Waebrania 2 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Waebrania 2:1-18

Wokovu Mkuu

12:1 Rum 11:22Kwa hiyo, imetupasa kuwa waangalifu sana kuhusu kile tulichosikia, ili tusije tukakiacha. 22:2 Ebr 1:1; Kum 33:2; Mdo 7:53; Gal 3:19; Ebr 10:28Kwa kuwa kama ujumbe ulionenwa na malaika ulikuwa imara, na kila uasi na kutokutii kulipata adhabu ya haki, 32:3 Ebr 10:29; 12:25; 1:2; Lk 1:2je, sisi tutapaje kupona kama tusipojali wokovu mkuu namna hii? Wokovu huu, ambao mwanzo ulitangazwa na Bwana, ulithibitishwa kwetu na wale waliomsikia. 42:4 Mk 16:20; Yn 4:48; 1Kor 12:4; Efe 1:5Pia Mungu aliushuhudia kwa ishara, maajabu na kwa miujiza mbalimbali, na karama za Roho Mtakatifu alizozigawa kulingana na mapenzi yake.

Yesu Alifananishwa Na Ndugu Zake

52:5 Ebr 6:5; 2Pet 3:13Mungu hakuuweka ulimwengu ujao ambao tunanena habari zake chini ya malaika. 62:6 Ebr 4:4; Ay 7:17; Za 144:3; 8:4-6Lakini kuna mahali mtu fulani ameshuhudia akisema:

“Mwanadamu ni kitu gani hata unamfikiria,

binadamu ni nani hata unamjali?

7Umemfanya chini kidogo kuliko malaika;

ukamvika taji ya utukufu na heshima,

82:8 Za 8:4-6; Mt 22:44; 28:18; 1Kor 15:27; Efe 1:22; Ebr 1:13; 1Kor 15:2nawe umeweka vitu vyote chini ya miguu yake.”

Kwa kuweka vitu vyote chini yake, Mungu hakuacha kitu chochote ambacho hakukiweka chini ya mwanadamu. Lakini kwa sasa, hatuoni kwamba kila kitu kiko chini yake. 92:9 Ebr 2:7; Mdo 3:13; Flp 2:7-9; 2Kor 5:15; Mdo 2:33; Yn 3:16; 12:32; Rum 5:18; 8:32; 2Kor 5:15; 1Tim 2:6; 1Yn 2:2; Ufu 5:9Lakini twamwona Yesu, aliyefanywa chini kidogo kuliko malaika, sasa akiwa amevikwa taji ya utukufu na heshima kwa sababu alistahimili mauti, ili kwamba kwa neema ya Mungu apate kuonja mauti kwa ajili ya kila mtu.

102:10 Rum 11:36; Lk 24:26; Ebr 5:8, 9; 7:28; Lk 24:46; Mdo 3:15; 5:31; Ebr 12:2; Lk 13:32; Ebr 5:9Ili kuwaleta wana wengi katika utukufu, ilifaa kwamba Mungu, ambaye ni kwa ajili yake na kupitia kwake kila kitu kimekuwepo, amkamilishe mwanzilishi wa wokovu wao kwa njia ya mateso. 112:11 Ebr 10:10; Mdo 17:26; Mt 28:10; Yn 20:17; Rum 8:29; Efe 5:26; Ebr 13:12Yeye awafanyaye watu kuwa watakatifu, pamoja na hao ambao hufanywa watakatifu, wote hutoka katika jamaa moja. Hivyo Yesu haoni aibu kuwaita ndugu zake. 122:12 Za 22:22, 25; 68:26Yeye husema,

“Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu;

mbele ya kusanyiko nitaimba sifa zako.”

132:13 Isa 8:17, 18; Yn 10:29; Za 18:2; Isa 12:2; Yn 20:17; 17:6, 9, 11, 12Tena,

“Nitaweka tumaini langu kwake.”

Tena anasema,

“Niko hapa, pamoja na watoto ambao Mungu amenipa.”

142:14 Yn 1:14; Rum 8:3Basi kwa kuwa watoto wana nyama na damu, yeye pia alishiriki katika ubinadamu wao, ili kwa kifo chake, apate kumwangamiza huyo mwenye nguvu za mauti, yaani ibilisi, 152:15 2Tim 1:7; Lk 1:74; Rum 8:15na kuwaweka huru wale waliokuwa utumwani maisha yao yote kwa sababu ya kuogopa mauti. 162:16 Isa 41:8, 9; Lk 3:8Kwa kuwa ni dhahiri kwamba hakuja kusaidia malaika, bali uzao wa Abrahamu. 172:17 Ebr 2:14; 5:1; 5:2; 3:1; 4:14, 15; Flp 2:7; Rum 3:25; Za 22:22Kwa sababu hii ilibidi afanane na ndugu zake kwa kila hali, ili apate kuwa Kuhani Mkuu mwenye huruma na mwaminifu katika kumtumikia Mungu, ili pia apate kufanya upatanisho kwa ajili ya dhambi za watu. 182:18 Ebr 4:15, 16; 5:2; 7:2; 4:15Kwa kuwa yeye mwenyewe aliteswa alipojaribiwa, aweza kuwasaidia wale wanaojaribiwa.

New International Reader’s Version

Hebrews 2:1-18

A Warning to Pay Attention

1So we must pay the most careful attention to what we have heard. Then we will not drift away from it. 2Even the message God spoke through angels had to be obeyed. Every time people broke the Law, they were punished. Every time they didn’t obey, they were punished. 3Then how will we escape if we don’t pay attention to God’s great salvation? The Lord first announced this salvation. Those who heard him gave us the message about it. 4God showed that this message is true by signs and wonders. He showed that it’s true by different kinds of miracles. God also showed that this message is true by the gifts of the Holy Spirit. God gave them out as it pleased him.

Jesus Was Made Fully Human

5God has not put angels in charge of the world that is going to come. We are talking about that world. 6There is a place where someone has spoken about this. He said,

“What are human beings that you think about them?

What is a son of man that you take care of him?

7You made them a little lower than the angels.

You placed on them a crown of glory and honor.

8You have put everything under their control.” (Psalm 8:4–6)

So God has put everything under his Son. Everything is under his control. We do not now see everything under his control. 9But we do see Jesus already given a crown of glory and honor. He was made lower than the angels for a little while. He suffered death. By the grace of God, he tasted death for everyone. That is why he was given his crown.

10God has made everything. He is now bringing his many sons and daughters to share in his glory. It is only right that Jesus is the one to lead them into their salvation. That’s because God made him perfect by his sufferings. 11And Jesus, who makes people holy, and the people he makes holy belong to the same family. So Jesus is not ashamed to call them his brothers and sisters. 12He says,

“I will announce your name to my brothers and sisters.

I will sing your praises among those who worship you.” (Psalm 22:22)

13Again he says,

“I will put my trust in him.” (Isaiah 8:17)

And again he says,

“Here I am. Here are the children God has given me.” (Isaiah 8:18)

14Those children have bodies made out of flesh and blood. So Jesus became human like them in order to die for them. By doing this, he could break the power of the devil. The devil is the one who rules over the kingdom of death. 15Jesus could set people free who were afraid of death. All their lives they were held as slaves by that fear. 16It is certainly Abraham’s children that he helps. He doesn’t help angels. 17So he had to be made like people, fully human in every way. Then he could serve God as a kind and faithful high priest. And then he could pay for the sins of the people by dying for them. 18He himself suffered when he was tempted. Now he is able to help others who are being tempted.