Waebrania 1 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Waebrania 1:1-14

Mwana Ni Mkuu Kuliko Malaika

11:1 Efe 3:1; 2Kor 1:1; Hes 12:6, 8; Yn 9:29; Ebr 2:3; 4:8; 12:25; Lk 1:70; Mdo 2:30Zamani Mungu alisema na baba zetu kwa njia ya manabii mara nyingi na kwa njia mbalimbali, 21:2 Kum 4:30; Ebr 9:26; 1Pet 1:20; Ebr 1:5; Mt 3:17; Ebr 3:6; 5:8; 7:28; Za 2:8; Mt 28:18; Yn 1:3; Ebr 11:3lakini katika siku hizi za mwisho anasema nasi kwa njia ya Mwanawe, ambaye amemweka kuwa mrithi wa vitu vyote, na ambaye kupitia kwake aliuumba ulimwengu. 31:3 Yn 1:14; 14:9; Kol 1:17; Tit 2:14; Ebr 7:27; Mk 16:19Mwana ni mngʼao wa utukufu wa Mungu na mfano halisi wa nafsi yake, akivihifadhi vitu vyote kwa neno lake lenye uweza. Akiisha kufanya utakaso kwa ajili ya dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Aliye Mkuu huko mbinguni. 41:4 Efe 1:21; Flp 2:9, 10; Ebr 8:6Kwa hiyo alifanyika bora kuliko malaika, kama jina alilorithi lilivyo bora kuliko lao.

51:5 Za 2:7; Mt 3:17; 2Sam 7:14Kwa maana ni malaika yupi ambaye wakati wowote Mungu alipata kumwambia,

“Wewe ni Mwanangu;

leo mimi nimekuzaa?”

Au tena,

“Mimi nitakuwa Baba yake,

naye atakuwa Mwanangu?”

61:6 Yn 3:16; Kol 1:18; Ebr 10:5; Kum 32:43; Za 97:7Tena, Mungu amletapo mzaliwa wake wa kwanza ulimwenguni, anasema,

“Malaika wote wa Mungu na wamsujudu.”

71:7 Za 104:4Anenapo kuhusu malaika asema,

“Huwafanya malaika wake kuwa pepo,

watumishi wake kuwa miali ya moto.”

81:8 Lk 1:33; Za 45:6, 7Lakini kwa habari za Mwana asema,

“Kiti chako cha enzi, Ee Mungu,

kitadumu milele na milele,

nayo haki itakuwa fimbo ya utawala

ya ufalme wako.

91:9 Flp 2:9; Isa 61:1, 3; Za 45:6, 7; Mdo 4; 27; 10:38Umependa haki na kuchukia uovu;

kwa hiyo Mungu, Mungu wako,

amekuweka juu ya wenzako

kwa kukupaka mafuta ya furaha.”

101:10 Za 8:6; 102:25; Zek 12:1Pia asema,

“Hapo mwanzo, Ee Bwana, uliweka misingi ya dunia,

nazo mbingu ni kazi ya mikono yako.

111:11 Isa 34:4; 51:6; Ebr 12:27; Mt 24:35; 2Pet 3:7; 3:10; Ufu 21:1Hizo zitatoweka, lakini wewe utadumu;

zote zitachakaa kama vazi.

121:12 Ebr 13:8; Za 102:25, 27Utazikungʼutakungʼuta kama joho,

nazo zitachakaa kama vazi.

Lakini wewe hubadiliki,

nayo miaka yako haikomi kamwe.”

131:13 Ebr 1:3; Mk 16:19; Yos 10:24; Ebr 10:13; Za 110:1; Mt 22:44Je, ni kwa malaika yupi ambaye Mungu amepata kumwambia wakati wowote,

“Keti mkono wangu wa kuume,

hadi nitakapowaweka adui zako

chini ya miguu yako”?

141:14 Za 91:11; 103:20; Dan 7:10; Mt 25:34; Mk 10:17; Mdo 20:32; Rum 11:14; Ebr 2:3; 5:9; 9:28Je, malaika wote si roho watumikao, waliotumwa kuwahudumia wale watakaourithi wokovu?

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

希伯來書 1:1-14

劃時代的啟示

1在古代,上帝曾藉著先知以各種方式多次向我們的祖先說話; 2在這世界的末期,祂又藉著自己的兒子親自向我們說話。上帝早已立祂承受萬物,並藉著祂創造了宇宙萬物。 3祂正是上帝榮耀的光輝,是上帝本體的真像。祂用自己充滿能力的話語維繫萬物。祂洗淨了世人的罪之後,便坐在天上至高上帝的右邊。 4祂既承受了比天使更高的名分,就遠超越天使。

5上帝從未對任何一個天使說:

「你是我的兒子,我今日成為你父親。」

或說:

「我要作你的父親,你要作我的兒子。」

6上帝差遣祂的長子到世上來時,說:

「上帝的天使都要敬拜祂。」

7上帝提到天使的時候,也只是說:

「上帝使祂的天使成為風,使祂的僕役成為火焰。」

8但論到祂的兒子,祂卻說:

「上帝啊,你的寶座永遠長存,

你以公義的杖執掌王權。

9你喜愛公義,憎惡邪惡。

所以上帝,你的上帝,

用喜樂之油膏你,使你超過同伴。」

10此外又說:

「主啊,太初你奠立大地的根基,

親手創造諸天。

11天地都要消亡,但你永遠長存。

天地都會像衣服漸漸破舊,

12你要像捲外衣一樣把天地捲起來。

天地將如衣服一樣被更換,

但你永遠不變,

你的年日永無窮盡。」

13上帝從未對任何一個天使說:

「你坐在我的右邊,

等我使你的仇敵成為你的腳凳。」

14天使豈不都是服役的靈嗎?他們奉差遣,豈不是去為那些將要承受救恩的人服務嗎?