Waefeso 4 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Waefeso 4:1-32

Umoja Katika Mwili Wa Kristo

14:1 Efe 3:1; Kol 1:10; 1The 2:12Basi, mimi niliye mfungwa wa Bwana, nawasihi mwenende kama inavyostahili wito wenu mlioitiwa. 24:2 Kol 3:12, 13; Efe 1:4Kwa unyenyekevu wote na upole, mkiwa wavumilivu, mkichukuliana kwa upendo. 34:3 Kol 3:14; Rum 15:5Jitahidini kudumisha umoja wa Roho katika kifungo cha amani. 44:4 1Kor 12:13Kuna mwili mmoja na Roho mmoja, kama vile mlivyoitwa katika tumaini moja. 54:5 1Kor 8:6; 2Kor 11:4; Yud 3; Gal 3:27, 28; Ebr 6:6Tena kuna Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja, 64:6 Rum 11:36; 1Kor 12:6; Mal 2:10; 1Kor 8:6; 12:6; Rum 11:36Mungu mmoja ambaye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote, katika yote na ndani ya yote.

74:7 1Kor 12:7, 11; Rum 12:3Lakini kila mmoja wetu amepewa neema kwa kadiri ya kipimo cha kipawa cha Kristo. 84:8 Kol 2:15; Za 68:18Kwa hiyo husema:

“Alipopaa juu zaidi, 4:8 Juu zaidi hapa ina maana mbingu za mbingu.

aliteka mateka,

akawapa wanadamu vipawa.”

94:9 Yn 3:13; 6:33, 62(Asemapo “alipaa juu,” maana yake nini isipokuwa ni kusema pia kwamba Kristo alishuka pande za chini sana za dunia?4:9 Pande za chini sana za dunia hapa maana yake Sheol kwa Kiebrania, yaani Kuzimu. 104:10 Mdo 1:9, 11; 1Tim 3:16; Ebr 4:14; 7:26; 9:24; Mdo 2:13; Mit 30:1-4; Efe 1:23Yeye aliyeshuka ndiye alipaa juu zaidi kupita mbingu zote, ili apate kuujaza ulimwengu wote.) 114:11 2Pet 3:2; Mdo 21:8Ndiye aliweka wengine kuwa mitume, wengine kuwa manabii, wengine kuwa wainjilisti, wengine kuwa wachungaji na walimu, 124:12 1Kor 12:27; 1Pet 2:5; 2Tim 3:17kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu kwa ajili ya kazi za huduma, ili kwamba mwili wa Kristo upate kujengwa 134:13 Kol 1:28mpaka sote tutakapoufikia umoja katika imani na katika kumjua sana Mwana wa Mungu na kuwa watu wazima kwa kufikia kimo cha ukamilifu wa Kristo.

144:14 1Kor 14:20; Yn 1:6; Efe 6:11Ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwatupwa huku na huku na kuchukuliwa na kila upepo wa mafundisho kwa hila za watu, kwa ujanja, kwa kufuata njia zao za udanganyifu. 154:15 Efe 1:22Badala yake, tukiambiana kweli kwa upendo, katika mambo yote tukue, hata tumfikie yeye aliye kichwa, yaani, Kristo. 164:16 Kol 2:19Kutoka kwake, mwili wote ukiwa umeungamanishwa na kushikamanishwa pamoja kwa msaada wa kila kiungo, hukua na kujijenga wenyewe katika upendo, wakati kila kiungo kinafanya kazi yake.

Maisha Ya Zamani Na Maisha Mapya

174:17 Rum 1:21Hivyo nawaambia hivi, nami nasisitiza katika Bwana kwamba, msiishi tena kama watu wa Mataifa waishivyo, katika ubatili wa mawazo yao. 184:18 Rum 1:21; Efe 2:12; 2Kor 3:14Watu hao akili zao zimetiwa giza na wametengwa mbali na uzima wa Mungu kwa sababu ya ujinga wao kutokana na ugumu wa mioyo yao. 194:19 1Tim 4:2; Rum 1:24; Kol 3:5Wakiisha kufa ganzi, wamejitia katika mambo ya ufisadi na kupendelea kila aina ya uchafu, wakiendelea kutamani zaidi.

20Lakini ninyi, hivyo sivyo mlivyojifunza Kristo. 214:21 Efe 1:13Kama hivyo ndivyo ilivyo, ninyi mmemsikia, tena mmefundishwa naye, vile kweli ilivyo katika Yesu. 224:22 1Pet 2:1; Rum 6:6Mlifundishwa kuuvua mwenendo wenu wa zamani, utu wenu wa kale, ulioharibiwa na tamaa zake za udanganyifu, 234:23 Kol 3:10ili mfanywe upya roho na nia zenu, 244:24 Rum 6:4; Efe 2:10mkajivike utu mpya, ulioumbwa sawasawa na mfano wa Mungu katika haki yote na utakatifu.

Kanuni Za Maisha Mapya

254:25 Law 19:11; Rum 12:15Kwa hiyo kila mmoja wenu avue uongo na kuambiana kweli mtu na jirani yake, kwa maana sisi sote tu viungo vya mwili mmoja. 264:26 Za 4:4; Yak 1:19, 20; Mt 5:22Mkikasirika, msitende dhambi, wala jua lisichwe mkiwa bado mmekasirika, 274:27 Yak 4:7; 1Pet 5:9wala msimpe ibilisi nafasi. 284:28 Mdo 20:35; 1The 4:11; Lk 3:11Yeye ambaye amekuwa akiiba, asiibe tena, lakini lazima ajishughulishe, afanye kitu kifaacho kwa mikono yake mwenyewe, ili awe na kitu cha kuwagawia wahitaji.

294:29 Kol 3:8; Mt 12:36; Efe 5:4; Kol 3:8; 4:6; 1The 5:11Maneno mabaya yasitoke vinywani mwenu, bali yale yafaayo kwa ajili ya kuwajenga wengine kulingana na mahitaji yao, ili yawafae wale wasikiao. 304:30 1The 5:19; Rum 8:23Wala msimhuzunishe Roho Mtakatifu wa Mungu, ambaye kwake mlitiwa muhuri kwa ajili ya siku ya ukombozi. 314:31 Kol 3:8; Tit 3:2; Yak 4:11; 1Pet 2:1; Tit 3:3Ondoeni kabisa uchungu, ghadhabu, hasira, makelele na masingizio pamoja na kila aina ya uovu. 324:32 Mt 6:14, 15Kuweni wafadhili na wenye kuhurumiana ninyi kwa ninyi, mkisameheana, kama vile naye Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.

King James Version

Ephesians 4:1-32

1I therefore, the prisoner of the Lord, beseech you that ye walk worthy of the vocation wherewith ye are called, 2With all lowliness and meekness, with longsuffering, forbearing one another in love; 3Endeavouring to keep the unity of the Spirit in the bond of peace. 4There is one body, and one Spirit, even as ye are called in one hope of your calling; 5One Lord, one faith, one baptism, 6One God and Father of all, who is above all, and through all, and in you all. 7But unto every one of us is given grace according to the measure of the gift of Christ. 8Wherefore he saith, When he ascended up on high, he led captivity captive, and gave gifts unto men. 9(Now that he ascended, what is it but that he also descended first into the lower parts of the earth? 10He that descended is the same also that ascended up far above all heavens, that he might fill all things.) 11And he gave some, apostles; and some, prophets; and some, evangelists; and some, pastors and teachers; 12For the perfecting of the saints, for the work of the ministry, for the edifying of the body of Christ: 13Till we all come in the unity of the faith, and of the knowledge of the Son of God, unto a perfect man, unto the measure of the stature of the fulness of Christ: 14That we henceforth be no more children, tossed to and fro, and carried about with every wind of doctrine, by the sleight of men, and cunning craftiness, whereby they lie in wait to deceive; 15But speaking the truth in love, may grow up into him in all things, which is the head, even Christ: 16From whom the whole body fitly joined together and compacted by that which every joint supplieth, according to the effectual working in the measure of every part, maketh increase of the body unto the edifying of itself in love.

17This I say therefore, and testify in the Lord, that ye henceforth walk not as other Gentiles walk, in the vanity of their mind, 18Having the understanding darkened, being alienated from the life of God through the ignorance that is in them, because of the blindness of their heart: 19Who being past feeling have given themselves over unto lasciviousness, to work all uncleanness with greediness. 20But ye have not so learned Christ; 21If so be that ye have heard him, and have been taught by him, as the truth is in Jesus: 22That ye put off concerning the former conversation the old man, which is corrupt according to the deceitful lusts; 23And be renewed in the spirit of your mind; 24And that ye put on the new man, which after God is created in righteousness and true holiness.

25Wherefore putting away lying, speak every man truth with his neighbour: for we are members one of another. 26Be ye angry, and sin not: let not the sun go down upon your wrath: 27Neither give place to the devil. 28Let him that stole steal no more: but rather let him labour, working with his hands the thing which is good, that he may have to give to him that needeth. 29Let no corrupt communication proceed out of your mouth, but that which is good to the use of edifying, that it may minister grace unto the hearers. 30And grieve not the holy Spirit of God, whereby ye are sealed unto the day of redemption. 31Let all bitterness, and wrath, and anger, and clamour, and evil speaking, be put away from you, with all malice: 32And be ye kind one to another, tenderhearted, forgiving one another, even as God for Christ’s sake hath forgiven you.