufikia Lengo

12Si kwamba nimekwisha kufikia, au kwamba nimekwisha kuwa mkamilifu, la hasha! Bali nakaza mwendo ili nipate kile ambacho kwa ajili yake, nimeshikwa na Kristo Yesu. 133:13 Lk 9:22Ndugu zangu, sijihesabu kuwa nimekwisha kushika. Lakini ninafanya jambo moja: Ninasahau mambo yale yaliyopita, nakaza mwendo kufikia yale yaliyo mbele. 143:14 Ebr 6:1; 1Kor 9:24; Rum 8:28Nakaza mwendo nifikie ile alama ya ushindi iliyowekwa ili nipate tuzo ya mwito mkuu wa Mungu ambao nimeitiwa huko juu mbinguni katika Kristo Yesu.

153:15 1Kor 2:6; Gal 5:10; Efe 1:17; 1The 4:9Hivyo sisi sote tuliokuwa kiroho tuwaze jambo hili, hata mkiwaza mengine katika jambo lolote, Mungu ataliweka wazi hilo nalo. 163:16 Gal 6:16; Rum 12:16; 15:15; Flp 2:2Lakini na tushike sana lile ambalo tumekwisha kulifikia.

173:17 1Kor 4:16; Tit 3:12Ndugu zangu, kwa pamoja fuateni mfano wangu na kuwatazama wale wanaofuata kielelezo tulichowawekea. 183:18 Mdo 20:31; Gal 6:12Kwa maana, kama nilivyokwisha kuwaambia mara nyingi kabla, nami sasa nasema tena hata kwa machozi, watu wengi wanaishi kama adui wa msalaba wa Kristo. 193:19 Za 73:17; Rum 16:18; 5:21; Yud 13; Rum 8:5, 6; Kol 3:2Mwisho wa watu hao ni maangamizi, Mungu wao ni tumbo, na utukufu wao ni aibu, na mawazo yao yamo katika mambo ya dunia. 203:20 Efe 2:19; Kol 3:1; Ebr 12:22; 1Kor 1:7Lakini uenyeji wetu uko mbinguni. Nasi tunamngoja kwa shauku Mwokozi kutoka huko, yaani, Bwana Yesu Kristo, 213:21 Efe 1:19; 1Kor 15:43-53; Rum 8:29; Kol 3:4atakayeubadili mwili wetu wa unyonge, ili upate kufanana na mwili wake wa utukufu, kwa uweza ule ambao kwa huo aweza hata kuvitiisha vitu vyote chini yake.