Waamuzi 9 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Waamuzi 9:1-57

Abimeleki Ajaribu Kuanzisha Ufalme

19:1 Amu 8:31; 6:32Siku moja Abimeleki mwana wa Yerub-Baali akaenda kwa ndugu ya mama yake huko Shekemu na kuwaambia yeye na ukoo wote wa mama yake, 29:2 Mwa 29:14“Waulizeni watu wote wa Shekemu, ‘Lipi lililo bora kwenu: Kutawaliwa na wana wote sabini wa Yerub-Baali, au mtu mmoja peke yake?’ Kumbukeni kwamba, mimi ni mfupa wenu nyama yenu hasa.”

3Ndugu za mama yake walipowaeleza watu wote wa Shekemu, wakaelekea kumkubali Abimeleki, kwa kuwa walisema, “Yeye ni ndugu yetu.” 49:4 Amu 8:33; 11:3; 1Sam 25:25; 2Nya 13:7; Ay 30:8Wakampa shekeli sabini9:4 Shekeli 70 za fedha ni sawa na gramu 800. za fedha kutoka hekalu la Baal-Berithi, naye Abimeleki akaitumia kuajiri watu ovyo wasiojali, wakawa ndio wafuasi wake. 59:5 Amu 8:30; 2Fal 11:2; 2Nya 22:9Akaenda nyumbani kwa baba yake huko Ofra, na juu ya jiwe moja wakawaua ndugu zake sabini, ambao ni wana wa Yerub-Baali. Lakini Yothamu, mwana mdogo wa wote wa Yerub-Baali, akaokoka kwa kujificha. 69:6 2Fal 12:20; Mwa 12:6; Amu 4:11Ndipo watu wote wa Shekemu na Beth-Milo wakakusanyika pamoja chini ya mti mkubwa wa mwaloni penye nguzo iliyoko Shekemu wakamvika Abimeleki taji kuwa mfalme.

79:7 Kum 27:12; Yn 4:20Yothamu alipoambiwa hayo, akapanda juu ya kilele cha mlima Gerizimu, akawapazia sauti yake akawaambia, “Nisikilizeni enyi watu wa Shekemu, ili Mungu naye apate kuwasikiliza ninyi. 8Siku moja miti ilitoka ili kwenda kujitawazia mfalme. Ikauambia mzeituni, ‘Wewe uwe mfalme wetu.’

9“Lakini mzeituni ukaijibu, ‘Je, niache kutoa mafuta yangu ambayo kwake miungu na wanadamu huheshimiwa, ili nikawe juu ya miti?’

10“Kisha miti ikauambia mtini, ‘Njoo na uwe mfalme wetu!’

11“Lakini mtini ukaijibu, ‘Je, niache kutoa matunda yangu mazuri na matamu, ili niende nikawe juu ya miti?’

12“Ndipo miti ikauambia mzabibu, ‘Njoo na uwe mfalme wetu.’

139:13 Mwa 14:18; Mhu 2:3; Wim 4:10“Lakini mzabibu ukaijibu, ‘Je, niache kutoa divai yangu inayofurahisha miungu na wanadamu ili nikawe juu ya miti?’

14“Mwishoni miti yote ikauambia mti wa miiba, ‘Njoo na uwe mfalme wetu.’

159:15 Isa 30:2; Kum 3:25; 1Fal 5:6; Za 29:5; 92:12; Isa 2:13“Nao mti wa miiba ukaijibu, ‘Kama kweli mnataka niwe mfalme wenu, basi njooni mpate kupumzika chini ya kivuli changu. Lakini kama sivyo, moto na utoke kwenye mti wa miiba ukateketeze mierezi ya Lebanoni!’

16“Basi ikiwa mmetenda kwa uaminifu na heshima kumfanya Abimeleki kuwa mfalme, na kama mmetendea vyema Yerub-Baali na jamaa yake kama ilivyostahili: 179:17 Amu 12:3; 1Sam 19:5; 28:21; Ay 13:14; Za 119:109kwa kuwa baba yangu aliwapigania ninyi na kuhatarisha nafsi yake na kuwaokoa ninyi kutoka mikononi mwa Wamidiani 189:18 Amu 8:30(lakini leo mmeasi dhidi ya jamaa ya baba yangu, na kuwaua wanawe sabini juu ya jiwe moja, nanyi mkamfanya Abimeleki mwana wa mwanamke mtumwa kuwa mfalme juu ya Shekemu, kwa kuwa yeye ni ndugu yenu), 19nanyi kama basi mmemtendea Yerub-Baali na jamaa yake kwa heshima na uaminifu, basi Abimeleki na awe furaha yenu, nanyi mwe furaha yake pia! 20Lakini kama sivyo, moto na utoke kwa Abimeleki na uwateketeze, ninyi watu wa Shekemu na Beth-Milo, nao moto utoke kwenu, watu wa Shekemu na Beth-Milo umteketeze Abimeleki!”

219:21 Hes 21:16Ndipo Yothamu akakimbia, akatoroka akaenda Beeri, akaishi huko, kwa sababu alimwogopa ndugu yake Abimeleki.

22Baada ya Abimeleki kutawala Israeli kwa muda wa miaka mitatu, 239:23 1Sam 16:14; 18:10; 19:9; 1Fal 22:22Mungu akaruhusu roho mbaya kati ya Abimeleki na watu wa Shekemu, nao watu wa Shekemu wakamtendea Abimeleki kwa hila. 249:24 Amu 8:30; Mwa 9; 6; Hes 35:33; 1Fal 2:32; Kum 27:25Hili lilitokea ili ule ukatili waliotendewa hao wana sabini wa Yerub-Baali upatilizwe, na damu yao iwe juu ya Abimeleki ndugu yao aliyewaua, na pia iwe juu ya watu wa Shekemu, ambao walimsaidia kuua ndugu zake. 25Hivyo, kutokana na uadui juu yake watu wa Shekemu wakaweka watu wa kumvizia katika vilele vya milima. Wakawanyangʼanya watu wote waliopita karibu nao, nayo haya yakaarifiwa kwa Abimeleki.

26Basi Gaali mwana wa Ebedi akaenda pamoja na ndugu zake wakaingia Shekemu, nao watu wa huko wakamtumainia yeye. 279:27 Isa 16:10; Amo 5:11; 9:13; Amu 8:33Wakaenda mashambani mwao kuvuna zabibu na kuzisindika hizo zabibu, wakafanya sikukuu katika hekalu la mungu wao. Wakati wakila na kunywa, wakamlaani Abimeleki. 289:28 1Sam 25:10; 1Fal 12:16; Mwa 33:19; 34:2-6Gaali mwana wa Ebedi akasema, “Abimeleki ni nani, na Shekemu ni nani, hata tumtumikie? Je, yeye si mwana wa Yerub-Baali? Naye Zebuli si ndiye msaidizi wake? Basi watumikieni watu wa Hamori, babaye Shekemu. Kwa nini tumtumikie Abimeleki? 299:29 2Sam 15; 4Laiti watu hawa wangekuwa chini ya amri yangu! Basi mimi ningemwondoa huyo Abimeleki. Ningemwambia Abimeleki, ‘Ondoa jeshi lako lote.’ ”

30Zebuli aliyekuwa mtawala wa mji aliposikia aliyosema Gaali mwana wa Ebedi, akakasirika sana. 31Akatuma ujumbe uende kwa Abimeleki kwa siri na kusema, “Gaali mwana wa Ebedi na ndugu zake wamekuja Shekemu, na wanauchochea mji huu kinyume chako. 329:32 Yos 8:2Sasa, basi, usiku huu wewe uondoke na watu wako ili mje kuwavizia mashambani. 339:33 1Sam 10:7Kisha asubuhi wakati wa kuchomoza jua, amka mapema na ujipange dhidi ya huo mji. Wakati yeye na jeshi lililo pamoja naye watakapotoka kukabiliana nanyi, mwaweza kuwatendea kwa kadiri mnavyoweza.”

34Kwa hiyo Abimeleki pamoja na jeshi lake lote wakaondoka usiku na kujificha karibu na Shekemu wakiwa vikosi vinne. 359:35 Yos 2:5; Za 32:7; Isa 28:15-17; Yer 49:10Basi Gaali mwana wa Ebedi alikuwa ametoka nje akawa amesimama katika ingilio la mji wakati ule ule ambao Abimeleki na watu wake walipokuwa wanatoka sehemu zao za maficho.

36Gaali alipowaona, akamwambia Zebuli, “Tazama, watu wanashuka kutoka kwenye vilele vya milima!”

Zebuli akajibu, “Wewe unaona vivuli vya milima kana kwamba ni watu.”

37Lakini Gaali akasema tena, “Tazama, watu wanashuka kutoka katikati ya nchi na kikosi kimoja kinakuja kutoka Tabur-Ezeri na kikosi kingine kutoka upande wa Elon-Meonenimu.”

38Ndipo Zebuli akamwambia, “Kuko wapi kujivuna kwako sasa, wewe uliyesema, ‘Huyo Abimeleki ni nani hata tumtumikie?’ Hawa si wale watu uliowadharau? Toka nje sasa ukapigane nao!”

39Basi Gaali akatoka akawaongoza watu wa Shekemu kupigana na Abimeleki. 40Abimeleki akamfukuza, watu wengi wakajeruhiwa katika kukimbia huko, njia nzima hadi kwenye ingilio la lango. 41Abimeleki akakaa Aruma, naye Zebuli akawafukuza Gaali na ndugu zake watoke Shekemu.

42Kesho yake watu wa Shekemu wakatoka wakaenda mashambani, Abimeleki akaambiwa juu ya jambo hili. 439:43 Amu 7:16; Yos 8:2Hivyo akawachukua watu wake, akawagawanya katika vikosi vitatu na kuwaweka waviziao huko mashambani. Alipowaona watu wanatoka kwenda nje ya mji, akainuka dhidi yao na kuwashambulia. 44Abimeleki pamoja na vile vikosi wakaharakisha kwenda mbele kwenye nafasi, mahali pa ingilio la lango la mji. Vile vikosi viwili vikawawahi wale waliokuwa mashambani na kuwaua. 459:45 Yer 48:9Siku hiyo nzima Abimeleki akazidisha mashambulizi yake dhidi ya mji hadi akawa ameuteka na kuwaua watu wa huo mji. Kisha akauangamiza mji na kusambaza chumvi juu yake.

469:46 Amu 8:33Kwa kusikia jambo hili watu wote katika mnara wa Shekemu, wakaingia kwenye ngome ya hekalu la El-Berithi. 47Abimeleki aliposikia kuwa wamekusanyika huko, 489:48 Za 68:14yeye na watu wake wote wakakwea kwenye Mlima Salmoni. Abimeleki akachukua shoka, akakata baadhi ya matawi, ambayo aliyachukua mabegani. Akawaagiza wale watu waliokuwa pamoja naye kuwa, “Fanyeni kile mlichoona mimi nikifanya!” 49Basi watu wote wakakata matawi na kumfuata Abimeleki. Wakayakusanya hayo matawi juu ya ngome na kuitia moto ili kuwachoma wale watu wote waliokuwa ndani yake. Hivyo watu wote katika mnara wa Shekemu, karibia watu 1,000 waume kwa wake, pia wakafa.

509:50 2Sam 11:21Baadaye Abimeleki akaenda Thebesi na kuuzingira kwa jeshi na kuuteka. 51Hata hivyo, ndani ya huo mji kulikuwa na mnara imara, ambako watu wote wa mji wanaume na wanawake, watu wote wa mji, walikimbilia ndani yake. Wakajifungia ndani yake na kupanda juu ya paa la mnara. 52Abimeleki akaja kwenye ule mnara na kuushambulia, lakini alipokaribia kwenye ingilio la mnara ili kuuchoma kwa moto, 539:53 2Sam 11:21mwanamke mmoja akaangusha sehemu ya juu ya jiwe la kusagia juu ya kichwa cha Abimeleki, likapasua fuvu la kichwa chake.

549:54 1Sam 31:4; 2Sam 1:9Akamwita kwa haraka kijana yule aliyechukua silaha zake, na kumwambia, “Chukua upanga wako na uniue, watu wasije wakasema kwamba, ‘Mwanamke amemuua.’ ” Basi yule kijana akamchoma upanga, naye akafa. 55Waisraeli walipoona kuwa Abimeleki amekufa, kila mtu akaenda nyumbani kwake.

56Hivyo ndivyo Mungu alivyolipiza uovu ule ambao Abimeleki alikuwa ameutenda kwa baba yake kwa kuwaua ndugu zake sabini. 579:57 Za 94:23Mungu akawapatiliza watu wa Shekemu uovu wao juu ya vichwa vyao, na juu yao ikaja laana ya Yothamu mwana wa Yerub-Baali.

New International Reader’s Version

Judges 9:1-57

Abimelek

1Abimelek was the son of Jerub-Baal. He went to his mother’s brothers in Shechem. He spoke to them and to all the members of his mother’s family group. He said, 2“Speak to all the citizens of Shechem. Tell them, ‘You can have all 70 of Jerub-Baal’s sons rule over you. Or you can have just one man rule over you. Which would you rather have?’ Remember, I’m your own flesh and blood.”

3The brothers told all of that to the citizens of Shechem. Then the people decided to follow Abimelek. They said, “He’s related to us.” 4They gave him 28 ounces of silver. They had taken it from the temple of the god named Baal-Berith. Abimelek used it to hire some men. They were wild and weren’t good for anything. They became his followers. 5Abimelek went to his father’s home in Ophrah. There on a big rock he murdered his 70 brothers. All of them were the sons of Jerub-Baal. But Jotham escaped by hiding. He was Jerub-Baal’s youngest son. 6All the citizens of Shechem and Beth Millo came together. They gathered at the stone pillar that was beside the large tree in Shechem. They wanted to crown Abimelek as their king.

7Jotham was told about it. So he climbed up on top of Mount Gerizim. He shouted down to them, “Citizens of Shechem! Listen to me! Then God will listen to you. 8One day the trees went out to anoint a king for themselves. They said to an olive tree, ‘Be our king.’

9“But the olive tree answered, ‘Should I give up my olive oil? It’s used to honor gods and people alike. Should I give that up just to rule over the trees?’

10“Next, the trees said to a fig tree, ‘Come and be our king.’

11“But the fig tree replied, ‘Should I give up my fruit? It’s so good and sweet. Should I give that up just to rule over the trees?’

12“Then the trees said to a vine, ‘Come and be our king.’

13“But the vine answered, ‘Should I give up my wine? It cheers up gods and people alike. Should I give that up just to rule over the trees?’

14“Finally, all the trees spoke to a bush that had thorns. They said, ‘Come and be our king.’

15“The bush asked the trees, ‘Do you really want to anoint me as king over you? If you do, come and rest in my shade. But if you don’t, I will destroy you! Fire will come out of me and burn up the cedar trees of Lebanon!’

16“Did you act in an honest way when you made Abimelek your king? Did you really do the right thing? Have you been fair to Jerub-Baal and his family? Have you given him the honor he’s worthy of? 17Remember that my father fought for you. He put his life in danger for you. He saved you from the power of Midian. 18But today you have turned against my father’s family. You have murdered his 70 sons on a big rock. Abimelek is only the son of my father’s female slave. But you have made him king over the citizens of Shechem. You have done that because he’s related to you. 19Have you citizens of Shechem and Beth Millo acted in an honest way toward Jerub-Baal? Have you done the right thing to his family today? If you have, may you be happy with Abimelek! And may he be happy with you! 20But if you haven’t, let fire come out from Abimelek and burn you up! And let fire come out from you and burn Abimelek up!”

21Then Jotham ran away. He escaped to a town named Beer. He lived there because he was afraid of his brother Abimelek.

22Abimelek ruled over Israel for three years. 23Then God stirred up trouble between Abimelek and the citizens of Shechem. So they turned against Abimelek. They decided not to follow him anymore. 24God made that happen because of what Abimelek had done to Jerub-Baal’s 70 sons. He had spilled their blood. God wanted to punish their brother Abimelek for doing that. He also wanted to punish the citizens of Shechem. They had helped Abimelek murder his brothers. 25The citizens of Shechem didn’t want Abimelek to be their ruler anymore. So they hid some men on top of the hills. They wanted them to attack and rob everyone who passed by. Abimelek was told about it.

26Gaal and his relatives moved into Shechem. Gaal was the son of Ebed. The citizens of Shechem put their trust in Gaal. 27The people of Shechem went out into the fields. They gathered the grapes. They pressed the juice out of them by stomping on them. Then they held a feast in the temple of their god. While they were eating and drinking, they cursed Abimelek. 28Then Gaal, the son of Ebed, said, “Who is Abimelek? And who is Shechem? Why should we citizens of Shechem be under Abimelek’s rule? Isn’t he Jerub-Baal’s son? Isn’t Zebul his helper? It would be better to serve the family of Hamor. He was the father of Shechem. So why should we serve Abimelek? 29I wish these people were under my command. Then I would get rid of Abimelek. I would say to him, ‘Call out your whole army!’ ”

30Zebul was the governor of Shechem. He heard about what Gaal, the son of Ebed, had said. So he was very angry. 31Zebul secretly sent messengers to Abimelek. They said, “Gaal, the son of Ebed, has come to Shechem. His relatives have come with him. They are stirring up the city against you. 32So come with your men during the night. Hide in the fields and wait. 33In the morning at sunrise, attack the city. Gaal and his men will come out against you. Then take that opportunity to attack them.”

34So Abimelek and all his troops started out at night. They went into their hiding places near Shechem. Abimelek had separated them into four fighting groups. 35Gaal, the son of Ebed, had already gone out. He was standing at the entrance of the city gate. He had arrived there just as Abimelek and his troops came out of their hiding places.

36Gaal saw them. He said to Zebul, “Look! People are coming down from the tops of the mountains!”

Zebul replied, “You are wrong. Those aren’t people. They are just the shadows of the mountains.”

37But Gaal spoke up again. He said, “Look! People are coming down from the central hill. Another group is coming from the direction of the fortune tellers’ tree.”

38Then Zebul said to Gaal, “Where is your big talk now? You said, ‘Who is Abimelek? Why should we be under his rule?’ Aren’t these the people you made fun of? Go out and fight against them!”

39So Gaal led the citizens out of Shechem. They fought against Abimelek. 40He chased Gaal from the field of battle. Abimelek chased them all the way to the entrance of the city gate. Many men were killed as they ran away. 41Abimelek stayed in Arumah. And Zebul drove Gaal and his relatives out of Shechem.

42The next day the people of Shechem went out to work in the fields. Abimelek was told about it. 43So he gathered his men together. He separated them into three fighting groups. Then he hid them in the fields and told them to wait. When he saw the people coming out of the city, he got up to attack them. 44Abimelek and the men with him ran forward. They placed themselves at the entrance of the city gate. Then the other two groups attacked the people in the fields. There they struck them down. 45Abimelek kept up his attack against the city all day long. He didn’t stop until he had captured it. Then he killed its people. He destroyed the city. He scattered salt on it to make sure that nothing would be able to grow there.

46The citizens in the tower of Shechem heard about what was happening. So they went to the safest place in the temple of the god named El-Berith. 47Abimelek heard that they had gathered together there. 48He and all his men went up Mount Zalmon. He got an ax and cut off some branches. He carried them on his shoulders. He ordered the men with him to do the same thing. “Quick!” he said. “Do what you have seen me do!” 49So all the men cut branches and followed Abimelek. They piled them against the place where the people had gone for safety. Then they set the place on fire with the people still inside. There were about 1,000 men and women in the tower of Shechem. All of them died.

50Next, Abimelek went to Thebez. He surrounded it. Then he attacked it and captured it. 51But inside the city there was a strong tower. All the people in the city had run to it for safety. All the men and women had gone into it. They had locked themselves in. They had climbed up on the roof of the tower. 52Abimelek went to the tower and attacked it. He approached the entrance to the tower to set it on fire. 53But a woman dropped a large millstone on him. It broke his head open.

54He quickly called out to the man carrying his armor. He said, “Pull out your sword and kill me. Then people can’t say, ‘A woman killed him.’ ” So his servant stuck his sword through him. And Abimelek died. 55When the Israelites saw he was dead, they went home.

56That’s how God punished Abimelek for the evil thing he had done to his father. He had murdered his 70 brothers. 57God also made the people of Shechem pay for all the evil things they had done. The curse of Jotham came down on them. He was the son of Jerub-Baal.