Waamuzi 18 – NEN & BPH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Waamuzi 18:1-31

Wadani Wahamia Laishi

118:1 Amu 17:6; Yos 19:47; Amu 1:34Katika siku hizo Israeli walikuwa hawana mfalme.

Katika siku hizo kabila la Wadani walikuwa wanatafuta mahali pao wenyewe pa kuishi, kwa sababu walikuwa hawajafika kwenye urithi wao miongoni mwa makabila ya Israeli. 218:2 Mwa 30:6; Hes 21:32; Yos 2:1; Amu 17:1Hivyo Wadani wakatuma mashujaa watano kutoka Sora na Eshtaoli ili kupeleleza nchi na kuichunguza. Hawa watu waliwakilisha koo zao zote. Waliwaambia, “Nendeni mkaichunguze hiyo nchi.”

Watu hao wakaingia katika nchi ya vilima ya Efraimu, nao wakafika nyumba ya Mika, ambako walilala usiku huo. 318:3 Amu 17:7Walipofika karibu na nyumba ya Mika, waliitambua sauti ya yule kijana Mlawi; hivyo wakaingia humo na kumuuliza, “Ni nani aliyekuleta hapa? Unafanya nini mahali hapa? Kwa nini uko hapa?”

418:4 Amu 17:12Akawaeleza yale Mika aliyomtendea, naye akasema, “Ameniajiri nami ni kuhani wake.”

518:5 Mwa 25:22; Amu 20:18, 23, 27; 1Sam 14:18; 2Sam 5:19; 2Fal 1:2; 8:8Kisha wakamwambia, “Tafadhali tuulizie kwa Mungu kama safari yetu itafanikiwa.”

618:6 1Fal 22:6Yule kuhani akawajibu, “Enendeni kwa amani. Safari yenu ina kibali cha Bwana.”

718:7 Yos 19:47; Mwa 34:25; Yos 11:8Basi hao watu watano wakaondoka na kufika Laishi, mahali ambapo waliwakuta watu wanaishi salama, kama Wasidoni, kwa utulivu na bila mashaka. Nchi yao haikupungukiwa na kitu chochote, hivyo wakawa tajiri. Pia walikaa mbali sana na Wasidoni, wala hawakushughulika na mtu yeyote.

8Waliporudi kwa ndugu zao huko Sora na Eshtaoli, ndugu zao wakawauliza, “Mlionaje mambo huko?”

918:9 Hes 13:30; 1Fal 22:3Wakajibu, “Twendeni, tukapigane nao! Tumeona kuwa nchi ni nzuri sana. Je, hamtafanya chochote? Msisite kupanda ili kuimiliki. 1018:10 Kum 8:9; 1Nya 4:40Mtakapokwenda huko mtakuta watu waliotulia walio salama, nayo nchi hiyo ni kubwa na Mungu ameitia mikononi mwenu, nayo ni nchi ambayo haikupungukiwa na kitu chochote kilicho duniani.”

1118:11 Amu 13:2Ndipo watu 600 toka ukoo wa Wadani, waliojifunga silaha za vita, wakaondoka Sora na Eshtaoli. 1218:12 Yos 9:17; Amu 13:25Walipokuwa wakisafiri wakapiga kambi huko Kiriath-Yearimu katika Yuda. Hii ndiyo sababu sehemu ya magharibi ya Kiriath-Yearimu inaitwa Mahane-Dani18:12 Mahane-Dani maana yake Kambi ya Dani. mpaka leo. 1318:13 Amu 17:6Kutoka hapo wakaendelea mbele mpaka nchi ya vilima ya Efraimu na kufika katika nyumba ya Mika.

1418:14 Yos 19:47; Amu 8:27; Mwa 31:19; Amu 17:5Ndipo wale watu watano waliopeleleza nchi ya Laishi wakawaambia ndugu zao, “Je, mwajua kuwa mojawapo ya nyumba hizi kuna naivera, sanamu ndogo za nyumbani, sanamu ya kuchonga na sanamu ya kusubu? Sasa basi fikirini mtakalofanya.” 15Basi wakaingia humo na kwenda kwenye nyumba ya yule kijana Mlawi katika nyumba ya Mika na kumsalimu. 16Wale Wadani 600, waliovaa silaha za vita, wakasimama penye ingilio la lango. 1718:17 Mwa 31:19; Mik 5:13Wale watu watano waliokwenda kupeleleza nchi wakaingia ndani na kuchukua ile sanamu ya kuchonga, ile naivera, na zile sanamu nyingine ndogo za nyumbani pamoja na ile sanamu ya kusubu, wakati yule kuhani akiwa amesimama pale penye ingilio la lango pamoja na wale watu 600 waliokuwa wamejifunga silaha za vita.

1818:18 Isa 46:2; Yer 43:11; 48:7; 49:3; Hos 10:5; Mwa 31:19Hao watu walipoingia katika nyumba ya Mika na kuchukua ile sanamu ya kuchonga, ile naivera, na zile sanamu nyingine ndogo za nyumbani, pamoja na ile sanamu ya kusubu, yule kuhani akawauliza, “Mnafanya nini?”

1918:19 Ay 13:5; 21:5; 29:9; 40:4; Isa 52:15; Mik 7:16; Amu 17:10; Hes 26:42Wakamjibu, “Nyamaza kimya! Weka mkono wako juu ya kinywa chako na ufuatane nasi, uwe baba yetu na kuhani wetu. Si ni afadhali utumikie kabila na ukoo katika Israeli kama kuhani kuliko kumtumikia mtu mmoja na watu wa nyumbani mwake?” 20Yule kuhani akafurahi. Akachukua ile naivera, zile sanamu nyingine ndogo za nyumbani, na sanamu ya kuchonga, naye akaenda pamoja na wale watu. 21Ndipo wakageuka na kuondoka wakiwatanguliza mbele watoto wao wadogo, wanyama wao wa kufugwa na mali zao.

22Walipokuwa wamesafiri umbali kidogo toka nyumbani kwa Mika, watu walioishi karibu na Mika wakaitwa wakakusanyika pamoja, nao wakawafikia Wadani. 23Walipofuatilia wakipiga kelele Wadani wakawageukia na kumwambia Mika, “Una nini wewe hata ukaja na kundi la watu namna hii ili kupigana?”

24Akawajibu, “Mmechukua miungu yote niliyoitengeneza, mkachukua na kuhani wangu, nanyi mkaondoka. Nimebaki na nini kingine? Mnawezaje kuniuliza, ‘Una nini wewe?’ ”

25Wadani wakamjibu, “Usibishane na sisi, la sivyo watu wenye hasira kali watakushambulia, nawe na watu wa nyumbani mwako mtapoteza maisha.” 2618:26 2Sam 3:39; Za 18:17; 35:10Basi Wadani wakaenda zao, naye Mika alipoona kuwa wana nguvu kumliko yeye, akageuka na kurudi nyumbani kwake.

2718:27 Mwa 34:25; Hes 31:10; Mwa 49:17; Yos 19:47Kisha wakachukua vile Mika alivyokuwa ametengeneza, na kuhani wake, wakaendelea hadi Laishi, dhidi ya watu walio na amani, wasiokuwa na wasiwasi. Wakawashambulia kwa upanga na kuuteketeza mji wao kwa moto. 28Hapakuwa na yeyote wa kuwaokoa, kwa kuwa kulikuwa mbali sana na Sidoni na hawakuwa na ushirikiano na mtu mwingine yeyote. Mji ulikuwa kwenye bonde karibu na Beth-Rehobu.

Wadani wakaujenga upya huo mji na kuishi humo. 29Wakauita ule mji Dani kwa kufuata jina la baba yao aliyezaliwa na Israeli, ingawa mji huo ulikuwa ukiitwa Laishi hapo kwanza. 3018:30 Kut 2:22; Amu 17:3-5Kisha Wadani wakajisimamishia sanamu ile ya kuchonga, naye Yonathani mwana wa Gershomu, mwana wa Mose pamoja na wanawe walikuwa makuhani wa kabila la Wadani mpaka nchi hiyo ilipotekwa. 3118:31 Amu 19:18; 20:18; Yos 18:1; Yer 7:14Wakaisimamisha na kuiabudu hiyo sanamu ya kuchonga ya Mika aliyokuwa ameitengeneza, wakati wote ule nyumba ya Mungu ilipokuwa huko Shilo.

Bibelen på hverdagsdansk

Dommerbogen 18:1-31

Dans stamme stjæler Mikas afgudsbilleder

1På den tid var der som sagt ingen konge i Israel. Dans stamme søgte efter et sted, hvor de kunne slå sig ned, eftersom det endnu ikke var lykkedes dem at indtage det område, de havde fået tildelt. 2De udvalgte fem tapre krigere som repræsentanter for deres forskellige klaner fra byerne Zora og Eshtaol. De blev sendt af sted for at udspionere hele landet. I Efraims højland overnattede de i Mikas hus. 3Da de hørte den unge levits dialekt, gik de hen til ham og spurgte: „Hvordan er du kommet herhen? Hvad laver du her?” 4Så fortalte han dem, hvordan Mika havde taget imod ham og ansat ham som sin personlige præst.

5„Bed så Gud om at vise os, om vores ærinde vil lykkes!” sagde de. 6Præsten svarede: „Vær ved godt mod! Herren vil være med jer på rejsen!”

7Derefter fortsatte de fem mænd til byen Lajish. De så, at byens folk levede ubekymret i fred og sikkerhed ligesom sidonierne, at de var velstående og ikke manglede noget, og at de boede langt fra Sidon og ingen kontakt havde med de omkringboende aramæere.

8Da spionerne kom tilbage til Zora og Eshtaol, spurgte deres stammefæller dem: „Hvordan gik det? Hvad fandt I ud af?” 9-10Mændene svarede: „Lad os tage af sted og erobre Lajish! Vi har set, at landet er virkelig godt. Der er ikke noget at betænke sig på. Folket dér lever fredeligt og bekymrer sig ikke om noget, for de mangler intet. Gud har givet os et frugtbart og rummeligt land.”

11Så rykkede danitterne op fra Zora og Eshtaol med en hær på 600 bevæbnede krigere, 12og de slog lejr ved det sted vest for Kirjat-Jearim i Juda, som den dag i dag kaldes Dans Lejr. 13Derfra gik de ind i Efraims højland.

Da de kom til Mikas hus, 14sagde spionerne til krigerne: „I gudehuset derhenne er der en efod, nogle husguder, et gudebillede og en støbt gudestatuette. Mon ikke vi er enige om, hvad vi skal gøre?”

15-16Så gik de fem mænd hen til gudehuset, mens de 600 krigere blev stående uden for porten. Da den unge præst kom ud til porten, hilste mændene hjerteligt på ham. 17Mens præsten stod udenfor sammen med krigerne, kom de fem mænd ud fra Mikas gudehus med gudebilledet, efoden, husguderne og den støbte gudestatuette. 18„Hvad er det, I gør?” udbrød præsten forbavset. 19„Ti stille og følg med!” svarede de. „Fra nu af skal du være vejleder og præst for os! Er det ikke bedre at være præst for en hel stamme end bare for en enkelt mand?” 20Det forslag syntes præsten godt om, og uden yderligere indvendinger tog han efoden, husguderne og gudebilledet og fulgte med dem.

21Hele gruppen fortsatte nu rejsen mod Lajish med deres børn, kvæg og ejendele forrest. 22Da de var kommet lidt på afstand, tilkaldte Mika sine naboer og satte efter dem, der havde stjålet hans guder. Da de havde indhentet dem, 23råbte de til dem, at de skulle standse.

„Hvad er der i vejen?” spurgte danitterne. „Hvorfor kommer du med alle de folk?” 24„Hvad tror I?” råbte Mika tilbage. „I har stjålet mine guder og min præst, så nu har jeg ingenting tilbage. Og så spørger I, hvad der er i vejen!” 25„Du gør bedst i at passe dig selv!” svarede danitterne. „Ellers kunne det være, at nogle af os blev sure og huggede jer alle sammen ned!”

26Da Mika blev klar over, at der ikke var noget at stille op, vendte han om og gik hjem, og danitterne fortsatte deres rejse 27-28med hans afgudsbilleder og hans præst.

Da de nåede frem til Lajish, der lå fredeligt og trygt i dalen ved Bet-Rehob, huggede de indbyggerne ned og brændte byen af. Der var ingen, der kom til undsætning, afstanden til Sidon var for stor, og de havde ingen kontakt med de omkringboende aramæere. Efter sejren genopbyggede danitterne byen og blev boende der. 29De gav byen et nyt navn og opkaldte den efter deres forfar Dan, en af Jakobs sønner.

30Derefter opstillede de afgudsbillederne i byen og udnævnte Jonatan fra Gershoms slægt18,30 Teksten siger: „Gershom, søn af Moses”, men nogle håndskrifter siger „Manasse” i stedet for Moses. Jonatan er sikkert den føromtalte levit. til præst. Jonatans efterkommere vedblev at være præster for danitterne, indtil byens befolkning blev ført bort som fanger til et fjendtligt land. 31Danitterne brugte Mikas afgudsbilleder, imens Herrens helligdom var i Shilo.