Waamuzi 3 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Waamuzi 3:1-31

Mataifa Yaliyobaki Katika Ile Nchi

13:1 Kut 15:25Haya ndiyo mataifa Bwana aliyoyaacha ili kuwajaribu Waisraeli wote ambao hawakujua vita vyovyote vya Kanaani 2(alifanya hivi ili tu kuwafundisha wazao wa Waisraeli ambao hawakuwa wamejua vita hapo awali): 33:3 Yos 13:2; Mwa 10:14; 10:17; Kut 3:8; Kum 3:8; Hes 13:21wafalme watano wa Wafilisti, Wakanaani wote, Wasidoni, Wahivi waishio katika milima ya Lebanoni kuanzia Mlima wa Baal-Hermoni hadi Lebo-Hamathi. 43:4 Kut 12:25Waliachwa ili kuwajaribu Waisraeli kuona kama wangetii amri za Bwana, alizokuwa amewapa baba zao kwa mkono wa Mose.

53:5 Za 106:36; Yos 3:10; 11:3; Ezr 9:1Waisraeli wakaishi miongoni mwa Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi. 63:6 Ezr 10:18; Neh 13:23; Mal 2:11; Kut 34:16; Kum 7:3-4, 16Wakawaoa binti zao, nao wakawatoa binti zao waolewe na wana wa hayo mataifa, na kuitumikia miungu yao.

Othnieli

73:7 Kum 4:9; 32:18; Amu 8:34; Za 78:11; 106:7; Yer 23:27; Amu 2:11-13; 1Fal 16:33; 2Nya 34:7; Isa 17:8Waisraeli wakafanya maovu machoni pa Bwana, wakamsahau Bwana Mungu wao na kutumikia Mabaali na Maashera. 83:8 Amu 2:14; Za 44:12; Isa 50:1; 52:3; Mwa 24:10Hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Israeli, hivyo akawauza na kuwatia mikononi mwa Kushan-Rishathaimu mfalme wa Aramu-Naharaimu3:8 Yaani Mesopotamia ya Kaskazini-Magharibi. ambaye Israeli walikuwa chini yake wakimtumikia kwa muda wa miaka minane. 93:9 Amu 6:6-7; 10:10; 1Sam 12:10; Za 106:44; 107:13; Kum 28:29; Neh 9:27Waisraeli walipomlilia Bwana, yeye akawainulia mwokozi, Othnieli mwana wa Kenazi, ndugu mdogo wa Kalebu, ambaye aliwaokoa. 103:10 Hes 11:25; Amu 6:34; 11:29; 13:25; 14:6; 15:14; 1Sam 11:6; 16:13; 1Fal 18:46; 1Nya 12:18; 2Nya 24:20; Isa 11:2; Mwa 10:22Roho wa Bwana akaja juu yake, hivyo akawa mwamuzi wa Israeli, akaenda vitani. Bwana akamtia Kushan-Rishathaimu mfalme wa Aramu mikononi mwa Othnieli, naye akamshinda. 113:11 Yos 14:15; Amu 5:31; 8:28; Kut 16:35; 15:17Hivyo nchi ikawa na amani kwa muda wa miaka arobaini, mpaka Othnieli mwana wa Kenazi alipofariki.

Ehudi

123:12 Amu 2:11; 1Sam 12:9Waisraeli wakafanya maovu mbele za Bwana tena, kwa kuwa walifanya maovu hayo Bwana akamtia nguvu Egloni mfalme wa Moabu dhidi ya Israeli. 133:13 Mwa 19:38; Amu 10:11; Mwa 14:7; Amu 1:16Egloni akawataka Waamoni na Waamaleki waungane naye, akaja kuishambulia Israeli, nao wakatwaa Mji wa Mitende3:13 Yaani Yeriko. 143:14 Yer 48:1Waisraeli wakawa chini ya Egloni mfalme wa Moabu kwa muda wa miaka kumi na minane.

153:15 Amu 1:4; 20:16; 1Nya 12:2; 2Sam 8:2-6; 1Fal 4:21; 2Fal 17:3; Es 10:1; Za 68:29; 72:10; 89:22; Mhu 2:8; Isa 60:5; Hos 10:6; Za 107:13Waisraeli wakamlilia tena Bwana, naye akawapa mwokozi: Ehudi, mtu wa shoto, mwana wa Gera, Mbenyamini. Waisraeli wakatuma kwa Egloni mfalme wa Moabu ushuru kwa mkono wa Ehudi. 16Basi Ehudi alikuwa ametengeneza upanga wenye ukatao kuwili, urefu wake ni kama dhiraa moja,3:16 Dhiraa moja ni sawa na sentimita 45. akaufunga upanga huo ndani ya nguo yake kwenye paja lake la mkono wa kuume. 173:17 Ay 15:27; Za 73:4Akamkabidhi ushuru Egloni mfalme wa Moabu, ambaye alikuwa mtu mnene sana. 18Baada ya Ehudi kumkabidhi ule ushuru, wale watu waliokuwa wameubeba huo ushuru aliwaruhusu waende zao. 19Yeye mwenyewe akafuatana nao hadi kwenye sanamu ya kuchora kwenye mawe karibu na Gilgali, ndipo yeye akarudi, akafika kwa Egloni na kusema, “Ee Mfalme, ninao ujumbe wa siri kwa ajili yako.”

Mfalme akasema, “Nyamazeni kimya!” Nao wale waliomhudumia wote wakamwacha, wakatoka nje.

203:20 Amo 3:15; Neh 8:5Ndipo Ehudi akamsogelea alipokuwa ameketi peke yake kwenye chumba cha juu cha jumba lake la kifalme la majira ya kiangazi, na kusema, “Ninao ujumbe kutoka kwa Mungu kwa ajili yako.” Mfalme alipokuwa anainuka kutoka kwenye kiti chake, 213:21 2Sam 2:16; 3:27; 20:10Ehudi akaunyoosha mkono wake wa kushoto na kuufuta ule upanga aliokuwa ameufunga kwenye paja lake la kulia, akamdunga Mfalme Egloni tumboni mwake. 22Hata mpini nao ukazama tumboni pamoja na upanga wenyewe, nao upanga ukatokea mgongoni mwake. Ehudi hakuuchomoa huo upanga, nayo mafuta yakashikamana juu ya upanga. 23Ehudi akatoka nje barazani; akamfungia milango ya chumba cha juu na kuifunga kwa funguo.

243:24 1Sam 24:3Baada ya kuondoka, watumishi wakaja na kukuta milango ya chumba cha juu imefungwa kwa funguo. Wakasema, “Bila shaka amejipumzisha kwenye chumba cha ndani cha nyumba yake ya majira ya kiangazi.” 253:25 2Fal 2:17; 8:11Wakangoja hata wakawa na fadhaa, basi wakati hakufungua milango ya chumba, wakachukua funguo na kuifungua. Tazama wakaona bwana wao amelala sakafuni, amekufa.

26Walipokuwa wangali wanangoja, Ehudi akatoroka, akapita hapo kwenye sanamu ya kuchora kwenye mawe na kukimbilia Seira. 273:27 Law 25:9; Amu 6:34; 7:18; 2Sam 2:28; Isa 18:3; Yer 42:14Alipofika huko, akapiga tarumbeta katika nchi ya vilima ya Efraimu, nao Waisraeli wakateremka pamoja naye kutoka vilimani, yeye akiwa anawaongoza.

283:28 Mwa 19:37; Yos 2:24; Amu 1:2; Hes 13:29; Yos 2:9Akawaagiza, “Nifuateni, kwa kuwa Bwana amewatia Moabu, adui zenu, mikononi mwenu.” Kwa hiyo wakateremka wakamfuata, wakavishika vivuko vya Yordani kuelekea Moabu, wala hawakuacha mtu yeyote kuvuka. 29Wakati huo wakawaua Wamoabu watu waume wapatao 10,000 ambao wote walikuwa wenye nguvu na mashujaa; hakuna mtu yeyote aliyetoroka. 303:30 Mwa 36:35Siku ile Moabu wakashindwa na Israeli, nayo nchi ikawa na amani kwa miaka themanini.

Shamgari

313:31 Amu 5:6; Yos 23:10; 13:2; Amu 10:11; 13:1; 1Sam 5:1; 31:1; 2Sam 8:1; Yer 25:30; 47:1Baada ya Ehudi akaja Shamgari mwana wa Anathi, aliyewapiga Wafilisti 600 kwa fimbo iliyochongoka ya kuongozea ngʼombe. Naye pia akawaokoa Waisraeli.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

士师记 3:1-31

迦南余族

1-2耶和华为了考验那些没有经历过迦南战事的以色列人,让他们学习作战,就留下了以下各族: 3五个非利士王、所有的迦南人、西顿人和住在巴力·黑门山到哈马口一带的黎巴嫩山区的希未人。 4耶和华留下这几个外族是要考验以色列人,看他们是否愿意遵从祂借摩西向他们祖先颁布的诫命。 5以色列人住在这些迦南人、人、亚摩利人、比利洗人、希未人和耶布斯人当中, 6跟他们通婚,祭拜他们的神明。

士师俄陀聂

7以色列人做耶和华视为恶的事,忘记他们的上帝耶和华,祭拜假神巴力亚舍拉8耶和华向他们发怒,把他们交在美索不达米亚古珊·利萨田的手中,受古珊·利萨田统治八年。 9他们向耶和华呼求,耶和华就使一位名叫俄陀聂的拯救者兴起,他是迦勒弟弟基纳斯的儿子。 10耶和华的灵降在俄陀聂身上,他就做了以色列的士师,领兵出战。耶和华将美索不达米亚古珊·利萨田交在他手中,他便战胜了古珊·利萨田11此后,国内安享太平四十年,直到俄陀聂去世。

士师以笏

12之后,以色列人又做耶和华视为恶的事,耶和华就使摩押伊矶伦强盛起来,攻打以色列人。 13伊矶伦联合亚扪人和亚玛力人进攻以色列人,占据了棕树城, 14以色列人受摩押伊矶伦统治十八年。 15他们呼求耶和华,耶和华就使一位名叫以笏的拯救者兴起。他是便雅悯基拉的儿子,善用左手。以色列人派他去向摩押伊矶伦进贡。 16他造了一把约半米长的两刃利剑,绑在右腿的衣服里。 17他带着贡物去见肥胖的摩押伊矶伦18以笏献上了贡物之后,便和抬贡物的人一起离去。 19到了吉甲附近雕石神像的地方,他让抬贡物的人先回去,自己则折回王宫,对王说:“王啊,我有机密禀告。”王就命左右的人回避,众人便都退去了。 20当时王独自坐在楼上的房间乘凉,以笏近前说:“我有从上帝而来的讯息要禀告。”王站起来的时候, 21以笏左手拔出藏在右腿上的剑刺进王的肚腹, 22连剑柄也刺了进去,深深嵌入肥肉。以笏没有拔剑, 23便走出房间,把门都关上,锁好。

24以笏走后,王的仆人过来,见房门紧锁,以为王在大解。 25等了很久,门还没开,他们很焦急,就拿钥匙开门,发现他们的主人已经倒毙在地上。

26他们等待的时候,以笏已经逃走了。他经过雕石神像的地方,逃往西伊拉27到了那里,他就在以法莲的山区吹响号角,召集以色列人。众人跟随以笏下山, 28以笏对他们说:“跟我来!耶和华已经把仇敌摩押人交在你们手中了。”于是,众人跟着他占领了通往摩押约旦河各渡口,不许任何人渡河。 29当时他们杀了约一万名强悍善战的摩押勇士,没有一人逃脱。 30这样,以色列人征服了摩押人,国中安享太平八十年。

珊迦

31以笏之后,亚拿的儿子珊迦拯救了以色列人。他曾用一根赶牛棍杀了六百名非利士人。